Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 80 uku. 188-uku. 189 fu. 1
  • Yesu Anachagua Mitume Kumi na Wawili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anachagua Mitume Kumi na Wawili
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Achagua Mitume Kumi na Wawili
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kuchagua Mitume Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kuchagua Mitume Wake
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Yesu Anafundisha Juu ya Mlima
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 80 uku. 188-uku. 189 fu. 1
Yesu na mitume wake 12

SOMO LA 80

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Wawili

Baada ya Yesu kuhubiri kwa karibu mwaka mmoja na nusu, alihitaji kufanya uamuzi muhimu. Angewachagua nani wafanye kazi kwa ukaribu pamoja naye? Angewazoeza nani ili waongoze katika kutaniko la Kikristo? Ili afanye maamuzi hayo, Yesu alihitaji mwongozo wa Yehova. Kwa hiyo, akaenda kwenye mlima ambapo angekuwa peke yake, naye akasali usiku wote. Asubuhi ilipofika, Yesu akawaita baadhi ya wanafunzi wake kisha akachagua mitume 12. Unakumbuka majina yao? Walikuwa Petro, Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, Tomasi, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni, na Yuda Iskariote.

Andrea, Petro, Filipo, Yakobo

Andrea, Petro, Filipo, Yakobo

Mitume hao kumi na wawili wangesafiri na kuhubiri pamoja na Yesu. Baada ya kuwazoeza, Yesu aliwatuma wakahubiri peke yao. Yehova aliwapa mamlaka ya kufukuza roho waovu na kuponya wagonjwa.

Yohana, Mathayo, Bartholomayo, Tomasi

Yohana, Mathayo, Bartholomayo, Tomasi

Yesu aliwaita Mitume hao kumi na wawili rafiki zake, na aliwaamini. Mafarisayo walifikiri kwamba mitume walikuwa watu wasio na elimu na wa kawaida tu. Lakini Yesu aliwazoeza kwa ajili ya kazi yao. Wangekuwa pamoja na Yesu pindi muhimu zaidi maishani mwake, kama vile kabla ya kifo chake na baada ya ufufuo wake. Kama Yesu, wengi kati ya wale Mitume kumi na wawili walitoka Galilaya. Baadhi yao walikuwa wameoa.

Yakobo mwana wa Alfayo, Yuda Iskariote, Thadayo, Simoni

Yakobo mwana wa Alfayo, Yuda Iskariote, Thadayo, Simoni

Mitume walikuwa wanaume wasio wakamilifu ambao walifanya makosa. Nyakati nyingine, walizungumza bila kufikiri na wakafanya maamuzi mabaya. Nyakati nyingine, walikosa subira. Hata walibishana kuhusu ni nani aliyekuwa mtu mkuu zaidi kati yao. Lakini walikuwa watu wema ambao walimpenda Yehova. Wao ndio wangefanyiza msingi wa kutaniko la Kikristo baada ya Yesu kuondoka.

“Nimewaita rafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.”​—Yohana 15:15

Maswali: Yesu aliwachagua nani wawe mitume wake 12? Yesu aliwatuma mitume wake wakafanye kazi gani?

Mathayo 10:1-10; Marko 3:13-19; 10:35-40; Luka 6:12-16; Yohana 15:15; 20:24, 25; Matendo 2:7; 4:13; 1 Wakorintho 9:5; Waefeso 2:20-22

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki