‘Ni Neno Jema Kama Nini Wakati Ufaao!’
“NENO linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!” akapaza sauti mwandikaji wa mithali ya Biblia. (Mit. 15:23) Na hiyo ni kweli kama nini!
Katika nchi fulani ya mashariki ya Ulaya, Mashahidi wa Yehova wawili walikuwa wakitembea kwa miguu katika bustani ya maua siku moja wakaanzisha mazungumzo na mwanamume kijana aliyekuwa akitembea humo akiwa na mtoto wake. Jambo hilo likaongoza kwenye mwaliko kwenye nyumba ya mmojawapo wa Mashahidi hao. Humo nyumbani, mwanamume huyo pamoja na mke wake wakafahamishwa ujumbe wa Biblia. Mwishowe, mwanamume huyo kijana na mke wake pamoja na mama ya mwanamume huyo waliikubali kweli ya Neno la Mungu.
Jambo lenye kupendeza ni kwamba, katika siku hiyo alipokutana na Mashahidi hao wawili kwa mara ya kwanza, mwanamume huyo kijana alikuwa ametua kanisani humo bustanini akaomba hivi: ‘Mungu, ikiwa wewe uko, tafadhali acha nikujue.’ Kwa muda wa miaka mitatu, mwanamume huyo alikuwa amekuwa akitembea katika bustani hiyo. Walakini katika siku iyo hiyo akakutana na mashahidi hao wawili wa Yehova. Ni vema kama nini kwamba walitamani sana kuieneza “habari njema”! Mwanamume huyo kijana aliona hilo kuwa jibu la Mungu kwa sala yake.