Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 12/15 kur. 5-8
  • “Ee Mlinzi Habari Gani za Usiku?”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ee Mlinzi Habari Gani za Usiku?”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU GANI UMWULIZE “MLINZI”?
  • TANGAZO BAADA YA KUWEKWA KWA MLINZI
  • Wakati wa Kuwapo kwa Mlinzi kama Ezekieli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • “Babeli Umeanguka”!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Kutumikia Pamoja na Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • ‘Juu ya Mnara wa Ulinzi Mimi Ninasimama’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 12/15 kur. 5-8

“Ee Mlinzi Habari Gani za Usiku?”

1. Kwa kusema kwa njia ya mfano, sasa ulimwengu umo katika nini, na je! kuna msingi wo wote wa kutazamia mazuri kuhusiana na taratibu hii ya mambo?

ULIMWENGU umo katika “usiku”! Sasa unakaribia kipindi chenye giza zaidi cha usiku huo wa mfano. Kuonekana kwa mambo wakati asubuhi itakapopambazuka kungali kutaonekana. Jambo linalowasumbua wanadamu zaidi na zaidi ni kuharibika zaidi kwa hali ya mambo ya kibinadamu katika kila sehemu ya maisha. Historia ya ulimwengu inaweka kuanza kwa jambo hilo wakati mmoja na vita ya ulimwengu ya kwanza. Wanasiasa, viongozi wa kidini, viongozi wa kijamii na wanauchumi huenda wakafikiri wanaona miali fulani ya kupambazuka nao huenda wakajaribu kutokeza uchangamshi. Walakini hakuna sababu nzuri ya kutazamia mazuri kuhusiana na taratibu hii ya mambo inayotikisika.

2. Ni jambo gani linaloonyesha kama kuja kwa “usiku” huo kulionekana kabla, nao watu wote walijulishwaje kuja kwa “mchana”?

2 Kuingia kwa “usiku” huo kulionekana makumi mengi ya miaka kabla. Maandishi yaliyopo ya karne iliyopita yathibitisha jambo hilo. Kupambazuka kwa “siku” yenye mwangaza zaidi katika historia yote ya kibinadamu kulitangulia kuonwa pia. Watu wote walijulishwa kwa maneno ya vinywa na kwa karatasi zilizochapwa.

3. Ni gazeti gani, ambalo lingali linachapwa leo lilikuwa uthibitisho wa jambo hilo, na sababu gani kichwa chake kilifaa mgawo wake?

3 Gazeti ambalo sasa linaenezwa milioni nyingi za nakala kila toleo, katika lugha nyingi, linashuhudia uhakika huo. Wakati toleo lake la kwanza lilipotokea katika Julai wa mwaka 1879 gazeti hilo liliitwa “Mnara wa Mlinzi wa Sayuni na Kutangaza Kuwapo kwa Kristo” (Kiingereza). Toleo la kwanza lilikuwa na kurasa nane, nazo kurasa zake zilikuwa kubwa kuliko zile za gazeti hilo leo. Lilikuwa na mgawo wa wakati wake wa kutimiza. Jambo hilo lilionyeshwa na kichwa chake kilichokuwa na maneno yenye maana “Mnara wa Mlinzi.” Kwa kufaa, basi, juu yake chini ya kichwa hicho palikuwa na maneno ya maana kutoka katika kitabu cha zamani zaidi duniani. Yalisema hivi: “Ee-Mlinzi, Habari gani za Usiku? ” “Asubuhi Yaja.” Maneno hayo yalitajwa kutoka katika Biblia Takatifu, kutoka katika unabii wa Isaya sura ya 21, mistari 11, 12, kulingana na Authorized Version. Katika nyakati za Kibiblia (za kuandikwa kwa Biblia) mlinzi alishirikishwa na mnara wa mlinzi juu ya ukuta wa mji wenye maboma. Hali hiyo ya kuinuka iliwezesha kuona vizuri. Wachapaji wa gazeti hilo walikusudia kutumikia kama jamii ya mlinzi. Kupitia kwa safu za gazeti hilo, wachapaji hao walijitahidi kujibu ulizo, “Ee mlinzi, habari gani za usiku? ” Ulizo hilo zito liliendelea kuonekana kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti hilo hata kufikia toleo lake la Desemba 15, 1938.

4. Gazeti Mnara wa Mlinzi lilichapwa katika wakati wenye kuogopesha kwa sababu ya matukio gani yenye maana ya miaka iliyoanzia na 1870?

4 Gazeti Mnara wa Mlinzi lilipotokea mara ya kwanza katika Julai, 1879, likichapwa nakala chache, 6,000, tamasha ya ulimwengu ilikuwa inachukua sura yenye kuogopesha. Vita ya Wafaransa na Wajeremani ya 1870 ilikuwa imepiganwa, nayo Enzi au Milki ya Ujeremani ya pili ilikuwa imetokea. Mashindano ya kuunda silaha yalikuwa yanakaribia kutokea kati ya Milki ya Uingereza na washindani wake, Milki ya Ujeremani. Katika mwaka 1878 Mkutano wa Berlin wa Mataifa ulikuwa umefanywa ili kusuluhisha Suala la Mashariki lililohusu kuondoa milki ya Uturuki kama mwanachama kati ya milki za Ulaya, sana sana Uingereza na Urusi. Kama matokeo yake, uadui wa wakati ujao kati ya mataifa ukatokea!

5. Kwa hiyo ulikuwa wakati wa uchunguzi wa namna gani, na, kwa kufaa, katika Januari 1, 1895, gazeti Mnara wa Mlinzi lilionyesha jambo gani katika jalada yake ya juu?

5 Hakika ulikuwa wakati wa kutazama unabii wa Biblia kuona kama ulikuwa na yo yote ya kusema juu ya maana ya matukio ya ulimwengu na matokeo yake. Kwa kufaa, katika Januari 1, 1895, gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) lilibadilishwa sura yake ya ukurasa wa kwanza kuonyesha mnara wa mlinzi pembeni mwa bahari yenye msukosuko. Vilevile, chini ya ukurasa huo yalikuwako maneno yafuatayo ambayo msingi wake ni Luka 21:​25-31 (AV) katika herufi zilizolazwa: “Juu ya dunia taabu ya mataifa pamoja na wasiwasi; bahari na mawimbi (wasiotulia, wasiotosheka) yakivuma; mioyo ya wanadamu ikizimia kwa kuogopa na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia (jamii)! kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikiswa. . . . Mwonapo mambo hayo yakipita, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia sana. Angalieni juu, inueni vichwa vyenu juu, furahini, kwa kuwa ukombozi wenu unakaribia.​—⁠Luka 21:​25-28-31.”

6. Karne ya ishirini iliyokuwa ikaanza wakati huo ilipata kuwa wakati wenye kusisimua kwa jamii ya “mlinzi” kwa sababu gani?

6 Vita ya Waspania na Waamerika ikafuata katika mwaka 1898 ambayo katika hiyo Milki ya Spania ilipata hasara. Katika mwaka 1899 ikatokea Vita ya Makaburu katika Afrika ya Kusini, nayo Milki ya Uingereza ikapata faida. Mashindano ya mataifa yote ya uundaji wa silaha yakawa ya kasi zaidi. Ndege-ulaya ilipovumbuliwa, ikawezesha vita ipiganwe angani. Kufikia wakati huo, pia, namna za manowari za kupitia chini ya bahari zikawa zimevumbuliwa na kutumiwa vitani. Hivyo karne ya 20 ikawa wakati wenye kusisimua kwa jamii ya “mlinzi” kuripoti kwa watu wenye kutaka kujua sana. Sana sana ndivyo, kwa kuwa jamii ya “mlinzi” ilikuwa intazamia “nyakati za Mataifa” zimalizike katika vuli ya mwaka 1914.​—⁠Luka 21:​24, AV.

SABABU GANI UMWULIZE “MLINZI”?

7. Ulizo analoulizwa “mlinzi” limo katika kikao cha namna gani, kama inavyooneshwa na mistari inayofuata?

7 Ulizo katika Isaya 21:​11, analoulizwa “mlinzi,” limo katika kikao chenye hali ya vita. Mazungumzo ya mistari inayofuata yanasema hivi: “[Tangazo] juu ya [uwanda wa jangwa]. Ndani ya mwitu wa [uwanda wa jangwa] mtalala, Enyi misafara ya Wadedani. Waleteeni wenye kiu maji, Enyi wenyeji wa nchi ya Tema; Nendeni kuwalaki wakimbiao na chakula chao. Kwa maana wanakimbia mbele ya panga, Upanga uliofutwa, na upinde uliopindwa, na mbele ya ukali wa vita. Kwa sababu [Yehova] ameniambia hivi, Katika muda wa mwaka, kama miaka ya mtu mwenye kuajiriwa, utaangamia utukufu wote wa Kedari. Na mabaki ya hesabu ya wavuta pinde, hao mashujaa wa Kedari watakuwa wachache; maana [Yehova], Mungu wa Israeli, amenena neno hili.”​—⁠Isa. 21:​13-17.

8. Mistari inayotangulia mazungumzo kati ya mwenye kutaka kujua mlinzi ina hali gani, naye mwenye kutaka kujua huyo yuko katika sehemu gani?

8 Vivyo hivyo, ‘tangazo’ linalotangulia mazungumzo kati ya mwenye kutaka kujua na mlinzi lina hali ya vita. Kwa hiyo mwenye kutaka kujua ana sababu ya kuhangaika. Mwenye kuuliza huyo yuko sehemu gani? Kwa wazi katika njia ya mshindi wa ulimwengu. Isaya 21:11 lasema hivi: “[Tangazo] juu ya Duma. Mtu ananililia toka Seiri, Ee mlinzi, habari gani za usiku? Ee mlinzi, habari gani za usiku? ”

9. (a) Jina la mahali ambapo tangazo hilo linaelekezwa linamaanisha nini, nalo lapasaje? (b) Edomu, ndugu pacha wa Yakobo, alikujaje kushirikishwa na Seiri?

9 Jina la mahali ambapo tangazo hilo linatolewa juu yake ni Duma, jina ambalo maana yake ni “Unyamavu.” Kwa wazi jina hilo ni la kiunabii, likitabiri kwamba mahali hapo patakuwa penye unyamavu. Jina hilo kwa lazima halimaanishi kwamba unyamavu unaoletwa na kufanywa ukiwa na kifo tayari upo. Mahali ilipo Duma panaonyeshwa na uhakika wa kwamba mwito unaotolewa kwa mlinzi unatoka Seiri, nchi ya Seiri. Nchi hiyo inahusianishwa na Idumea, nchi ya Edomu. Hiyo yaweza kuwa sababu ya Septuagint Version ya Kigiriki kuzungumza juu Idumea mahali pa Duma. Edomu lilikuwa jina la ziada alilopewa Esau, ndugu mkubwa pacha wa Yakobo. Watu wa nchi ya Edomu walilipinga taifa la Yakobo, ,au taifa la Israeli.

10. Sababu gani wazao wa Edomu, au Esau, wakaja kuchukia taifa lililo ndugu yao na kufurahia msiba uliolipata katika mwaka 607 K.W.K.?

10 Ndugu mkubwa pacha wa Yakobo aliitwa Esau, ambalo maana yake ni “mwenye malaika,” kwa kuwa wakati wa kuzaliwa alikuwa mwenye malaika Jina Seiri lamaanisha “mwenye malaika au malaika nyingi,” walakini nchi yenye jina hilo haikuitwa vile kwa sababu ya Esau. Wazao wake waliitwaa nchi ya Seiri kwa kuwashinda wakaaji wake wa kwanza. Esau, au Edomu, ana sifa mbaya kwa kuwa na nia ya kuuza haki yake ya kuzaliwa ya mwana mzaliwa wa kwanza kwa Yakobo. Yehova, Mungu wa Yakobo, alikubali uuzaji huo naye akampa baraka ya kimungu mnunuzi, Yakobo. Kwa sababu hiyo Yakobo akachukiwa na Esau. Wababeli walipouharibu Yerusalemu katika mwaka 607 K.W.K., wazao wa Esau, Waedomu, walisimanga (walifurahi) kwa sababu ya msiba mbaya sana uliopata taifa lililo ndugu yao, Israeli. Msiba huo wa taifa zima, pamoja na kuchukuliwa kwa Waisraeli waliookoka mpaka Babeli, ulitokea katika karne iliyofuata unabii wa Isaya juu ya mlinzi.

11. Chanzo cha jibu la ulizo lile kipo wapi, na, kwa hiyo, Isaya anafananisha nani leo?

11 Hata hivyo, alipo mlinzi ni wapi, ambapo mwenye kutaka kujua katika nchi ya Edomu ya Seiri anaelekeza ulizo lake? Unabii huo unaohusu mwenye kutaka kujua na mlinzi ulitolewa na Isaya, naye alijikuta katika nchi iliyokuwa ingali huru ya Israeli. Kwa hiyo chanzo cha jibu la mlinzi huyo kilikuwa katika nchi ya Israeli, hata iwe Waisraeli walijikuta wapi wakati wa kutimizwa kwa unabii wa Isaya. Wakati wa kutoa unabii huo Isaya aliwakilisha mlinzi aliyewekwa kwa amri ya Mungu ili atoe majibu sahihi kwa maulizo. Isaya na watoto wake walikuwa wamekubaliwa na Mungu. Basi, kwa kufaa sana, Isaya alifananisha jamii ya “mlinzi” wa leo, mabaki ya Waisraeli wa kiroho walio na urithi wa kimbinguni. Wao ndio ambao wamepewa maarifa kwa habari ya hali yenye giza ya ulimwengu leo.

12. (a) Katika mwaka 1879 W.K., ni nani waliojitoa watumikie kama kikundi cha mlinzi kwa ajili ya jamii kubwa zaidi ya “mlinzi”? (b) Jibu la ulizo lililokuwa likitokea wakati huo lilipaswa kutoka wapi, nalo lilikuwa nini?

12 Katika mwaka 1879 W.K., mhariri wa gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) pamoja na washiriki wake walikuwa wamejiweka wakf kabisa, Wakristo waliobatizwa. Walijitoa kutumikia kama kikundi cha mlinzi kwa ajili ya ndugu zao Wakristo waliozaliwa kwa roho. Wote pamoja wakawa jamii kubwa zaidi ya “mlinzi.” Wasingeweza kuepa ulizo lililokuwa linatokea wakati huo, “Ee mlinzi, habari gani za usiku? ” Jibu peke yake lenye kuaminika ambalo wangeweza kutoa ni lile ambalo Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho liliweka kwenye kinywa cha mlinzi wa kale. Jibu hilo lilikuwa, “Asubuhi yaja, nao usiku pia.” (Isa. 21:​12,AV) E, ndiyo, kulingana na maono yaliyotolewa na Yehova Mungu, kipindi chenye uangavu zaidi, “asubuhi,” ilikuwa imekuja. Hiyo ingeingiza mileani, au miaka elfu, ya utawala wa Masihi wa Yehova, Mwanawe Yesu aliyetukuzwa. Walakini kabla ya hilo ulipaswa kuja “usiku” wa taabu ya ulimwengu!

13. (a) Mfululizo wa vitabu Studies in the Scriptures vilivyoanzwa kuchapwa katika mwaka 1886 viliitawaje, na kwa sababu gani? (b) Sababu gani mwenye kutaka kujua katika Seiri alihangaikia “usiku” uliokuwa umepata nchi hiyo?

13 Bila shaka, kwa sababu ya “asubuhi” iliyoahidiwa ambayo ingeleta utawala wa mileani wa Kristo, mfululizo wa vitabu Studies in the Scriptures ambavyo mhariri wa Mnara wa Mlinzi alianza kuchapa katika mwaka 1886 viliitwa “Kupambazuka kwa Mileani” (Kiingereza). Na chini ya kichwa hicho maneno ya Mithali 4:​18, AV, yalitajwa: “Kijia cha Mwenye Haki ni kama Mwangaza Unaong’aa, Unaong’aa Zaidi na Zaidi Mpaka Mchana Mkamilifu.” Walakini mwenye kuuliza katika nchi ya Seiri alikuwa anahangaikia “usiku.” Katika siku za nabii Isaya giza lo lote la “usiku” ambalo lilikuwa juu ya nchi ya.Edomu ya Seiri lilikuwa karibu kuongezeka. Ingekuwa hivyo kwa kuwa nchi hiyo ingekuja chini ya utawala wa mshindi mwingine wa ulimwengu, mwenye kupendelea, si Waedomu wa Mlima Seiri, bali, mahali pake, taifa lililo ndugu la Israeli.

14. Ni nani leo aliye na jibu linalofaa la ulizo juu ya “usiku” uliopo ulimwenguni pote, nako kutaka kujua zaidi juu yake kunakatazwa?

14 Leo, zaidi ya karne moja baada ya gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) kutokea mara ya kwanza, watu wa ulimwengu wanaopapasa-papasa ili kupata mwangaza wanaendelea kutokeza ulizo lenye uharaka, “Habari gani za usiku? ” Mmoja tu aliye na jibu lenye maana la ulizo hilo ni jamii ya “mlinzi.” Jamii hiyo haijashindwa kupata jibu linalofaa, jibu la Biblia. Imekaribisha maulizo yote mengine, kama ambavyo katika unabii wa Isaya mlinzi alivyoendelea kusema hivi: “Mkitaka kuuliza, ulizeni; njoni tena.”​—⁠Isa. 21:2

15. Kwa sababu ya kukaribisha maulizo zaidi, gazeti Mnara wa Mlinzi limejiendeshaje, nalo limeendelea kutangaza bila kukatiza ujumbe gani unaohusu “usiku”?

15 Ili kutimiza jambo hilo gazeti Mnara wa Mlinzi limeendelea kuchapwa mpaka sasa. Kama vile mlinzi wa halisi anavyopaswa kuwa macho wakati wote anapokuwa katika mahali pake pa kulinda, ndivyo gazeti Mnara wa Mlinzi limeendelea kuwa macho nalo halijakosa kuchapwa toleo moja tangu toleo lake la kwanza Julai ya mwaka 1879. Hiyo imekuwa hivyo yajapokuwa mateso ya ulimwenguni pote juu ya jamii ya “mlinzi” wakati wa Vita vya Ulimwengu vya Kwanza na Pili. Limeripoti juu ya kuendelea kwa “usiku,” pasipo kuogopa kutangaza kwamba utafikia sehemu yake yenye giza zaidi Kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” ambayo unabii wa Biblia huiita ­Har–​Magedoni. Hivyo jamii ya “mlinzi” iliyotiwa mafuta inaendelea kutimiza mgawo wake wa “kutangaza . . . siku ya kisasi cha Mungu wetu.”​—⁠Ufu. 16:​14-16; Isa. 61:​1, 2.

TANGAZO BAADA YA KUWEKWA KWA MLINZI

16. Sababu gani ilihitaji ujasiri kwa “mlinzi” kutangaza ‘tangazo’ lililowekwa kinywani mwake, na sababu gani tangazo hilo linatuvutia sana leo?

16 “Mlinzi” wa Mungu anapaswa kuwa na ujasiri na kuwa mwaminifu ili kutangaza yale yanayowekwa kinywani mwake, kutangazia wote wanaoweza kusikia. Tangazo hilo halikuwa zuri, bali lilikuwa baya kwa ambayo ingekuwa mamlaka ya ulimwengu yenye nguvu zaidi kufikia wakati huo. Walakini lilionyesha mema kwa watu waliokuwa wa mlinzi huyo, taifa la Israeli, wakati wa matukio yenye kutikisa ulimwengu ya nyakati hizo za kale. Jambo hilo lisingekuwa lenye kuvutia sana kwetu sisi watu wa kisasa, kama isingekuwa uhakika wa kwamba mambo yanayotajwa katika ‘tangazo’ hilo kali yanatimizwa kwa kadiri kubwa na kwa mara ya mwisho juu ya ulimwengu wote wakati wa karne yetu yenye kusumbuliwa na vita. Kwa hiyo hatuna budi kupatwa na matokeo yake kama vile Isaya wakati mrefu uliopita.

17, 18. Usemi ‘jangwa la bahari’ ulihusu nini, nazo ni mamlaka gani zenye nguvu zilizotawala katika sehemu hiyo?

17 Mwanzo wenyewe wa ujumbe ulioongozwa na Mungu uliopewa kupitia kwa Isaya unatia wasiwasi: “[Tangazo] juu ya [jangwa la] bahari. Kama tufani za [kusini] zikaribiavyo kwa kasi, inakuja kutoka [jangwani], toka nchi itishayo.” ​—⁠Isa. 21:1.

18 Sehemu inayomaanishwa na usemi ‘jangwa la bahari’ ilipata kuwa na maana kwa ulimwengu wote katika historia ya kibinadamu. Sehemu hiyo ni nchi yenye mto unaoingia baharini unaojigawanya sehemu mbili ukifanyiza Mto Frati na Mto Tigri, au mto Hidekeli, mito yote miwili hiyo ikiwa inatajwa kuhusiana na kuumbwa kwa Adamu, mwanamume wa kwanza. (Mwa. 2:14) Wakati mmoja mito yote miwili ilimwaga maji yake kila mmoja ukiwa peke yake katika sehemu inayoitwa leo Guba la Uajemi, mito yote miwili ikiwa inakaribiana inapoyamwaga maji yake. Wakati wa mafuriko, wakati mito hiyo ilipokuwa ikifurika kingoni zake, sehemu zilizo chini katikati zilikuwa zinakuwa kama bahari iliyo ukiwa, ‘jangwa la bahari.’ Matokeo yake yalikuwa sehemu za nchi zenye matope. Mamlaka ya pili ya ulimwengu ya historia ya Biblia, Ashuru, ilikuwa ikitawala juu ya sehemu hiyo katika siku za nabii Isaya. Katika karne iliyofuata, mamlaka hiyo ingefuatwa na mamlaka yenye nguvu zaidi, ya tatu.

19. Mamlaka ya Tatu ya Ulimwengu ingeletea watu wa Isaya jambo gani, nalo jambo hilo linapendeza nani kwa njia ya pekee leo?

19 Hiyo Mamlaka ya Tatu ya Ulimwengu ndiyo ingeletea watu wa Isaya majonzi mengi. Ni jambo la kawaida kwamba yale ambayo yangeipata yalikuwa yenye kumvutia sana Isaya mwenyewe kama mlinzi, vilevile kwa ye yote yule ambaye angekuwa akitumikia kama mlinzi wakati wa utimizo wa ‘tangazo lote juu ya jangwa la bahari.’ Ndiyo sababu utimizo wake leo wa mwisho ni wenye kuvutia jamii ya “mlinzi” ya leo na wote wale wanaotaka kujua wapate kuongozwa na yale yanayo-onwa na jamii ya “mlinzi.”

20. Kisababishaji cha msiba unaokuja kinafananishwa na nini, nayo nguvu yenye kuharibu inasemekana kuwa inatoka wapi?

20 Kitu kisichozuilika na chenye nguvu nyingi ‘kama tufani za kusini’ kilikuwa kinaonekana kwa njia yenye kuogopesha kikiwa kule-e kwenye upeo wa macho. Tufani hizo zilikuwa zenye nguvu sana na zenye kuharibu sana. Vitu vilivyotengenezwa na wanadamu vinavyokuwa katika njia ya tufani zenye kusonga mbele vinaelekea hatari ya kufutiliwa mbali. Sehemu yenye kuogopesha ya msiba unaokaribia inaonyeshwa na uhakika wa kwamba msiba huo unasemekana kuwa ‘unatoka bara, toka nchi itishayo.’ (Isa. 21:1) Kule nyuma nabii Isaya akiwa kama mtu mwenye kuweka maandishi ya hali ya hewa alitoa ishara ya kuonya ili kuwajulisha watu waliokuwa katika njia ya tufani hiyo wajitayarishe kukabili mabaya yote yale.

21. Katika karne yetu, ishara ya kuonya imetolewa na nani, nao ni akina nani wamefanywa kuwa na daraka kwa kupewa onyo?

21 Kwa kufanana na hilo, ishara ya kuonya imetolewa na jamii ya “mlinzi,” sana sana tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza katika mwaka 1918. Gazeti Mnara wa Mlinzi limeokoka vitisho vya kulifutilia mbali wakati wa kipindi hicho chenye hatari wakati jamii ya “mlinzi” ilipoteseka vikali sana ulimwenguni pote. “Mlinzi” huyo pamoja na chombo chake, gazeti Mnara wa Mlinzi, ameendelea kuishi ili kusikizisha onyo zaidi ambalo limesikilika katika sehemu zote za dunia. Watu, sana sana viongozi wao, wameonywa. Ndio wenye daraka!

22. Ni tangazo gani litakalosemwa kwa sauti kuu hivi karibuni, nao “mkutano mkubwa” utakuwa wenye furaha wakati huo kwa sababu gani?

22 Tangazo lenye kugutusha litasemwa kwa sauti kuu hivi karibuni na jamii ya “mlinzi.” Kwa kushangaza, wakati litakaposemwa kwa sauti kuu, wenye furaha utakuwa ule “mkutano mkubwa” wa pekee uliotii mara moja ishara yenye kuonya.​—⁠Ufu. 7:​9-15.

[Sanduku/Ramani katika kurasa za 8, 9]

“Usiku” utafikia sehemu yake yenye giza zaidi kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika ­Har–​Magedoni

Mlinzi mwenye kusimama juu ya mnara wa mlinzi katika Israeli anafananisha jamii ya mlinzi ya Israeli wa kiroho. Wakiwa mashahidi wa kisasa wa Yehova, wao wanatangaza kwamba “asubuhi” ya utawala wa mileani wa Kristo karibuni utaufuata “usiku” wa taabu ya ulimwengu

Unyamavu utaipata Duma ya kidini, ambayo kutoka kwayo kilio hiki kilitoka, “Ee mlinzi, habari gani za usiku? ”

Hayo “maono magumu” yanaonyesha kuanguka kwa Babeli, ambako kulitangulia kuonyesha kuanguka kwa kiroho kwa Babeli Mkuu katika mwaka 1919 na uharibifu wa mwisho wa milki hii ya ulimwengu ya dini ya uongo muda mfupi kabla ya ­Har–​Magedoni

Dario wa Umedi anamfananisha Yehova Mungu

Koreshi wa Uajemi anamfananisha Mwana wa Mungu, Kristo Yesu

‘Tangazo’ kali la Mungu linatolewa juu ya ‘jangwa la bahari,’ iliyotawalwa kwa zamu na Ashuru na Babeli

[Ramani]

(Ona nakala iliyochapishwa)

UMEDI

UAJEMI

ELAMU

BABELI

Babeli

EDOMU

Duma

ISRAELI

Yerusalemu

Bahari ya Kati

[Picha katika ukurasa wa 8]

1879 Watchtower

1895 Watchtower

1938 Watchtower

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki