Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 6/1 kur. 260-264
  • Tangazo na Azimio

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tangazo na Azimio
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Uwe Mwenye Shukrani—Ufalme wa Kimesiya wa Yehova Watawala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Ni Nani Awezaye Kuisoma “Ishara” Sawasawa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • “Ufalme wa Bwana Wetu na wa Kristo Wake” Waanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • “Israeli wa Mungu” na Mwisho wa Nyakati za Mataifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 6/1 kur. 260-264

Tangazo na Azimio

1. Ni akina nani waliokusanyika katika kusanyiko la mataifa yote, nao walifanya tangazo na azimio kwa jina la nani?

SISI, kundi la mawakili wa serikali iliyo bora iwezayo kupatikana kwa ajili ya jamaa yote ya kibinadamu, tuliokusanyika pamoja Jumamosi hii, tarehe ya ‐‐‐‐ mwezi wa ‐‐‐‐ mwaka wa 197​—penye “Ushindi wa Kimungu” Kusanyiko la Mataifa Yote la mashahidi wa Kikristo wa Yehova linalofanywa katika ‐‐‐‐‐‐‐‐, ‐‐‐‐‐‐‐‐, twafanya tangazo lifuatalo la watu wote na kuazimia katika jina lake yeye aliye Chanzo cha pekee cha serikali yote yenye haki, Bwana Mwenye Enzi Yote wa ulimwengu wote:

2. Uchunguzi wa Maandiko Matakatifu umeonyesha nini juu ya mwanzo wa taabu ya wanadamu iliyopo, na namna gani juu ya kufa ko kote kwa Mwenye Enzi Yote wa Ulimwengu Wote kwa habari ya mambo ya wanadamu?

2 Kama viumbe wenzi wa vingine vya kibinadamu tunavutwa sana mioyoni mwetu kwa sababu ya taabu inayoendelea na kuongezeka ya wanadamu wote tangu Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilipotokea katika mwaka wa 1914. Sisi tuishio mnamo kizazi kilichojua, kikaiona na kuiokoka vita hiyo ya kwanza ya ulimwengu tumetafuta maelezo ya taabu ya wanadamu katika Neno lililoongozwa na roho ya Mungu na kuandikwa kutoka Chanzo cha serikali yote iliyo kamilifu, yaani, Maandiko Matakatifu au Biblia Takatifu. Kutokana na kurasa zake kama zinavyoangazishwa na nuru ya matukio ya kisasa tumejifunza kwamba taabu ya ulimwenguni pote na huzuni kuu ya mataifa haikuanzia nyuma huko katika mwaka wa 1914 kwa bahati tu, bila ya kusudi lenye akili, bila ya kutukia katika wakati uliotangulia kuamriwa, wakati ufaao. Bali, taabu hii isiyolinganika ya wanadamu ilianza katika wakati wake ulioonyeshwa na Mtunza Saa Aliye Mkuu Zaidi ya wote, Mwenye Enzi Yote wa Ulimwengu Wote, Muumba wa jua lenye kushika saa, mwezi na nyota. Yeye si mfu kuelekea mambo ya kibinadamu, bali anapendezwa sana na mapendezi ya wanadamu wote. Yeye anaishi kweli kweli kwa habari ya mahitaji ya wanadamu.

3. Katika wakati barabara, mwaka wa 1914 ulionyesha nini, na je! Mungu ndiye wa kulaumiwa kwa ajili ya taabu ya wanadamu tangu wakati huo, au n’nani?

3 Wanahistoria wa ulimwengu wanaelekeza kwenye mwaka wa 1914 kama unaoonyesha mwisho wa kipindi maalum. Yeye aliyejifanya kusikika mara kwa mara katika historia ya kibinadamu, yaani, Muumba wa mwanadamu, aliuonyesha mwaka uo huo kama wa kumalizika kwa “nyakati zilizowekwa za mataifa,” yanayoitwa Majira ya Mataifa. Mwisho wa haya Majira ya Mataifa ulitazamiwa kwa muda mrefu, kwa maana katika mwaka wa 33 C.E., zaidi ya miaka 1,900 iliyopita, Mwana wa Mungu mwenyewe Yesu Kristo alizungumza juu ya hayo Majira ya Mataifa na kutabiri juu ya kutimizwa kwayo. (Luka 21:24) Alitabiri juu ya mambo ambayo Baba yake wa kimbinguni, Yehova Mungu, angefanya mwishoni mwa hayo Majira ya Mataifa. Mambo ambayo wanadamu na mataifa duniani walifanya wakati wa tarehe hiyo ya muhimu yalikuwa wajibu wao wenyewe. Yeye hakuwalazimisha kulichukua tendo walilolichukua wakati huo, na kwa hiyo anatolewa katika lawama yote kwa ajili ya taabu ya wanadamu ambayo imeendelea kidogo kidogo hata leo hii.

4. Ni juu ya mji gani Majira ya Mataifa yalipoanzia, nayo yafikia utimizo wayo juu ya “mji” gani, na kwa sababu gani?

4 Katika karne za majuzi, tangu kuchapwa na kugawa kwa Biblia Takatifu ulimwenguni pote katika tafsiri nyingi za lugha, wanafunzi wa Biblia wamefanyiza maoni juu ya ambavyo Mungu Aliye Juu Zaidi Sana angefanya mwishoni mwa Majira ya Mataifa. Uangalifu wao umekazia fikira kwenye Yerusalemu wa Mashariki ya Kati, aliyekuwa chini ya uongozi wa Kituruki kwa karne nyingi, kisha kupita chini ya uongozi wa Kiingereza katika mwaka wa 1917, na sasa aliye chini ya uongozi wa Kiisraeli. Wakiyapima Majira ya Mataifa kulingana na hesabu yao ya wakati, wanafunzi wa Biblia hao wametazamia jambo lenye makosa mwishoni mwa Majira ya Mataifa. Wao wanashindwa kujua kwamba kupendezwa kwa Mungu kumeondoka katika Yerusalemu wa kidunia wa siku za Yesu Kristo na mitume wake kuja kwenye “Yerusalemu wa mbinguni,” ambao sasa ndio mji unaoitwa na Biblia Takatifu “mji wa Mungu aliye hai.” (Ebr. 12:22) Miaka 2,520 ya Majira ya Mataifa ilianza katika mwaka wa 607 B.C.E., Yerusalemu wa kidunia ulipoachwa ukiwa na majeshi ya Babeli. Hayo Majira ya Mataifa, kwa sababu hiyo, hayakutimia kabisa juu ya Yerusalemu wa kidunia wa siku za Yesu. Yalikuja kutimia kabisa juu ya “Yerusalemu wa mbinguni,” kikao cha serikali kisichoweza kuharibiwa.

5. Tangu kuharibiwa kwa Yerusalemu na Yuda mwaka wa 607 B.C.E. ni haki gani ya kifalme iliyokanyagwa, na kwa sababu gani Yesu, alipokuwa duniani, hakusimamisha ufalme Yerusalemu?

5 Mwishoni mwa Majira ya Mataifa tofauti ya yale yaliyotukia mwanzoni mwa mwaka wa 607 B.C.E. imepaswa kutazamiwa. Kuharibiwa kwa Yerusalemu na Uyahudi wakati huo silo jambo lililo muhimu. Sivyo, bali kulikuwa ni kupinduliwa kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi uliokuwa umesimamishwa Yerusalemu mikononi mwa jamaa ya kifalme ya Daudi wa Bethlehemu. Tangu mapinduzi hayo na kuendelea haki ya jamaa ya kifalme ya Mfalme Daudi ya kupata serikali juu ya dunia imekanyagwa na mamlaka za ulimwengu za Mataifa zilizofuatana, yaani, ya Kibabeli, ya Wamedi na Waajemi wakiwa wameungana, ya Kigiriki, ya Kirumi, na ya Waingereza na Waamerika wakiwa wameungana. Mnamo Majira ya Mataifa hayo yote Yehova Mungu hakujiingiliza katika mambo ya kibinadamu kwa kuusimamisha upya ufalme wa Kimasihi katika Yerusalemu uliojengwa upya duniani. Hiyo yaeleza kwa nini Mwanawe Yesu Kristo hakuipindua Milki ya Kirumi wala kusimamisha ufalme wa kidunia wa jamaa ya kifalme ya Daudi katika Yerusalemu wa kidunia. Kuliko hivyo, alikutabiri kuendelea kwa Majira ya Mataifa mpaka wakati wa Mungu wa kukoma kwayo. Mahali pa kujiketisha katika kiti cha enzi cha Daudi katika Yerusalemu, yeye alikufa bila ya hatia kama Mrithi wa kifalme wa Mfalme Daudi, siku ya tatu akafufuliwa kutoka kifo chake kisicho na hatia, na kupaa kufuata hapo mbinguni akaketi mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Baba yake wa kimbinguni.​—Matendo 2:32-36.

6. Ni wapi na wakati gani kusimamishwa upya kwa ufalme wa Kimasihi kulipotukia, na je! hili ndilo jambo lililoianzisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

6 Juu huko Mwana wa Mungu Yesu Masihi aliendelea kungoja mpaka mwisho wa Majira ya Mataifa. (Ebr. 10:12, 13) Vivyo hivyo, Yehova Mungu alijizuia mpaka wakati huo. Lakini katika mwaka wa 1914, au miaka 2,520 tangu kuachwa ukiwa kwa Yerusalemu na Yuda na Wababeli, Mtawala Aliye Mkuu Zaidi wa ulimwengu wote alichukua tendo lililofaa. Aliusimamisha upya ufalme wa Kimasihi wa Daudi, wakati huu mikononi mwa Mrithi wa Daudi wa kimbinguni, Yesu Kristo. Mataifa yasiyo ya Kiyahudi duniani yasingeweza kujiingiliza katika hili. Wasingeweza tena kuikanyaga haki ya jamaa ya Mfalme Daudi ya uwezo wa Kifalme. “Nyakati zilizowekwa za mataifa yasiyo ya Kiyahudi” zilikuwa zimekwisha kumalizika. Tangu wakati huo na kuendelea, Mrithi wa Milele wa Daudi, Yesu Masihi, anatawala katika “Yerusalemu wa mbinguni.” (Ufu. 12:1-11) Kuzaliwa huko kwa kimbinguni kwa ufalme wa Kimasihi hakukuianzisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu duniani. Tayari, mbele ya kumalizika kwa Majira ya Mataifa katika mwaka wa 1914, mataifa yasiyo ya Kiyahudi yalikuwa yamekwisha kwenda vitani​—miezi miwili mapema. Walianza vita yao wenyewe katika dunia nzima, kwa ajili ya utawala wa ulimwengu. Wao hawakuujua mwisho wa Majira ya Mataifa.

7. Tangu wakati huo na kuendelea mataifa yametenda kwa maongozi ya nani?

7 Je! ni chini ya maongozi ya nani mataifa yasiyo ya Kiyahudi yalitenda wakali huo hata sasa? Bila shaka si chini ya maongozi yapitayo yale ya kibinadamu ya Yehova Mungu, wala Mungu hakuwa upande wo wote katika Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, kwa maana wao wote walikuwa wakipiga vita juu ya utawala wa ulimwengu kwa njia ya mwanadamu, siyo kwa ajili ya utawala wa ulimwengu kwa njia ya “Yerusalemu wa mbinguni” na Mfalme wake mpya, Yesu Masihi. Kwa busara, basi, mataifa yasiyo ya Kiyahudi yalikuwa yakitenda chini ya maongozi ya adui ya Yehova Mungu na Masihi wake Yesu. N’nani huyo Adui Mkuu wa Yehova Mungu mwenye uwezo upitao ule wa kibinadamu? Ndiye aliyeitwa na Yesu Kristo “mtawala wa ulimwengu huu,” na aliyeitwa na mtume wa Kikristo Paulo “mungu wa hii taratibu ya mambo.” Yeye ndiye Shetani Ibilisi.​—Yohana 12:31; 14:30; 2 Kor. 4:4, NW; Ufu. 12:7-13.

8. Ni watu gani wakuu waliomo katika shindano hili juu ya utawala wa ulimwengu, na ni ulizo gani tusiloweza kulikwepa kwa habari ya shindano hili?

8 Kwa kuwa hawayaendeshi mambo yao ya kisiasa upande wa Mungu kwa kuitoa enzi yao ya kidunia kwa ufalme wa Mungu wa Yerusalemu wa kimbinguni, mataifa yasiyo ya Kiyahudi yanaweza kujipata yenyewe upande mmoja tu, upande wa Adui Mkuu wa Mungu, Shetani Ibilisi. Ushindani juu ya utawala wa ulimwengu tangu mwaka wa 1914 unatia ndani si mataifa ya wanadamu peke yake. Unatia ndani zaidi Mungu Aliye Juu Zaidi Yehova na Shetani Ibilisi. Nani atakayetia fora kati ya washindani hawa wawili? ndilo ulizo. Nani atakayejipatia ushindi? Hakuwezi kukawako mashaka juu ya matokeo. Biblia Takatifu, Neno la Mungu lililo hakika, latangaza kwa matumaini kwamba Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Yehova, atajipatia ushindi wa kimungu. (Ufu. 16:16; 19:11 mpaka 20:3) Ulizo asiloweza ye yote kati yetu kuliepuka sasa ni, Je! mimi nataka kuwa na nani, Mshinde au Mshindi?

9. Ni kwa sababu gani watu wataendelea kuiona “huzuni kuu ya mataifa” na kushindwa kupata njia ya kutokea?

9 Ni wazi sana kwamba hakuna aliyeko upande wa adui za Mungu na wapinzani anayeweza kupata baraka Yake ya kimungu. Hii yaeleza kwa nini, tangu mwaka wa 1914, wanadamu wameishi katika “kizazi cha jeuri” nao wakaona “huzuni kuu ya mataifa,” sawa na alivyotabiri Yesu Kristo. (Luka 21:25, 26, NW) Maadamu watu wanashindwa kusimama upande wa Yehova Mungu na Masihi wake katika ushindani huu wa ulimwengu wote, hawatapata njia ya kutoka katika mashaka yao wala ya ‘kutazamiwa kwa hofu kwa mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.’

10. Kwa sababu gani wanadamu wote sasa wamo katika hatari kuu, na ni akina nani peke yao wawezao kutumainia kufurahia baraka nyuma ya Ushindi wa kimungu?

10 Kama vile ambavyo “dhiki kubwa” ilivyokuwako mbele ya taifa lililokataa kumkubali Mwana wa Mungu Yesu Masihi katika mwaka wa 33 C.E., ndivyo na “dhiki kubwa,” isiyo na kifani katika historia ya kibinadamu, inavyongoja mbele ya wanadamu wote waliokwisha kutaabika tayari. Yesu Kristo alipokuwa duniani alitoa onyo la kufaa juu yake karne kumi na tisa zilizopita, naye akayatabiri matukio ya ulimwengu ambayo yangeitangulia. (Mt. 24:3-22; Ufu. 6:1 mpaka 7:14) Ulimwengu wote wa wanadamu sasa wasimama hatarini. Wahitaji kulipata onyo linaloendelea kutangazwa kwake bila ya kukatizwa. Wokovu wa “dhiki kubwa” inayokaribia sana waweza kutumainiwa na wale tu wanaolitii onyo lake lililoongozwa na roho ya Mungu.

11. Mashahidi wa Yehova wa Kikristo waliamua kuendelea kutangaza nini, na kwa akina nani?

11 KWA HIYO, NA IAZIMIWE kwamba, sisi, kama mashahidi wa Yehova wa Kikristo, tutaendelea kuiweka imani yetu katika Ushindi wa Kimungu. Tutaendelea bila ya kuchoka kulitangaza onyo kutoka katika Neno la Mungu lililoandikwa kwa wapenda serikali ya haki wote waliopotoshwa na Adui Mkuu wa Mungu, Shetani Ibilisi, na ambao kwa njia hiyo wameyaweka matumaini yao katika taratibu za utawala zilizoundwa na mwanadamu, kwa huzuni yao nyingi na taabu. Tutaendelea kuutangaza ufalme wa Mungu wa Kimasihi wa miaka 1,000 kama dawa ya kuponya maumivu yote, kwa ajili ya wanadamu waliotaabika.

12. (a) Ni njia gani za elimu na za kuenezea habari njema walizoazimia kutumia? (b) Wao waliazimia kusonga mbele na kuwasimulia wanadamu baraka gani na furaha za ufalme wa Mungu wa Kimasihi?

12 Tukiufuata mfano wa mitume, tutahubiri waziwazi kutoka nyumba kwa nyumba na kufundisha kwa faragha katika nyumba za watu wenye kupendezwa kwa njia ya mafunzo ya Biblia ya kila juma. Tutavitumia vitabu na kinywa vile vile, ndiyo, njia zote zinazokubaliwa na Mungu za kuenezea habari njema kote kote. Kwa uaminifu tutasonga mbele katika kuwaambia wanadamu waliohatirishwa juu ya baraka na furaha inayokuja ya ufalme wa Mungu wa Kimasihi​—juu ya serikali isiyopotoshwa na ya haki, juu ya kurudishwa kwa wanadamu kwenye afya kamili katika miili yao, juu ya ufufuo wa wafu wote waliokombolewa utakaofanya rafiki wapenzi na jamaa kuungana tena, juu ya amani ya milele na kutoshelezwa kwa mahitaji yote ya wanadamu katika Paradiso iliyosimamishwa katika dunia iliyosafishwa, juu ya uhuru wa hofu, hatari na utawala mbaya wa Shetani Ibilisi na mawakili wake wa kidunia, juu ya upendo wa kidugu kati ya jamaa nzima ya kibinadamu, na juu ya dini iliyo moja ya kweli, ibada safi ya Mungu Muumba wetu kupitia kwa Yesu Kristo Mwanawe. Ndiyo, tutaendelea kuusimulia ushindi ambao Mungu Mwenye Nguvu Zote ataupata juu ya adui ya wanadamu anayehofiwa, Kifo, na namna ambavyo atawabariki raia zake wote walio waaminifu na uzima wa milele katika ujamaa uliobarikiwa pamoja na Yeye kama Baba yao wa kimbinguni.

13. Kwa sababu ya wakati, ni amri gani waliyoazimia kuitimiliza hata mwisho, nao watategemea msaada gani kulitimiza azimio hili?

13 Kwa kuwa sasa twaona waziwazi zaidi kupita wakati mwingine wo wote kwamba ufalme wa Mungu wa miaka 1,000 umekaribia na kwamba wakati unazidi kuwa mchache zaidi na zaidi kwa wanadamu waliotaabika kujifaidi na habari njema za wokovu, tutauonyesha upendo mwaminifu kwa Mungu na vile vile upendo kwa mwanadamu mwenzetu. Kwa njia hii tutamtii Mungu kuliko mwanadamu nasi hatutalegea katika kuitimiliza amri yake kupitia kwa Kristo ya ‘kuzihubiri habari njema hizi za Ufalme katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote,’ mbele ya mwisho wa hii taratibu ya mambo iliyohukumiwa kuja. (Mt. 24:14, NW; Marko 13:10) Twamtegemea Mungu atusaidie kulitimiza azimio hili. Na atupate Yeye tukiwa waaminifu hata mwisho na kutuhesabia kustahili kushiriki furaha na baraka zinazotokana na Ushindi wake wa Kimungu!

14. Nini kilichofanywa na Tangazo na Azimio lililotangulia penye “Ushindi wa Kimungu” makusanyiko ya mataifa yote, na ni kitabu gani kilichotolewa mara tu kufuata hapo, katika lugha gani?

14 Tangazo na Azimio lililotangulia lilitolewa kwa “Ushindi wa Kimungu” Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova wa Kikristo ilipokwisha kutolewa hotuba iliyopangwa iliyounganisha habari za makala mbili zilizotangulia za Mnara wa Mlinzi juu ya “Kupata Utajiri kwa Ajili ya Mfalme Mpya wa Dunia” na “Waokolewa Wasichinjwe Pamoja na Adui za Mfalme.” Kusanyiko lilipolikubali Tangazo na Azimio kwa nafsi yote na kwa moyo wa bidii, kitabu kipya, chenye ngozi ngumu na chenye kurasa 416 kiitwacho “God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached” kilitolewa. Katika nchi wanakozungumza Kijeremani, vile vile kilitolewa katika lugha ya Kijeremani. Kitabu hiki kipya cha kusaidia kujifunza Biblia, kinachopatikana sasa kwa Kiingereza na Kijeremani peke yake, kinakuwa msaada mkubwa sana na wenye kusisimua kwa wale waliolihudhuria “Ushindi wa Kimungu” Kusanyiko katika kulitimiliza Tangazo na Azimio ambalo walilikubali kwa umoja.

15. Kufikia tarehe ya toleo hili (toleo la Kiingereza la Desemba 1, 1973) la Mnara wa Mlinzi ni makusanyiko mangapi yaliyofanywa, katika nchi ngapi, yakiwa na hudhurio gani la jumla?

15 Mpaka tarehe ya toleo hili la Mnara wa Mlinzi (toleo la Kiingereza), Makusanyiko ya namna hiyo 43 ya “Ushindi wa Kimungu” yamefanywa katika nchi 20 yakiwa na hudhurio la jumla ya watu 1,447,235.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki