Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 5/1 kur. 7-11
  • Jinsi Siku Ilivyo Katika Maisha ya Misionari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Siku Ilivyo Katika Maisha ya Misionari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUSUDI LETU TUKIWA MISIONARI
  • KAWAIDA YETU YA KILA SIKU
  • MSAADA WA KUTOSHA
  • SIKU YA KUPIKA
  • MAZINGIRA YA KIJAMAA YA KWELI
  • JE! INASTAHILISHA?
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Bidii ya Umisionari—Alama ya Wakristo wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • ‘Mkono wa Yehova Ulikuwa Pamoja Nao’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Wahudumu wa Wakati Wote Wanaiongoza Kazi
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 5/1 kur. 7-11

Jinsi Siku Ilivyo Katika Maisha ya Misionari

“HIYO ilikuwa kengele ya saa 12:30?”

“Pengine ilikuwa kengele ya saa 12:55 na tuna dakika tano peke yake za kwenda kwenye meza ya kiamsha-kinywa. Hapana, starehe, bado ni saa 12:30. Kungali na wakati mwingi wa kutosha.”

Hayo ni mazungumzo ya mapema asubuhi kati yangu na yule tunayekaa naye chumbani. Tungali tunaona saa 12:30 ni mapema sana kuamka, hata ingawa tumekuwa tukifanya hivyo kwa miaka mingi. Tukiwa Mashahidi wa Yehova wanaoishi katika makao ya misionari hapa katika Taipei, Taiwan, tunakusanyika pamoja na misionari wenzetu kwa ajili ya mazungumzo ya kiroho yanayotangulia kiamsha-kinywa saa moja.

Washiriki mbalimbali wa “jamaa” yetu wanapeana zamu kupika, kununua vitu sokoni, kusafisha nyumba na kazi nyinginezo. Hiyo inatia kupiga kengele zinazotusaidia kujitayarisha kwa ajili ya chakula na utendaji mwingine.

KUSUDI LETU TUKIWA MISIONARI

Unaposikia neno “misionari,” huenda ukapiga picha akilini mwako ya mwuguzi aliyevaa vazi jeupe, au mwalimu akifundisha darasa la watoto katika kijiji fulani kilicho peke yake. Walakini huo sio mgawo ambao Yesu aliwapa wafuasi wake. Yeye aliwaagiza wafanye wanafunzi. (Mt. 28:19, 20, NW) Hivyo, kama ilivyo kwa Mashahidi wa Yehova kila mahali, kazi yetu kuu ni ile ya kufundisha watu kweli za Biblia, katika mgawo wetu wa umisionari wa ugenini.

Tukiwa misionari, tunatumia angaa saa 140 kila mwezi katika utendaji wa kuhubiri na kufundisha. Ili kuwapata wale wanaopenda kujifunza zaidi juu ya Neno la Mungu, tunatumia karibu nusu ya wakati huo tukifanya ziara za nyumba kwa nyumba, tukiwa na mazungumzo ya Biblia pamoja na watu milangoni pao. Kisha tunautumia wakati huo uliobaki tukiwatembelea tena wale waliotangulia kuonyesha kupendezwa fulani na ujumbe wa Ufalme, tukiongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani bila malipo pamoja na watu mmoja mmoja na jamaa zinazotaka kujifunza zaidi. Kwa kufuata njia ya utaratibu ya kujifunza inayotumiwa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, tunaona inawezekana kuwasaidia Wabuddha na wengine, ambao hapo mbeleni pengine hawakujua lo lote juu ya Biblia, wajifunze mafundisho yake ya msingi. Jambo hilo laweza kuchukua tangu miezi sita mpaka mwaka mmoja, walakini wakiisha kupata ufahamu huo, watu wanakuwa katika hali bora ya kuamua kama wangependa kuwa mashahidi Wakristo wa Yehova au la.

KAWAIDA YETU YA KILA SIKU

Mkazo katika maisha yetu ni mambo ya kiroho. Ndiyo sababu mazungumzo yetu ya Kimaandiko yanakuwa mapema sana asubuhi katika lugha ya Kichina cha Mandarin, ambayo ndiyo lugha rasmi ya Taiwan. Mazungumzo hayo yanaifanya siku yetu ianze kwa njia yenye kuchangamsha na yenye kutia imani. Nyakati nyingine vilevile yanachekesha, kama wakati ambapo misionari mmoja mpya zaidi alipofadhaishwa na kicheko cha wengine alipokuwa akitoa maelezo juu ya andiko fulani la Biblia. Yeye hakuona jambo lo lote la kuchekesha katika usemi wake kwamba Yesu ndiye Kuhani Mkuu wetu. Yeye alidhani alisema hivyo. Oo-o, kosa dogo lilikuwa limebadili elezo lake liwe usemi kwamba Yesu ndiye kuku wetu mkuu!

Baada ya kiamsha-kinywa, dakika 15 zinatumiwa katika kujizoeza kutumia maneno na semi mpya za Kichina. Kila juma tunajaribu kujifunza 20. Kila asubuhi zinaandikwa juu ya ubao, dada Mchina anayeishi nyumbani mwetu anajaribu kwa uhodari kusahihisha usemi wetu. Sisi tunathamini msaada wake wa kurekebisha mwundo wa sentensi zetu na matamshi yetu (kutia namna ya milio katika Kichina), kwa maana jitihada zake zinatusaidia tuwe wenye matokeo zaidi katika kufundisha Neno la Mungu.

Kisha tunaondoka baada ya sala na kujitayarisha kwa ajili ya utendaji wetu wa siku. Kila misionari wawaili wana kisehemu cha mji cha kukazia jitihada zao. Tunajaribu kuwapata watu wenye kupendezwa na polepole tunasitawisha kikundi cha wasifaji wa Yehova ambacho huenda hatimaye kikawa kiini cha kundi jipya la Mashahidi wa Yehova.

Kazi ya kutoa ushuhuda hapa inaendeshwa hapa sana kama ilivyo katika mahali penginepo ulimwenguni. Hata hivyo, kuna tofauti fulani. Tofauti moja ni jinsi tunavyofika kwenye eneo letu. Ninakumbuka vizuri sana kwamba wazo langu la kwanza juu ya nchi za Mashariki lilikuwa kwamba zimejawa sana na watu, watu wengi, wengi. Mwenzi wangu nami tunatembea kwa bas kwenda na kutoka katika eneo. Bas zenyewe ni nyingi lakini sikuzote zimesongamana watu. Wakati wa saa zenye watu wengi zaidi, lazima ulione jambo hilo ili uamini! Sasa tumezoea kufanya harara kuingia na kushuka katika bas. Hata hivyo, mpaka tulipozoea lilikuwa jambo la kawaida kukuta kwamba mifuko yetu ya vitabu ilikuwa bado ndani ya bas nyuma ya milango iliyofungwa nasi tukiwa barabarani, tukiwa tunashikilia bas kiwazimu! Misionari wengi kidogo wanapendelea kutumia pikipiki ndogo au skuta, kwa kuwa hizo ni njia za kusafiria zinazofaa na zenye kuokoa fedha.

Kama ilivyo na sehemu kubwa ya ulimwengu katika siku hizi, watu wanashukiana zaidi na zaidi. Walakini urafiki wa kidesturi wa Wachina unaonyeshwa mara nyingi tunapotembea milangoni. Tungali tunaliona kuwa jambo la kawaida kualikwa ndani na kupewa kiti, pamoja na chai au maji yaliyo moto sana hata tunalazimika kurefusha mazungumzo yetu mpaka yawe baridi kutosha kuweza kunywa! Katika Taiwan ni jambo la kawaida kwa watu ambao wanapendezwa kidogo na Biblia kuchukua vitabu vyetu. Kwa hiyo, tunaweza kuacha vitabu vingi katika nyumba, na vitabu hivyo vyaweza kusomwa na watu wanaopendezwa hata zaidi ya wale waliotusikiliza hapo kwanza.

Tunapofanya ziara za kurudia kwa watu, tunakuta kwamba wengi, kutia wale wenye imani ya Kibuddha au wengine wanaofuata falsafa (filosofia) ya Confucius, wana nia ya kuwa na mazungumzo zaidi na hata wanakubali mafunzo ya Biblia ya kawaida ya kila juma. Kwa hiyo kwa kawaida naweza kuongoza mafunzo ya Biblia 10 au zaidi kila juma, kipimo hicho kikiwa kinawekwa na wakati niliyo nao kwa ajili ya utendaji huo. Wengi wa watu hao wanahudhuria mikutano yetu tangu mwanzo kabisa, hata kwamba asilimia 20 kufika 50 ya watu wapo zaidi ya Mashahidi waliopo katika eneo hilo.

MSAADA WA KUTOSHA

Tukiwa misionari tunaangaliwa vizuri sana. Sosaiti inatambua kwamba misionari wanaoishi katika nchi ya ugenini hawawezi kujiangalia wenyewe kwa urahisi kama ambavyo pengine wangeweza katika nchi zao za nyumbani. Kwa kweli, katika nchi nyingi, serikali zinaweka sharti la kwamba misionari hawawezi kufanya kazi za kimwili. Kwa hiyo, tunapewa misaada ya mahitaji yetu ya kimwili. Sisi hatupokei mishahara (malipo), bali Sosaiti ama inakodisha au kununua makao yanayofaa kikundi cha misionari watakaokuwa wakifanya kazi katika mji. Katika visa vingi katika Taiwan, hiyo inamaanisha kwamba kati ya watu wanne mpaka wanane watakaa katika makao ya misionari. Hata hivyo, kwa kuwa mwenzi wangu nami tunaishi kwenye makao ya misionari ambayo pia ndiyo afisi ya tawi ya Sosaiti, tuna watu 18 wanaoishi hapa.

Fedha zinatolewa ili kuwezesha misionari wanunue chakula na kulipa kodi ya nyumba, matumizi, na kadhalika. Pamoja na hayo, tunapokea alawansi ndogo ya kibinafsi inayotuwezesha kununua vitu vinavyohitajiwa maishani mwetu. Katika Taiwan alawansi hiyo inapungua kidogo shilingi 100 kila mwezi. Vilevile tunapokea alawansi ya kusaidia kulipia gharama zetu za kusafiri, na Sosaiti inatoa malipo ya pekee ya kadiri ya kutusaidia kununua nguo tunazohitaji, kulipia safari zetu za kwenda kwenye makusanyiko na mambo kama hayo. Kwa hiyo tunashukuru sana kwamba hatulazimiki kuhangaikia mambo ya kimwili bali tunaweza kutumia wakati wetu na kukaza fikira zote kwenye kutimiza mradi wetu tukiwa misionari.

Tukiwa tunajua kwamba misaada yote hiyo inapatikana kupitia michango ya upendo ya waamini wenzetu wasioweza kushiriki moja kwa moja katika utumishi wa umisionari wa ugenini, tunajitahidi kuonyesha kuthamini kwetu katika njia mbili za msingi. Kwanza, tunajaribu kufanya utumishi wetu wa umisionari uwe wenye matokeo kwa kadiri iwezekanavyo. Pili, tunaziona fedha hizo kuwa ni za Bwana na kwa hiyo tunajaribu kuzitumia kwa hekima. Siku ya kupika inatoa nafasi ya kufanya hivyo.

SIKU YA KUPIKA

Kila mtu ana migawo yake ya kutayarisha chakula katika siku fulani​—siku ya kupika, ndivyo tunavyoiita.

Baada ya kiamsha-kinywa na baada ya vyombo kusafishwa, tunakwenda sokoni. Wakati wa asubuhi, masoko mawili yaliyo karibu na nyumbani mwetu yamejaa kwa wingi mboga, nyama, samaki na matunda. Wauzaji Wachina wanapenda kupiga bei, na jambo hilo laweza kufurahisha, wakati ule ule likiwa linaokoa fedha. Tumekwisha kuwa wataalamu wanaojua kiasi tunachopaswa kulipa na katika kununua vitu ambavyo vinapatikana katika majira mbalimbali, hivyo tunaweza kutumia kwa hekima kiasi kile cha fedha za makao tulichopewa wakati wa siku ya kupika.

Tumepata mboga nyingi na matunda pia ambayo hatukuwa tumeona hapo mbele. Kama ilivyo, tulijihadhari kununua hivyo kwa sababu hatukujua namna ya kuvipika. Walakini, usiogope. Ukiisha kuuliza mwuzaji anapendezwa kukuambia namna yeye anavyopika kitu hicho. Kwa. hiyo tumeweza kufurahia mboga hizo mpya kama majani ya viazi vitamu na kijiti kidogo cha chanikiwiti chenye pembe nne na kichipuo kidogo juu pamoja na harufu kama ya kitunguu saumu kisicho kikali sana. Kwa kujifunza kutumia chakula cha mahali hapa, tunakula vizuri na wakati huo huo hatuharibu yo yote ya misaada ya Bwana.

Mazingira na harufu ya sokoni inatofautiana na ile ambayo tulikuwa tumezoea katika nchi nyingine kwa sababu ya kuku walio hai, samaki walio hai, nguruwe na ng’ombe waliochinjwa karibuni na mboga zote mbichi juu ya meza zisizofunikwa. Kwa mfano, ilitaka kujiweza kwingi sana upande wangu kuzuia kilio kilichokuwa kooni mwangu mara ya kwanza nilipomwona mwuzaji mmoja akichukua kisu na kukata koo ya kuku aliyekuwa amechaguliwa kwa jitihada nyingi na mtu mwenye kutaka kumnunua!

Pamoja na soko lote kwa ujumla, ni jambo la kawaida kuona barabara na vijia vikiwa karibu kuzuiwa kabisa na vionyesho vya nguo, nguo za vitambaa vya kushonea nguo na vitu vingine vidogo-vidogo vya kuuzwa. Tusiporuhusu utafiti (kutaka kujua) wetu utushinde, tunaweza kununua haraka haraka na kurudi nyumbani tuanze kutayarisha chakula cha mchana, ambacho nyumbani mwetu ndicho chakula kikubwa kwa siku. Jioni mtu anakula chakula cha jioni wakati wo wote anapokuja, kwa kuwa hiyo inaruhusu kubadilikana katika orodha ya wale wote wanaoongoza mafunzo ya Biblia nyakati za alasiri na jioni. Vilevile katika siku zetu za kupika hiyo inatoa wakati wa kufanya kazi ya nyumbani na kusafisha mavazi ya kibinafsi na kujitayarisha kwa utendaji wetu wakati wa siku saba zitakazofuata.

MAZINGIRA YA KIJAMAA YA KWELI

Ingawa jamaa yetu ni kubwa zaidi ya jamaa nyingi za misionari katika Taiwan, tuna mazingira ya kijamaa kweli kweli, Kwa mfano, tuna funzo letu wenyewe la jamaa usiku wa Jumatatu. Kwanza tunatumia saa moja tukijifunza Biblia kwa msaada wa Mnara wa Mlinzi. Kisha tunajifunza kisehemu cha kimojawapo cha vitabu vya karibuni vya Sosaiti, ili kwamba, ingawa hatuna baadhi ya vitabu hivyo katika Kichina, tungali tunaweza kufuatana na habari zote za karibuni. Kwenye meza yetu ya kiamsha-kinywa tunasoma yaliyoonwa na ripoti kutoka Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova na habari kutoka Utumishi Wetu wa Ufalme (Kichina) ambao tutakuwa tukiuzungumza kwenye mkutano wa kundi wakati wa juma hiyo. Pindi kwa pindi, tunakuwa na vikusanyiko vya vivi hivi au tunakwenda kwenye pikiniki tukiwa kikundi. Hayo yote yanatufanya tuwe kama jamaa.

JE! INASTAHILISHA?

Wasomaji wengine huenda wakaona kwamba kujitahidi kujifunza lugha mpya kungeweza kufanya maisha ya misionari yawe mzigo zaidi ya kuwa yenye kustahilisha. Walakini mimi sioni hivyo, ingawa kujifunza Kichina hakukuwa jambo rahisi kwangu. Kwa mfano, kujua kwamba kuna uhitaji mkubwa wa kutangaza “habari njema” katika eneo letu sikuzote kunanichochea. Hata ingawa hesabu ya Mashahidi katika Taipei imeongezeka mara tatu katika wakati ambao nimekuwa huko, hatuwezi kulieneza eneo letu hata mara moja kwa mwaka! Wakati kwa wakati, wale wenye njaa ya haki wanautambua mlio wa kweli, hata inapozungumzwa na misionari mwenye uwezo mdogo wa kusema lugha. Ebu fikiria mfano huu, uliofurahiwa na mmoja wa misionari wenzangu miaka michache iliyopita.

Alikuwa amekuwa Taiwan kwa miezi mitatu tu na alikuwa angali anajifunza Kichina alipomkuta mwanafunzi mchanga wa chuo kikuu aliyekuwa ametoka katika jamaa ya Wabuddha. Maisha ya msichana huyo yalikuwa yamejawa na mambo mengi ya kusikitisha, kutia vifo vya washiriki wawili wa jamaa. Alikuwa amekwenda kwenye baadhi ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo akiwa anajitahidi kupata faraja, lakini bila kufanikiwa, naye alishuku kwamba misionari huyo mpya angeweza kumsaidia.

Tangu mwanzo, mwanamke huyo kijana alivutiwa na namna misionari huyo alivyoweza kutumia Biblia kujibu maulizo yake, kijapokuwa kizuizi chake cha kuweza kusema lugha. Upesi akaanza kuhudhuria mikutano na kufanya maendeleo ya haraka. Baada ya miezi minane ya funzo la Biblia, alikuwa mwenye furaha kuwa shahidi wa Yehova aliyejiweka wakf na kubatizwa. Kwa miaka kadha mwanamke huyo alitumikia kila mwezi akiwa painia msaidizi, na kutumia saa 60 kila mwezi kwenye kazi ya kuuhubiri Ufalme, hata ingawa alikuwa ameajiriwa akiwa mwalimu wa shule mwenye kufundisha wakati wote. Sasa amekwisha kuacha kazi hiyo na akawa mshiriki wa jamaa ya Betheli ya Taipei. Mambo yaliyoonwa mengine mengi kama hilo yanaweza kusimuliwa kuonyesha kwamba kweli kweli inastahilisha kuwa misionari katika shamba la ugenini.

Kila mtu mwenye moyo mnyofu anafurahia kushiriki mambo mazuri pamoja na wengine, na hilo ndilo linalowasukuma Mashahidi wa Yehova wawe wenye bidii katika kazi yao ya kuhubiri na kufundisha, hata wajikute wapi. Walakini ninathamini sana pendeleo la kutumikia katika nchi ambayo mamilioni wangali hawajaiona Biblia. Kuna furaha kama nini kuwasaidia wengine wapate maarifa ya tumaini la ajabu ambalo limeandikwa katika Neno la Mungu! Ingawa sisi misionari hatupati mshahara (malipo), tuna zawadi bora sana. Baadhi ya zawadi hizo ni uhusiano wa karibu pamoja na watu wengi wa nchi za Mashariki ambao wameacha ibada ya bure ya sanamu na kuanza kumwabudu Mungu aliye hai Yehova, kwa sababu ya kazi ya juhudi ya misionari kutoka nchi nyingine. Sisi binafsi tumepata baraka kubwa zinazoletwa na kumtumikia Yehova na tengenezo lake linaloonekana tunapojitoa kwa utumishi wa umisionari wa ugenini.

Kwa hiyo, kwa kweli, ingawa mimi pamoja na yule tunayekaa naye chumba kimoja hatuamki mapema kwa sababu tunapendelea hivyo, tunafurahi kwamba mtu fulani hupiga kengele saa 12:30 kila asubuhi. Tukifanya hivyo tunaianza siku mapema, siku ambayo tunajua itajawa na utendaji wa umisionari wenye kupendeza na unaostahilisha.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Lugha tunayofunzwa mapema asubuhi tunaitumia baadaye katika utumishi wa Ufalme

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki