Hatari za Tumbako kwa Afya Zafichwa
Katika barua iliyochapwa katika “Jarida la Shirika la Kiamerika la Utibabu” (la Kiingereza), Dakt. Elizabeth M. Whelan aliandika hivi: “Kwa sababu magazeti mengi yapendwayo na watu wengi yanategemea sana mapato yao kutokana na utangazaji wa sigara, yanaficha matokeo mabaya ya tumbako kwa afya ya watu. Baada ya kuchunguza hesabu ya magazeti kadha makuu ya wanawake, sikupata hata hadithi moja yenye habari za maana juu ya tumbako na afya.”
Dakt. Whelan alieleza kwamba yeye aliombwa aandike makala yenye kichwa “Mlinde na Kansa Mwanamume Umpendaye” itumiwe katika gazeti la wanawake linalosomwa sana lenye habari za urembo na mitindo ya kujipamba. Yeye anasema, “Nililipwa pesa kamili kwa sababu ya kipande cha habari nilizoandika lakini mhariri akanieleza wazi kwamba wangeweza kutumia kisehemu tu cha habari hizo kwa sababu mimi nilitaja-taja sana tumbako na kwamba wao walikuwa wakiandika kila mwezi matangazo ya kurasa tata kamili yenye kutia watu moyo waitumie. Nyakati nyingine, nimeambiwa kwa ujasiri na mhariri wa gazeti fulani, ‘hatutaki safu za habari au hadithi zenye kueleza mambo ya tumbako.’”—Novemba 7, 1980, ukurasa wa 2045.