Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 11/15 kur. 3-6
  • Kwa Sababu Gani Ni Lazima Wakristo Waendelee Kujitenga na Ulimwengu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Gani Ni Lazima Wakristo Waendelee Kujitenga na Ulimwengu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vitu Vinavyojumlika Kuwa Ulimwengu
  • Sababu ya Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu
  • Upande wa Ulimwengu wa Shetani, au Upande wa Mfumo Mpya wa Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Lazima Waokokaji Wawe “Si Sehemu ya Ulimwengu”
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Sababu kwa Nini Ni Lazima Tusiwe Sehemu ya Ulimwengu Huu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Yanayohitajiwa Ili Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 11/15 kur. 3-6

Kwa Sababu Gani Ni Lazima Wakristo Waendelee Kujitenga na Ulimwengu?

LEO kuna mamilioni mengi sana sana ya watu wanaojisema kuwa wafuasi wa Yesu Kristo. Walakini, ni jambo moja mtu kudai yeye ni Mkristo na ni jambo tofauti kuwa Mkristo hasa-a. Yesu mwenyewe alionyesha jambo hilo katika Mahubiri yake ya Mlimani: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, . . . na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”​—Mathayo 7:21-23.

Kati ya mambo mengi yanayotofautisha Wakristo wa kweli na wale walio hivyo kwa jina tu ni kuendelea kwao kujitenga na ulimwengu. Yesu alikazia sana jambo hilo katika usiku ule wa kusalitiwa kwake, akiwaambia wafuasi wake hivi: “Ulimwengu ukiwachukia ninyi, mjue kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngalikuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungalikipenda kilicho chake wenyewe. Sasa kwa kuwa ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali mimi nimewachagua kutoka katika ulimwengu, kwa sababu hii ulimwengu unawachukia ninyi.” Alitaja jambo ilo hilo katika sala aliyopelekea Baba yake wa kimbingu jioni hiyo, akisema: “Wao si sehemu ya ulimwengu, sawa na vile mimi si sehemu ya ulimwengu.”​—Yohana 15:18, 19; 17:16, NW.

“Si sehemu ya ulimwengu.” Hiyo maana yake ni kuendelea kujitenga na ulimwengu. Jambo hilo ni wazi kabisa. Lakini Yesu alikuwa akimaanisha nini kwa kusema “ulimwengu”? Yesu alionyesha tofauti kati ya wafuasi wake na “ulimwengu” huo wakati aliposema hivi katika sala: “Mimi nawaombea hao [wanafunzi wake]; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako.” (Yohana 17:9) Kwa kutumia neno “ulimwengu,” hapo Yesu anaonyesha kwamba anamaanisha ulimwengu mwovu usiomcha Mungu, au kosmos, ulio wa watu ambao Yohana anawasema kwamba “hukaa katika yule mwovu.” (1 Yohana 2:15-17; 5:19) Mungu na mtawala wa ulimwengu huo ni Shetani Ibilisi.

Vitu Vinavyojumlika Kuwa Ulimwengu

Shetani ameupanga ulimwengu huu katika sehemu au migawanyiko mbalimbali. Moja ya sehemu zilizo kubwa zaidi ni Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, inayoelezwa kwenye Ufunuo 17 : 3-6 kuwa ‘mama wa makahaba na machukizo ya nchi.’ Anasemwa kuwa amelewa kwa damu ya watakatifu, mashahidi wa Yesu.

Pia sehemu nyingine iliyo kubwa ya ulimwengu wa Shetani ni falme za kisiasa za dunia, zinazoelezwa na mtume Yohana kuwa mnyama aliyetokea baharini, mwenye vichwa saba na pembe 10. (Ufunuo 13:1) Kwamba falme hizo ni sehemu ya ulimwengu wa Shetani inaonekana kutokana na uhakika wa kwamba yeye aliweza kumtolea Yesu Kristo falme hizo kama Yesu angefanya tendo la kumwabudu Shetani.​—Mathayo 4:8, 9.

Shetani anaongoza pia, ukiwa sehemu ya ulimwengu wake, mfumo wa kibiashara wenye pupa mbaya sana na uonezi, unaotajwa kwenye Ufunuo 18:11 kuwa “wafanya biashara.” Mfumo huo unawanyonya watu wenye cheo cha kawaida na kujaribu kuwadumisha utumwani, katika utumwa wa kiuchumi, sawa na vile Babeli Mkuu inavyojaribu kudumisha watu katika utumwa wa kidini na serikali za ulimwengu huu kujaribu kudumisha watu katika utumwa wa kisiasa.

Ulimwengu wa Shetani umechafuliwa pia na mazoea ya ufisadi wa namna zote, sawa na vile Yohana anavyoonyesha kwenye 1 Yohana 2:15, 16, NW: “Msiwe mkipenda wala ulimwengu wala vitu vilivyomo katika ulimwengu. Mtu ye yote akipenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo katika yeye; kwa sababu kila kitu kilichomo katika ulimwengu​—tamaa ya mwili na tamaa ya macho na kujionyesha kwa mtu mali yake​—hakitokani na Baba, bali chatokana na ulimwengu.”

Sababu ya Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu

Kwa sababu gani Wakristo wanaamriwa waendelee kujitenga na ulimwengu ulio chini ya uongozi wa Shetani? Kwanza kabisa, acha tuone yasiyomaanishwa na kuendelea kujitenga na ulimwengu. Haimaanishi kwamba tujiepushe kabisa kabisa na wale walio na roho ya ulimwengu, wanaohusika katika dini ya uongo, siasa chafu, au katika shughuli za biashara yenye pupa au zenye ufisadi. Kama ingekuwa hivyo, basi kama mtume Paulo anavyotukumbusha, ingetupasa tutoke katika ulimwengu kwa njia halisi. (1 Wakorintho 5:9, 10) Wala kuendelea kujitenga na ulimwengu hakumaanishi kwamba hatuwezi kufurahia tafrija zinazofaa wala kwamba hatuwezi kutembelea watu wa ukoo wetu au kuwaruhusu watutembelee kwa sababu wao si waamini ati.

Bali, kuendelea kujitenga na ulimwengu kunahusiana na suala lililoanza wakati Yehova Mungu alipotabiri kwamba kungekuwa na uadui katika ya uzao wa mwanamke, tengenezo takatifu la Mungu, na uzao wa mungu wa ulimwengu huu, Shetani Ibilisi. Kunamaanisha kuendeleza usawaziko, kutokuwa mtumwa wa kitu cho chote kinachoweza kutolewa na ulimwengu huu. Kunamaanisha kuepuka kukubaliana na ulimwengu katika mambo yasiyofaa. Ni wazi kwamba kukubaliana nao katika mambo hayo kungemchukiza Yehova Mungu. Kunamaanisha ‘kutokwenda katika shauri la wasio haki, kutosimama katika njia ya wakosaji, kutoketi barazani pa wenye mizaha.’​—Zaburi 1:1.

Jambo linalofaa kuangaliwa hapa ni maoni ambayo Wakristo wa karne ya pili W.K. walikuwa nayo juu ya ulimwengu, kama yanavyoripotiwa na mwanahistoria Cadoux katika kitabu chake The Early Church and the World (Kanisa la Kwanza na Ulimwengu, cha mwaka wa 1925 W.K.): “Kuhusu hali ya jamii ya kibinadamu isiyo katika Kanisa la Kikristo, waandikaji wa kipindi hiki kwa ujumla wana maoni ya kutopendezwa nayo. Tabia nyingi za uovu zinashikiliwa kuwa zinauhusu ‘ulimwengu’ au ‘kizazi hiki’: yaani, makosa, giza, upofu, hali ya kulewa, udanganyifu, uovu, udhalimu, unajisi, ufisadi, ubatili, utovu wa tabia, kukosa kumcha Mungu, kutokuheshimu Mungu, kutokuamini, na kukufuru.”

Ni lazima sisi tuendelee kujitenga na ulimwengu wa Shetani kwa sababu ya hali yake ya kutomcha Mungu na kumchukia Yesu Kristo. Kuchangamana na ulimwengu huu, au kuwa sehemu yake, kunatufanya sisi tuwe nini? Mwanafunzi Yakobo anajibu hivi: “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.” (Yakobo 4:4) Je! kweli sisi tutathubutu kutaka Yehova Mungu awe adui yetu? Mtume Paulo anajibu ulizo hilo kwenye 1 Wakorintho 10:21, 22: “Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani. Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. Au twamtia Bwana wivu? Je! tuna nguvu zaidi ya yeye?”

“Kikombe” na “meza” ya mashetani kinapatikana katika ‘Babeli Mkuu.’ Yeye anafundisha mambo ya uongo, anamchongea Yehova Mungu na ametumiwa na Shetani kudanganya dunia yote inayokaliwa na watu. (Ufunuo 12:9) Basi watumishi wa kweli wa Mungu wanawezaje kuchangamana na yo yote ya dini za ulimwengu huu? Yesu hakuzoea kuchangamanisha imani yake na imani nyinginezo. Yeye hakujiunga na yo yote ya madhehebu mbalimbali za dini ya Wayahudi ili kupinga Waroma kwa sababu ya nira waliyowafunga kwa kuwatawala. Wala wafuasi wake wa leo walio wa kweli hawawezi kuchangamanisha imani yao na imani nyinginezo. Ni lazima watii maneno ya Isaya 52:11: “Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya [Yehova].” Kweli kuna sababu thabiti sana zinazopasisha Wakristo kuendelea kujitenga na sehemu ya kidini ya ulimwengu wa Shetani!

Pia kuna sababu thabiti za kufanya iwe lazima watumishi wa kweli wa Mungu, wafuasi wanyofu wa Yesu Kristo, waendelee kujitenga na sehemu ya kisiasa ya ulimwengu wa Shetani, na utukuzo wa taifa na siasa. Je! kwani sehemu hizo pia hazipingi ufalme wa Mungu? Wakati Yesu alipokuwa amesimama mbele ya mjumbe mwenye kuwakilisha Milki ya Roma, yaani Pontio Pilato, yeye alishuhudia hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungalikuwa sehemu ya ulimwengu huu, wahudumu wangu wangalikuwa wamepiga vita kwamba nisitolewe nipewe kwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu si wa kutoka chanzo hiki.” (Yohana 18:36, NW) Kwa kuwa wala Yesu wala wafuasi wake hawakuwa sehemu ya ulimwengu wa kisiasa huko nyuma, wala wafuasi wa Yesu leo hawapaswi kuwa. Inaweza kuonekana kwamba mataifa ya ulimwengu hayana umoja na Mungu wa kweli kwa sababu yanaendelea kukusanywa na mungu wa ulimwengu huu, kupitia semi zake alizoziongoza mwenyewe, yakafike kwenye vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenye Nguvu Zote katika Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Kama vile mtume Petro anavyoandika kwa uzuri, Wakristo ni wageni na wakaaji wa muda. (1 Petro 2:11) Maneno ya mtume Paulo kwenye Wafilipi 3:20 yanapatana na uhakika huo, yakionyesha kwamba uraia wa wafuasi wa kweli wa Kristo uko katika mbingu. Hiyo ndiyo sababu mashahidi Wakristo wa Yehova hawajiingizi katika siasa, wala hawanunui kadi za chama cha kisiasa wala kwenda wakiwa wamezichukua.

Na kwa kuwa 1 Yohana 2:15, 16 inatuonya juu ya utafutaji wa mali za ulimwengu na ufisadi, hayo yakiwa ndiyo kinyume chenyewe cha kujitolea utumishi wa kimungu, ni lazima tujiepushe pia na vitu hivyo ndipo tuweze kama watakatifu kama Yehova Mungu alivyo mtakatifu.​—1 Petro 1:15, 16.

Ni mambo gani yanayohitajiwa ili kuendelea kujitenga na ulimwengu? Makala inayofuata itajibu ulizo hili.

[Picha katika ukurasa wa 4]

DINI YA UONGO

SIASA ZENYE UFISADI

BIASHARA YENYE PUPA

MAISHA YA UPOTOVU

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki