Wewe Unaalikwa Kwenye “Amani ya Kimungu” Mikusanyiko
KILA shahidi Mkristo wa Yehova anatazamia kwa hamu nyingi kama nini mikusanyiko ya wilaya ya kila mwaka! Hakuna shaka kwamba hiyo inakuwa tukio la kila mwaka. Zile hotuba nzuri, michezo ya kuigiza ya Biblia, vitolewaji, ule ushirika—nyakati nyingine pia ile hadhirina kubwa—yote hayo yanajumlika kuyafanya makusanyiko hayo yawe ya pekee kweli kweli.
Kwa mfano, fikiria “Washika Ukamilifu” Mikusanyiko ya wilaya iliyofanywa mwaka uliopita. Ile miwili iliyofanywa katika Sao Paulo na Rio de Janeiro, Brazili, ilikuwa na kilele cha hadhirina ya 249,351 na watu 2,645 walionyesha wakfu wao kwa Yehova Mungu kwa kubatizwa katika maji. Mkusanyiko uliofanywa Montreal, Kanada, ulihudhuriwa na watu 78,804, ulikuwa wa kutokeza kwanza kwa sababu ulikuwa na uwanja wa kuegeshea magari-nyumba na kwa kuwa ulifanywa katika lugha 11 mbalimbali. Waliohudhuria kusanyiko kule Zurich, Uswisi, walisema kwamba katika maisha yao yote hawajapata kuona shauku wala furaha ya namna iliyokuwa katika mkusanyiko huo. Wajumbe wenye kuhudhuria mmoja au zaidi ya mikusanyiko iliyofanya katika Polandi walitoa maoni kama hayo.
Ripoti ya ulimwenguni pote isiyo kamili yaonyesha hadhirina ya watu 5,653,689 kwenye “Washika Ukamilifu” Mikusanyiko, na Mashahidi wapya 75,202 walibatizwa. Yehova aliyabariki makusanyiko hayo ya watu wake kiajabu kama nini!
Kinyume cha vile inavyotazamiwa kwa ukawaida, wenye kuihudhuria mikusanyiko hiyo waliona mambo yakitimizwa kuliko yalivyotazamiwa. Karibu kila mahali watu walikubaliana kwamba mikusanyiko hiyo ya karibuni zaidi ndiyo iliyokuwa bora zaidi kufikia hapo. Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wote watakuwa wakitazamia kwa hamu nyingi “Amani ya Kimungu” mikusanyiko ya wilaya ya mwaka huu, itakayofanywa ulimwenguni pote—6 ya hiyo katika Kenya.
Ni kichwa kizuri kama nini kwa mkusanyiko wa wilaya wetu: “Amani ya Kimungu”! Leo jamii ya kibinadamu inatatanishwa na ugomvi. Si kwamba vita halisi tu vinapigwa sasa duniani pote, bali kuna aina nyingine pia za mapigano: vita ya kiuchumi na ugomvi kati ya wenzi wa ndoa, na pia kati ya wazazi na watoto. Lakini tofauti sana na hilo, kuna amani kati ya watu wa Yehova walio wakfu. Yao ni amani ya kimungu, inayotokana na yule Mwenye Uungu, Yehova Mungu, yule Mungu wa amani apaye amani. Wao wana amani naye kwa sababu ya imani na matendo, na kwa hiyo wanaweza kuwa na amani kati ya mtu na mwenzake, katika kundi na ndani ya jamaa—Wafilipi 4:7; Warumi 16:20.
Na iangaliwe, pia, kwamba amani ya kimungu hii si kukosekana tu kwa ugomvi. Neno la kusema amani katika Kiebrania ni sha·lohmʹ, nayo haimaanishi hali ya kuwa na amani tu bali masilahi na ufanisi. Ndiyo, si kwamba Mashahidi wa Yehova wanafurahia kukosekana kwa ugomvi tu bali pia ufanisi kwa sababu ya kuwa katika paradiso ya kiroho. Mkusanyiko huu utawezesha wote watakaohudhuria wajali zaidi sana kuwa wenye amani na kuhangaikia kuendeleza amani, kwa kadiri ambavyo jambo hilo limo katika uwezo wao.—Warumi 12:18.
Kama ilivyo katika miaka iliyotangulia, mikusanyiko hii itaanza alasiri ya Alhamisi saa saba na nusu. Kila siku ina kichwa kinachohusiana na amani, kile cha siku ya kwanza kikiwa ni “Mungu Atawabariki Watu Wake kwa Amani,” kikitegemea Zaburi 29:11. Sala yenye maana itazungumzwa, na upeo wa kipindi hicho utakuwa hotuba juu ya jinsi Yehova anaendelea kuvifanya vitu vyote kuwa vipya.
Siku ya Ijumaa hotuba ya msingi, “Amani ya Kimungu kwa Wale Wanaofundiswa na Yehova,” itakazia chanzo cha amani yetu. Kati ya mambo mengine yatakayokuwa katika programu ni mchezo wa kuigiza wa Biblia unaochangamsha moyo wenye kuhusianisha nyakati za kale na siku zetu.
Zaidi ya hotuba ya ubatizo, programu ya Jumamosi asabuhi itakazia wajibu wetu wa Kikristo kuelekea mtu na mwenzake na uhitaji wa kufanya maendeleo wakati wote tukiwa mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Alasiri, kutakuwa na mashauri mazuri kwa washiriki wa jamaa na waangalizi wanaosafiri.
Mchezo wa kuigiza wa kisasa wenye kutoboa na kugonga mambo waziwazi utaonyeshwa Jumapili asabuhi. Alasiri, ile hotuba ya watu wote yenye mkazo mwingi “Hatimaye Amani —Wakati Mungu Anenapo” itakuwa mojapo mambo makuu ya mkusanyiko huo. Bila shaka wote wenye kuhudhuria mkusanyiko watatoka hapo wakijisikia wametayarishwa kikamili na yule Mungu wa amani ili kufanya mapenzi yake.
Basi, uje siku zote nne ukiwa na hamu kubwa ya kula chakula cha kiroho, ukiutambua kwa ukamili uhitaji wako wa kiroho. (Mathayo 5:3) Panga mambo yako kwa njia itakayokuwezesha uwepo wakati wa wimbo wa kwanza na sala bila kuchelewa kila siku. Uje ukiwa na vifaa vya kuandikia habari, pia, kwa maana kuandika mawazo makuu kutakusaidia ukaze fikira juu ya anayosema mhutubu. Zaidi ya hilo, kwa njia hiyo mawazo yanayotajwa yataweza zaidi kukazika kikiki katika moyo na akili yako.
Lakini tusiusahau kamwe uhakika wa kwamba ibada safi ya Yehova Mungu haihusu kupokea tu. Inahusu pia kutoa. Tunataka kuizingatia kanuni hii ya Biblia: “Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.” (2 Wakorintho 9:6) Kuongezea hilo, kwa kuwa Yesu alisema kwamba “Kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea,” acheni tupate furaha iliyo kubwa zaidi kwenye mkusanyiko kwa kutoa kadiri tunavyoweza, tukijitolea kwa hiari kutoa utumishi wetu. (Matendo 20:35, NW ) Kwa kweli, isihitajiwe kamwe kuombwa-ombwa tujitolee.
Tena, na tuuchukue kwa uzito uandalizi wa kushiriki katika ushuhuda wa shambani Ijumaa alasiri. Kisha na tuwe macho siku zote nne kutafuta nafasi za kutoa ushuhuda wa ivi hivi. Jambo hilo linatukumbusha kanuni nyingine ya Biblia: Nafsi yenye ukarimu itapata ufanisi, naye anyweshaye atanyweshwa. (Mithali 11:25) ndiyo, acheni tuwaalike wote tunaoweza wajijulie wao wenyewe jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyojipasha moto katika amani ya kimungu.