Sababu Wewe Unapaswa Kuhudhuria “Kweli ya Ufalme” Kusanyiko la Wilaya
Programu yenye kusisimua ya siku nne ya maagizo ya Biblia inakungojea kwenye “Kweli ya Ufalme” Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova. Kupitia maonyesho yanayolingana na hali zetu, mahubiri kwa njia ya michezo ya kuigiza na hotuba zenye kuagiza, uongozi wa Biblia wa maana sana utatolewa. Vilevile, utapokea kitu ambacho kitakuwa na uongozi mkubwa sana kwa kazi ambayo Wakristo watakuwa wakifanya katika siku zilizoko mbele.
Na uwepo alasiri ya Alhamisi saa 7.20, wakati programu ya kusanyiko itakapoanza. Ni jambo la lazima kwamba ukabili moja kwa moja ulizo la hotuba ya msingi: “Wewe Uko Upande Gani wa Lile Suala la Ufalme?” Bila shaka siku ya Ijumaa utathamini sana utakayopokea hata uchochewe kuyashiriki pamoja na wengine mtaani.
Programu ya Jumamosi imejawa na maagizo yanayofaa na yanayohitajiwa ili kuishi katika ulimwengu wa leo wenye choyo na matendo mapotovu. Utasikia hotuba kama “Kuzuia Wendekevu kwa Kutumia Kanuni za Biblia” na “Jihadhari na Muziki Unaovunja Heshima.” Kwa vyo vyote, usikose mahubiri hayo ambayo yatamaliziwa katika programu ya Jumamosi—habari zitakazokuwa na matokeo ya kudumu juu ya kazi ya kuhubiri Ufalme ulimwenguni pote zitatolewa.
Jumapili mafundisho ya mchezo wa kuigiza “Mtangazaji Asiyeogopa wa Ujumbe Usiopendwa na Wengi” yatakuchochea uwe kama nabii wa Mungu, Yeremia. Halafu hutataka kukosa hotuba ya watu wote “Ile Kweli Inayoweza Kukuweka Huru.”
UNAKARIBISHWA