Usikose “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya
Siku tatu zenye kuthawabisha za maagizo ya Biblia zakungoja. Uwepo wakati programu ianzapo kwa muziki saa 3:40 Ijumaa asubuhi. Furahia hotuba ya kufungua, “Karibuni, Enyi Wasifaji Wenye Shangwe wa Yehova!,” na vilevile hotuba ya msingi, “Waliowekwa Kando Kuwa Wasifaji Wenye Shangwe Ulimwenguni Pote.”
Programu ya Ijumaa alasiri itakazia fikira kwa vijana, wazazi wao, na elimu. “Je, Niko Tayari Kufunga Ndoa?” ni hotuba ambayo wengi watapenda kusikiliza. Wazazi wapaswa kusikiliza kwa uangalifu mazungumzo “Wazazi Wanaofurahia Watoto Wao.” Programu ya alasiri itamalizia kwa mhadhara “Elimu—Itumie Kumsifu Yehova.” Kile kitakachoandaliwa chapasa kusaidia vijana kuendelea kwa mafanikio katika shule.
Mfululizo wa Jumamosi asubuhi, “Kuitikia Wito wa Kumsifu Yehova,” wapasa kutia wengi moyo. Kipindi cha asubuhi kitamalizia kwa hotuba ya ubatizo. Wakati wa alasiri, kutakuwa na mazungumzo ya wazi juu ya jinsi Shetani tangu nyakati za mapema ametumia tamaa ya kingono ili kunasa watu. Programu ya siku hiyo itamalizia kwa utoaji wa habari ambayo yapasa kutayarisha watu wa Mungu ili watimize huduma yao kwa matokeo zaidi.
Kipindi cha Jumapili asubuhi kitakuwa na habari yenye kusisimua ikikazia uangalifu kwenye uhitaji wa haraka wa kukimbilia usalama bila kukawia kabla ya “dhiki kubwa.” (Mathayo 24:21) Kipindi hicho kitamalizia kwa drama yenye umuhimu “Kuheshimu Wastahiki Katika Miaka Yao ya Uzee.” Wakati wa alasiri, hotuba ya watu wote “Msifuni Mfalme wa Umilele!” itakuwa jambo jingine kuu la mkusanyiko.
Pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa mahali penu kwa ajili ya wakati na mahali pa mkusanyiko ulioko karibu nawe.