Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 6/15 kur. 11-17
  • Kushiriki Katika Kazi Takatifu ya Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushiriki Katika Kazi Takatifu ya Habari Njema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “KAZI TAKATIFU YA HABARI NJEMA”
  • JE! HIYO NI NJIA YENYE MATOKEO YA KUTOA USHUHUDA?
  • KAZI AMBAYO MUNGU ANABARIKI
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kwa Nini Huduma ya Nyumba kwa Nyumba Ni ya Maana Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je! Wewe Unayo Roho ya Kueneza Injili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Fundisha Peupe Na Kutoka Nyumba Kwa Nyumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 6/15 kur. 11-17

Kushiriki Katika Kazi Takatifu ya Habari Njema

“Nilipewa fadhili zisizostahilika na Mungu ili niwe mtumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa, mwenye kushiriki katika kazi takatifu ya habari njema.”—Rum. 15:15, 16, NW.

1, 2. Sababu gani usemi na mwenendo wetu ni mambo ya maana?

MSINGI wa sifa ambayo mtu anapata ni utendaji na usemi wake. Wengine wanakata kauli juu yake mara nyingi ikitegemea yale wanayoona akifanya na wanayosikia akisema. Mfalme Sulemani aliandika hivi: “Hata mutoto anajijulisha kwa njia ya matendo yake, kama kazi yake ni safi, na kama ni ya haki.”—Mit. 20:11, Zaire Swahili Bible; Mt. 7:16-20.

2 Hiyo inamaanisha nini kwako iwapo wewe ni Mkristo? Je! si wengine wanapaswa kuona kutokana na mwenendo na usemi wetu kwamba tunamtumikia Mungu wa kweli, Yehova? Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu ni mtakatifu na safi, kwamba kanuni zake ni za haki nazo zinatokeza mema. (Isa. 6:3; Ayubu 34:10; Kum. 32:4) Ikiwa tunakubali namna alivyo Mungu, jambo hilo linapasa kuwa wazi maishani mwetu.—Efe. 5:1.

3, 4. (a) Matokeo ya ibada na historia ya Israeli yalikuwa nini? (b) Kunapaswa kuwa na matokeo gani juu ya wengine wanaochunguza Ukristo?

3 Kwa kuwa ibada ya kweli inaonyeshwa wazi katika maisha ya kibinadamu, watu wengine wanaweza kufaidika. Kwa mfano, kwa wakati fulani Yehova alishughulikia Israeli sana sana. Yeye aliwaambia hivi: “Inawapasa mjithibitishe wenyewe kuwa watakatifu, kwa sababu mimi Yehova Mungu wenu ni mtakatifu.” (Law. 19:2, NW; linganisha Kutoka 19:5, 6.) Sheria za chakula, usafi na adili ambazo Mungu alipatia Israeli zilisadia kuwalinda na mazoea mengi yenye kuchafua yaliyokuwa ya kawaida katika mataifa jirani. Wageni wengi waliona namna njia ya ibada ya kweli ilivyokuwa ikifanikiwa na namna Mungu alivyokuwa akiongoza na kulinda Israeli. Jambo hilo liliwavutia, na likawachochea wengi wamwabudu Yehova.—1 Fal. 8:41, 42; 10:1; Ruthu 1:16.

4 Matokeo ayo hayo mazuri yanakuja wakati Wakristo wa kweli wanapoongoza maisha yao kupatana na maongozi ya Mungu. Maisha yaliyogeuzwa na ‘mwendo mwema’ wa Wakristo yanawasukuma wenye kushuhudia ‘wamtukuze Mungu.’ (1 Pet. 2:12, 15; 3:1, 2; Tito 2:7, 8;1 The. 4:11, 12) Walakini Biblia inaonyesha wazi kwamba mkazo wa Ukristo si kuishi tu maisha safi ya adili na kusitawisha utu bora unaoonyesha “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23; Efe. 4:22-24) Ingawa sehemu hizo za Ukristo ni za maana, kungali kazi ya pekee ya kufanya iwapo ye yote atakuwa mfuasi wa kweli wa Yesu.

“KAZI TAKATIFU YA HABARI NJEMA”

5. (a) Mfano wa Yesu unaonyesha ni jambo gani jingine la maana kwetu? (b) Sababu gani utendaji huu ni wa maana?

5 Akiwa kivulana na baadaye akiwa mwanamume mkamilifu, Yesu alimheshimu Baba yake wa kimbinguni. Maisha yake na utu wake ulikuwa mfano bora kwa wengine, ukiwasukuma watazamaji wengi wamtukuze Mungu. (Luka 2:49, 52) Mara tu alipobatizwa Yesu ‘alianza kazi yake,’ akijikaza alipokuwa akienda huku na huku ‘akihubiri habari njema ya ufalme.’ (Luka 3:23; Mt. 4:17, 23) Hata alizoeza wengine washiriki katika kazi hiyo, akiwatuma wakafundishe watu. (Luka 10:1, 8, 9) Hapo kwanza kazi hiyo ya kufundisha na kufanya wanafunzi ilikuwa ikifanywa kati ya Wayahudi tu. Walakini baadaye ingepanuliwa, maana, kama ambavyo mtume Paulo alieleza katika Warumi 15:8, 9, mapenzi ya Mungu yalikuwa kwamba watu wote wa dunia wasaidiwe wapate kumtukuza.

6, 7. Mtume Paulo alifanya “kazi takatifu” gani?

6 Paulo mwenyewe alifanya kazi kutimiza jambo hilo. Katika Warumi 15:16 NW, alijiita mwenyewe “mtumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa.” ‘Utumishi’ huo ulitia nini ndani? Yeye aliongeza kwamba alikuwa “mwenye kushiriki katika kazi takatifu ya habari njema za Mungu, ili kwamba toleo hilo, yaani, mataifa hayo, yapate kukubalika.” Hiyo maana yake nini?

7 Katika Warumi 15:16, NW ndipo tu panapotumika kiarifa cha Kigiriki (heirourgounta) katika Biblia kinachomaanisha ‘kufanya kazi au kushiriki katika jambo takatifu.’a Kwa hiyo Paulo alikuwa anasema kwamba alikuwa anashiriki katika kazi takatifu ya kuhubiri habari njema za Mungu, ujumbe wa Kikristo, kwa watu wa mataifa. Wale waliokubali ujumbe huo na kuwa Wakristo walikuwa kama toleo kwa Mungu, toleo ambalo Yehova alikubali na kubariki kwa roho yake.—Rum. 1:1, 16, NW.

8. Paulo aliifanyaje kazi hiyo kati ya Wayahudi?

8 Paulo na wengine waliifanyaje hii “kazi takatifu ya habari njema za Mungu,” kuhubiri ujumbe wa Kikristo? “Habari njema” zingeweza kuokoa maisha, basi ingefaa wafikie watu wengi kwa kadiri ambayo ingewezekana. Nyakati nyingine Paulo, mwenyewe akiwa Myahudi, alihutubia Wayahudi waliokusanyika katika masinagogi. (Matendo 13:14-42; 14:1; 18:4) Lakini je! yeye na Wakristo wengine wangeweza kufikia “mataifa” mengi, wale wasio Wayahudi?

9. Wakristo wa kwanza wangeweza kutumia njia zipi ili kusaidia wasiokuwa Wayahudi?

9 Wakristo waliweza kuzungumza na watu katika mahali pa watu wote, kama vile sokoni. (Matendo 17:17-22) Hata hivyo kufanya hayo kusingeweza kufikia watu wote. Namna gani kwenda kwenye nyumba za watu, kama ambavyo wanafunzi wa Yesu walifanya alipowatuma wakahubiri katika miji mbalimbali? (Mt. 10:5-13; Luka 19:2-6) Wakristo wa kwanza walitumia njia hiyo pia, walipokuwa ‘wakishiriki katika kazi hiyo takatifu’ ya kueneza Ukristo kwa watu wote wakiwa na shauku.

10. Kuna ushuhuda gani kwamba kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kulifanywa ili kuwafikia na kuwasaidia wasioamini?

10 Twaweza kuona jambo hilo kutokana na maelezo ambayo Paulo alitoa kwa wanaume ambao walikuwa wamekuwa wazee katika kundi la Efeso. Akizungumza juu ya kuhubiri kwake kwa wakati uliopita, alipowaletea Ukristo, Paulo alisema hivi: Sikujiepusha kuwaambia ninyi lo lote la mambo yaliyokuwa yenye faida wala kuwafundisha waziwazi na nyumba kwa nyumba. Lakini nilitoa ushuhuda kikamilifu kwa wote Wayahudi na Wagiriki [au, Mataifa] juu ya toba kwa Mungu na kumwamini Bwana yetu Yesu.” (Matendo 20:20, 21, NW)b Kwa wazi, hapa Paulo alikuwa anazungumza juu ya jitihada zake za kuhubiri watu hao wakati walipokuwa hawajaamini, watu wenye uhitaji wa toba na kumwamini Yesu. Paulo alikwenda kwenye nyumba za watu hao wasioamini. Hakuwa na sababu ya kusita kuwahubiri wageni hao, maana alikuwa anafanya “kazi takatifu” ambayo Mungu aliikubali na ambayo angeibariki.

11. (a) Wakristo wanaifanyaje hiyo “kazi takatifu”? (b) Sababu gani kushiriki katika kuhubiri nyumba kwa nyumba ni kwa maana?

11 Vilevile, katika nyakati za kisasa Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakitoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kama njia kuu ya kuwafikia watu na kuhubiri kweli ya Mungu. Bila shaka, kila Mkristo anayeona wajibu wake na pendeleo la kutangaza “habari njema” atatumia kila nafasi inayofaa kutoa ushuhuda—kwa watu wa ukoo, wanashule wenzake na wafanya kazi wenzake katika mazungumzo ya vivi hivi. Kwa hiyo, hata katika nchi ambazo kuteswa kiwazimu na vikundi vya kidini au polisi kunafanya isiwezekane au liwe si jambo la akili kutoa ushuhda waziwazi nyumba kwa nyumba, Wakristo wanaendelea kufanya yote wawezayo kutoa ushuhuda katika njia nyinginezo. Hata hivyo, katika sehemu zote zisizokuwa na magumu hayo, Mashahidi wa Yehova hutembelea kila nyumba kwa utaratibu. Hiyo inatokeza ‘kutoa ushuhuda kikamilifu’ na kufikia watu wengi ambao kama sivyo wasingeweza kukutana na Wakristo wa kweli na kusikia “habari njema.”—Matendo 4:19, 20; 20:21, NW; linganisha Ezekieli 9:3, 4.

JE! HIYO NI NJIA YENYE MATOKEO YA KUTOA USHUHUDA?

12-14. Ni nini kinachoonyesha kwamba kuhubiri nyumba kwa nyumba kunaweza kuwa na matokeo?

12 Walakini je! njia hiyo ya kueneza Injili ingali yenye matokeo katika “kushiriki katika kazi takatifu ya habari njema”? Ushuhuda unasema wazi hivi, NDIYO! Katika mwaka 1977 jarida Social Compass lilichapa makala “Mashahidi wa Yehova katika Japan,” iliyoandikwa na mtaalamu wa ujamii wa watu, Bryan Wilson. Aliandika kwamba ‘wanaelekeza akili zao katika kazi ya kueneza Injili peke yake kuliko dini yo yote mpya’ katika Japan. Vilevile, aliongoza uchunguzi uliofunua yafuatayo:

“Wengi [58.3%] wa wale ambao wamekuwa Mashahidi wanasema kwamba kupendezwa kwao kwa kwanza kuliamshwa na ziara ya nyumbani” iliyofanywa na mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

13 Hata wanadini wanaokataa kukubali mafundisho yenye msingi wa Biblia yanayoenezwa na Mashahidi wa Yehova wanakubali kueneza Injili nyumba kwa nyumba kunakofanywa na Mashahidi ni kwenye matokeo sana. Twasoma hivi:

‘Pengine [makanisa] wanapuza sana ile ambayo ndiyo kazi kubwa ya Mashahidi—ziara ya nyumbani, njia ya kimtume ya kanisa la kwanza. Ingawa makanisa, pindi nyingi, yanahubiri katika mahali pao pa kukutania, [Mashahidi ] wanafuata njia ya kimtume ya kwenda nyumba kwa nyumba.’—“El Catholicismo,” Bogota, Colombia, Sept. 14, 1975.

“Wakatoliki wanapaswa kufuata mfano wa Mashahidi wa Yehova katika kueneza Injili, washiriki wa Mkutano wa kwanza wa Taifa juu ya Kueneza Injili waliambiwa.’​—Minneapolis “Tribune,” Ago. 29, 1977.

14 Kueneza Injili nyumba kwa nyumba kunafanywa na Mashahidi wa Yehova peke yao hata kwamba katika nchi nyingi mwenye nyumba anafungua mlango na kusema, “O, bila shaka wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova.” Hata ikiwa hakuna lo lote limezungumzwa kutoka katika Biblia, mema yamefanywa. Kwa njia hiyo fikira zimekazwa juu ya jina takatifu la Mungu, ambalo linastahili kutakaswa. Naye mwenye nyumba amekaziwa kwamba watumishi wa Mungu walikuwapo wakiwa na ujumbe Wake. (Mt. 6:9; Isa. 12:4; Eze. 33:6-9, 29) Walakini, kama ambavyo maneno yaliyotajwa juu yanavyoonyesha, wakati mwingi kunakuwa na matokeo zaidi.

15. Kazi hiyo yenye matokeo imefanywaje katika sehemu fulani ambako kuna vizuizi?

15 Kutolea watu ushuhuda nyumbani kunafaa sana na ni kwenye matokeo sana katika kufikia watu hata kwamba jitihada nyingi ya kushiriki inafanywa na Mashahidi chini ya magumu. Ndivyo ilivyokuwa katika nchi moja ya Afrika ambako wenye mamlaka walipiga marufuku utendaji huo wenye msingi wa Biblia. Wakristo wa mahali hapo walijua kwamba njia hiyo ya kueneza Injili ni yenye thamani, kwamba wanapaswa ‘kumtii Mungu kuliko mwanadamu’ na kwamba wanapaswa kufuata shauri la Yesu wawe “na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.” (Matendo 5:29, NW; Mt. 10:16, 17) Wangepaswa kufanyaje?

Waliweza kupanga mambo ili wachache kati yao wagawanye barabara ndefu au eneo kwa kulingana na namba za nyumba. Mmoja alichukua nyumba zote zenye kumalizika na 2 (2, 12, 22, 32, n.k.) naye alikuwa akizitembelea kwa utaratibu aliotaka, wakati wo wote akiweza. Mwingine alichukua nyumba zenye kumalizika na 3 (3, 13, n.k.) naye alitembelea nyumba hizo siku tofauti. Kwa njia hiyo ushuhuda wa kikamilifu ungeweza kutolewa.

Njia tofauti za kufikia watu zinaweza kutumiwa, pia. Mkristo mmoja anaweza kuwa na kikapu chenye mayai au matunda, na kumwuzia mwenye nyumba, lakini kwa bei ya juu kuliko sokoni. Wachache wananunua, walakini mazungumzo mengi yanaanzishwa juu ya bei zilizo juu, magumu ya maisha leo na kisha, ikifaa, utimizo wa unabii wa Biblia.

“Au, Mkristo anayetaka kununua mboga anaweza kutumia njia hii ili afikie watu katika “eneo” lake. Kabla ya kwenda sokoni anaweza kutembelea nyumba zenye shamba, akiuliza kama anaweza kununua mboga hizo. Anunue ama asinunue, mara nyingi mazungumzo yanawezekana pamoja na matumizi ya mawazo ya Biblia.

Katika njia hizo Wakristo wa mahali hapo waliepuka kusumbuliwa na wafanya ghasia wa kisiasa ambao hapo mbeleni walikuwa wamesumbua wale wenye kuhubiri nyumba kwa nyumba. Vilevile, ushuhuda wa kikamilifu ulitolewa kwenye ujamii huo.

16. Ni marekebisho gani mengine yanayoweza kufanywa ili Mashahidi waendelee kuwa na matokeo katika njia hiyo ya kuhubiri?

16 Huenda rekebisho tofauti likahitajiwa mahali pengine. Pengine katika miaka iliyopita lilikuwa jambo la kawaida kutembelea nyumba wakati wa asubuhi, wakati wenye nyumba wengi wanakuwa nyumbani. Walakini hali zikibadilika na wengi wao sasa wanakuwa kazini, je! hiyo inamaanisha njia hiyo ya kuhubiri haifai? La, maana ni kwa njia gani nyingine—katika kila nyumba—watafikiwa na kupewa nafasi ya kufaidika kutokana na “habari njema”? Huenda ikafaa kufanya ziara hizo wakati wa alasiri au mapema jioni, wakati washiriki wa jamaa wanapokuwa nyumbani. Lengo ni kufikia na kusaidia watu, wengi iwezekanavyo.—Linganisha Matendo 16:13.

17. Tukikumbuka mfano wa Paulo, sisi binafsi tunawezaje kufanya marekebisho tunapoendelea kufanya kazi hiyo?

17 Mtume Paulo alikuwa na nia ya kurekebisha njia na namna ya kufikia watu ili ifae wasikilizaji wake. Yeye alisema: “Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.” (1 Kor. 9:19-23) Kujirekebisha vivyo hivyo kwaweza kusaidia leo. Vipi, kwa mfano, ikiwa unaishi katika eneo ambalo watu wengi wameacha kupendezwa na dini na Biblia? Je! unaweza kurekebisha namna unavyowafikia?

Shahidi mmoja katika Ubelgiji anasimulia hivi: ‘Ninakuwa na Biblia mkononi ikiwa imefunguliwa walakini siitaji mara moja. Ninasema, “Nilipokuwa nikikungojea uje mlangoni nilikuwa nikitazama jambo ambalo limeandikwa hapa . . . ‘Heri wenye upole; maana hao watairithi nchi.’ [Mt. 5:5] Je! unadhani kungali na watu wapole kati yetu?” Sikuzote mazungumzo huanza na baadaye Biblia inakubaliwa kwa urahisi.’

KAZI AMBAYO MUNGU ANABARIKI

18. Tuna sababu gani za kujulisha kwamba Mungu anapendezwa na ‘‘kazi takatifu ya habari njema”?

18 Wakristo duniani pote wanapendezwa sana na “kazi takatifu ya habari njema.” Ndivyo na Yehova Mungu. Paulo alisema kwamba Wakristo wapya waliotokezwa na kushiriki kwake katika kazi hiyo walikuwa kama toleo lenye kukubalika kwa Mungu, aliyemwaga roho yake juu yao.—Rum. 15:16.

19. Kazi hiyo inawezaje kuwa na matokeo hata wengi wasiposikiliza?

19 Kibali na baraka ya Mungu inaendelea kuwa juu ya kazi hii ya kuhubiri, kutia ndani utendaji wa maana wa nyumba kwa nyumba wa kutafuta na kusaidia watu. Mfano mmoja ni huu, mhudumu mmoja anayetembelea makundi katika wilaya kubwa alikubali mwaliko wa kwenda pamoja na Mkristo mmoja huko Maryland kwenye ziara ya kuongoza funzo la Biblia. Anasema hivi:

“Nilimwuliza mwenye nyumba kilichomchochea ajifunze Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Alisema kwamba mara nyingi alikuwa anafungua Biblia mahali po pote, na kuelekeza kidole kwenye mstari mmoja na kuusoma. Walakini mara nyingi hakuelewa aliyosoma.

“Siku moja alikuwa ameshuka moyo sana kwa ajili ya matatizo makubwa ya jamaa. Kwa mara nyingine akafungua Biblia na kuchukua mstari mmoja. Hakuweza kuufahamu, naye akiwa ameshuka moyo na kukata tamaa akaanza kulia. Alimwomba Mungu atume mtu kwake ili amsaidie kufahamu Neno lake. Mara tu aliposema hivyo, kengele ya mlango ikapigwa. Alipofungua akakuta ni Shahidi, aliyeanza kwa kusema, ‘Ungependa kuifahamu Biblia? ’ Mwenye nyumba huyo akamwingiza ndani haraka na upesi funzo la kawaida likaanza.”

20-23. Kwaweza kuwa na baraka gani kwa sababu ya kuongeza kushiriki katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba?

20 Matokeo mazuri yanaweza kuwapo hata inapoonekana kwamba wengi wanaofikiwa wanakataa “habari njema” wanazoletewa.

Tineja (kijana) mmoja alikuwa akitembea mlango kwa mlango katika kijiji cha mashambani huko Afrika Kusini alasiri ya Jumamosi moja. Alipata kupendezwa kidogo sana, maana tengenezo moja la kidini katika ujirani huo lilikuwa limetokeza chuki nyingi juu ya jitihada za kusaidia za Kikristo za Mashahidi wa Yehova. Mlango baada mlango ukafungwa haraka-haraka akiwa amesimama hapo. Ikaonekana kuwa kazi bure.

Walakini bila kujua, macho yenye kutaka kujua yalikuwa yakimtazama kutoka dirishani ng’ambo nyingine ya barabara. Mwanamke mmoja mzee aliona uvumilivu wa Shahidi huyo yajapokuwa maitikio yenye uadui. Kwa wazi Mkristo huyo alikuwa tofauti na vijana wengine.

Nyumba yake ilipofikiwa mwanamke huyo mzee alimwalika ndani Shahidi huyo. Ingawa msichana huyo sana sana alizungumza Kiingereza naye mwanamke Kiafrikaani, waliweza kuzungumza juu ya ujumbe wa maana wa Biblia kwa wakati wetu. Baadaye mhudumu mwenye kuzungumza Kiafrikaani akatembelea mwanamke huyo mwenye kupendezwa, naye mwanamke huyo mzee kwa furaha akakubali awe na funzo la Neno la Mungu la kawaida.

21 Kweli kweli, baraka ya Mungu juu ya “kazi takatifu ya habari njema” inaonekana katika njia mbalimbali. Mhudumu mmoja mwenye kusafiri anayetembelea makundi katika eneo la New Orleans, Louisiana, aliandika hivi: “Roho ya kueneza Injili inakuwa na nguvu zaidi. Makundi nane au tisa ya mwisho ambayo tumetembelea yamekuwa yakitumia wakati zaidi katika utendaji wa kuhubiri. Kukiwa ongezeko hilo la jitihada, watu wengi wenye kupendezwa na ‘habari njema’ wanafikiwa. Na kwa kuwa akina ndugu na dada wanashughulika zaidi kutangaza ‘habari njema,’ roho ya amani na furaha inaonekana wazi kweli kweli katika makundi hayo.”

22 Amani na furaha hiyo inaongezeka pia katika maisha ya mtu binafsi na ya jamaa za Wakristo wale wanaohubiri kwa bidii “habari njema” na kuona baraka za Mungu. Jamani, kutakuwako matatizo fulani na mahangaiko maishani. Twajua kwamba yote hayo yatakuwako maadamu hatujakamilika na maadamu taratibu hii mbovu ya mambo inaendelea. Walakini kwa kadiri Mkristo anavyoshughulika na “kazi takatifu ya kuhubiri habari njema” ambayo imeamriwa na Mungu ndivyo maisha yatakavyokuwa yenye kutosheleza zaidi, yenye baraka zaidi, yenye furaha zaidi. (Matendo 20:35) Hilo si wazo tu. Inatokea hivyo. Ilikuwa hivyo kwa mtume Paulo. Inakuwa hivyo kwa mamilioni ya Mashahidi wa Yehova leo. Itakuwa hivyo kwako.

23 Vilevile, wengine wataweza kuona wewe ni Mkristo wa namna gani. Wataona ukishiriki katika kazi ya kutangaza “habari njema.” Wataona furaha na amani ambayo inaletwa maishani mwako na utendaji huo pamoja na utendaji mwingine. Wataona njia nyingi ambazo katika hizo unaonyesha utu wa Kikristo na “tunda la roho.” (Efe. 4:24; Gal. 5:22, 23) Ndiyo, utawaonyesha wengine wengi kwamba unamtumikia Mungu mtakatifu kwa kufanikiwa.

24. Kwa kushiriki kikamilifu katika kazi hiyo unaweza kuonaje?

24 Baada ya maelezo ya Paulo juu ya “kushiriki katika kazi takatifu ya habari njema,” aliongeza hivi: “Kwa hiyo nina sababu ya kushangilia katika Kristo Yesu inapokuwa ni mambo yanayohusu Mungu.” (Rum. 15:17, NW) Acheni sisi sote tukiwa Wakristo tufanye kazi ili sisi, pia, tuweze kushangilia katika Kristo Yesu.

—Kutoka The Watchtower—Jan. 1, 1981.

[Maelezo ya Chini]

a Watafsiri wengine wametafsiri hierourgounta kuwa “kutenda kama kuhani,’ au kwa usemi kama huo. Linganisha Luka 1:8 ambapo kiarifa kinachohusiana na hayo kinatumiwa kwa habari ya Zekaria, baba ya Yohana Mbatizaji.

b Tafsiri ya kwanza ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika lugha nyingine kwa wazi ilikuwa katika lugha ya Kishami. Mwalimu wa chuo kikuu James Murdock anatafsiri hivi kutoka Kishami: “Sikuepuka yale yaliyofaa nafsi zenu, ili niwahubiri, na kufundisha barabarani na nyumbani, wakati uo huo nikishuhudia Wayahudi na Mataifa.”

[Picha katika ukurasa wa 14]

‘Kazi kubwa zaidi’ zilianza siku ya Pentekoste

[Picha katika ukurasa wa 15]

Leo ‘kazi kubwa zaidi’ zinafanywa na Mashahidi duniani pote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki