“Washika Ukamilifu” Kusanyiko Limekaribia
Siku nne zenye kuthawabisha za maagizo ya Biblia zinakungojea kwenye “Washika Ukamilifu” Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova katika mwezi Desemba. Kupitia hotuba zenye kuagiza, mahoji ya wahudumu wenye ujuzi, na mawonyesho halisi, uongozi wa maana sana wa Kikristo utatolewa.
Uwepo kwa kipindi cha kufungua saa 5:00 asubuhi ya Alhamisi. Hotuba ya mwenyekiti, “Acheni Ukamilifu Utulinde,” inakazia kichwa cha kusanyiko nayo itatufanya tutarajie kwa hamu programu yote ya siku nne. Pia, katika kipindi cha kufungua mtapokea mambo ambayo yatakuwa msaada wa kudumu muda mrefu katika kuzungumza na wengine kwa kutoa sababu za Maandiko.
Ijumaa asubuhi, kutakuwako mchezo wa kuigiza Wakati Ujao Wako—Ni wa Kukazaniwa. Hicho kitakuwa ni kitia moyo kweli kweli kwa vijana. Bila shaka utathamini sana utakayopokea siku ya Ijumaa hata kwamba utakuwa na shauku ya kushiriki hayo na wengine mtaani.
Programu ya siku ya Jumamosi imejawa na maagizo halisi ya maisha ya Kikristo. Maana ya kutunza jicho lako likiwa rahisi na jinsi ya kuuchunguza moyo wako wa mfano ni mambo yatakayozungumzwa. Habari ya kumalizia siku, “Ukamilifu kwa Ukweli Katika Ulimwengu Usiomwogopa Mungu,” itakupa jambo zuri ambalo litakuwa hazina kwako na pia linalopasa kuwa na uvutano mkubwa kwenye utendaji wetu katika huduma ya shambani.
Programu siku ya Jumapili, siku ya mwisho, itakazia mchezo wa kuigizwa unaoitwa Ogopa Mungu, Epuka Uovu, ambao waigizaji watavaa mavazi ya kimchezo. Pia itakazia hotuba ya watu wote, “Nyakati na Majira ya Mungu—Yanaelekeza Kwenye Nini?” Hakika hiyo ni programu ya siku nne yenye kuagiza na kusisimua kama nini! HUDHURIA!