Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/1 uku. 3
  • Ujumbe kwa Wasomaji Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujumbe kwa Wasomaji Wetu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Toleo Jipya la Funzo la Mnara wa Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kukesha Kwa Miaka 100 Moja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • ‘Juu ya Mnara wa Ulinzi Mimi Ninasimama’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/1 uku. 3

Ujumbe kwa Wasomaji Wetu

Toleo la kwanza la Mnara wa Mlinzi lilichapwa Julai 1879. Hiyo yamaanisha kwamba gazeti hili limechapwa kwa muda wa karne moja (katika chapa yake ya kwanza ya Kiingereza). Nako kupendezwa kwingi nanyi, wasomaji wetu, kumetuongoza tuchape toleo hili la pekee.

Makala inayoanzia ukurasa unaofuata inasimulia hadithi ya Mnara wa Mlinzi katika muda wa hii miaka mia moja ya kwanza. Inatukumbusha namna ulimwengu ulivyokuwa katika miaka ya mwanzo-mwanzo ya gazeti hili, namna ulimwengu ulivyobadilika na namna gazeti Mnara wa Mlinzi lilivyojirekebisha pia ili liambatane na nyakati. Makala hiyo inataja nyingine za habari za maana sana zilizochapwa katika gazeti hili katika muda huo wa miaka mingi na kusimulia namna lilivyowashinda wenye kulaumu na wapinzani wake.

Makala inayoanzia ukurasa 8 inazungumza ukweli wa mengine ya mafundi-sho ya Biblia, ambayo yametokeza ubishi kati ya dini nyingi za Jumuiya ya Wakristo.

Katika toleo hili la mwaka wa mia moja, makala mbili za kujifunza zinapatikana katika ukurasa wa 12 mpaka wa 22. Ya kwanza, “Kwa Kweli Ni Nani Walio na Kweli?” inamtambulisha Yehova kuwa Mungu wa kweli, ambaye hutaka watu wa dunia watembee katika njia za kweli. Inatoa mifano yenye kutokeza sana ya wale waliotembea na Mungu katika nyakati zilizopita na katika nyakati za kisasa. Vilevile inawatambulisha waziwazi wale wanaotembea katika kweli ya Yehova katika siku zetu.

Makala ya pili ya kujifunza inajibu ulizo, Mungu anawaongozaje watu wake? Kwa mfano, Wakristo wa kwanza walipata kujuaje kweli? Je! nyakati nyingine walikuwa na mawazo yenye makosa? Ikiwa ndivyo, maoni hayo yalisahihishwaje? Leo, watu wa Mungu wanafunuliwaje kweli? Je! kundi la Kikristo ni kundi lisiloweza kufanya makosa? Je! kuna wakati wo wote linapokuwa na mawazo yenye makosa yanayohitaji kurekebishwa? Nalo linatofautianaje na dini za Jumuiya ya Wakristo? Maulizo haya na mengine yanajibiwa.

Twakukaribisha usome na kutafakari habari zilizomo katika toleo hili la Mnara wa Mlinzi la mwaka wa 100 moja. Vilevile, tunatumaini kwamba utafurahia matoleo ya gazeti hili ya wakati ujao linapoingia katika karne ya pili ya kuchapwa kwake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki