Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 3/1 kur. 3-4
  • Ahadi Iliyo Hakika ya Taratibu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ahadi Iliyo Hakika ya Taratibu Mpya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAHALI AMBAPO USALAMA WA KWELI UTAPATIKANA
  • Namna Gani Wakati Ujao?
    Amkeni!—1991
  • Ishi Milele Juu ya Dunia-paradiso
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Ule Ulimwengu Mpya Mzuri Ajabu Wenye Kufanyizwa Na Mungu
    Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani
    Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 3/1 kur. 3-4

Ahadi Iliyo Hakika ya Taratibu Mpya

“Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”—Zab. 37:11

WAKATI MUNGU alipomwumba mwanamume na mwanamke, alikusudia waishi katika paradiso. Aliwatayarishia ‘bustani katika Edeni,’ ambayo kwa habari zake Biblia inasema, “[Yehova] Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa.” (Mwa. 2:8, 9) Zaidi ya hayo, “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” (Mwa. 1:28) Hali za maisha za wazazi wetu wa kwanza ‘zilikuwa njema sana.’​—⁠Mwa. 1:31.

Basi, pasipo shaka wakati Mungu alipoumba mwanamume na mwanamke aliwapa maisha yaliyokuwa salama sana. Walikuwa na mahali pa kuishi pazuri sana, afya bora kabisa, chakula kitamu, kazi ya kufurahisha, na pendeleo la kuangalia aina nyingine za wanyama. Wangekuwa pia na pendeleo la kuzaa watoto na kuwafundisha jinsi ya kuwasaidia wapanue mipaka ya paradiso ya Edeni, hata baadaye paradiso hiyo ienee duniani mwote. Basi ni wazi kwamba Yehova alipoumba wanadamu, alikusudia jamaa yote ya kibinadamu ifurahie wingi wa baraka zionekanazo. Nao wangezifurahia wakiwa na usalama wa kweli​—⁠usalama mwingi sana. Basi, ilifaa nao watii sheria za Mungu, kisha jamaa yote ya kibinadamu ifaidike kabisa.​—⁠Mwa. 2:17; Zab. 19:7-11.

Walakini, kwa uasi wao, wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walipoteza faida hizo. Walivunja sheria ya Mungu, wakajitakia uamuzi wao wa yaliyo mema na mabaya. (Mwa. 3:1-6) Walichagua njia yao ya kuwa huru bila kumtegemea Mungu. Lakini kwa kufanya hivyo waliacha uongozi na baraka zinazoweza kutoka kwa Muumba peke yake. Na kwa kuwa wanadamu hawakuumbwa waweze kufaulu wasipoongozwa na Mungu, njia yao iliwaingiza katika matatizo tu. (Yer. 10:23) Karne nyingi ambazo jamaa ya kibinadamu imepatwa na huzuni zinatosha kuonyesha jambo hilo. Masikitiko pia yalitokea kwa sababu ya kupoteza usalama wa kweli. Kwa hiyo, kwa maelfu ya miaka baada ya uasi wa mwanadamu, mamilioni mengi ya watu wameingia katika hali za ufukara, njaa, nyumba zisizofaa na woga. Mamilioni mengi ya watu wameuawa na vita au matendo mengine ya jeuri. Kinachozidisha mambo hayo yote ni kwamba, viongozi wasiotumia dhamiri, wa kisiasa, wa kibiashara na wa kidini wamewanyonya watu wa kawaida. (Mhu. 8:9) Nayo jamaa ya kibinadamu inaudhika kwa sababu ya kutazamia kuuawa na uzee au magonjwa.​—⁠Rum. 5:12.

MAHALI AMBAPO USALAMA WA KWELI UTAPATIKANA

Walakini, jambo hili limebadili kusudi la Mungu kwa dunia na jamaa ya kibinadamu? Hasha, yeye bado anakusudia dunia nzima igeuzwe iwe paradiso katika wakati aliouweka. Dunia yote itakuwa makao ya kupendeza yaliyo kama bustani, nao watakaoikaa wataifurahia milele. Chini ya utawala wa ufalme wa Mungu wa kimbinguni ulio mikononi mwa Kristo, ni hakika kwamba mambo hayo mazuri ajabu yatakuwako. (Mt. 6:10) Hata watu waliokufa watarudishiwa uzima. (Matendo 24:15) Hiyo ndiyo sababu Yesu alimwahidi mtenda mabaya mwenye huruma aliyeuawa pamoja naye, kwamba: “Utakuwa pamoja nami katika paradiso.”​—⁠Luka 23:43, ZSB.

Katika taratibu hiyo mpya, chini ya utawala wa ufalme wa Mungu, kwa mara nyingine watu watafurahia usalama wa kweli. Watajisikia salama wakijua kwamba wanatumikiwa na serikali iliyo bora kupita zote zilizopata kuwako. (Isa. 9:6, 7) Na kama ilivyoonyeshwa na miujiza aliyofanya Yesu akiwa hapa duniani, wanadamu watapata faida nyingi sana za kimwili. Kwa mfano, afya mbaya, magonjwa ya kipuku, uzee na mauti yataondolewa, kisha kuwe na afya njema na uzima wa milele. (Mt. 15:30, 31; Yohana 11:43, 44; 1 Kor. 15:25, 26) Kwa njia hiyo, katika taratibu hiyo mpya Mungu “atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—⁠Ufu. 21:4.

Hata hayawani (wanyama-mwitu) hawatahatirisha usalama wa watu katika taratibu mpya ya Yehova. Sababu ni kwamba tunaweza kutazamia hali za paradiso ya kiroho zilizotabiriwa katika unabii ufuatao, zinazoonekana hata sasa miongoni mwa watu wa Mungu, zionyeshwe pia katika paradiso ya taratibu mpya: “Nami nitafanya agano la amani nao, nami nitawakomesha wanyama wakali kati yao; nao watakaa salama jangwani, na kulala misituni.” (Eze. 34:25) “Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe.”​—⁠Isa. 11:6, 7.

Ingawa Biblia haielezi habari zote vile hali hizi zitakavyoletwa, tunaweza kuwa na tumaini la kwamba zitakuwapo bila shaka lo lote, kwani Yehova anakusudia ‘kuwa’ pamoja na wanadamu na kuwabariki. Yeye ‘hawezi kusema uongo’ kuhusu makusudi yake. (Ufu. 21:3; Tito 1:2) Na zaidi ya hayo, unabii mwingi wake umetimia, ama kwa Israeli wa kale, ama kwa watu wa kisasa wa Yehova, kwa njia halisi au ya kiroho. Hii inatupa uhakikisho kwamba unabii mbalimbali kuhusu taratibu mpya ya Mungu utatimia pia. (Isa. 55:11) Taratibu hiyo mpya yenye usalama imekaribia sana!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki