“Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova
Siku tatu zenye kuthawabisha za maagizo ya Biblia zakungoja. Mikusanyiko 17 ikiwa imepangiwa Afrika Mashariki na Rwanda, yaelekea kwamba kutakuwa na mkusanyiko karibu na sehemu unayoishi. Uwepo wakati programu ianzapo kwa muziki saa 3:40 Ijumaa asubuhi.
Programu ya Ijumaa asubuhi itakuwa na maelezo ya ukaribishaji na vilevile hotuba ya msingi, “Waliowekwa Kando Kuwa Wasifaji Wenye Shangwe Ulimwenguni Pote.” Wakati wa alasiri, programu itakazia fikira vijana, wazazi, na elimu. “Je, Niko Tayari Kufunga Ndoa?” ni hotuba ambayo vijana watapenda kusikiliza. Wazazi wapaswa kusikiliza kwa uangalifu hotuba “Wazazi Wanaofurahia Watoto Wao.” Programu ya alasiri itamalizika kwa hotuba “Elimu—Itumie Kumsifu Yehova.” Yale yatakayozungumzwa yapasa kusaidia vijana kuendelea kwa mafanikio shuleni.
Programu ya Jumamosi asubuhi itakuwa na ubatizo, na kutakuwa na fursa kwa wale wanaostahili kubatizwa. Wakati wa alasiri kutakuwa na mazungumzo ya wazi juu ya jinsi Shetani tangu nyakati za kale ametumia tamaa ya kingono kunasa watu. Pia kutakuwa na hotuba yenye nguvu “Epuka Mitego ya Ibilisi.” Programu ya siku hiyo itamalizika kwa hotuba muhimu “Sababu kwa Nini Wanadamu Wahitaji Ujuzi Juu ya Mungu.”
Jumapili asubuhi, mfululizo wenye kichwa “Wasifaji Wenye Shangwe Katika Umalizio wa Mfumo Huu” utakazia fikira matukio yenye kutikisa ulimwengu yatakayotukabili hivi karibuni. Utakazia umuhimu wa kutorokea mahali pa usalama kabla ya kuanza kwa “dhiki kubwa” ambayo Yesu Kristo alitaja, kama ilivyorekodiwa kwenye Mathayo 24:21.
Programu ya Jumapili asubuhi itamalizika kwa drama yenye umuhimu “Kuheshimu Wastahiki Katika Miaka Yao ya Uzee.” Kisha, alasiri, hotuba ya watu wote, “Msifuni Mfalme wa Umilele!” itatolewa. Itakuwa jambo kuu la mkusanyiko.
Fanya mipango sasa uhudhurie. Ili ujue mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi na kwako, pata habari katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la kwenu, au andikia wachapishaji wa gazeti hili. Toleo la Juni 8, la Amkeni! litaorodhesha mahali pa mikusanyiko katika Afrika Mashariki na Rwanda.