Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 12/15 uku. 23
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Ili Waone ya kuwa Wao Ni Wanyama’
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    Amkeni!—2007
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 12/15 uku. 23

Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

‘Ili Waone ya kuwa Wao Ni Wanyama’

Huenda wanadamu wakajisifu kwa sababu ya uwezo wao pamoja na maarifa. Walakini kwa habari ya njia ambayo katika hiyo maisha yao yanafikia mwisho wake, wanadamu si afadhali kuliko wanyama wasio na akili. Mfalme Sulemani Mwenye Hekima alivuta fikira kwenye jambo hili, akisema: “Nikasema moyoni mwangu, Ni kwa sababu ya wanadamu, ili Mungu awajaribu, nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama. Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo [roho] moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili. Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.”​—Mhu. 3:18-20.

Kabla tu ya kutokeza wazo hili, Sulemani aliandika hivi: “Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.” (Mhu. 3:17) Hivyo, katika mstari wa 18, Sulemani anaposema kwamba Mungu ‘huwajaribu’ wanadamu, hilo laweza kumaanisha kwamba nafasi anazowatolea, pamoja na mambo anayoruhusu yawapate, kutia na magumu pamoja na kutokuwa na hakika, yatafunua baada ya wakati kupita ama wao ni wenye haki ama ni wasio haki. Uhakika wa kwamba maisha yanajawa na magumu pamoja na kutokuwa na hakika na mwishowe yanakomeshwa na mauti, wapaswa ufahamishe wanadamu kwamba, kwa habari ya uwezo wao, mwishowe wao wanafanana na wanyama. Roho ile ile, ikiendelezwa kwa kuvuta hewa, yawahuisha wote wanyama na wanadamu. Baada ya kufa wote wanyama na wanadamu wanayarudia mavumbi yasiyo na uhai. Mhu. 9:4-6.

Kwa msingi wa mambo yanayoonwa na wanadamu, hakuna ye yote awezaye kujibu ulizo ambalo sasa Sulemani anatokeza. “Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?”​—Mhu. 3:21.

Kwa kuwa mauti inakomesha utendaji wote wa kibinadamu kama vile kwa habari ya wanyama, Sulemani anafikia uamuzi huu: “Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye”? (Mhu. 3:22) Hekima inaonyesha kwamba inafaa mtu afurahie ifaavyo kazi yake ngumu. Mtu afapo, anakuwa hana sehemu yo yote katika utendaji wa kibinadamu. Akiwa maiti, hawezi hata kutazama yanayotukia kati ya wanadamu.​—Mhu. 9:5, 10.

Kukumbuka kwamba mauti yaweza kufanya mtu asiwe kitu kama vile mnyama asiye na akili kwapaswa kuwe na matokeo yenye kutupa akili. Kwapaswa kutukumbushe umuhimu wa kutumia maisha yetu katika njia yenye mafaa yajapokuwapo magumu pamoja na kutokuwa na hakika. Kwapaswa vilevile kutuongoze tumgeukie Mungu, tukitambua kwamba mataraja yo yote ya uzima wa wakati ujao baada ya kifo yamtegemea yeye.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki