Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 7/1 uku. 3
  • Ulimwengu Utakuwaje Kesho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Utakuwaje Kesho?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Kuna Wakati Ambao Wewe Utaishi Katika Ulimwengu Wenye Furaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • 2000—Je, Ni Mwaka wa Pekee?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Mwaka wa 2000—Je, Kuvurugika kwa Kompyuta Kutakuathiri?
    Amkeni!—1999
  • Mwaka wa 2000 Ni Wenye Maana Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 7/1 uku. 3

Ulimwengu Utakuwaje Kesho?

NI JAMBO gani lililo katika upeo wa macho? Ni ulimwengu tofauti.

Hilo ndilo jambo linaloonyeshwa na mipango ya mashirika ya serikali ya United States (Amerika) kama ilivyoandikwa katika taarifa inayoitwa “Ripoti kwa Rais Kuhusu Hali ya Dunia Kufikia Mwaka wa 2000.” Sehemu ya Kwanza ya kitabu chenye taarifa hiyo, iliyotayarishwa na Baraza la Ubora wa Mazingira na Idara ya Serikali, ilisema hivi: “Ulimwengu kufikia mwaka wa 2000 utakuwa tofauti na ulimwengu wa leo kwa njia mbalimbali za maana.” Katika njia gani?

Kati ya mambo mengine, ripoti hiyo inatabiri kwamba:

● “Watu wataongezeka. kwa kila watu wawili waliokuwa duniani mwaka wa 1975 kutakuwa na watatu mwaka wa 2000.”

● “Pengo lililo kati ya matajiri zaidi na maskini zaidi litakuwa limeongezeka.”

● “Mali za asili zinazotegemewa zitakuwa zimepungua.”

● “Mazingira yatakuwa yamepoteza nguvu kuu za namna mbalimbali zinazosaidia kuendeleza uhai.”

● “Bei za vitu zitakuwa zimepanda.”

● “Ulimwengu utakuwa zaidi na maelekeo ya kupatwa na maafa yanayosababishwa na nguvu za asili na kuletewa misukosuko ya ghafula na wanadamu.”

● “Mwishowe, lazima ikaziwe kwamba njia ya kuendesha mambo ya watu wote isipobadilishwa kwa ujumla ulimwengu utakuwa tofauti kwa sababu ya kukosa kutumia vizuri hali ambazo zingaliweza kuleta mafaa.”

Bila shaka utakubali kwamba mataraja ya kutazamia mambo hayo hayapendezi. Kwa uhakika huo si msingi mzuri wa kuleta furaha nyingi zaidi.

Hata hivyo Maandiko yanawatia watu moyo wafurahi, yakisema: “Furahini, Mataifa, pamoja na watu wake.” (Warumi 15:10; linganisha Kumbukumbu la Torati 32:43.) Wanaotajwa hapa ni watu wanaomwabudu Mungu katika njia inayokubalika kwake. Wanafanya hivyo “katika roho na kweli.” (Yohana 4:23, 24) Lakini kwa sababu sasa tunakabili matatizo mengi, je! kweli kuna sababu yo yote ya kufikiri kwamba siku moja utaishi katika ulimwengu wenye furaha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki