“Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya—Usiukose!
Siku tatu kamili, za maagizo ya Biblia yenye kuthawabisha na ushirika wa Kikristo wenye kujenga zinakungojea wewe kwenye “Tumaini Katika Yehova” mkusanyiko wa wilaya wa Mashahidi wa Yehova. Wakati wa Desemba mikusanyiko imeratibiwa, kwa hivyo kutakuwa mmoja si mbali sana na mahali unapoishi. Panga ili uweko tangu kipindi cha kufungua kuanzia saa 4:20 Ijumaa asubuhi, na uhudhurie mpaka kipindi cha kumalizia Jumapili alasiri
Kipindi cha kufungua kitakuwa na hotuba yenye kuarifu, “Watu Waliowekwa Mbali na Ulimwengu.” Alasiri shauri lenye kutoboa mambo na kuyasema wazi litaelekezwa kwa wazazi kisha kwa vijana Vijana watasaidiwa wajilinde dhidi ya kuishi yale ambayo yangeweza kuitwa maisha ya namna mbili. Halafu jambo hilo litakaziwa katika mchezo wa kuigiza wa kisasa wenye kusukuma moyo.
Asubuhi ya Jumamosi itakazia hotuba inayohusu wakfu na ubatizo, pia agizo kuhusu njia tunazoweza kuonyesha tumaini letu katika Yehova, kulingana na kichwa cha mkusanyiko. “Uzaaji-Watoto Wenye Madaraka Katika Huu Wakati wa Mwisho” itakuwa hotuba kuu katika programu ya alasiri ambayo itatia ndani mfululizo wa hotuba zenye kichwa “Neno la Mungu Li Hai.”
Programu ya Jumapili itakazia hotuba yenye kichwa “Chukia Kabisa Kabisa Mwendo Wenye Aibu wa Ulimwengu,” pia mchezo wa kuigiza wenye mavazi kamili utaonyesha uharaka wa nyakati zetu. Alasiri ya siku hiyo, hotuba ya watu wote yenye kichwa “Nyakati Zetu Zenye Hofu, Ni Nani Unayeweza Kutumaini Kikweli?” itakuwa jambo jingine la kukaziwa na mkusanyiko.
Waulize Mashahidi wa Yehova wakati na mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi na wewe.