Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 12/1 kur. 531-534
  • Makao Makuu ya Serikali ya Ulimwengu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Makao Makuu ya Serikali ya Ulimwengu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU “MAKAO MAKUU” MAPYA YALIKUSUDIWA NA MUNGU
  • “YERUSALEMU MPYA”
  • NAMNA UNAVYOKUWA MAMLAKA YA ULIMWENGU WOTE
  • Shauri Lililokatwa Lisitokee Tena Kamwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ufalme
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • “Ufalme wa Bwana Wetu na wa Kristo Wake” Waanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Mambo Ambayo Mfalme Anatufanyia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 12/1 kur. 531-534

Makao Makuu ya Serikali ya Ulimwengu Wote

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1, 2. Biblia yafunua nini juu ya ulimwengu wote na Mpaji-uzima wake?

BILA shaka umezitazama mbingu zenye nyota na umeiona miendo yazo yenye utaratibu mzuri na kufuata wakati wazo. Halafu umetazama chini duniani, pamoja na taratibu yake ya ajabu ya mazingira. Katika kufanya hivyo, je! hujafikiri utake kujua kama Muumba wa maajabu haya anayo serikali kuu ambayo kutoka hiyo vitu hivi vyote vinaongozwa?

2 Biblia yajibu kwamba anayo. Hasa, Biblia inatuambia pia kwamba, zaidi ya kuumba kunakoonekana, kuna “mbingu” zisizoonekana, zinazokaliwa na watu wenye akili, na hawa wako juu zaidi na ni wengi zaidi kuliko mbingu na dunia zionekanazo. Watu hawa wa kimbinguni, pia, ni viumbe vya Mungu. Hawa ni maelfu maelfu ya malaika wanaofanya mapenzi ya Mungu katika ulimwengu wote. (Ufu. 5:11; Zab. 91:11; 103:20) Yehova Mungu ndiye Baba mkuu wa wote, nao ni jamaa, na Mungu akiwa Mpaji-Uzima wao. Yeye ndiye Mwanzishi wa mpango wa jamaa, akisemwa kama “Baba, ambaye kwake kila jamaa mbinguni na duniani huitwa jina lake.”​—Efe. 3:14, 15, NW.

SABABU “MAKAO MAKUU” MAPYA YALIKUSUDIWA NA MUNGU

3. Kizuizi na mchafuko yaliingizwaje katika jamaa ya Mungu?

3 Sikuzote Yehova Mungu amekuwa Kichwa na Mwenye Enzi Kuu juu ya ulimwengu wake wote. Lakini enzi yake kuu ilipingwa na kiumbe kilichoasi. Kiumbe huyu wa kiroho mwenye uasi aliweza kupata wenye kumwunga mkono upande wake wa ulizo kwa kushawishi Adamu na Hawa, wanadamu wawili wa kwanza na wazazi wa wanadamu wote, wampinge Mungu kwa kujitegemea. Jambo hili lilichafua jamaa ya kibinadamu mara ilipokwisha kuanza na mwishowe kuharibika kwa jamaa yote ya kibinadamu.​—Mwa. 3:1-6; Yohana 8:44; Ufu. 12:9.

4. Kwa sababu ya uasi wa Shetani na wa Adamu, Mungu alikusudia nini?

4 Kwa sababu hii, Mungu alikusudia uweko usimamizi wa mambo ambao kulingana na huo ‘angevikusanya pamoja tena vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.’ Usimamizi huu wa Mungu ungetia ndani kusimamisha kwake ufalme mbinguni utakaotawala wanadamu wote. (Efe. 1, 9, 10, NW) Kwa kuwa watawala walio katika ufalme huu watakwezwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu mwenyewe, watafanyiza tengenezo kuu la ulimwengu wote wa Mungu. (Efe. 1:20; Ufu. 3:21) Tengenezo kuu hili litaitwa nini?

“YERUSALEMU MPYA”

5. (a) Tengenezo kuu la ulimwengu wote liko wapi? (b) Ufalme una uhusiano gani na Mungu, ijapo watawala dunia yote?

5 Kwa kufaa, tengenezo kuu hilo lapaswa liwe mbinguni, katika ulimwengu usioonekana. Litakuwa na mamlaka juu ya ulimwengu wote ulioumbwa. Lakini litakuwa chini ya enzi kuu ya Msimamizi, Mungu Aliye Juu Zaidi mwenyewe. Lijapokuwa juu ya vitu vingine vyote vilivyoumbwa, kutia na malaika mbinguni, lazima liwe chini ya Mungu. Kwa maana Mungu ni mkubwa zaidi ya ulimwengu wake wote, na enzi yake iko juu ya vyote. (Zab. 29:10; 145:13) Hili lilionyeshwa mfano katika unabii wa Danieli, ambamo “jiwe” lilisimuliwa kama likichongwa katika “mlima” mkubwa, na maelezo yalipewa kwamba Mungu angesimamisha ufalme ambao ungevunja vipande vipande falme zote za kidunia. (Dan. 2:34, 44, 45) Ufalme wa Yesu Kristo, lile “jiwe,” wafunuliwa hapa kama ukitokana na ufalme wenye enzi kuu wa Yehova mwenyewe.

6. Unabii wa Zekaria vile vile waonyeshaje uhusiano kati ya enzi kuu ya Mungu na ufalme chini ya Kristo?

6 Unabii wa Zekaria watoa mfano unaofanana na huu, kuonyesha mlima kama ukipasuka katika sehemu mbili, mlima wa kwanza ukifananisha ufalme mkuu wenye enzi kuu wa Yehova juu ya wote, na mlima wa pili ukifananisha ufalme chini ya Kristo ukitawala dunia yote. Katika njia hii “[Yehova] atakuwa Mfalme juu ya nchi yote.”​—Zek. 14:4, 9.

7. Ni jina gani la “mji” utakaotawala wanadamu, na sehemu zake ni nini?

7 Tengenezo kuu ambalo kwa hilo utawala wa ulimwengu wote utaongozwa laitwa katika Biblia “Yerusalemu mpya.” (Ufu. 21:2, 9, 10; 3:12) Hili lapatana na uhakika wa kwamba Mungu alichagua Yerusalemu wa kale kama makao makuu ya serikali, kufananisha enzi yake kuu katika Israeli wa kale. Huko wafalme wa ukoo wa Daudi waliketi katika “kiti cha enzi cha [Yehova]” na huko ndiko ukuhani wa Mungu ulifanyia kazi. (1 Nya. 29:23) Kwa hiyo, kulingana na mfano “Yerusalemu mpya” wa kimbinguni wafananisha “ukuhani wa kifalme,” ambao washiriki wake wanachaguliwa kutoka kati ya wanadamu wawe wafalme wa kimbinguni. Ni kundi la Kikristo la watu waliotiwa muhuri 144,000 washiriki wake wakiisha kufufuliwa kuingia katika mbingu.​—1 Pet. 2:9; Ufu. 14:1, 3, 4.

NAMNA UNAVYOKUWA MAMLAKA YA ULIMWENGU WOTE

8. Ni jambo gani linaloonyesha kwamba “Yerusalemu mpya” kwa hakika utatawala kama wafalme na makuhani pamoja na Kristo?

8 Ni jambo gani linaloonyesha kwamba mamlaka ya “Yerusalemu mpya” hakika itakuwa kubwa sana hata kuufanya kuwa makao makuu ya serikali ya ulimwengu wote? Basi, washiriki hawa wa Kristo 144,000, wanaokuwa sehemu ya “Yerusalemu mpya,” ni wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho ambao si ‘warithi wa Mungu’ tu, bali pia “warithi washirika pamoja na Kristo.” (Rum. 8:16-18, NW) Kristo akiwa Mfalme, watashiriki katika utawala wake kama Mfalme kama warithi pamoja naye. Kama wale walionunuliwa kwa damu yake, Kristo anawafanya “ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala kama wafalme juu ya dunia.” (Ufu. 5:9, 10, NW) Tena, “Yerusalemu mpya” ndiye “bibi-arusi” au “mke” wa Yesu Kristo naye ashiriki pamoja naye ufalme ambao anatawala. (Ufu. 21:2, 9-11; 22:17) Watatawala kama makuhani na wafalme juu ya wanadamu wote, walio hai na waliokufa kwa miaka elfu.​—Ufu. 20:4, 6.

9. Utawala wa Yesu Kristo utakuwa mkubwa na wenye kadiri gani, kulingana na mitume Petro na Paulo?

9 Walakini, mtume Petro alisema juu ya kadiri ya mamlaka ya Kristo hivi: “Yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.” (1 Pet. 3:22) Mtume Paulo pia anaandika juu ya cheo kikuu ambacho Mungu amempa Yesu Kristo hivi: “Alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti [juu ya mti wa mateso]. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba [ambaye ufalme wake waendelea kuwa mkuu kuliko zote].”​—Flp. 2:7-11.

10. Ile njozi ya “Yerusalemu mpya” yaonyeshaje kutawala kwake kutakavyomaanisha kwa dunia?

10 Mtume Yohana alipewa njozi ya “Yerusalemu mpya” na utawala wake utakavyomaanisha kwa dunia. Yohana aliandika hivi: “Nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”​—Ufu. 21:2-4.

11, 12. Njozi ya Yohana yasimuliaje utukufu na uzuri wa “Yerusalemu mpya”?

11 Tukiitazama njozi zaidi, twauona utukufu wa mji, usafi na uzuri wake. “Mwongozi” wa Yohana wa kimalaika alisema hivi: “Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.” Yohana asema hivi: “Akanichukua katika [nguvu za roho] mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu; wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri.”

12 Yohana aendelea kusema: ‘Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana Yehova Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake. Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-kondoo. Na Mataifa watatembea katika nuru yake. . . . Na ndani yake hakitaingia cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.’​—Ufu. 21:9-14, 22-27.

13. Njozi yasaidiaje kutuhakikishia kwamba utawala wa “Yerusalemu mpya” utawapatia wote haki?

13 Wakiwa na Yehova Mungu na Yesu Kristo wenyewe mbele yao, wale 144,000 ambao ni sehemu ya “mji” huo hawatahitaji hekalu la kumkaribia Mungu kupitia kwa hilo. Warithi hawa wa kimbinguni pamoja na Kristo watafika mbele za Yehova mwenyewe. (1 Yohana 3:2; Ufu. 22:3, 4) Twaweza kuwa na hakika kwamba “mji” huu, utawapatia haki wote watakaokuwa chini ya utawala wake kwa ile nuru ambayo kwa hiyo mataifa watatembea.​—Ufu. 21:24.

14. Utawala wa miaka elfu wa “Yerusalemu mpya” utatimiza nini?

14 Miaka elfu ya utawala wa “mji” huu juu ya wanadamu itatimiza kusudi la Mungu kuvikusanya pamoja vitu vyote duniani chini ya Kristo. (Ufu. 20:4, 6) Hii itatia ndani vile “vya chini ya nchi,” yaani, wale waliokufa, watakaofufuliwa wajifunze njia ya haki. (Flp. 2:10) Kristo atavipatanisha vitu vyote na Mungu.

15. Mtume Paulo anasimuliaje yatakayotukia wakati wa utawala wa miaka elfu?

15 Akionyesha mambo ambayo utawala huu wa miaka elfu utatimiza, mtume Paulo asema hivi: “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti. Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo. Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.”​—1 Kor. 15:24-28.

16. Ni wakati gani enzi kuu ya Mungu itakapokuwa tena kama ilivyokuwa juu ya paradiso ya kwanza na katika njia gani?

16 Usimamizi wa pekee wa Mungu wa mambo utakapokwisha kutimiza kusudi lake, ‘vitu vyote vikiisha kukusanywa tena pamoja,’ ndipo Mwana wa kifalme wa Mungu atakapomrudishia Mungu Mwenye Nguvu Zote mamlaka yake. (Efe. 1:10, NW) Kwa njia hiyo enzi kuu itakuwa ya Yehova peke yake, kama ilivyokuwa hapo mwanzoni, wakati Adamu na Hawa walipowekwa duniani wakaambiwa “zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha,” na kuwatawala wanyama wote. (Mwa. 1:28) Mungu atakuwa “yote katika wote.”

17. Ni nini litakalotukia mwishoni mwa miaka elfu, na matokeo yatakuwa nini?

17 Shetani Ibilisi, ambaye, wakati wa miaka elfu alikuwa katika shimo refu la kutotenda, ndipo atakapofunguliwa kwa “muda mchache,” ili atoe jaribu la mwisho. Atajaribu kugeuza wanadamu waipinge enzi ya Mungu. (Ufu. 20:1-3, 7, 8) Wale watakaoiunga mkono enzi kuu ya Mungu kwa uaminifu wakati wa miaka elfu na katika wakati wa kufunguliwa kwa Shetani watapokea uzima wa milele, wakiandikishwa majina yao bila kufutika katika “kitabu cha uzima.” Wale watakaochukua mwendo wa kuasi wataharibiwa. (Ufu. 20:9-15) Ikiisha kushuhudiwa, ndipo wakati wote baadaye, enzi kuu ya Mungu itakapokuwa na uhusiano unaofaa kwa wanadamu na ulimwengu wote, kwa baraka ya milele ya jamaa yake ya kibinadamu mbinguni na duniani.

​—Kutoka Kitabu Paradise Restored to Mankind​—by Theocracy!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki