Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 5/1 kur. 206-211
  • Washindi Wenzake Juu ya Ulimwengu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Washindi Wenzake Juu ya Ulimwengu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WACHUKIWA KWA AJILI YA KINACHOHUBIRIWA
  • Ushindi Juu ya Ulimwengu Bila Vita Yenye Silaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ushindi wa Kimungu—Maana Yake kwa Wanadamu Wanaotaabika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Chanzo cha Taabu ya Wanadamu Chakaribia Kuondolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Faida za Wanadamu Kutokana na Ushindi Katika Har–Magedoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 5/1 kur. 206-211

Washindi Wenzake Juu ya Ulimwengu

1. Ushindi wa Yesu juu ya ulimwengu uliwekea akina nani mfano, naye mtume Yohana mzee alipataje kuwa mfano wa hili?

USHINDI wa Yesu juu ya ulimwengu bila ya kujitia katika vita pamoja nao kwa matumizi ya silaha za kijeshi unasimama kama mfano kwa wanafunzi wake. Mitume wake waaminifu wa karne ya kwanza C.E. waliuiga mfano huo. Chuki yote ya ulimwengu kwa makumi ya miaka ilishindwa kuvunja kujitoa kwao kusikogeuka kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi wala kunyamazisha kuhubiri kwao juu yake ulimwenguni pote. Miaka michache tu mbele ya mwisho wa karne hiyo mtume wa Kikristo Yohana, yaelekea ndiye wa mwisho wa mitume kuendelea kuwa hai, aliwaandikia Wakristo wenzake naye akasema: “Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.” (Ufu. 1:9) Kama mitume hao waaminifu, wanafunzi wa kweli wa Yesu wanauiga mfano wake ili wapate ushindi juu ya ulimwengu huu wa karne ya 20.

2. Kulingana na unabii wa Yesu juu ya magumu ya wafuasi wake, ni kwa njia gani yeye alivyo chombo cha kuchukiwa na ulimwengu?

2 Ajapokuwa hayupo tena duniani, Yesu Kristo ni chombo cha chuki ya ulimwengu hata leo. Huenda maneno haya yakapingwa na washiriki wale karibu milioni elfu moja wa makanisa ya Kristendomu, watakaosisitiza, “Sisi hatumchukii!” Na hali kunalo jaribio ambalo kwalo twaweza kujua kama twamchukia Yesu leo. Katika unabii juu ya mambo ambayo wanafunzi wake wangepatwa nayo Yesu aliyasema maneno haya ya onyo la mapema kwao: “Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” “Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.” (Mt. 10:22; 24:9) Kwa busara, basi, kuchukiwa kwa wanafunzi wa Kristo kwa ajili ya jina lake kwamaanisha kuchukiwa kwa Kristo mwenyewe wakati ule ule.

3. Ili aendelee kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu, vivyo hivyo lazima mtu apate ushindi gani, na pamoja na zawadi gani?

3 Hakuna kuuepa ukweli ulio wazi: wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo lazima wapambane na chuki ya ulimwengu na kuivumilia sawa na alivyofanya yeye. Kwa hiyo, ili mwanafunzi aendelee kuwa hivyo katika maana ya kweli, yamaanisha kwamba lazima apate ushindi juu ya ulimwengu. Si kwa njia ya jeuri, bali bila vita yenye silaha, kama vile katika habari ya Yesu mwenyewe. Ulizo kwa mwanafunzi ni, Je! ulimwengu utamshinda yeye, au yeye ataushinda huo? Akishindwa, lazima vile vile ayapate matokeo yenye huzuni ya kushindwa. Lakini, akiushinda ulimwengu, atathawabishwa na zawadi ya ajabu ya ushindi​—kwenye upande wa Mungu.

4. Nini kinachohakikisha kwamba, kuchukiwa kwa mtu leo na mataifa yote na watu kwa ajili ya jina la Kristo hakumaanishi kuchukiwa kwa ajili ya kuitwa tu Mkristo?

4 Kuchukiwa huku na watu wote na mataifa kwa ajili ya jina la Kristo, maana yake nini? Je! maana yake ni kuchukiwa na watu na mataifa kwa ajili tu ya kuitwa Mkristo? Sivyo, siyo leo. Leo kuna mamia ya mamilioni ya watu wa kidini wanaoitwa “Wakristo” na ambao ni wenye msimamo mzuri katika sehemu nyingine yote ya ulimwengu wa wanadamu na katika ujamaa wa kirafiki nao. Ni akina nani hawa wanaoitwa Wakristo wanaofurahia urafiki wa ulimwengu na wasiopatwa na chuki ya ulimwengu? Kulingana na uchunguzi wote, hawa ndio washiriki wa madhehebu ya kidini ya Kristendomu. Wao hawapatwi na mateso kama jamii, sivyo? Wao hawapigwi marufuku wala kugombezwa kama jamii wala kusukumiwa chini-chini, sivyo? Oh, wao wanapigana kati yao wenyewe, si kwa ajili ya kuitwa Wakristo, bali kwa ajili ya kuwa katika madhehebu mbalimbali ya kidini ya Kristendomu. Ulizo la mamlaka gani ya kidini wanayotaka iwatawale latiwa ndani.

5. Kwa hiyo, basi, maneno ya Yesu “kwa ajili ya jina langu” yanamaanisha kwa ajili ya nini?

5 Maneno ya Yesu “kwa ajili ya jina langu” yamaanisha kwa ajili ya kushikamana na Yesu kwa ambavyo alivyo rasmi, Mfalme wa Kimasihi aliyewekwa na Yehova Mungu. Yamaanisha kwa ajili ya kumkiri kwetu na kumtii yeye kama Bwana halisi, Bwana wetu wa kimbinguni ambaye amri zake twazitimiliza kama zinazozitangulia zile za mtawala ye yote wa kidunia. Yamaanisha kushikamana na serikali ya Kimasihi anayoiwakilisha wala si kuugawanya uaminifu wa mtu kwa kujichangamanisha na mambo ya serikali yo yote ya kidunia iliyoundwa na mwanadamu. Yamaanisha kujisikia na kutenda kama mtumwa wake Yesu Kristo, mtumwa si aliye mali yake mwenyewe bali mali ya Yesu Kristo kwa gharama ya damu yake mwenyewe ya uhai. Ndiyo, vile vile yamaanisha kuwa shahidi wa Mungu na Baba ya Yesu Kristo, yaani, Yehova, Chanzo cha ufalme wa Kimasihi.

6. Kwa hiyo, kuitwa kwa jina la Kristo kwamaanisha nini, nako kuishi kulingana na jina lake kunatuwekea sharti kwa njia gani?

6 Kwa hiyo, kuitwa kwa jina la Kristo kwamaanisha mengi zaidi kuliko kuishi maisha safi tu. Kwahitaji mtu ajitambulishe si kama mali ya taratibu ya mambo ya ulimwenguni pote ambayo Kristendomu ndiyo sehemu iliyo kuu zaidi na yenye nguvu, bali kama mali ya taratibu mpya ya Mungu iliyo safi, ambayo yeye ameiweka akibani kwa ajili ya wakaaji wa dunia. Kwamweka mtu katika hali ya kuwa mgeni, mkaaji wa muda katika hii taratibu ya mambo ya kilimwengu. (1 Pet. 2:11) Hii inamzuia Mkristo wa kweli kutokuwa mmoja na watu wa ulimwengu na kutojipatanisha na njia zao, kutokuchochewa moyoni wala kuongozwa na utukuzo wa taifa wa kilimwengu, kiburi cha nchi ya kidunia. Kwa habari yake, Yesu aliwaambia Wayahudi wenye kulitukuza taifa: “Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.” (Yohana 8:23) Hivyo Yesu hakujifanya sehemu ya ulimwengu huu pamoja na tamaa zake za kichoyo. Kuishi kulingana na jina lake vile vile kunamwekea mwanafunzi wake sharti la kutokuwa sehemu ya ulimwengu huu.​—Yohana 17:14, 16.

7. Walimwengu wanaonaje kwa kawaida juu ya kutokushiriki kwa Wakristo wa kweli katika mambo yapendwayo sana ya kilimwengu, naye Yesu alilielezaje hili?

7 Je! hali hiyo inachochea uchungu au kusababisha hasira ya ghafula katika mtu aliye na urafiki na ulimwengu huu? Nia hii ya ukatili ina maoni ya kawaida juu ya kutokushiriki kwa mwanafunzi wa kweli wa Kristo katika mambo yanayopendwa sana ya ulimwengu huu. Walimwengu hawaupendi msimamo huo wa Kikristo. Kama vile Yesu alivyowaambia mitume wake: “Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.” (Yohana 15:19) Jina la Kristo lasimamia kujitenga na ulimwengu huu. Kuchukiwa kwa ajili ya jina la Kristo kwamaanisha kuchukiwa kwa sababu mtu si sehemu iliyoungana na ulimwengu huu, kwa sababu Kristo amemchagua huyo atoke katika ulimwengu huu.

WACHUKIWA KWA AJILI YA KINACHOHUBIRIWA

8. Kuhubiriwa kwa ufalme wa Mungu na Kristo kutaupambanishaje ulimwengu na mhubiri wa Ufalme, na kwa sababu gani?

8 Mbele ya Gavana Pontio Pilato, Yesu alisema: “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. . . . Lakini ufalme wangu sio wa hapa.” (Yohana 18:36) Ni namna gani, basi, mtu ambaye ni Mkristo wa kweli anavyoweza kuwa sehemu ya ulimwengu huu na wakati ule ule awe anaupendelea ufalme wa Mungu kwa njia ya Kristo, ambao si sehemu ya ulimwengu huu na usio na chanzo chake katika ulimwengu huu? Mkristo wa kweli asingeweza kufanya hivyo, kwa maana Yesu alisema kwamba Shetani Ibilisi ndiye “mtawala wa ulimwengu.” (Yohana 12:31; 14:30; 16:11, NW) Kwa sababu hii kuhubiriwa kwa ufalme wa Yesu Masihi usio wa kilimwengu kutaileta chuki ya ulimwengu juu ya mhubiri; kutaupambanisha ulimwengu na mhubiri. Kulifanya hivyo katika habari ya Yesu mwenyewe; kumefanya hivyo nako kutafanya hivyo katika habari ya wanafunzi wake wa kweli.

9. Ni kwa sababu gani inampasa mhubiri wa Ufalme kuvumilia hata mwisho ili apate ushindi juu ya ulimwengu?

9 Na hali, nyuma ya kueleza juu ya chuki ya ulimwengu inayokuja juu ya wanafunzi wake, Yesu alisema: “Mwenye kuvumilia hata mwisho ndiye atakayeokoka. Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.” (Mt. 24:13, 14) Kuhubiriwa kwa ufalme huu, zijapokuwa ni habari njema, kutapatwa na chuki ya ulimwengu. Kwa nini hivyo? Kwa maana ufalme wa Mungu wa Kimasihi na falme za kisiasa za ulimwengu ni maadui. Ili ufalme wa Mungu kwa njia ya Kristo uchukue uongozi kamili wa dunia, inahitaji kukomeshwa milele kwa falme za ulimwengu huu zilizoundwa na mwanadamu. (Dan. 2:44) Hapa, basi, ndipo ambapo Wakristo wa kweli inawapasa kupata ushindi juu ya ulimwengu.

10. Kusudi apate ushindi, inampasa Mkristo kushindana na chuki ya ulimwengu ili afanye nini, nao imewapasa wauige mfano wa nani?

10 Namna gani hivyo? Siyo kwa kubeba Biblia katika mkono mmoja na upanga, kombora au bunduki yenye kumimina risasi katika mkono ule mwingine! Bali kwa kupambana na chuki ya ulimwengu na kusonga mbele kwa amani, bila silaha, katika kuzihubiri “habari njema hizi za ufalme” (NW) ulimwenguni pote kwa ushuhuda kwa mataifa yote bila ya kukataa, mbele ya mwisho wa hii taratibu ya mambo kuja. Haimpasi mhubiri wa Ufalme airuhusu chuki ya ulimwengu, ukatili na upinzani vimshinde. Yeye yuko chini ya maagizo makuu ya yeye ambaye alimwagiza kuzihubiri hizi habari njema, Yesu Kristo, ambaye ndiye Bwana wake. Lazima awe kama Bwana wake. Yesu Kristo huyu ndiye aliyekuwa Mhubiri mkuu kupita wote wa habari njema wa wakati wo wote duniani. Wale wanaoitwa kwa jina lake wanafanya kama yeye alivyofanya; lazima wafanye kama alivyosema na alivyofanya vile vile. Kwanza alipokuwa amemaliza kuhubiri kwake kwa Ufalme ijapokuwa chuki ya ulimwengu na upinzani yeye alisema: “Mimi nimeupata ushindi juu ya ulimwengu.” (Yohana 16:33, Weymouth) Katika hili alituwekea mfano.

11. Kungali kuna kazi gani ya kufanywa, nao ushindi kamili waweza kudaiwa wakati gani peke yake?

11 Kungali kuna kazi ya kuhubiri “habari njema hizi za ufalme” ulimwenguni pote. Tangu mwaka uliofuata vita wa 1919, habari njema hizi zimehubiriwa na mashahidi wa Yehova wa Kikristo bila ya kukatizwa moja kwa moja kupita Vita ya Pili ya Ulimwengu hata sasa. Wao wako chini ya amri ya kimungu kupitia kwa Kristo kutokuacha kuuchukua ushuhuda huu wa ufalme wa Mungu wa Kimasihi ulimwenguni pote mpaka mwisho wa hii taratibu ya mambo utakapokuja. Watakapokwisha kuzihubiri “habari njema hizi” na Ufalme wenye ushindi utakapokwisha kuileta hii taratibu ya kilimwengu kwenye mwisho wake ulio kamili ndipo tu watakapoweza kusema, kila mtu akijisemea mwenyewe: “Mimi nimeupata ushindi juu ya ulimwengu.”

12. Ili kupata ushindi huo, ni moyo wa namna gani unaohitajiwa, kama anavyosema mtume Yohana?

12 Ushindi huo wawezekana kwetu! Yesu Kristo atakuwa na washindi wenzake juu ya ulimwengu huu. Ushindi huu utakuwa umepatikana kwa shida, lakini waweza kupatikana kama vile ushindi wa Yesu mwenyewe unavyotuhakikishia. “Jipeni moyo,” alisema Yesu. Nako kuupata ushindi kutahitaji moyo. Lazima uwe moyo uliotokezwa na imani katika Mungu Mwenye Nguvu Zote. Juu ya hili mtume Yohana, aliyeyaandika maneno yenye ushindi ya Yesu, alisema hivi, muda mfupi tu mbele ya ushindi wake mwenyewe wakati wa kufa: “Kumpenda Mungu ni kuzishika amri zake; nazo hazilemezi, kwa maana kila mtoto wa Mungu ni mshindi juu ya ulimwengu usiomcha Mungu. Ushindi uushindao ulimwengu ni imani yetu, kwa maana n’nani aliye mshindi juu ya ulimwengu isipokuwa yeye aaminiye kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu?”​—1 Yohana 5:3-5, NE.

13. Ni akina nani leo wenye “kanuni yenye ushindi” ya imani, nalo hili laonyeshwaje kwa habari ya Yesu mwana wa Mariamu?

13 Ni muhimu kuwa na sifa hiyo ya kiroho ya imani. Kama vile tafsiri ya Weymouth ya mwaka wa 1902 invyoyatafsiri maneno ya Yohana: “Kwa maana kila mtoto wa Mungu huushinda ulimwengu; nayo kanuni yenye ushindi iliyoushinda ulimwengu ni imani yetu. N’nani isipokuwa mtu aaminiye kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu anayeushinda ulimwengu?” (1 Yohana 5:4, 5) Kanuni hiyo yenye ushindi ya imani ndiyo nguvu ya ndani inayowavuta mashahidi wa Yehova wa Kikristo leo na kuendelea kuwafanya kuwa kweli kwa Mwana wa Mungu. Wao wanaamini, si kwamba yeye alikuwa mwanamume tu aliyezaliwa na mwanamume wa kawaida tu aliyeoa mke, bali kwamba yeye alizaliwa na bikira wa Kiyahudi ambaye kwa tumbo lake la uzazi Mungu Mwenye Nguvu Zote aliuhamisha uhai wa Mwana wake mzaliwa wa pekee kutoka mbinguni, akazaliwe kama Mwana wa Mungu wa kibinadamu. Wao wanaamini kwamba mara tu nyuma ya ubatizo wake katika Mto wa Yordani, alizaliwa kwa roho takatifu ya Mungu na kutiwa mafuta kama Masihi; lakini kwamba siku tatu nyuma ya kifo chake cha dhabihu ‘alidhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu.’​—Rum. 1:3, 4; Matendo 13:32, 33.

14. Mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanaonyeshaje kwamba wanalitii onyo la Yohana juu ya wapinga Kristo?

14 Wakiyatii maonyo ya mtume Yohana juu ya wapinga Kristo ambao wangeinuka, mashahidi wa Yehova wa Kikristo mnamo huu “mwisho wa taratibu ya mambo” hawajiachilii wadanganywe na kuvutwa kwenye Makristo wa uongo, wapinga Kristo wanaojionyesha katika Kristendomu au chini ya udhamini wa Kristendomu, kama vile Umoja wa Mataifa kwa ajili ya amani ya ulimwengu na usalama. Wao wamemtambua Masihi wa kweli, Kristo wa kweli, nao wanashikamana naye na Ufalme uliotolewa na Mungu anaouwakilisha. Wanayo imani kwamba ufalme huu wa Kimasihi ulisimamishwa mbinguni katika mwaka wa 1914 C.E., mwishoni mwa Majira ya Mataifa. Kwa hiyo hawawezi kumkubali wala kumwabudu “mnyama” wa mfano, yaani, taratibu ya utawala wa kisiasa ya ulimwenguni pote ya Ibilisi, kama serikali ifaayo ya dunia. Wala hawawezi kuiabudu na kuweka matumaini yao kwenye “sanamu” ya kisiasa ya huyo “mnyama,” yaani, Umoja wa Mataifa ambao Kristendomu ameudhamini kwa ajili ya kuendelezwa milele kwa utawala usiokamilika wa kibinadamu juu ya wanadamu wote kwa wakati usiojulikana.

15. Wao wanasimamaje pamoja na wale wanaosimuliwa katika Ufunuo 15:2-4?

15 Hasha, sivyo, wao hawawezi kufanya jambo kama hilo la kuabudu sanamu hata kidogo. Wakiwa na imani yenye ushindi juu ya madanganyo ya ulimwengu huu, wao wanasimama upande wa wale wanaoonyeshwa katika sura ya kumi na tano ya Ufunuo aliopewa Yohana, mstari wa pili mpaka wa nne, ambapo mtume Yohana anasema: “Nikaona kilichoonekana kama bahari ya kioo kilichoangazishwa na moto, na kando ya bahari ya kioo, walioshika vinubi ambavyo Mungu alikuwa amewapa, walikuwa wale waliokuwa wameupata ushindi juu ya mnyama na sanamu yake na hesabu ya jina lake. Walikuwa wakiuimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakiimba hivi: ‘Yaliyo makuu na ya ajabu ni matendo yako, Ee Bwana Mungu, mwenye enzi yote juu ya vyote; za haki na kweli ni njia zako, ewe mfalme wa vizazi. Nani asiyekuheshimu wewe, Bwana, na kuliabudu jina lako? Kwa maana wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yasimama yamefunuliwa.’”​—Ufu. 15:2-4, NE; Weymouth; NW; Young.

16. Kufikia hapo mashahidi wa Yehova wa Kikristo wametoka wapi wakiwa washindi, na ni wakati gani tu ushindi wao utakapokamilika?

16 Kwa kutenda kupatana na imani yao katika Yehova Mungu Mwenye Nguvu Zote na katika Mwana wake Yesu Kristo, mashahidi wa Kikristo wa Yehova kwa njia hiyo ‘wametokea wakiwa washindi kutoka kwa mnyama wa mwitu na kutoka kwa sanamu yake na kutoka kwa hesabu ya jina lake.’ (NW; An American Translation; Rotherham) Wamefanya hivi ajapokuwa “mnyama wa mwitu” huyu wa kisiasa amefanya vita juu yao na kuwashinda kwa muda mnamo Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. (Ufu. 13:7) Lakini ushindi juu ya taratibu ya kisiasa ya utawala ya ulimwenguni pote ya Ibilisi na sanamu yake ya kisiasa (Umoja wa Mataifa) haujakamilika bado, maadamu Mungu Bwana Mwenye Enzi Yote anaviruhusu vibaki duniani. Tutatokea tukiwa washindi kabisa “mnyama wa mwitu” huyo wa kisiasa pamoja na hesabu yenye aibu ya 666 atakapokwisha tu kulala ameharibiwa katika uwanja wa vita wa Har–​Magedoni. (Ufu. 13:18) Ikiwa twatamani kuwa washindi wenzi wake Yesu Kristo Mwana wa Mungu juu ya tengenezo hilo lililo adui, lazima tuendelee kujiepusha tusitiwe alama kama mtumwa kwa jina lenye hesabu la “mnyama wa mwitu” na kutokuiabudu sanamu yake ya kisiasa.

17. Ikiwa tunayo imani hiyo yenye ushindi, hatutajiacha hata kidogo tuzuiwe tusifanye nini, na kwa hiyo azimio letu ni kufanya nini?

17 Je! sisi tunayo imani yenye ushindi ya kufanyia hili? Ikiwa tunayo, basi hatutamwacha “mnyama wa mwitu” atuondoshe tusizihubiri “habari njema hizi za ufalme” mpaka ushuhuda wa Ufalme katika dunia yote inayokaliwa na wanadamu umemalizika. Ushindi wetu utakuwa, si juu ya “mnyama wa mwitu” na “sanamu” yake tu, lakini juu ya ulimwengu, sawa na vile ule wa Yesu Kristo ulivyokuwa. Kwa hiyo hatutaiacha chuki ya ulimwengu wala dhiki inayosababishwa nayo itushinde wala kutulazimisha kumwasi Mungu. Mpaka yeye atakapojipatia ushindi wake mwenyewe penye Har–​Magedoni, tutaendelea kuziimba sifa zake kusudi kwamba watu mmoja mmoja kutoka mataifa yote waweze kuja na kuabudu mbele zake kupitia kwa Mwana wa Mungu mwenye ushindi, Yesu Kristo.

​—Kutoka The Watchtower, Nov. 1, 1973.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki