Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 30-31
  • Yerusalemu Na Hekalu La Siku Za Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yerusalemu Na Hekalu La Siku Za Yesu
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • Yerusalemu Siku za Mitume
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • B11 Hekalu la Mlimani Katika Karne ya Kwanza
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani
    ‘Ona Nchi Nzuri’
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 30-31

Yerusalemu Na Hekalu La Siku Za Yesu

Yerusalemu/Hekalu la Herode

MUDA mfupi baada ya Yesu kuzaliwa, Yosefu na Maria walimpeleka Yerusalemu, jiji ambalo Baba yake wa kimbingu alikuwa ameweka jina Lake. (Lu 2:22-39) Alipokuwa na umri wa miaka 12 Yesu alienda huko tena kwa ajili ya Pasaka. Walimu waliokuwa hekaluni walishangazwa na uelewevu wake. (Lu 2:41-51) Ujenzi wa hekalu hilo ambao ulikuwa sehemu ya programu ya ujenzi ya Herode Mkuu ulichukua zaidi ya “miaka 46.”—Yoh 2:20.

Wakati wa huduma yake, Yesu alihudhuria sikukuu huko Yerusalemu, ambapo mara nyingi alifundisha umati. Mara mbili aliwafukuza wabadili fedha na wafanyabiashara kutoka kwenye ua wa hekalu.—Mt 21:12; Yoh 2:13-16.

Kwenye dimbwi la Bethzatha lililokuwa kaskazini ya hekalu hilo, Yesu alimponya mtu aliyekuwa ameugua kwa miaka 38. Mwana wa Mungu alimponya kipofu na kumwambia aende akanawe katika dimbwi la Siloamu lililokuwa kusini mwa jiji hilo.—Yoh 5:1-15; 9:1, 7, 11.

Mara kwa mara Yesu aliwatembelea marafiki wake Lazaro, Maria, na Martha huko Bethania, jiji lililokuwa “karibu kilometa tatu” mashariki ya Yerusalemu. (Yoh 11:1, 18, kielezi-chini, New World Translation of the Holy Scriptures—With References; 12:1-11; Lu 10:38-42; 19:29; ona “Eneo la Yerusalemu,” ukurasa wa 18.) Siku chache kabla ya kifo chake, Yesu alienda Yerusalemu akipitia Mlima wa Mizeituni. Wazia Yesu akisimama na kutazama upande wa magharibi mahali ambapo jiji hilo lilikuwa na kulililia. (Lu 19:37-44) Yesu aliliona jiji kama unavyoliona katika picha iliyo upande wa juu wa ukurasa unaofuata. Kisha aliingia Yerusalemu akiwa juu ya mwana-punda, labda kwa kupitia mojawapo ya malango yaliyokuwa mashariki mwa jiji hilo. Umati wa watu walimkaribisha kwa shangwe akiwa Mfalme wa Israeli wa wakati ujao.—Mt 21:9-12.

Mambo muhimu yaliyotendeka kabla ya kifo cha Yesu yalitukia Yerusalemu au karibu na jiji hilo: bustani ya Gethsemane, ambapo Yesu alisali; jumba la Sanhedrini; nyumba ya Kayafa; jumba la Gavana Pilato na, hatimaye Golgotha.—Mk 14:32, 53–15:1, 16, 22; Yoh 18:1, 13, 24, 28.

Baada ya kufufuliwa, Yesu alionekana Yerusalemu na maeneo yaliyokuwa karibu na hapo. (Lu 24:1-49) Kisha akapaa mbinguni akiwa kwenye Mlima wa Mizeituni.—Mdo 1:6-12.

[Mchoro katika ukurasa wa 31]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Yerusalemu/Hekalu la Herodi

Sehemu Za Hekalu

1. Patakatifu Zaidi

2. Patakatifu

3. Madhabahu ya Toleo la Kuteketezwa

4. Bahari ya Kuyeyushwa

5. Ua wa Makuhani

6. Ua wa Israeli

7. Ua wa Wanawake

8. Ua wa Mataifa

9. Kizuizi (Soreg)

10. Nguzo za Kifalme

11. Nguzo za Sulemani

HEKALU

Lango

Ua wa Makuhani

Lango

Patakatifu Madhabahu

Zaidi Patakatifu ya Toleo Ua wa Ua wa

Kuteketezwa Israeli Wanawake

Bahari

Kuyeyushwa

Lango Nguzo za

Kizuizi (Soreg) Sulemani

Ua wa Mataifa

Mlango

Nguzo za Kifalme

Malango

Mnara wa Antonia

Daraja

Jumba la Sanhedrini?

BONDE LA TIROPOA

Dimbwi la Siloamu

Mfereji

Nyumba ya Kayafa?

Jumba la Gavana

Golgotha?

Golgotha?

Dimbwi la Bethzatha

Bustani ya Gethsemane?

MLIMA WA MIZEITUNI

BONDE LA KIDRONI

En-rogeli

Chemchemi ya Maji ya Gihoni

BONDE LA HINOMU (GEHENA)

[Picha katika ukurasa wa 30]

Picha hii inaonyesha upande wa mashariki wa Yerusalemu la kisasa: (A) eneo la hekalu, (B) bustani ya Gethsemane, (C) Mlima wa Mizeituni, (D) nyika ya Yuda, (E) Bahari ya Chumvi

[Picha katika ukurasa wa 31]

Picha hii imepigwa kutoka upande wa magharibi wa Mlima wa Mizeituni katika siku za Yesu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki