Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 23
  • Miujiza Zaidi Katika Kapernaumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Miujiza Zaidi Katika Kapernaumu
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Miujiza Mingi Zaidi Katika Kapernaumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Yesu Afanya Miujiza Huko Kapernaumu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Miujiza Ambayo Yesu Alifanya Katika Mji Alimokaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Sababu Iliyomfanya Yesu Aje Duniani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 23

Sura 23

Miujiza Zaidi Katika Kapernaumu

KATIKA Sabato iliyofuata baada ya Yesu kuwaita wanafunzi wake wanne wa kwanza—Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana—wote waenda kwenye sinagogi la kwao katika Kapernaumu. Huko Yesu aanza kufundisha, nao watu washangaa sana kwa sababu awafundisha kama mtu mwenye mamlaka wala si kama waandishi.

Katika Sabato hii mtu aliyepagawa na roho mwovu yupo. Baada ya muda fulani, yeye apaaza sauti akisema: “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! umekuja kutuangamiza? Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu.”

Kwa kweli roho mwovu aongozaye mtu huyo ni mmoja wa malaika za Shetani. Akimkemea roho mwovu huyo, Yesu asema: “Fumba kinywa umtoke!”

Basi, roho mwovu huyo amtupa chini na kumtetemesha mwili kweli kweli na kupiga makelele makubwa. Lakini amtoka mtu huyo bila kumuumiza. Kila mtu ashangaa sana! “Nini hii?” wauliza. “Kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu [roho waovu, NW], nao wamtii.” Habari za jambo hilo zazambaa katika sehemu zote zinazokaribiana na eneo hilo.

Wakiondoka kwenye sinagogi, Yesu na wanafunzi wake waenda nyumbani kwa Simoni, au Petro. Huko mama-mkwe wa Petro ni mgonjwa sana akiwa na homa kali. ‘Tafadhali msaidie,’ wamsihi. Kwa hiyo Yesu asogea, amshika mkono, na kumwinua. Papo hapo apona na kuanza kuwatayarishia chakula!

Baadaye, jua limeshuka, watu kutoka sehemu zote waanza kuja nyumbani kwa Petro wakiwa na wagonjwa wao. Baada ya muda mfupi mji mzima umekusanyika mlangoni! Naye Yesu aponya wagonjwa wao wote, bila kujali wana magonjwa gani. Hata aweka huru waliopagawa na roho waovu. Wanapowatoka, roho aliowafukuza wapaaza sauti hivi: “Wewe u Mwana wa Mungu.” Lakini Yesu awakemea wala hawaruhusu waseme kwa sababu wajua yeye ndiye Kristo. Marko 1:21-34; Luka 4:31-41; Mathayo 8:14-17.

▪ Ni jambo gani latukia katika sinagogi siku ya Sabato baada ya Yesu kuwaita wanafunzi wake wanne?

▪ Yesu aenda wapi aondokapo katika sinagogi, na ni muujiza gani afanya humo?

▪ Ni jambo gani latukia baadaye jioni iyo hiyo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki