Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 4/1 kur. 16-23
  • “Msimamizi wa Nyumba” Huyo Anapoikabili Har–Magedoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Msimamizi wa Nyumba” Huyo Anapoikabili Har–Magedoni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MADARAKA YA USIMAMIZI WA NYUMBA
  • Mafundisho Kuhusu Kukosa Uaminifu
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Kutumia Mamlaka Vibaya Humfanya Mtu Apoteze Mapendeleo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • “Kwa Kweli ni Nani Yule Msimamizi wa Nyumba Mwaminifu Mwenye Akili?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Wajua?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 4/1 kur. 16-23

“Msimamizi wa Nyumba” Huyo Anapoikabili Har–Magedoni

1. Ni nini kitakachotokea kwenye Har–Magedoni ambacho jamii ya yule “msimamizi wa nyumba” inakabili sasa, na “msimamizi wa nyumba” huyo alifananishwa na nani katika siku za Mfalme Hezekia wa Yerusalemu?

HAR-MAGEDONI ni jina la Kiebrania la mahali ambapo “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” itapiganwa hivi karibuni. Mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” sasa yanaikabili “vita” hiyo ambayo kwayo mfumo huu wa mambo wa kilimwengu utakomeshwa milele. Kwa hiyo jamii ya “msimamizi wa nyumba” inaendelea kukesha kiroho ili ione namna bwana huyo aliyerudi, Yesu Kristo aliyetukuzwa, atakavyowaharibu adui wanaoonekana wa Ufalme huo ambao juu yake wanamwomba Yehova Mungu hivi: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mt. 6:9, 10; Ufu. 16:14-16) Hali hiyo ya mambo ya ulimwenguni pote ilifananishwa au ilitabiriwa na yale yaliyotukia wakati wa usimamizi wa Mwisraeli yule ambaye Mfalme Sedekia wa Yerusalemu alimfanya awe msimamizi wa nyumba wake wa kifalme wakati wa hatari sana.

2. Myahudi huyo alikuwa nani, naye alikuwa amechukua mahali pa nani katika usimamizi wa nyumba wa kifalme, kulingana na Isaya 22:15-25?

2 “Msimamizi wa nyumba” huyo alikuwa Myahudi ambaye jina lake aliitwa Eliakimu mwana wa Hilkia. Mara tatu anatajwa kuwa mtu yule “aliyekuwa msimamizi wa nyumba” ya Mfalme Hezekia. (Isa. 36:3, 22; 37:2) Yeye alikuwa amechukua mahali pa mtu aliyeitwa jina lake Shebna katika cheo hicho cha kifalme. Amri ya Mungu kwa Eliakimu na Sheba imeandikwa katika Isaya 22:15-25. Hapo twasoma hivi:

‘‘Bwana [Yehova] wa majeshi, asema hivi, Haya! enenda kwa huyu mtunza hazina, yaani, Shebna, aliye juu ya nyumba, ukamwambie, Unafanyaje hapa? nawe una nani hapa? hata ukachimba kaburi hapa; ukamchimbia kaburi huko juu, na kumchongea makao katika jabali! Tazama,[Yehova] atakutupa kwa nguvu, kama mtu mwenye nguvu; naam, atakuzonga-zonga. Hakika atakukunja na kukutupa kama mpira, mpaka nchi iliyo mbali; huko utakufa, na magari ya utukufu wako yatakuwa kuko huko, ewe uliye aibu ya nyumba ya bwana wako. Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo.a

Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nyumba ya Yuda. Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua. Nami nitamkaza kama msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake. Nao wataangika juu yake utukufu wote wa nyumba ya baba yake; wazao wake na watoto wao, kila chombo kidogo tangu vyombo vya vikombe hata vyombo vya makopo vyote pia.

Katika siku ile asema [Yehova] wa majeshi, ule msumari uliokazwa katika mahali palipo imara utalegea; nao utakatwa na kuanguka chini, na ule mzigo uliokuwa juu yake utakatiliwa mbali; maana [Yehova] amesema haya.”

3. (a) Jina Eliakimu linamaanisha nini, na maana yalo ilitimizwaje kwa habari ya mwenye jina hilo? (b) Ni nani waliotumwa wakasikilize kemeo la kukufuru mbele ya kuta za Yerusalemu, na mwishowe ni nani aliyeombwa msaada?

3 Kwa kupatana na jina lake, “Mungu huinua,” Yehova alimkweza Eliakimu awe mwenye usimamizi wa nyumba kwenye makao ya kifalme ya Mfalme Hezekia. Jambo hilo lilitokea kabla mtawala wa Ashuru, Senakeribu, hajaizingira nchi ya Yuda katika mwaka 732 K.W.K. Senakeribu aliweka jeshi lake kwenye kambi umbali fulani kutoka Yerusalemu na kisha akamtuma msemaji wake, Rabshake, pamoja na mlinzi, asimame mbele ya Yerusalemu na kudai ukubali kushindwa. Alipokuwa akifanya hivyo, Rabshake alimshusha Yehova akiwa Mungu na kukuza Ashuru na mtawala wake. Mfalme wa Yerusalemu, Hezekia, aliwapeleka wawakilishi wasikilize kemeo hilo lenye kumkaidi Mungu, kutia Eliakimu, ambaye sasa alikuwa msimamizi wa nyumba, na pia Shebna, ambaye alikuwa ameshushwa cheo akawa mwandishi, na Yoa, mtunza maandishi. Wakiwa wamehuzunishwa sana na yale waliyoyasikia, walitoa ripoti kwa Mfalme Hezekia. Akiwa anajiona hoi kabisa, mfalme huyo alimwomba msaada nabii Isaya, mwakilishi wa Yehova.​—Isa. 36:1–37:7.

4. Katika utimizo wa kisasa wa matukio hayo ya kale, Senakeribu anafananisha nani, Hezekia anafananisha nani, na Eliakimu anafananisha nani?

4 Hapo twaona hali zile zile zilizoko katika hali yenye hatari ya leo. Kwa kulinganisha Senakeribu mfalme wa Ashuru anafananisha adui ya ufalme wa Mungu, yaani, Shetani Ibilisi,b ambaye anadai watu wa Yehova walio tengenezo wakubali kushindwa wakiwa chini ya maumivu ya utumwa au uharibifu. Mfalme aliyetiwa mafuta Hezekia, ambaye jina lake linamaanisha “Yah ametia nguvu,” anafananisha Mfalme anayetawala sasa, Yesu Kristo ambaye anahisi (anaona) sana taabu ya wanafunzi wake washikamanifu duniani wanapopatwa na masuto na kukabili tisho la uharibifu mkononi mwa tengenezo la Ibilisi. Eliakimu, yule “msimamizi” wa nyumba ya Mfalme Hezekia, anafananisha mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” ambao wangali duniani wakati wa huu “umalizio wa mfumo wa mambo” tangu mwaka 1914 W.K. Kama vile msimamizi wa halisi Eliakimu alivyokuwa Myahudi au Mwisraeli, mabaki wa leo wanajumuishwa kuwa Waisraeli wa kiroho wakiwa chini ya uongozi wa Mfalme Yesu Kristo anayetawala.

5. Kwa kuendelea kueneza gazeti Mnara wa Mlinzi ulimwenguni pote, wale wa mabaki waliotiwa mafuta walijishirikisha na nani, na ni wakati gani walipokana majina yote ya kuwasuta waliyobandikwa?

5 Katika wakati huu ulioendelea sana washiriki wenye kupungua wa mabaki waliotiwa mafuta wangali wanaeneza ulimwenguni pote, na katika lugha nyingi, gazeti Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Kujitambulisha huko kwa pekee kuwa ni wa Yehova Mungu ndiyo matokeo ya kufaa ya kusonga kwa matukio ya kitheokrasi ya karne ya 20. Ndiyo, kwa maana katika mwaka wenye kukumbukwa wa 1931 maelfu mengi ya mabaki waliotiwa mafuta walikusanyika katika kusanyiko kuu katika Columbus, Ohio, na huko, katika Julai 26, kwa umoja walipitisha azimio ambalo katika hilo walitwaa jina “mashahidi wa Yehova” kwa ruhusa ya Biblia. Kwa njia hiyo walikana majina yote ya kusuta ambayo kwayo mifumo ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo iliwabandika na kuwaita hao wanafunzi wa Biblia wa shirika la mataifa yote. Baada ya muda mfupi makundi yote ya Waisraeli wa kiroho duniani pote kwa umoja yalikubali jina hilo.

6. Kwa kuchukua jina la Mungu kwa njia hiyo, wao kwa moyo wa kupenda walichukua nini juu yao?

6 Hivyo walichukua madaraka yanayotolewa katika maneno yaliyosemwa kwa Waisraeli wa siku za nabii Isaya:

“‘Ninyi ni mashahidi wangu, ndio usemi wa Yehova, ‘hata mtumishi wangu ambaye nimemchagua, ili mjue na kuwa na imani kwangu mimi, na ili mfahamu kwamba mimi ni Yule Yule. . . . Kwa hiyo ninyi ni mashahidi wangu,’ ndio usemi wa Yehova, ‘nami ni Mungu.’”​—Isa. 43:10-12, NW.

MADARAKA YA USIMAMIZI WA NYUMBA

7. (a) Wanadini wenye kudai ni wenye usimamizi wa nyumba kabla ya kumalizika kwa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza mwaka 1918 walishindwaje kulistahili dai lao? (b) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walijithibitishaje kuwa kama Shebna?

7 Kama Shebna katika serikali ya Mfalme Nebukadreza wakati wa Isaya, kuna viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wanaodai kuwa wana haki yote ya kuwa na usimamizi wa nyumba duniani chini ya uongozi wa Hezekia Mkuu Zaidi, Yesu Kristo. Walakini tofauti na viongozi wa kidini, washiriki waaminifu wa mabaki watiwa mafuta wa Mashahidi wa Yehova wamejitahidi sana kutimiza kikweli usimamizi wa nyumba wa Ufalme. Kwa kutokeza imekuwa hivyo tangu kumalizika kwa vita ya ulimwengu ya kwanza iliyoanza ndani ya Jumuiya ya Wakristo. Kufikia wakati huo viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo waliokuwa wakieneza vita walikuwa wametokeza maandishi yasiyofutika kuhusu usimamizi wanaodai kuwa waliupokea kutoka kwa Mfalme Yesu Kristo. Hata kufikia wakati huo ushuhuda ulikuwa mwingi ukionyesha kwamba “majira ya Mataifa” au “nyakati zilizowekwa za mataifa” zilikuwa zimekwisha katika vuli ya mwaka 1914. Ndiyo, vilevile, kwamba wakati huo Yesu Kristo aliyetukuzwa alikuwa ameanza kutawala mbinguni akiwa Hezekia Mkuu Zaidi. (Eze. 21:25-27; Luka 21:24, Union Version; New World Translation) Walakini Je! viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walijitokeza waunge mkono ufalme wa Yehova uliosimamishwa kupitia Kristo? Hapana!

8. Baada ya ule Ushirika kushindwa, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walichukua tendo gani tofauti na lile la mabaki ya Waisraeli wa kiroho?

8 Katika mwaka 1919 viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walijitoa watumikie kama wasimamizi wa nyumba, wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukikusudiwa. Walakini Ushirika huo ulishindwa kabisa mwaka 1939. Sasa umekwisha kufuatiwa na shirika lililoundwa upya la kulinda amani, Umoja wa Mataifa. Tofauti kabisa na viongozi hao wa kidini, mabaki ya Waisraeli wa kiroho wanaendelea kuunga mkono ufalme wa Mungu uliosimamishwa kupitia Kristo.

9. Kulingana na mambo ya hakika ya kihistoria, jibu la kisasa la ulizo la Yesu katika Luka 12:42 ni nini?

9 Kwa hiyo, tangu mwanzo wa hukumu ya kimungu katika mwaka 1918, ni nani wamepewa usimamizi wa nyumba au waliothibitishwa ndio wenye usimamizi huu? Mambo ya hakika ya kihistoria tangu mwaka 1918, ambayo yanajisemea yenyewe, yanajibu: Mabaki waliotiwa mafuta wa Waisraeli wa kiroho. Wao wakiwa jamii ndio jibu la ulizo la Yesu mwenyewe, “Kwa kweli ni nani yule msimamizi wa nyumba mwaminifu, mwenye akili, ambaye bwana yake atamweka juu ya baraza yote ya watumishi wake ili aendelee kuwapa kipimo chao cha chakula kwa wakati unaofaa?” (Luka 12:42, NW) Wao wanajumuishwa kuwa Eliakimu Mkuu Zaidi wa leo. Yaani, wao ndio jamii ya “msimamizi wa nyumba” iliyofananishwa na Eliakimu mwaminifu na mwenye akili wakati wa utawala wa Mfalme Hezekia (745-716 K.W.K.), wakati wa shambulio la Ashuru katika nchi ya Yuda.

10. Kulingana na unabii wa Yesu wa Luka 12 : 43, 44, huyo mtumishi “msimamizi wa nyumba,” ambaye anafananisha mabaki ya Waisraeli wa kiroho, angefanywaje kuwa mwenye “furaha”?

10 Zijapokuwa ole juu ya Jumuiya ya Wakristo na sehemu nyingine ya ulimwengu wa wanadamu, mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” mwaminifu, hakika, ni wenye “furaha” kama Yesu mwenyewe alivyotabiri, kwa kusema hivi: “Mwenye furaha ni mtumwa huyo, iwapo bwana yake anaporudi atamkuta akifanya hivyo!” Kwa sababu gani? Kwa ajili ya uhakika wa kwamba, kama Yesu alivyoendelea kusema, “Mimi nawaambia kikweli, Yeye atamweka juu ya vitu vyake vyote.”​—Luka 12:43, 44, NW.

11. Kulingana na Isaya 22:20, 21, Yehova alisemaje kwamba mahali pa Shebna pangechukuliwa na mwingine?

11 Kwa njia ya kiroho imetokea kwa mabaki waaminifu wa Waisraeli wa kiroho kama ilivyotokea kwa Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alichukua mahali pa Shebna mwenye kujitukuza mwenyewe akawa “msimamizi wa nyumba” juu ya nyumba ya Mfalme Hezekia. Kama Yehova alivyomwambia nabii wake Isaya: “Na itakuwa katika siku ile [ya Yehova kumwondoa Shebna katika cheo chake] nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako [Shebna], nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nyumba ya Yuda.”​—Isa. 22:20, 21.

12. Hayo yalilingana na tendo gani lililofanywa na Yesu Kristo tangu masika ya mwaka 1919?

12 Hayo yanalingana na kuwekwa na Yesu kwa jamii ya “msimamizi wa nyumba” mwaminifu na mwenye akili juu ya vitu vyake vyote vya Ufalme. Sana-sana tangu masika ya mwaka uliofuata baada ya vita wa 1919 tukio jipya lilifunuka katika historia ya kidini. Wakati huo ndipo, kama Eliakimu, mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” mwaminifu na mwenye akili walipovishwa heshima ya kuwa mabalozi wa ufalme wa Yehova Mungu uliosimamishwa kupitia Kristo. (2 Kor. 5:20) Wakiwa katika cheo hicho wametangaza ufalme huo uliosimamishwa “katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14, NW; Marko 13:10) Kwa kusema kwa njia ya mfano, Mungu Mwenye Nguvu Zote amewafunga viuno ili waitimize huduma yao nzito kwa kuwafunga “mshipi” wa msimamizi wa nyumba au majordomo (Kiebrania, so·khenʹ; Septuagint ya Kigiriki oikonómos).​—Linganisha Zekaria 3:1-7.

13. Wale wanaojumuishwa kuwa “msimamizi wa nyumba” mwenye washiriki wengi walitoka katika Babeli Mkuu wakati gani, na “mamlaka” ya “msimamizi wa nyumba” huyo yamezidishwa kufika kwa nani?

13 Kwa kutokeza tangu masika ya mwaka 1919, Yehova Mungu ametoa mwito wake kwa watu wake wote waliojiweka wakf watoke katika “Babeli Mkuu,” milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. (Ufu. 18:2, 4) Wale wanaojumuishwa kuwa jamii ya “msimamizi wa nyumba” kwa kutii walitoka, na Bwana yao wa kimbinguni, Bwana Yesu Kristo aliyepo pasipo kuonekana, amewatumia kama jamii ili wawape wale wote watakaoupokea ufalme wa kimbinguni “kipimo chao cha chakula kwa wakati unaofaa.” Kwa habari hiyo jamii ya Eliakimu imekuwa “baba” anayewaruzuku wale wote wanaofananishwa na “wenyeji wa Yerusalemu, na . . . nyumba ya Yuda.” Yehova kupitia Kristo ameipa jamii hiyo ya “msimamizi wa nyumba” “mamlaka,” na huyo “msimamizi wa nyumba” mwenye washiriki wengi ametumia kwa uaminifu na kwa akili “mamlaka” hiyo mpaka sasa. Sana-sana tangu mwaka 1935 ndipo “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo wamefaidika na utunzaji huo kama wa baba, kama “mgeni [aliyekuwa] ndani ya malango” ya Yerusalemu wa kale.​—Kut. 20:10; Yohana 10:16; Ufu. 7:9-17.

14. “Msimamizi wa nyumba” hiyo alitekelezaje daraka lake kama inavyofananishwa na Eliakimu akichukua daraka la “ufunguo wa nyumba ya Daudi”?

14 Jamii ya Eliakimu ya leo imepewa daraka zito sawa na lile linalosimuliwa na maneno ya Yehova juu ya Eliakimu wa siku za Mfalme Hezekia: “Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.” (Isa. 22:22) Jamii hiyo ya “msimamizi wa nyumba” yenye washiriki wengi imeonyesha inastahili kuchukua daraka la kuwa na “ufunguo wa nyumba ya Daudi.” Imeendelea kukesha ili ilinde faida za kidunia za ufalme wa Mungu wa Kimashihi unaofananishwa na “nyumba ya Daudi.” Iliwakaribisha wale ambao Bwana alichagua wajumuishwe wawe washiriki wa mwisho wa mabaki ya warithi wa Ufalme. Katika mwaka 1935 ilianza kukaribisha “kondoo wengine” ambao yule Mchungaji Mwema alipendezwa kuwakusanya pamoja wawe “kundi moja” pamoja na mabaki waliotiwa mafuta. Ilifungia mlango waasi-imani wote waliofukuzwa na wale waliojaribu kujipenyeza ndani waharibu Mashahidi wa Yehova.​—Linganisha Ufunuo 3:7.

15. Yehova alikusudia kumgongomelea Eliakimu kama kitu gani mahali pa kudumu, na ni vitu gani vingeangikwa juu yake?

15 Akitoa unabii zaidi juu ya jamii ya kisasa ya Eliakimu, Yehova alisema hivi: “Nami nitamkaza kama msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake. Nao wataangika juu yake [kama juu ya kiangiko] utukufu wote wa nyumba ya baba yake; wazao wake na watoto wao, kila chombo kidogo tangu vyombo vya vikombe hata vyombo vya makopo vyote pia.”​—Isa. 22:23, 24.

16. Eliakimu alichukua mahali pa nani, na Eliakimu wa mfano aliwekwa kwenye utumishi gani kwa niaba ya “baraza ya watumishi”?

16 “Msumari” uliowekwa ukae daima ambao juu yake vyombo hivyo vya nyumbani vingeangikwa ulifananisha Eliakimu, yule msimamizi mpya ambaye alichukua mahali pa Shebna. Kwa hiyo alipewa daraka la kutoa chakula na kinywaji kwa washiriki wa nyumba ya mfalme. Kuwekwa kwa Eliakimu atumikie katika cheo hicho kulifananisha kwamba Hezekia Mkuu Zaidi, Yesu Kristo, wakati wa kuja kwake katika utukufu, alikubali jamii ya “msimamizi wa nyumba mwaminifu” isimamie mabaki ya warithi wake washirika ambao wangali duniani ili kutoa kwa hiyo “baraza ya watumishi” ‘kipimo cha chakula kinachohitajiwa kwa wakati unaofaa,’ kiwe ni kipimo kikubwa au kiwe ni kidogo. Hiyo ilitegemea namna ya chakula kigumu au namna ya kinywaji. Bila shaka, “chakula” hicho kingetoka katika Neno la Mungu. Hata hivyo, kwa maoni mengine ya Biblia, “vyombo” hivyo vingefananisha watumishi wenyewe wa Mungu, wenye vyeo vya utumishi mbalimbali.​—2 Tim. 2:20-22.

17. Ni katika njia gani Eliakimu angekuwa “kiti cha utukufu” kwa nyumba ya babaye, na ‘wazao na watoto’ wa babaye wangefaidikaje kutokana na hilo?

17 Eliakimu angekuwa “kiti cha utukufu” kwa nyumba ya baba yake mwenyewe, Hilkia. Hiyo ilimaanisha kwamba hangeaibisha nyumba ya babaye au kuaibisha sifa yayo tofauti na msimamizi wa nyumba aliyetangulia, Shebna. Yeye angekwezwa juu zaidi katika utumishi wa kifalme wa Mfalme Hezekia. Kuwa kwake kama “kiti cha utukufu” kulifananisha hayo yote. Yeye hangejiketisha kama mfalme anayetaka kutumikiwa, bali, kama mtumishi wa mfalme, yeye angekuwa na uwezo na “mamlaka” katika makao yake mapya aliyogawiwa. Kwa kadiri fulani yeye angemwakilisha na kusema kwa niaba (ajili) ya mfalme wa Yerusalemu. “Nyumba ya baba yake” haingeharibiwa sifa, bali, nyumba ya baba yake ingepata “utukufu” na ingeendelezwa kama kwamba iko juu ya msumari usioweza kuondoleka. ‘Wazao na watoto’ wa nyumba ya babaye hawangeharibiwa sifa kwa sababu ya kumtegemea Eliakimu awaletee sifa. Watu wote wa ukoo wa Eliakimu wangeweza kumtumaini awawakilishe kwa heshima, kwa njia yenye kuleta sifa. Watu wote wa ukoo wake wangeweza kumtumainia awawakiilishe vizuri katika cheo chake cha juu. Kwa hiyo watu hao wa ukoo wenye kumtegemea wangetiwa moyo watumikie kama “vyombo” katika utumishi wa kifalme kwa sababu ya kuungwa mkono kwa nguvu.

18. (a) Daraka la pekee limewekwa juu ya nani leo, na ni kwa namna gani hilo ni daraka la kifalme? (b) Ni nani leo walio ‘wazao na watoto, na wanafananishwa na vyombo gani?

18 Vivyo hivyo, leo, daraka zito sana limewekwa juu ya jamii ya “msimamizi wa nyumba, mwaminifu.” Ina daraka la kifalme, la kutukuza, kwa sababu linachukuliwa katika utumishi wa Mfalme wa Yehova ambaye sasa amewekwa, Yesu Kristo. Hilo ni daraka la kiroho kuwaelekea wale wote wenye uhusiano na jamii ya Eliakimu katika tumaini la Ufalme, kama ‘wazao na watoto’ wa Baba yao wa kiroho. Wanategemea au wameangikwa juu ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” iliyo kama msumari na wao wenyewe ni kama “vyombo” vyenye akili, vilivyo hai vya kuchukua chakula kwa vipimo vinavyotofautiana na washiriki wengine wa ujamaa wao wa kiroho.​—2 Tim. 2:20, 21; 2 Kor. 4:7.

19. (a) Eliakimu alipandishwa cheo awe na usimamizi wa nyumba wa kifalme katika wakati gani wenye hatari? (b) Mfalme wa Yuda aligeukia msaada upande gani chini ya hali za kutisha zilizokuwapo?

19 Katika nyakati za kale, katika karne ya nane kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, Eliakimu alipandishwa cheo cha usimamizi wa nyumba wa kifalme wakati wa kipindi cha hatari cha ufalme wa Yehova wa mfano kule Yerusalemu. Yeye alisikia moja kwa moja matisho yenye kuogopesha yaliyosemwa kwa sauti kuu na mjumbe wa Mfalme Senakeribu Mwashuri aliyekuwa anashambulia. Eliakimu alimtajia matisho hayo bwana yake, Mfalme Hezekia. Naye, Mfalme Hezekia hakutafuta msaada wa kijeshi kutoka Misri bali kwa Mungu wake, Yehova. Kwa kuitikia, Yehova alitoa jibu lenye kutia nguvu sana kupitia nabii wake Isaya. Halafu ni nini kilichotokea ili kutimiza ujumbe wa Yehova wenye kukaidi? Twasoma hivi:

20. Kisha Yehova alifanya nini ili kutimiza ujumbe Wake wa kukaidi kupitia nabii Isaya?

20 “Malaika wa [Yehova] alitoka, akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! hao walikuwa maiti wote pia. Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka akaenda zake, akarudi akakaa Ninawi. Ikawa, alipokuwa akiabudu nyumbani mwa Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza wakampiga kwa upanga.”​—Isa. 37:36-38; 2 Fal. 19:35-37.

21. (a) Tendo hilo la kivita la Yehova la wakati huo lilifananisha nani? (b) Jamii ya “msimamizi wa nyumba” leo inakabili nini, na ni tangu wakati gani na ni kwa nani onyo limesikizishwa na jamii hiyo?

21 Huko nyuma tendo hilo la kivita la Yehova kwa ajili ya ufalme wake katika Yerusalemu lilifananisha tendo lake ambalo litakuwa kuu zaidi wakati wa “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni. Hapo malaika wake wa uharibifu atakuwa malaika mkuu, Mfalme aliyewekwa, Yesu Kristo, akiwa mwenye amri juu ya malaika wote wa kimbinguni. (Ufu. 16:14-16; 19:11-21) Mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba” wanaielekea vita hiyo yenye kivumbi kushinda vyote, ambayo haitarudiwa tena. Jamii hiyo ya “msimamizi wa nyumba,” yenye daraka la “chakula” katika Neno la Mungu, imetumiwa, sana-sana tangu mwaka 1919, kusikizisha onyo la hii “vita” inayokuja kwenye ile inayoitwa Har–Magedoni. Kama kwa habari ya Eliakimu wakati wa siku za Mfalme Hezekia, wanalielekea shambulio linalokuja la “Mwashuri” Mkuu Zaidi, Shetani Ibilisi, na majeshi yake. (Mik. 5:5, 6) Wanaendelea kuwaonya washiriki wote wa nyumba ya Bwana yao wa kimbinguni na wanadamu wote pia.

22. Ni kina nani wameitikia onyo hilo, na ni kwa sababu gani wanatiwa moyo na yale yaliyompata Eliakimu na wenyeji wengine wa Yerusalemu na maana ya hayo?

22 “Mkutano mkubwa” wa mataifa yote umeitikia onyo hilo nao umelisikizisha kwa wengine pia. (Ufu. 7:9-17) Wao wanatiwa moyo na yale yaliyompata Eliakimu, aliyepewa usimamizi na Mfalme Hezekia, na wale wenyeji wengine wa Yerusalemu, kwa maana wao waliokoka wasiangamizwe katika vita baada ya washambulizi Waashuri kuharibiwa kabisa. Vivyo hivyo jamii ya “msimamizi wa nyumba” katika huu “wakati wa mwisho,” pamoja na ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo, watahifadhiwa wasiharibiwe pamoja na mfumo wa mambo wa ulimwengu katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni. (Dan. 12:4) Hapo, baada ya ushindi wa Yehova, yule Senakeribu Mkuu Zaidi, Shetani Ibilisi, na malaika wake wote wa kishetani watawekwa ndani ya shimo kwa miaka 1000 ya utawala wa Hezekia Mkuu Zaidi, Yesu Kristo.

23. Ni wakati gani hakutakuwapo shaka juu ya jibu linalofaa la ulizo lililotokezwa na Yesu katika Luka 12:42?

23 Hata Bwana yao anayetawala, Yesu Kristo, apendezwe kuwatumia zaidi duniani kwa muda mrefu namna gani, mabaki ya jamii ya “msimamizi wa nyumba mwaminifu” itatoa ‘kipimo cha chakula’ kinachohitajiwa na waokokaji wenzao, ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Bwana yao. Wakiwa wanaelekea kupokea taraja lile lenye kusisimua, watu wote wenye mfano wa kondoo na waendelee kujihadhari ‘wasikatwe’ kwenye Har–Magedoni kama wale walioangikwa juu ya ule “msumari” ulioondoshwa, jamii ya Shebna katika Jumuiya ya Wakristo. (Isa. 22:17-19, 25) Hakika, wenye furaha ni wale wote ambao wamehakikisha na kushikamana na jibu sahihi la ulizo la Yesu: “Kwa kweli ni nani aliye msimamizi wa nyumba mwaminifu, yule mwenye akili?” Kwa kuwa washikamanifu kwa usimamizi wake, na waendelee kukubali katika huu wakati unaofaa ‘kipimo cha chakula’ kinachohitajiwa kinachotolewa na huyo “msimamizi wa nyumba mwaminifu,” Eliakimu Mkuu Zaidi. “Msumari” huo wa mfano, kulingana na uwezo wa Mungu wa kutangulia kujua, umegongomelewa (umepigiliwa) “mahali palipo imara” ili udumu, kwa msaada wa Mungu. Kwa hiyo ushikilie kwa uhakika, kwa ushikamanifu wote.​—Kutoka The Watchtower, October 1, 1981.

[Maelezo ya Chini]

a Katika Tafsiri ya Kigiriki ya Septuagint ya Maandiko ya Kiebrania, Isaya 22:19 inasema hivi: “Na wewe utaondolewa kutoka kwa usimamizi wako wa nyumba [oi·ko·no·miʹa], na kutoka mahali pako.”​—Tafsiri ya Septuagint, Kigiriki na Kiingereza, ya Samuel Bagster and Sons Limited, London, Uingereza.

b Ona toleo la Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) la Aprili 1, 1945, ukurasa 102, fungu 1; pia, Desemba 1, 1951, ukurasa 719, fungu 10.

Je! kwa kurudia wewe unaweza kujibu maulizo haya?

◼ Eliakimu na Shebna walikuwa nani?

◼ Katika siku zetu, Eliakimu na Shebna wanafananisha nani?

◼ Mfalme Senakeribu na Mfalme Hezekia wanafananisha nani leo?

◼ Jamii ya Eliakimu inaunga mkono nini, tofauti na kile ambacho jamii ya Shebna inaunga mkono?

◼ Ni nani wanaofananishwa na “wenyeji wa Yerusalemu, na . . . nyumba ya Yuda”?

◼ Ni nani wengine licha ya ‘wenyeji wa Yerusalemu na Yuda’ wa kisasa wanaopata ulinzi kama wa baba wa jamii ya Eliakimu?

◼ Ni nini kinachofananishwa na “nyumba ya Daudi”?

◼ Ni nani “msumari” wa unabii wa Isaya, na anafananisha nani?

◼ Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba “msumari” huo unakuwa “kiti cha utukufu”?

[Picha katika ukurasa wa 21]

Mabaki waliotiwa mafuta na wafanya kazi wenzao wanaeneza MNARA WA MLINZI ulimwenguni pote katika lugha nyingi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki