Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 5/15 kur. 230-237
  • Kukusanywa kwa Wenye Kuchukua Nafasi Zilizo Wazi Karamuni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukusanywa kwa Wenye Kuchukua Nafasi Zilizo Wazi Karamuni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MTU ASIYE NA “VAZI LA ARUSI”
  • WENGI WAALIKWA, WACHACHE WACHAGULIWA
  • WANAWALI WA MFANO WA KUMTUMIKIA BIBI-ARUSI
  • Kielezi cha Karamu ya Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kielezi cha Karamu ya Ndoa
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Karamu ya Arusi ya Mfalme Katika Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mfalme Awaita Wale Walioalikwa Kwenye Karamu ya Ndoa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 5/15 kur. 230-237

Kukusanywa kwa Wenye Kuchukua Nafasi Zilizo Wazi Karamuni

1. (a) “Walioalikwa” kuja kwenye karamu ya arusi walionyeshaje kwamba “hawakustahili”? (b) Ingalimaanisha nini kwao kuacha mapendezi yao ya kichoyo?

KWA sababu gani “wauaji” wapinga Ukristo waliuawa penye uharibifu wa wa mji wao mtakatifu, Yerusalemu, na taifa lao la Kiyahudi likavunjwa mwaka wa 70 C.E.? Ilikuwa kwa sababu wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi “hawakustahili” kama vile mfalme katika mfano wa Yesu alivyosema. (Mt. 22:8) Wayahudi walikuwa wamehakikisha hili kwa kukataa kwao kwa matusi, dharau, kutoaminika na mara nyingi kwa jeuri kutenda kulingana na mwaliko wa Mfalme wa kimbinguni baada ya taarifa ya pili iliyotoka Kwake. Kuacha kwao mapendezi yao ya kichoyo ya vitu vya kimwili na kuja kwenye “karamu ya arusi” ya kiroho kungalimaanisha nini? Kungalimaanisha kutubu, si kwa sababu tu ya kupungukiwa kwao katika kushika agano la Torati la Musa, bali pia kwa sababu ya kumkataa kwa jeuri Masihi aliyetoka kwa Mungu halafu kukataa kubatizwa katika maji kama wanafunzi wa Yesu akiwa Masihi wao. Lakini wao walikuwa wenye kiburi mno, walikuwa wenye kujitakia haki yao wenyewe kupita kiasi, walikuwa wenye shughuli nyingi mno za mipango yao wenyewe, na kupinga sana kutimiza matakwa hayo. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa taifa la Israeli kwa ujumla.

2. (a) Kwa sababu gani nafasi zote za karamu ya arusi hazikuachwa bila kukaliwa katika kikomo cha taarifa ya pili? (b) Ni nafasi ngapi Mfalme alizokusudia kuzijaza na ‘wanaostahili’?

2 Je! hii yamaanisha kwamba nafasi zote penye “karamu ya arusi” ziliachwa bila kukaliwa? Sivyo, si zote! Maandishi ya Biblia yaonyesha kwamba Wayahudi wengine “walioalikwa” waliitikia baada ya taarifa ya kwanza na hata Wayahudi zaidi na waongofu waliotahiriwa wa Kiyahudi baada ya taarifa ya pili kuanza siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 C.E. Lakini hawa walikuwa wachache kweli kwa kulinganishwa na viti vingi vilivyokuwamo katika chumba cha karamu ya arusi. Mfalme alikusudia kujaza nafasi ngapi? Kwa kuwa wale waliokaa katika sehemu za kuegemea “mezani” kwa kustahili waliwafananisha wale wanaokuwa warithi wenzi wa Mwana wa Mfalme katika “ufalme wa mbinguni,” Mfalme wa kimbinguni Yehova alikusudia kujaza nafasi 144,000 ili kujaza “chumba cha sherehe za arusi” na ‘wanaostahili.’ Analoonyesha Yesu Kristo katika kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo, lahakikisha hivyo. (Ufu. 7:4-8; 14:1-3; 20:4-6) Hesabu hiyo yamaanisha nafasi nyingi penye kijio cha arusi.

3, 4. (a) Kulingana na mfano wa Yesu, nafasi 144,000 zilikuwa zimetolewa zijazwe na nani wakiwa peke yao? (b) Je! walikuwa wengi kutosha kujaza nafasi nyingi hizo?

3 Kulingana na mfano wa Yesu, Yehova Mfalme aliiacha wazi nafasi ya taifa zima la Israeli katika agano la Torati kuzijaza nafasi zote hizo 144,000. Wao walikuwa ndio “uzao” wa asili wa kimwili wa Ibrahimu ambaye Mungu alikuwa amefanya agano lake naye la kubariki jamaa zote za dunia kwa “uzao” huo. (Mwa. 12:3; 22:17, 18) Agano la Torati ambamo Mungu alikuwa amewaingiza kupitia kwa Musa liliwatia katika ukoo wa kuwa “ufalme wa makuhani” ambao Mungu alikusudia kusimamisha chini ya Masihi, Mpatanishi aliye mkuu kuliko Musa. Wao peke yao ndio waliokuwa wale “walioalikwa” kwenye karamu ya arusi ya kiroho.

4 Taifa lao zima lingaliweza kutokeza Wayahudi wa asili 144,000 wajaze nafasi nyingi zilizokuwako. Akiba ya Wayahudi ya kutolewa watu waliotakiwa ilikuwa kubwa vya kutosha, bila shaka, ikiwa na mamilioni mengi. Kwani, kulingana na Yosefo, walikuwako Wayahudi 1,197,000 penye mwadhimisho wa Kupitwa katika Yerusalemu mwaka wa 70 C.E. Na si Wayahudi wote waliotawanyika-tawanyika katika dunia ya wakati huo iliyokaliwa na watu waliokuwako siku ya Kupitwa.

5. (a) Wale wa “uzao” wa asili na wa kimwili wa Ibrahimu waliouitikia mwaliko walihesabiwa na Paulo kuwa nini? (b) Hata hivyo, kulikuwa na nafasi nyingi kama zilizokuwako kwanza?

5 Hivyo walikuwako wengi, 144,000 wote, walioalikwa kati ya “uzao” wa asili wa kimwili wa Ibrahimu. Lakini maandishi ya Biblia yaonyesha kwamba ni wachache tu wa uzao wa asili wa Ibrahimu waliotenda kulingana na mwaliko wao uliotegemea agano la Torati. Karibu na mwaka wa 56 C.E., Myahudi aliyefanywa Mkristo, mtume Paulo, alikadiri hesabu ya Wayahudi waliochaguliwa kuwa “mabaki” tu ya taifa la Israeli. (Rum. 9:27-29; 11:5) Hata hivyo, kuwapo kwa “mabaki” haya ya Kiyahudi katika “chumba cha sherehe za arusi” kuliacha nafasi chache zaidi kuliko wale wengi, hesabu kamili ya 144,000 waliokuwako wakati taarifa ya kwanza ilipoanza katika mwaka wa 29 C.E.

6. Katika mfano wa Yesu, ni kwa njia gani mfalme hakuacha kusudi lake lenye ukarimu lishindwe na apatwe na aibu?

6 Kulingana na mfano wa Yesu, wakati ulikuwa ukimwishia mfalme kwa habari ya karamu yake ya arusi ambayo sasa ilikuwa tayari. Kwa sababu ya kukataliwa na wengi sana walioalikwa, mfalme angekijazaje chumba cha karamu na wageni kwa heshima iufaayo wakati huo? Ingekuwa aibu kwake wakionekana wachache katika chumba hiki, kushindwa kwa kusudi lake lenye fadhili. Lakini mfalme hakupaswa ashindwe. Ikiwa walioalikwa kwanza hawakumheshimu yeye kwa kuhudhuria, basi angejaza nafasi zao zilizo wazi na watu wengine! Muda mfupi tu kabla ya uharibifu wa “mji” wa “wauaji” hao, mfalme aliwatuma watumwa wake kwenye maeneo yaliyokuwa nje ya mji huo, nje ya mtaa huo, “kwenye njia za kuondokea mjini.” Huko “watumwa” wa mfalme wangewaleta wengine wa kujazia, ndiyo, “ye yote” waliyemwona.

7. Ni nini kionyeshacho kama watumwa wa mfalme walikusanya wenye kujaza nafasi zilizokataliwa kwa namna ile ile ya mwaliko wa kwanza?

7 Watu hawa wasiojulikana, lakini si wasiojulikana wanakoishi, wangeweza kusihiwa na watumwa kuchukua nafasi moja penye karamu ya arusi. Huu uliitwa mwaliko, kwa maana wale ambao sasa walikusanywa hawakuchukua hatua ya kwanza na kujidukiza katika sherehe za arusi. Wale ambao sasa walikusanywa wachukue nafasi ya wale wengine hawakualikwa kwa njia ambayo wale wa kwanza walikuwa wamealikwa. Katika mfano unaolingana na huu uliotolewa na Yesu, katika Luka 14:15-24, mwito wa tatu na wa mwisho unapotolewa, mwenye nyumba aandaye “karamu kubwa” amwambia mtumwa wake: “Toka nje [yaani, nje ya mji] uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa. Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu.”​—Luka 14:23, 24.

8. Hawa waliokusanywa sasa walikuwa akina nani, na ni wakati gani na kwa njia gani hawa walianza kukusanywa?

8 Kazi hii ya kukusanya wageni wa kutosha kutoka “barabarani” nje ya “mji” wa walioalikwa ilianza katika vuli ya mwaka wa 36 C.E., si 70 C.E., miaka saba, au “juma ya miaka,” baada ya ubatizo na kutiwa mafuta kwa Yesu, Mwana wa Mfalme wa kimbinguni. (Dan. 9:2427) Mtumwa wa kwanza kutumwa alikuwa Myahudi aliyefanywa Mkristo, mtume Petro. Alitumwa Kaisaria, mji mkuu wa jimbo la gavana wa Kirumi Pontio Pilato, na huko akahubiri Mataifa wasiotahiriwa, wasio Wayahudi. Mungu alimimina roho takatifu juu ya akida Mwitaliano mwenye kusikiliza, Kornelio, na rafiki zake wenye kuamini, halafu mtume Petro akawabatiza. (Matendo 10:1 mpaka 11:18) Tangu wakati huo na kuendelea kukusanywa huku kwa watu wasio Wayahudi na wasiotahiriwa kumeendelea hata katika karne hii ya 20. Wote hawa wametiwa katika nafasi za wale waliokataa.

9. (a) Paulo afananisha Ibrahimu na wazao wake wa asili na wa kimwili na nini? (b) Kwa sababu gani “matawi” yalikatwa, na nafasi yao ilichukuliwaje na mengine?

9 Kulingana na mfano uliotolewa na mtume Paulo katika Warumi, sura ya kumi na moja, Wayahudi wa asili walio chini ya agano la Torati walikuwa kama matawi ya asili katika mzeituni. Mti huu una matawi machache. Walikuwa ndio wazao wa asili wa rafiki ya Mungu Ibrahimu na, wakiwa hivyo, walikuwa warithi wa asili wa ahadi ya agano la Mungu kwa Ibrahimu. Ibrahimu mzee wa ukoo alikuwa ndiye shina la mzeituni huu wa mfano, mizizi yake ikiwa imeimarishwa sana katika ahadi hiyo ya agano la Mungu. Lakini alichotaka Mungu kilikuwa “uzao” wa kiroho wa Ibrahimu, Israeli wa kiroho. Kwa hiyo, Wayahudi wa asili walioalikwa kuwa “ufalme wa makuhani” walipokataa kuyatimiza matakwa ya hili, walikatwa kutoka mzeituni wa mfano; hawakufanywa warithi wa “ufalme wa mbinguni.” Nafasi yao ilipaswa ichukuliwe na watu wengine, ili mzeituni wa mfano upate kuwa wenye matawi kamili. Ili kutimiza jambo hili la haraka, kwa rehema Mungu alipandikiza katika mahali pao Mataifa wenye kuamini, kama matawi kutoka kwa mzeituni-mwitu. Hivyo Mungu apata Israeli wake kamili wa kiroho, “uzao” wa kiroho wa Ibrahimu.

MTU ASIYE NA “VAZI LA ARUSI”

10. Wakati unakaribia wa sehemu gani ya mfano kutimizwa, na kwa sababu gani?

10 Sasa, basi, baada ya kazi yote ya kukusanya ya karne kumi na nane zilizopita, wamepaswa wawe wachache zaidi sana ambao nafasi zao zahitajiwa kujazwa na wengine katika kame hii ya 20. Kwa hiyo si wengi ambao wangekusanywa. Sasa tangu mwisho wa Majira ya Mataifa katika mwaka wa 1914 na mwanzo wa “wakati wa mwisho,” bila shaka wakati umetufikia ambapo “chumba cha sherehe za arusi” cha Mfalme kimepaswa kijazwe. Katika mfano wa Yesu habari hiyo inafikiwa, naye anaendelea kusema hivi: “Mfalme alipoingia awakague wageni [wenye kuegemea] humo alimwona mtu asiyevaa vazi la arusi. Kwa hiyo akamwambia, ‘Bwana, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Aliduwaa.”​—Mt. 22:11, 12, NW.

11. Kwa sababu gani mtu asiye na vazi aliduwazwa na ulizo la mfalme?

11 Mfalme alikuwa ametoa vazi la arusi kwa kila mgeni alivae penye sherehe za arusi, na kwa hiyo hakukuwa na udhuru kwa mtu huyo asiye na vazi. Kwa kufaa aliduwazwa, akanyamazishwa. Katika mfano wake Yesu hasemi kwamba mtu huyo alilivaa ili aingie kisha akalivua. Bali, mtu huyo alilikataa vazi wakati mtumishi wa mfalme alipompa au kumwonyesha chumba cha mavazi cha mfalme kwa wageni. Mfalme hakumwuliza, ‘Sababu gani ukalivua vazi la arusi?’ bali, “Uliingiaje humu bila vazi la arusi?” Alikataa kulivaa. Alikataa kulivaa penye meza ya karamu. Yeye hakuyatimiza matakwa ya kuwa pale mezani, wala hakustahili kuwapo. Anafananisha nani leo?

12. Kwa ufupi, mtu asiye na vazi afananisha nani, na wafafanuzi wa Biblia wanasema vazi la arusi lilifananisha nini?

12 Anafananisha wale wanaojidai kuwa Wakristo wenye kumcha Mungu lakini wasiovaa kile kilichofananishwa na “vazi la arusi.” Kulingana na habari, mavazi hayo yaliyotolewa bure na mkaribishaji yalikuwa mavazi marefu ya kitani, hivi kwamba wageni wote kwa nje walivalia sawasawa, bila kujali kama mmoja hapo kwanza alikuwa Myahudi aliyealikwa au Mtaifa aliyechaguliwa. Kwa hiyo, wafafanuzi wengi wa Biblia wanautaja Ufunuo 19:7, 8, ambapo inasemwa hivi juu ya mke wa Mwana-Kondoo: “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.” Kwa hiyo inadaiwa kwamba “vazi la arusi” linafananisha haki anayohesabiwa Mkristo aliyebatizwa, kufaa kwake.

13. Kwa sababu gani ‘‘vazi la arusi” lafananisha mengi zaidi kuliko “kuhesabiwa haki”?

13 Walakini, vazi la arusi lazima limaanishe mengi zaidi kuliko kutangazwa kwa mtu kuwa mwenye haki na Mungu kwa imani ya mtu katika Kristo kama dhabihu ya ukombozi. (Rum. 5:1, 9) Kufaa huko au kutangazwa kuwa mwenye haki sasa sicho kikomo; hakusimami peke yake sasa. Kusudi lake sasa ni kwamba mwenye kuhesabiwa haki amepaswa achaguliwe na Mungu Mwenye Kuhesabia Haki kama mwanawe wa kiroho na kuwa mshiriki wa “uzao” wa kiroho wa Ibrahimu na hivyo mshiriki wa Israeli wa kiroho. Akiwa hivyo, mwana huyu wa kulelewa wa Mungu anaingizwa katika agano jipya lililopatanishwa na Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. (Gal. 4:4-7; Rum. 8:16, 17; Luka 22:19, 20) Kwa hiyo, “vazi la arusi” lafananisha yote hayo kwa mgeni aliyetubu na kubatizwa penye karamu. Kwa hiyo ni kitambulisho cha mtu kama Mwisraeli wa kiroho, mmoja wa “uzao” wa Ibrahimu.

14. Kwa hiyo, basi, mtu asiye na vazi alifananisha nani?

14 Kwa kuwa mtu wa pekee ambaye mfalme alimgundua hakuwa amevaa vazi la arusi lililokuwapo, aliifananisha jamii ya wasiotumia imani na kuchukua hatua ifaayo kupatana na imani yao ili kutangazwa kuwa mwenye haki na Mungu na kulelewa kama mwanawe wa kiroho na kuingizwa katika agano jipya lililofanywa na Israeli wa kiroho kupitia kwa Kristo. Hafananishi Wakristo ambao wametiwa mafuta kwa roho ya Mungu na kufanywa warithi washirika na Kristo lakini wanaokuwa wasioaminika kwa Mungu na kupoteza ufalme wa kimbinguni. Bali, anafananisha Wakristo wa madanganyo, ambao wanafanyiza Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) leo na wanaojidai na kujifanya kuwa penye ‘meza’ ya karamu ya arusi. Mungu Mfalme hakuwatambua hata kidogo kama wenye kitambulisho kifaacho, na kwa hiyo hakuwatia mafuta kwa roho takatifu kama warithi wa Ufalme.

15, 16. (a) Lazima wakati uje wa Mfalme kufanya nini juu ya jamii isiyo na vazi? (b) Ni wakati gani Mfalme angeingia awakague wageni?

15 Lazima wakati uje ambapo Mungu ataufunua uongo wa dai hilo na kujifanya huko kwa Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) kuwapo penye ‘meza’ ya karamu ya arusi na kufikiliza hukumu kali juu yake mbele ya watazamaji wote. Mungu Mfalme anafanya hivyo wakati yeye ‘anapoingia kuwakagua wageni’ kama Mpangaji wa karamu ya arusi ya Mwanawe. Kulingana na mfano wa Yesu, lazima hili litukie wakati “chumba cha sherehe za arusi” ‘kitakapojazwa.’ (Mt. 22:10, 11, NW) Chumba hiki kikiisha kujazwa na wageni wa kutosha kazi ya kukusanya ya watumwa wa mfalme ingekoma. Kwa kuwa kukusanywa kwa ‘watakaoteuliwa’ kunafanywa chini ya uongozi usioonekana wa malaika za Mungu, Mfalme wa kimbinguni angeingia na kukagua wakati kazi iliyotabiriwa na Yesu imetimizwa mwishoni mwa taratibu ya mambo:

16 “Ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.”​—⁠Mt. 24:30, 31.

17, 18. (a) Kumalizika kwa kazi hiyo ya kukusanya kungekuwa wakati wa kuamua nini kwa habari ya jamii isiyo na vazi? (b) Mfano wa Yesu waonyeshaje litakalotendwa kwa jamii hiyo?

17 Kumalizwa kwa kukusanywa huku kwa “wateule” kungetukia muda mfupi kabla ya “dhiki kubwa” ambayo Yesu aliilinganisha na gharika ya siku za Nuhu kuanza. (Mt. 24:21, 22, 37-41) Kwa hiyo, wakati huo wa ukaguzi wa Mfalme wa kimbinguni, je! jamii iliyofananishwa na mtu asiye na vazi la arusi ingehesabiwa kati ya “wateule”? Au jamii hii ingeachwa ishiriki na “mataifa yote ya ulimwengu” wanaoomboleza kwa sababu ya uharibifu unaokuja? Jamii inayofanyiza Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) haina udhuru wa kutoa kwa Mfalme kwa sababu ya kujaribu kuwapo penye “karamu ya arusi” bila vazi la mfano. Jamii hiyo haiwezi kutoa sababu yo yote ya kuruhusiwa ifurahie “sherehe za arusi” na “karamu.” Wakati wa ukaguzi wa mwisho, jamii hiyo inapatikana ‘imeduwaa.’ Mfalme ataitendeaje jamii hiyo? Mfano wa Yesu waonyesha:

18 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu na kumtupa nje gizani. Huko ndiko kutakakokuwa kulia kwake na kusaga meno yake.’”​Mt. 22:13, NW.

19. Jamii hiyo itatupwa nje kwenye nini, nayo itakosa kufurahia nini?

19 Kwa hiyo jamii hii inafungwa kabisa isiweze kutoa upinzani. Inatupwa hivyo “nje gizani,” nje ambako giza halipunguzwi na mambo kama vile taa za barabarani. Huko, bila ya kuwa na mwangaza wa aina yo yote kutoka kwa Mungu, jamii hiyo italia na kusaga meno yake, katika “dhiki kubwa” ambamo Babeli Mkuu wa kidini na sehemu yote nyingine ya taratibu hii ya mambo itaharibiwa. (Ufu. 17:14-18) Jamii hiyo itaondolewa katika “ufalme wa mbinguni” nayo haitaishiriki “karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo” katika mbingu juu.​—Ufu. 19:9.

WENGI WAALIKWA, WACHACHE WACHAGULIWA

20. Yesu alimalizia mfano wake kwa maneno gani, na je! haya yalimmaanisha mtu asiye na vazi?

20 Ili kumalizia mfano na kuonyesha maana yake, Yesu alisema hivi: “Kwa maana kuna wengi walioalikwa, lakini wachache waliochaguliwa.” (Mt. 22:14, NW) Yesu hakuwa akiyasema maneno hayo kwa kummaanisha mtu aliyefukuzwa asiye na vazi la arusi lililohitajiwa.a Mtu huyu hakuwa aliyehusika zaidi sana katika mfano. Bila shaka mtu huyu hakuwafananisha waliobaki kati ya wale “wengi” walioalikwa baada ya wale “wachache” kuondolewa. Kwa hiyo, “wageni” wanaovaa vazi la arusi hawawafananishi “wachache” waliokuwa wamechaguliwa kutoka taifa la Kiyahudi baada ya idadi iliyo kubwa ya Wayahudi wote “walioalikwa” kujipa udhuru. Basi, je! Yesu alimaanisha nani kwa kusema “wengi” waliokuwa wamealikwa, na alimaanisha nani kwa kusema “wachache” waliochaguliwa?

21. Basi, wachache waliochaguliwa walikuwa nani, na je! wao walifanyiza “wageni” wote waegemeao penye “karamu ya arusi”?

21 “Wengi” walioalikwa walikuwa taifa la Kiyahudi lililokuwamo katika agano la Torati lililowasaidia Wayahudi wawe “ufalme wa makuhani” kwa Mungu. “Wachache” waliochaguliwa kama wenye kuustahili “ufalme wa mbinguni” walikuwa ndiyo “mabaki” ya Wayahudi wa asili waliotenda kupatana na taarifa ya Mfalme wa kimbinguni. Wayahudi hao waliacha shughuli za ulimwengu nyuma, wakaingia katika “chumba cha sherehe za arusi” na kulikubali “vazi la arusi” kutoka kwa Mfalme, wakalivaa kisha wakaegemea “mezani.” Kwa sababu ni (Wayahudi) “wachache” tu waliotenda kupatana na taarifa iliyotoka kwa Mungu Mfalme kufikia mwaka wa 36 C.E., aliona ni lazima kutuma “watumwa” wake nje ya “mji” wa Kiyahudi au mtaa wakiwa na maagizo kuleta watu wengine wa Mataifa wasiotahiriwa kujaza nafasi za waliokataa. Mwishowe wageni wanajaa chumbani. Kwa hiyo “wachache” waliofanyiza mabaki ya Kiyahudi walikuwa sehemu tu ya “wageni” karamuni.

22. (a) Mungu Mfalme alionyeshaje kuchagua kwake “wageni” waliovaa mavazi? (b) Mfano wa Yesu ulikusudiwa kuonyesha nini kwa habari ya Mfalme kuwa na karamu ya arusi?

22 Kwa hiyo, “wageni” wote waliovaa vazi la arusi wanafananisha watu zaidi kuliko “mabaki” tu ya Wayahudi ambao wakawa Waisraeli wa kiroho. “Wageni” wanatia na Mataifa wote waaminifu waliochukua nafasi za waliokataa. Wakati wake Mungu alionyesha kuchagua kwake “wageni” hawa wote waliovaa mavazi kwa kuwatia mafuta kwa roho takatifu yake kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo. Hakuna po pote ambapo mfano wa Yesu unafananisha kwamba idadi isiyojulikana ya Wakristo waliotiwa mafuta wangekuwa wasioaminika na kuonyesha hawaustahili “ufalme wa mbinguni” wala haukukusudiwa kufananisha hivyo. Mfano wa Yesu ulikusudiwa kuonyesha kwamba Mfalme wa kimbinguni angefaulu kuwa na “karamu ya arusi” yenye wahudhuriaji wa kutosha yajapokuwa magumu. Angekuwa na “karamu ya arusi” yenye mafanikio kwa utimizo na kusudi lake lenye fadhili.

23. Je! Mfalme Yehova aliagiza “watumwa” wake walete “wageni” waliotazamiwa wengi kupita kiasi, au yeye alifanya mambo kwa njia gani?

23 Wakati wote Mfalme Yehova alijua ni nafasi ngapi za kuegemea ambazo angekuwa nazo penye ‘meza’ ya karamu. Kwa hiyo asingewaagiza “watumwa” wake walete “wageni” waliotazamiwa wengi kupita kiasi. Angewaagiza watumwa wake walete idadi iliyohitajiwa kujaza nafasi zote zilizokuwapo. Katika wakati wake aliwaagiza “watumwa” wake walete mabaki kutoka kwa Wayahudi waliokuwa wamealikwa kwanza. Kisha akaagiza mataifa yote yasiyo ya Kiyahudi wasiotahiriwa waje kujaza nafasi zilizohitajiwa. Kidogo kidogo nafasi zote ‘zingejazwa.’

24. (a) Mfano wa Yesu hauonyeshi nini kwa habari ya kutupwa nje kwa mtu huyo? (b) Katika utimizo, kwa sababu gani hakuna haja ya kuleta watu wengine wajaze nafasi zilizokataliwa na jamii hiyo isiyo na vazi?

24 Pana jambo moja lisiloonyeshwa na mfano wa Yesu. Gani? Kwamba, baada ya yule mtu asiye na vazi la arusi kutupwa nje, mfalme angetuma mtumwa mmoja kumleta mtu mwingine badala yake. Bila shaka mfalme asingetuma mtumwa usiku, “nje gizani,” kutafuta mtu mwingine badala ya aliyetupwa nje. Ni mtu gani angekuwa “barabarani” nje ya mji saa hiyo ya usiku? Mfalme anawakubali wageni wa arusi waliovaa mavazi (wenye kuegemea), halafu karamu yaendelea hawa wakiwapo na bila ya mtu asiye na vazi aliyetupwa nje. Katika utimizo wa sehemu ya mwisho ya mfano wa Yesu leo, hakuna haja ya kumweka mtu mwingine badala ya Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) na kundi lake la kidini. Wao walijaribu kuingia tu penye meza ya karamu bila kutimiza matakwa ya kimungu. Kujifanya kwao kuwapo hakufai kitu.

25. (a) Kwa hiyo, ni nani anayetoa mwito au mwaliko, na kwa njia gani? (b) Uchaguzi waonyeshwaje, na ni nini kinachotakiwa kwa wale waliochaguliwa?

25 Yehova Mfalme ndiye anayetoa mwito au mwaliko. Kama vile katika habari ya Kornelio, mwongofu wa kwanza wa Mataifa kwenye Ukristo, kwanza Mungu asoma moyo wa mtu anayemfikiria. Kisha, kwa sababu ya hali nzuri ya moyo, Mungu atuma msaada unaohitajiwa kwa mwenye kuitikia. Hivyo huyu anapata maagizo ya Biblia juu ya tumaini la ufalme wa kimbinguni. Kwa hiyo, si mamia yote ya mamilioni wanaohubiriwa “habari njema ya ufalme” wanaopata mwaliko wa Mungu wahudhurie katika “karamu ya arusi” ya kiroho. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Idadi kubwa wanapokea tu “ushuhuda” juu ya Ufalme. Wale “walioalikwa” kweli, wanaotimiza matakwa ya Mungu, ndipo ‘wanapochaguliwa’ anapowatia mafuta kwa roho takatifu wakawe warithi washirika na Yesu Kristo. (2 Kor. 1:21; 1 Yohana 2:20, 27) Kwa sababu sasa wamechaguliwa hivyo, lazima wawe waaminifu hata mwisho,​—Ufu. 17:14; 2:10.

26. “Wageni” waliochaguliwa ambao wangali duniani wanafurahia nini sasa, na waaminifu watafurahia nini baada ya “dhiki kubwa”?

26 Leo ulimwengu mzima wa wanadamu umo taabani, katika huu “wakati wa mwisho” wa taratibu ya mambo. Lakini “wageni” waaminifu waliochaguliwa waliomo katika “chumba cha sherehe za arusi” kilichowashwa taa nyangavu wanapata furaha na baraka za ukubali wa Mfalme. Watakapokwisha kushikamana na ukamilifu wao hata kupita “dhiki kubwa” inayokaribia itakayoleta mwisho wa taratibu ya mambo ya kilimwengu, wataruhusiwa kuingia kwenye “karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo” katika mbingu zilizoko juu. (Ufu. 19:7, 9) Kwa kuwa ndio watakaokuwa “bibi arusi” wa Kristo, bila shaka hii ndiyo sababu mwana wa mfalme hatajwi wala hajulishwi alivyo katika mfano wa Yesu.b Washiriki waaminifu wote 144,000 waliochaguliwa wa kundi la Bibi-arusi watafurahia huko karamu hiyo na Bwana-arusi wao.

WANAWALI WA MFANO WA KUMTUMIKIA BIBI-ARUSI

27. Mabaki ya kundi la Bibi-arusi wanashirikiana na nani sasa duniani, nao hawa wanamheshimuje Mfalme na Mwana wake aliye Bwana-arusi?

27 Arusi na sherehe za arusi yaonyesha watakuwako wanawali wa kumtumikia bibi-arusi. Basi, Zaburi 45:13-15 ilionyesha kwa unabii kwamba wangekuwako wengine. Leo, wakati kundi la Bibi-arusi la Kristo ‘linapokaribia kukamilika, wao wanashirikiana na “mabaki” ya kundi hilo. Bila shaka, wanawali hawa wa mfano wa kumtumikia bibi-arusi hawatazamii kwenda mbinguni pamoja na “mabaki,” lakini wanamheshimu Mfalme wa kimbinguni na Mwanawe Bwana-arusi, na kuonyesha heshima ifaayo kwa mabaki ya kundi la Bibi-arusi. Ufunuo 7:9-17 waonyesha kwamba ungekuwako “mkutano mkubwa” usio na hesabu wa wenzi hawa.

28. Wale wa “mkutano mkubwa” huu wanasaidia nani sasa, na thawabu yao itakuwa nini kupitia kwa Baba wa Milele?

28 Wanafurahia kufanikiwa kwa sehemu hii nzuri ya kusudi la Mungu, na kutoa msaada wa upendo kwa mabaki ya jamii ya Bibi-arusi. Kwa heshima wanajiunga katika ibada na utumishi wa Mfalme wa kimbinguni penye jumba lake la hekalu la kiroho. Kutoka kwake Yeye watapokea faida za milele za uzima kupitia kwa Mwanawe Bwana-arusi kama Baba yao wa Milele. (Isa. 9:6, 7) Watapata baraka za milele katika dunia ya paradiso chini ya ufalme wa Mwana wa Mungu aliyeozwa.

​—Kutoka The Watchtower, Nov. 15, 1975.

[Maelezo ya Chini]

a “Maneno haya yaliyomo katika mstari wa 14 ndiyo maana ya mfano wote wala si ya sehemu iliyo juu ya mtu asiye na vazi la arusi.”​—Ukurasa wa 104 wa Barnes Notes on the New Testament, chapa ya 1963. The Jerusalem Bible (1966) yasema, katika maelezo ya chini juu ya Mathayo 22:14: “Sentensi hii yaelekea kumaanisha sehemu ya kwanza ya mfano badala ya ile ya pili. Maana si juu ya wateule kwa jumla bali juu ya Wayahudi, waliokuwa wa kwanza kualikwa. Mfano . . . wala haudai wala haukani kwamba wengine (‘wachache’) wa Wayahudi hawakuukubali mwaliko na kwamba wao si ‘waliochaguliwa’.”

b Linganisha mfano wa wanawali kumi (Mt. 25:1-12) katika habari ii hii.

[Picha katika ukurasa wa 233]

Katika mfano wa Yesu mfalme aliamuru watumishi wake wamtupe nje mtu aliyekataa kuvaa vazi la arusi. Mtu huyu alifananisha wa madanganyo, wanaofanyiza Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki