Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 3/15 uku. 19
  • Wanafanya Kazi Ingawa Wamepigwa Marufuku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanafanya Kazi Ingawa Wamepigwa Marufuku
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Mchawi Mwenye Wake Wengi Apata Ukweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Dawa za Vichakani—Je! Wakristo Watafute “Mapozo” Yake?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kutafuta Wachawi Huko Ulaya
    Amkeni!—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 3/15 uku. 19

Wanafanya Kazi Ingawa Wamepigwa Marufuku

Ingawa katika nchi fulani za Afrika waganga wamepigwa marufuku, watu wengi wanawaendea wanapokuwa na magonjwa badala ya kwenda kutibiwa na madaktari wa kisasa. Inasemekana kwamba katika nchi moja ya Afrika ambako waganga wamepigwa marufuku, wao wana shughuli nyingi sana kufikia kiasi cha kwamba hata wachezaji-mpira wanakataa kucheza mpaka kwanza mganga alaani timu (kikoa) ile nyingine. Hivi majuzi madaktari wawili Wajeremani walitembelea nchi hiyo wakapiga picha ya sinema kuhusu upasuaji wa ubongo uliofanywa na mganga bila kumtia mgonjwa katika hali ya kutokuona maumivu.

Kivulana mdogo alikuwa na maumivu makali baada ya kupigwa kichwani, basi ubongo wake ukawa na mkazo. Alishikiliwa chini na wanaume watano huku mganga akitumia saa tano kutoboa shimo kichwani mwake kwa kitu chenye ncha kali. Baadaye, mafuta yalimiminwa juu ya jeraha lenyewe kisha akafungwa kichwa kwa vitambaa. Jambo la kustaajabisha ni kwamba kivulana aliinuka na kwenda zake nyumbani.

Lakini waganga na wachawi wanatoa wapi uwezo wao? Biblia inaonyesha waziwazi ni kutokana na mashetani, roho waovu, na kwa hiyo “mtu ye yote anayewaendea” watu wa namna hiyo anaonwa na Mungu kuwa ‘wa kuchukiza sana.’​—Kumbukumbu la Torati 18:9-12, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki