Sababu Inayofanya Upaswe Kuhudhuria “Amani ya Kimungu” Mkusanyiko
WAKATI uvamizi, mapinduzi makuu, na vita ndiyo mambo ya kawaida siku hizi, ni vizuri kama nini kwamba unaweza kuhudhuria “Amani ya Kimungu” mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova! Zaidi ya kupokea mafundisho yanayofaa ya Kikristo juu ya kudumisha amani, kule utaona pia maelfu ya watu wakiyatumia mafundisho hayo.
Uwe kule tangu kipindi cha kufungua kuanzia saa 7:30 Alhamisi alasiri. Utasikia maelezo ya watangazaji amani wa muda mrefu. Pia, utaijua mitego inayopatikana katika vitumbuizo vya kirafiki, na jinsi ya kuviepuka. Na kwenye umalizio wa kipindi, utapokea kitu ambacho zaidi ya kuwa kinavutia macho, ni chenye mafaa pia katika kuhudumia wengine pia.
Programu ya asubuhi siku ya Ijumaa itakuwa na hotuba ya msingi, “Amani ya Kimungu kwa Wale Wanaofundishwa na Yehova.” Moyo wako utavutwa sana na mchezo wa kuigiza wenye wachezaji waliovaa mavazi kamili ya kimchezo, unaoitwa “Kuhifadhi Uhai Katika Wakati wa Njaa.” Usiukose!
Siku ya Jumamosi, mawonyesho, mahojiano, na hotuba zenye kufundisha zitatoa mwongozo wenye mafaa wa kudumishia amani ndani ya jamaa. Programu itamalizika na hotuba ya maana yenye kusema, “Usalama wa Ulimwenguni Pote Chini ya ‘Mwana-Mfalme wa Amani.’ ”
Asubuhi ya Jumapili mchezo wa kuigiza wa kisasa unaotoboa mambo waziwazi kabisa bila kuyaficha utaonyeshwa ukikazia uhitaji wa kutafuta uadilifu wa Mungu ili kuokolewa. Alasiri, hotuba ya watu wote yenye uthabiti mwingi, “Hatimaye Amani—Wakati Mungu Asemapo” itakuwa jambo jingine kuu la mkusanyiko.
Kwa kuwa mikusanyiko 6 imepangwa ifanywe katika Kenya, kutakuwa na mkusanyiko si mbali sana na mahali unapoishi. Waulize Mashahidi wa Yehova wakati na mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi na wewe.