Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 2/15 kur. 8-14
  • ‘Kuingiza Kisiri-siri Madhehebu Zenye Kuharibu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kuingiza Kisiri-siri Madhehebu Zenye Kuharibu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Elekeo la Mapema la Kuanzisha Madhehebu
  • Madhehebu Fulani za Kwanza-Kwanza
  • “Mtu wa Kuasi” Anaanza Kujipanga
  • “Madhehebu Zenye Kuharibu” Wakati wa Mwisho
  • Onyo kwa Wakristo wa Kweli
  • “Bwana Mmoja, Imani Moja, Ubatizo Mmoja”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mtu wa Uasi Sheria
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Kutambulisha “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Uasi-Imani
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 2/15 kur. 8-14

‘Kuingiza Kisiri-siri Madhehebu Zenye Kuharibu

“Watakuwako pia walimu wa uongo miongoni mwenu ninyi. Watu wenyewe hao wataingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu.”​—2 PETRO 2:1, NW.

1, 2. (a) Hapo kwanza makanisa yote ya Jumuiya ya Wakristo yalikuwa nini? (b) Kwa hiyo ni maulizo gani yanayostahili tuyafikirie?

MAKANISA yote ya Jumuiya ya Wakristo yalikuwa madhehebu ndogo-ndogo zilizogawanyika hapo kwanza. Mengine kati yayo​—hasa Kanisa la Roma na Makanisa ya kitaifa yo Orthodoski na ya Uprotestanti​—yanadai kuwa ndiyo yaliyoanzwa kwanza kabla ya zile zinazoitwa dini za Kikristo, ambazo wao wanazifanyia madharau kwa kuziita madhehebu zilizokatika kutoka dini kubwa-kubwa.

2 Lakini, huenda wengine wakauliza hivi: ‘Je! kwa kweli Yesu Kristo na mitume wake waaminifu walitabiri kwamba watu wangeanguka wauache Ukristo wa kweli? Je! walitoa onyo ili watu ambao wangetokeza madhehebu wasifuatwe? Karne 19 zilizopita, je! ilikuwa lazima kabisa wafuasi wa kweli wa Yesu wawe macho wasipatwe na maelekeo hayo ya kuleta mgawanyiko? Na je! kukesha kwa njia iyo hiyo kunahitajiwa leo?’

Elekeo la Mapema la Kuanzisha Madhehebu

3, 4. (a) Yesu alitoa onyo gani, na hilo linamaanishal nini kwa habari ya Ukristo wa kweli? (b) Petro alitoa onyo gani linalofanana na hilo?

3 Katika Mahubiri ya Mlimani ambayo Yesu alitoa, yeye alisema hivi: “Ingieni kupitia lile lango jembamba; kwa maana lango ni pana na njia ni rahisi, ambayo inaongoza kwenye uharibifu, na wale wanaoingia kupitia hilo ni wengi. Kwa maana lango ni jembamba na njia ni ngumu, ambayo inaongoza kwenye uzima, na wale wanaoipata ni wachache. Jihadharini na manabii wa uongo, ambao wanakuja kwenu wakiwa katika mavazi ya kondoo lakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wenye pupa. Ninyi mtawajua kwa matunda yao.” (Mathayo 7:13-16, Revised Standard Version) Yesu Kristo hakusema kwamba Ukristo wa kweli ungekuwa mpana, rahisi, wa kufuatwa na ulimwengu mzima, au “wa kikatoliki” (wenye kutia ndani watu wote wa dunia), uwe dini fulani yenye kuwafaa walio “wengi.” Alisema ungekuwa njia ngumu yenye kufinyana, yenye kupatikana na “wachache” tu. “Wachache” hao walionywa kwamba “manabii wa uongo” wenye kuonekana kama kwamba walikuwa hawana madhara wangejaribu kuwapotosha wafuate ile njia ‘rahisi ambayo inaongoza kwenye uharibifu.’

4 Zaidi ya miaka 30 baadaye mtume Petro aliandika hivi: “Wakawako pia manabii wa uongo miongoni mwa watu hao [wa Israeli], kama watakavyokuwako pia walimu wa uongo miongoni mwenu ninyi [Wakristo]. Watu wenyewe hao wataingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu nao hata watamkana mwenyeji aliyewanunua, wakijiletea uharibifu wa haraka. Zaidi ya hayo, wengi watafuata matendo yao ya mwenendo mpotovu, na kwa sababu ya hao njia ya kweli itatukanwa. Vile-vile, kwa tamaa watawatumieni ninyi kwa faida yao kwa kutumia maneno ya bandia.”​—2 Petro 2:1-3, NW.

5. Ni wakati gani “mbwa-mwitu” walipoanza kutokea, nao ‘waliingizaje kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu’?

5 Ile “njia ya kweli,” ile njia “ambayo inaongoza kwenye uzima,” ndiyo njia ya Ukristo wa kweli. Wale “manabii wa uongo,” au “walimu wa uongo,” ndio waasi-imani walio ‘majibwa-mwitu yenye kuvaa mavazi ya kondoo’ ambao walianza kujulisha kuwapo kwao kati ya Wakristo wa kwanza hata kabla ya kufa kwa mitume wa Yesu. (1 Yohana 2:18, 19; 4:1-3) Mtume Paulo pia alitoa onyo juu ya hao “mbwa-mwitu wakali.” Aliwatambulisha kuwa watu ambao ‘wangeinuka wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.’ (Matendo 20:29, 30) Kuanzia ile nusu ya pili ya karne ya kwanza na kuendelea, hao walimu wa uongo ‘waliingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu,’ wakawatumia Wakristo wa kwanza kwa faida yao wenyewe wakiwa na “maneno ya bandia.” Kwa sababu ya waasi-imani hao, ile “njia ya kweli,” Ukristo wa kweli, ‘ilitukanwa.’

Madhehebu Fulani za Kwanza-Kwanza

6. Kitabu cha Ufunuo kinaonyeshaje kwamba madhehebu za kuasi imani zilikuwa zimekwisha kutokea kufikia mwisho wa karne ya kwanza, na kwa sababu gani zilichukiwa na Kristo?

6 Katika Ufunuo uliopokewa na mtume Yohana karibu na mwaka wa 96 W.K., yeye anaandika mfululizo wa ujumbe mbali-mbali ulioongozwa na Mungu kuonyesha hali za kiroho zilizokuwa wakati huo ndani ya makundi ya Kikristo na ambazo zingeweza kutokea tena muda wote wa historia. Sehemu mbili za ujumbe huo zinafunua kwamba kulikuwako madhehebu za kuasi-imani ambazo zilichukiwa na Kristo, yule kichwa cha kundi la kweli la Kikristo. Inaonekana kwamba angaa moja ya madhehebu hizo iliachilia ibada ya sanamu na uasherati ufanywe.​—Ufunuo 2:6. 14, 15.

7. Barua za Paulo zinaonyeshaje kwamba vita ya kupambana na mgawanyiko wa madhehebu ilikuwa tayari ikiendelea siku zake?

7 Hesabu fulani ya barua za mtume Paulo, zilizoandikwa mapema zaidi, zinaonyesha kwamba yeye alikuwa tayari amekwisha kulazimika kupiga vita vikali juu ya elekeo la kuanzisha madhehebu mbalimbali. Katika barua ya kwanza aliyoandikia Wakristo katika Korintho, Paulo alihuzunishwa sana na mwelekeo wao wa kufuata wanadamu, kwa sababu jambo hilo lilileta “mitengano” na “migawanyiko.” (1 Wakorintho 1:10-13; 3:1-4, NW) Alionyesha hangaiko ilo hilo katika barua alizoandikia Wagalatia (1:6-9; 5:19-21), Tito (3:9, 10) na Timotheo.​—1 Timotheo 1:3-7; 4:1-3; 6:20, 21; 2 Timotheo 4:3, 4.

8. Wafuasi wa madhehebu ya kimaarifa waliamini nini, na kwa sababu gani walifanya ‘njia ya kweli itukanwe’?

8 Wanachuo fulani wa Biblia wana maoni ya kwamba katika barua ya kwanza ambayo Paulo aliandikia Wakristo na, hasa sana, katika barua aliyoandikia Waefeso na Wakolosai, alitumia kwa makusudi maneno fulani ya Kigiriki (kama gno’sis, maarifa, na ple’roma, ujazi) ili kukanusha madhehebu ya kimaarifa. Vyo vyote iwavyo, kwa uhakika Paulo alikuwa akipambana na mawazo fulani ya kuasi imani ambayo baadaye yalikuzwa na madhehebu za kimaarifa. Wafuasi wa madhehebu ya kimaarifa, ambao walisitawi sana wakati wa karne ya pili W.K., walikuwa wenye imani mbili. Waliamini kwamba asili ya vitu vyote ni mbovu na kwamba roho ni njema. Walishikilia maoni ya kwamba wokovu unakuja kupitia “maarifa” (gno’sis) ya mafumbo ya kiroho. Imani yao ya kwamba mwili wenye nyama ni mbovu iliwaongoza wafuate moja ya hali mbili za kupita kiasi: kuunyima mwili mambo mengi mno au kuuingiza mno katika anasa. Ile inayoitwa madhehebu ya Kikristo ya kimaarifa ilifanya ile ‘njia ya kweli itukanwe’ sana.

9. Taja na ueleze madhehebu nyingine za kwanza-kwanza za Ukristo wa kuasi imani.

9 Kati ya madhehebu nyingine za kwanza-kwanza walikuwako Wamarshoni, wafuasi wa Marshoni, mwana wa “askofu” Mkristo aliyekuwa mwasi-imani katika Asia Ndogo. Marshoni aliamini miungu wawili, mmoja akiwa ni Mungu wa “Agano la Kale” asiye mkamilifu na mwingine Mungu wa upendo aliyefunuliwa wazi katika “Agano Jipya,” au, tuseme aliamini sehemu fulani za maagano hayo ambazo alikubaliana nazo (mengine ya maandishi ya Paulo na Luka). Madhehebu nyingine ya karne ya pili ilikuwa ya Montano. Montano alikuwa “nabii” wa Asia Ndogo aliyehubiri kwamba kuja kwa pili kwa Kristo kulikuwa karibu sana na kwamba angeweka Yerusalemu Mpya katika Pepuza, karibu na mji wa kisasa wa Ankara, Uturuki. Yeye alilaumu mamlaka iliyoendelea kuongezeka ya jamii ya viongozi wa kidini wa Ukristo wenye uasi-imani pamoja na ukosefu wa adili wa viongozi hao. Tertulliani akaja kuwa Mmontani. Vikundi vingine viwili vyenye kupinga ukosefu wa adili kati ya wenye kuitwa Wakristo na kuachiliwa kwa waasi-imani vilikuwa Wanovatia wa karne ya tatu na Wadonati wa karne ya nne. Lakini, vikundi vyote hivyo viwili vyenye kupinga viliyakubali yale makosa makubwa-makubwa ya mafundisho yaliyofuatwa na makanisa yaliyokuwa yameanzishwa zamani.

“Mtu wa Kuasi” Anaanza Kujipanga

10. Ni nani wanaopaswa kutiwa kati ya “walimu wa uongo’’ ambao ‘wanaingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu’?

10 Madhehebu zote hizo, na nyingine ambazo hazikutajwa, zilikuwa namna mbalimbali za Ukristo wa kuasi imani. Lakini watu waliozitokeza si wale “walimu wa uongo” peke yao ambao ‘waliingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu.’ (2 Petro 2:1-3, NW) Petro pia alitabiri kwamba ‘wengi wangefuata matendo yao ya mwenendo mpotovu.’ Sasa hivi tu tumeona kwamba nyingine za madhehebu hizi za kwanza zilianzishwa ili kuupinga mwenendo mpotovu wa jamii ya viongozi wa kidini waliokuwa na mamlaka nyingi. Kwa hiyo viongozi hao wanapasa pia kuhesabiwa kati ya “walimu wa uongo” kisha makanisha yao yahesabiwe kuwa “madhehebu zenye kuharibu.”

11. Ni jamii gani mpya iliyokuwa ikianza kujiinua, na Paulo alikuwa ametabirije jambo hilo?

11 Kama ilivyokwisha kusemwa, madhehebu zote hizo za uasi-imani zilikuwa zikishindania kuwa na ukubwa unaozidi wa zile nyingine. Kila madhehebu ilifanya jitihada ili hiyo peke yake ihesabiwe kuwa ndiyo “ya kiorthodoksi” (ya kanuni inayofaa), “ya kimitume” na “ya kikatoliki” (ya ulimwengu mzima), na basi ikazichukua zile nyingine kuwa madhehebu zenye kujitenga. Wakati uo huo, jamii ya viongozi wa kidini ilikuwa ikijaribu kujiinua iwe juu ya watu wale wengine wa kundi katika yale makanisa makubwa zaidi na yenye nguvu nyingi zaidi. Akisema habari ya uasi-imani (ukengeufu) huo na kutokea kwa jamii ya viongozi wa kidini wenye mamlaka nyingi, mtume Paulo aliandika hivi: “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana [siku ya Yehova] haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.”​—2 Wathesalonike 2:2-4.a

12. (a) “Mtu wa kuasi” ni nini, na ni wakati gani “mtu” huyo alipofunuliwa wazi kwa ukamili? (b) Ni hatua gani zilizoongoza kwenye ukuzi kamili wa jamii ya viongozi wa kidini? (c) Eleza namna ulivyo mfumo wa utawala wa viongozi wa kidini.

12 Uasi-imani huo “tayari unafanya kazi” siku za Paulo. Lakini, ulifunuliwa kwa ukamili baada tu ya kifo cha mitume wa kweli wa Yesu, wakati “kizuizi” cha kuwapo kwao kilipoondolewa. (2 Wathesalonike 2:6, 7, NW) Jamii ya viongozi wa kidini ilianza kutokea kidogo kidogo. Katika mwanzo wa karne ya pili W.K., Ignasho, “askofu” wa Antiokia, aliandika juu ya utawala wa viongozi wa kidini wenye vyeo vitatu, wa maaskofu, wapresbiteri (mapadre) na mashemasi. “Mtu wa kuasi” alikuwa akianza kufanyika. Lakini “baba wa kanisa” ambaye kwa kweli ndiye aliyefanya mpango jamii ya viongozi wa kidini ikawa mfumo wa utawala wa viongozi wa kidini alikuwa Sipriano, “askofu” wa Carthage, Afrika ya Kaskazini, aliyekufa mwaka wa 258 W.K. Kamusi yenye kufafanua maneno inayoitwa Dictionnaire de Theologie Catholique inasema kwamba Sipriano alifanya mpango kukawa na utawala wa viongozi wa kidini wenye vyeo saba, cheo kilicho kikubwa zaidi kikiwa cha askofu. Chini yake walikuwako mapadri, mashemasi, mashemasi wadogo, watumikaji wa altare, wasomaji na wenye kutoa sala za kufukuza mashetani. Cheo cha nane, mtumishi wa lango, au bawabu​—kiliongezwa baadaye katika Kanisa la Magharibi, la Kilatini au la Kiroma, hali Kanisa la Mashariki, au la Kigiriki, lilibaki likiwa na utawala wenye vyeo vitano. Hivyo, kufikia karne ya tatu W.K. “mtu wa kuasi” mwenye kufanyizwa na watu wengi, yaani jamii ya viongozi wa dini ya Kikristo yenye kuasi imani, ‘alifunuliwa’ kwa ukamili. Jamii hiyo imeendelea kuwako muda wa karne zote katika makanisa yote na madhehebu za Jumuiya ya Wakristo ambazo zina huduma ya pekee au jamii ya viongozi wa kidini.

“Madhehebu Zenye Kuharibu” Wakati wa Mwisho

13. Ni kwa njia gani mbili madhehebu za Jumuiya ya Wakristo zinajithibitisha kuwa “zenye kuharibu”?

13 Katika Kigiriki cha kwanza, maneno ya Petro “madhehebu zenye kuharibu” yanamaanisha kwa halisi “madhehebu za uharibifu.” Maneno hayo yana maana mbili kubwa. Madhehebu na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yameuharibu Ukristo safi, ile “njia ya kweli.” Pia hizo ni “madhehebu za uharibifu” kwa sababu walimu wazo wa uongo ‘wanajiletea wenyewe uharibifu wa haraka’ na pia wanauleta juu ya wale ‘wanaofuata matendo yao ya mwenendo mpotovu.’ Petro anaongeza hivi: “Lakini kwa habari yao [walimu wa uongo], ile hukumu ya tangu zamani haisongi polepole, wala kuharibiwa kwao hakusinzii.” (2 Petro 2:1-3, NW) Huo “uharibifu wa haraka” utawapata kwenye “dhiki kubwa” inayokaribia mbio-mbio.​—Mathayo 24:21.

14. Ni wakati gani yule “mtu wa kuasi” ataharibiwa, na uharibifu huo utathibitisha nini?

14 Akionyesha kwamba “mtu wa kuasi” ambaye ni jamii yenye watu wengi hangeharibiwa mpaka wakati wa “kuwapo” kwa Kristo, mtume Paulo aliandika hivi: “Huyo asiyefuata sheria atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamharibia mbali kwa roho ya kinywa chake na kumfanya awe hayuko kwa udhihirisho wa kuwapo [pa.rou.sías] kwake.” (2 Wathesalonike 2:8, NW) Ndiyo, uharibifu wa “mtu wa kuasi” aliye jamii ya viongozi wa kidini, pamoja na sehemu ile nyingine yote ya milki ya Shetani ya dini za Kibabuloni, utakuja ukiwa “udhihirisho” wa kustaajabisha wa “kuwapo” kwa Kristo, au Parousia. Uharibifu huo utamthibitishia rafiki na hata adui kwamba Bwana Yesu yupo katika hali ya kutokuonekana na kwamba ile “dhiki kubwa” iliyotabiriwa imeanza.

Onyo kwa Wakristo wa Kweli

15. Ni onyo gani ambalo Wakristo wanapewa katika mfano wa Yesu wa ngano na magugu?

15 Mfano wa Yesu wa ngano na magugu ulionyesha kwamba makanisa na madhehebu za yale “magugu,” au Wakristo wenye kuasi imani, yangeruhusiwa kukua muda wa karne zote. Ni kufikia tu wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo” tofauti ya wazi ingeonyeshwa kati ya hao Wakristo wa udanganyifu na “wana wa ufalme” walio wa kweli, yaani “ngano.” (Mathayo 13:24-30, 37-40, NW) Lakini, mfano wa Yesu una onyo pia kwa Wakristo wa kweli, wawe ni “wana wa ufalme” waliopakwa mafuta au wawe ni wenzi wao. Yesu alisema hivi: “Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote [vitu vyote vinavyosababisha kikwazo] na hao watendao maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”​—Mathayo 13:41, 42.

16. (a) Ni kazi gani ya kutenganisha ambayo imeendelea tangu mwaka wa 1919? (b) Ni onyo gani zaidi ambalo mitume walitoa, naye Yuda aliongeza maelezo gani?

16 “Ngano” imekwisha kutenganishwa na “magugu” katika shamba la kidini tangu mwaka wa 1919. Lakini, hiyo haimaanishi kwamba tangu wakati huo malaika za Mwana wa Adamu wameacha ‘kukusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi.’ Yuda anatukumbusha kwamba “mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo” walitoa onyo linalofuata: “Katika wakati wa mwisho watakuwapo wadhihaki, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe kwa ajili ya mambo yasiyo ya kumwogopa Mungu.” Kisha Yuda akaongeza hivi: “Hao ndio wanaofanyiza matengano [wanaosababisha migawanyiko, Today’s English Version].”​—Yuda 17-19, NW.

17. Yesu alisema nini kumhusu “mtumwa yule mbaya”?

17 Jambo ambalo Yesu alisema lingewapata watu watendao maasi ambao ‘wanaleta kikwazo’ linatukumbusha juu ya aliyoyasema baadaye juu ya wale ambao wangekataa kumkubali “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” ile jamii ya “ngano” ya Wakristo waliopakwa mafuta ambao Kristo ‘angewaweka juu ya vitu vyake vyote.’ Yesu alionya hivi: “Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia; akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi; bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”​—Mathayo 24:45-51.

18. (a) Watu wengi leo wanaonyeshaje vitabia vya “mtumwa yule mbaya”? (b) Mwisho wao utakuwa nini ikiwa wataendelea ‘kusababisha migawanyiko’?

18 Leo watu fulani wasio washikamanifu wanaonyesha vitabia vya “mtumwa yule mbaya” kwa kusema ndani ya moyo wao, “Bwana wangu anakawia.” Wanajitambulisha wenyewe kuwa katika jamii moja na “wadhihaki” wanaosema: “Ku wapi huku kuwapo kwake kulikoahidiwa?” (2 Petro 3:1-7, NW) Kama vile Yuda alivyoonya, wanajaribu ‘kusababisha migawanyiko.’ (Yuda 19, TEV) Kwa kuilaumu-laumu jamii ya “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ambayo kutoka kwayo walijipatia mara ya kwanza maarifa ya kuijua “njia ya kweli,” wao ‘wanaanza kuwapiga wajoli wenzao.’ Lakini wakiendelea kufuata nia yao ya kuleta migawanyiko, wakati utafika ‘wakusanywe’ na malaika na ‘kuwekewa fungu lao pamoja na wanafiki’ wa Jumuiya ya Wakristo. ‘Hapo ndipo wanalilia na kusaga meno,’ nyakati nyingine wakitumia vifaa vya uenezaji wa habari kueleza mambo ya kuudhi wanayodhani walitendwa.

19. (a) Paulo alisema nini juu ya “madhehebu” kati ya watu wa Mungu? (b) Tunaweza kujithibitishaje kwamba sisi ni watu “waliokubaliwa”?

19 Jambo hilo linatukumbusha maneno ambayo Paulo aliwaandikia Wakorintho: “Kwa maana lazima kuwapo na uzushi [madhehebu, NW] kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.” (1 Wakorintho 11:19) Ndiyo, wo wote leo wakijaribu ‘kuingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu’ kati ya Mashahidi wa Yehova, jambo hilo linawapa nafasi nzuri Wakristo washikamanifu wajithibitishe kuwa watu “waliokubaliwa” na Mungu na Kristo. Wao wanaweza kuonyesha na ni lazima waonyeshe kwamba wanauthamini umoja wa kweli wa Kikristo. Umoja huo utazungumzwa katika makala inayofuata.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate mazungumzo kamili juu ya “mtu wa kuasi,” tafadhali ona sura ya 18 ya kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached (au Le Royaume Millénaire de Dieu S’est Approché kwa Kifaransa), kilichochapwa na Sosaiti.

Wewe Unakumbuka?

◻ Ni wakati gani na namna gani uasi-imani wa Jumuiya ya Wakristo ulivyoanza?

◻ “Mtu wa kuasi” ni nani au ni nini?

◻ Ni kwa njia gani mbalimbali makanisa ya Jumuiya ya Wakristo ‘ni yenye kuharibu’?

◻ Ni onyo gani ambalo Yesu anatoa juu ya “mtumwa yule mbaya”?

[Picha katika ukurasa wa 9]

Yesu alionya kwamba manabii wa uongo wanafanana na mbwa-mwitu waliovaa mavazi ya kondoo

[Picha katika ukurasa wa 12]

Wakristo wa uongo wanafanana na “magugu” yanayofaa kuharibiwa tu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki