Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 6/15 uku. 288
  • Yehova Afungua Mioyo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Afungua Mioyo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Kabla na Baada ya Kujifunza Biblia—Neno la Mungu Lina Matokeo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Mipango ya Mahali pa Ibada
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Je! Wewe Unastahi Jumba la Ufalme Lenu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Umaridadi Wenye Kuvutia wa Opali
    Amkeni!—1993
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 6/15 uku. 288

Yehova Afungua Mioyo

NYAKATI nyingine hali zifanyazo watu waupate ujumbe wa Biblia ni za ajabu sana nazo zaonyesha kwamba Yehova Mungu anafungua mioyo ili isikilize kweli.​—Matendo 16:14.

Mmoja wa mashahidi wa Yehova, mhudumu painia wa pekee anayetumikia Australia, atoa habari hii:

“Tulipokuwa ndiyo tunafika kwanza Coonamble, tulipata habari za kijana mwanamume aliyependezwa na Neno la Mungu. Jina lake lilikuwa Tony naye aliishi katika hema yenye kuegemea jengo jingine katika Lightning Ridge, umbali wa maili 120. Tukadhani tusingekuwa na shida yo yote kumpata, mpaka tulipouona Lightning Ridge! Kuna hema yenye kuegemea jengo jingine chini ya karibu kila mti. Tukaendesha gari hapa na pale kwa muda na mwishowe tukakaza macho yetu kwenye hema moja. Tulipokaribia, kijana mwanamume akatoka nje. Tukamwambia tulikuwa tunatafuta kijana mwanamume aliyekuwa akipendezwa na kujifunza Biblia pamoja nasi. Alisisimka sana akasema ndiye.

“Kijana mwanamume huyu alipata kitabu kidogo alipokuwa anatembea kupitia kibonde cha kijito kikavu katika Annarke akitafuta johari, kitabu ambacho jalada yake ilikuwa imevimba sana hata alipokiokota, jalada yenyewe ilianguka. Alikisoma kitabu hicho mara mbili, akakitafsiri katika Kislovenia akatuma tafsiri yake kwa wazazi wake Ulaya. Kilikuwa ndicho kitabu Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele.

“Kwa miezi miwili tulimtembelea Tony kila usiku wa Jumatatu tukajifunza kitabu Kweli kwa kutumia mwanga wa mshumaa. Kisha akaamua kuacha kuchimbua vito akaja Coonamble na kuishi pamoja nasi katika Jumba la Ufalme. Mbali na kujifunza kwa kipekee, alifanya kazi katika jumba, akilisafisha na kulitengeneza. Na, kwa kuwa alikuwa fundi wa umeme, alitia taa zote katika Jumba la Ufalme.

“Mwishowe akabatizwa katika kijito nyuma ya jumba letu, baada ya kulazimika kuchimba shimo kubwa lenye kina kirefu kutosha aingie, kwa maana mto ulikuwa karibu umekauka.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki