Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/1 kur. 15-20
  • Kujipatanisha na “Akili ya Yehova” kama Inavyofunuliwa Sasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujipatanisha na “Akili ya Yehova” kama Inavyofunuliwa Sasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wokovu Kupitia Kuamini na Kuungama
  • Kuendelea Kuwa Mshikamanifu kwa Sababu ya Moyo “Mkamilifu”
  • Baada ya Agano Jipya—Ufalme wa Mileani
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Agano Jipya la Mungu Lakaribia Kutimizwa
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Kufaidika Kutokana na “Mpatanishi Mmoja kati ya Mungu na Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • “Mwana-Mfalme wa Amani” Aelekeza Fikira kwa Walio Nje ya Agano Jipya
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/1 kur. 15-20

Kujipatanisha na “Akili ya Yehova” kama Inavyofunuliwa Sasa

1. Ni taifa gani lililochukua nafasi ya Israeli wa asili, na katika agano gani?

MWANA wa Mungu amechukua nafasi ya nabii Musa, aliyekuwa mpatanishi wa agano la sheria kati ya Mungu na Israeli wa asili. Yesu Kristo amekuwa Mpatanishi aliyewekwa wa agano jipya lililotabiriwa la Yehova. Agano hilo lilifanywa pamoja na taifa lililochukua mahali pa Israeli wa asili wa kale nalo ni Israeli wa kiroho, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Amri Kumi na sheria nyingine zote zilizohusiana nazo za agano lililopatanishwa na Musa mwanadamu asiye mkamilifu ziliandikwa katika hati lakini kwa kweli hazikuandikwa katika mioyo na akili za Wayahudi au Waisraeli wa kimwili waliotahiriwa. Yehova Mungu alipoona agano la Sheria ya Musa likishindwa kwa njia hiyo, alitabiri kufanywa kwa agano jipya kupitia nabii Yeremia, kama ilivyoandikwa kwenye Yeremia 31:​31-34.

2.(a) Yesu alipataje kuwa Mpatanishi wa agano hilo? (b) Ni namna gani na wakati gani lilipoanza kufanya kazi?

2 Yesu Kristo alilitia muhuri hilo “agano jipya” lililoahidiwa kwa damu ya uhai wake mwenyewe alipokufa akiwa na moyo wenye majonzi katika mti wa mateso nje ya Yerusalemu. Ule usiku wa mwisho, alipokuwa akisherehekea kijio chake cha mwisho cha Kupitwa akiwa pamoja na mitume wake waaminifu kwa kutii agano la Sheria ya Musa, Yesu aliwapitishia kikombe cha divai na akakipa maana mpya kwa kusema: “Kikombe hiki [maana yake] ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.” (Luka 22:20; 1 Wakorintho 11:​23-26) Kwa njia hiyo akawa Mpatanishi wa agano jipya hilo, ambalo lilithibitika kuwa “agano lililo bora” kuliko agano la Sheria ya Musa. (Waebrania 8:6; 9:​11-28) Kwa hiyo tangu alipoonyesha ubora wa damu ya uhai wake mkamilifu mbinguni katika mwaka wa 33 W.K. ametumikia akiwa Mpatanishi kwa ajili ya wanafunzi wale ambao Yehova Mungu anaingiza katika agano jipya.​—1 Timotheo 2: 5, 6.

3. Kulingana na Waebrania 10:​15, 16, Yehova anaandika wapi sheria za agano hilo?

3 Mtume anapozungumza juu ya agano jipya, kwenye Waebrania 10:​15, 16, yeye anatumia maneno ya unabii wa Yeremia kulingana na Biblia ya Kigiriki ya Septuagint Version na kuandika hivi: “Zaidi ya hilo, roho takatifu pia inatutolea sisi ushuhuda, kwa maana ikiwa imekwisha kusema: ‘ “Hili ndilo agano ambalo nitawaagia baada ya siku hizo,” anasema Yehova. “Nitaweka sheria zangu katika mioyo [kar·diʹas] yao, na katika akili [di·aʹnoi·an] zao nitaziandika.” ‘ “

4. (a) Moyo wa usemi wa mfano unatofautianaje na akili? (b) Kupatana na Zaburi 119, Wakristo katika agano jipya wanatumiaje moyo na akili? (c) Kuandikwa kwa sheria za Mungu juu ya mioyo na akili kulianzaje?

4 Kulingana na kazi za moyo wa usemi wa mfano na utendaji wa akili, Wakristo wanaoingizwa katika agano jipya kupitia Kristo Mpatanishi wangependa sheria za Yehova kwa mioyo yao, kwa njia hiyo wakichochewa kutii sheria hizo, na pia wangezikumbuka sana sheria hizo za kimungu. Ni kama vile mtunga zaburi alivyosema, “Sheria yako naipenda mno ajabu, ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.” (Zaburi 119:97) Kuingizwa kwa sheria za Yehova katika mioyo ya usemi wa mfano ya wanafunzi wa Kristo na kuandikwa kwazo juu ya akili zao kulianza siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K. Wakati huo ndipo roho takatifu ilipomiminwa juu ya wanafunzi wa Yesu Kristo waliokuwa wakingoja kisha ‘ndimi kama za moto’ zikakaa juu ya vichwa vya wale wanafunzi 120 nao wakaanza kusema kwa lugha za kigeni ambazo hawakuwa wamejifunza wala kusomea. Muujiza ulioje! Kwa sababu ya ushuhuda uliotolewa huko kwa watazamaji waliokusanyika, watu 3,000 walibatizwa wakiwa wanamwamini Yesu kuwa Kristo, au Masihi, wakaingizwa katika agano jipya akiwa ndiye Mpatanishi wao.​—Matendo, sura ya 2; Yoeli 2:​28-32.

5. Ni nani leo ambao wameingizwa katika agano jipya, na ni ushuhuda gani unaowaonyesha kuwa “matawi”?

5 Leo, miaka 1,900 baadaye, kuna mabaki ya “Israeli wa Mungu” ambaye washiriki wake wanaonyesha ushuhuda wa kwamba wameingizwa katika agano jipya, wakabatizwa kwa roho takatifu. Wanaonyesha ushuhuda wa kwamba sheria za Yehova Mungu ziliwekwa ndani ya mioyo yao ya usemi wa mfano na zikaandikwa juu ya akili zao. Wanatimiza matabiri ya Mpatanishi wao yaliyoandikwa kwenye Mathayo 24:14 na Marko 13:10. Wao ni “matawi” katika mzeituni huo wa kiroho uliosimuliwa na mtume Paulo katika Warumi sura ya 11, na wanazaa matunda mengi.

6. (a) Ni sehemu gani nyingine ya “akili” ya Yehova imefunuliwa tangu mwaka wa 1935? (b) “Kondoo wengine” wanatoaje uthibitisho unaosadikisha kwamba wao wanapenda “sheria” ambayo Mungu ametolea siku hizi?

6 Sehemu nyingine ya “akili” ya Yehova imefunuliwa tangu ule mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova uliofanywa Washington, D.C., mwaka wa 1935. Ni nini lililokuwa , katika “akili” ya Yehova kuhusu “mkutano mkubwa” uliotabiriwa katika Ufunuo 7:​9-17? Umati huo uliotabiriwa wa wasifaji wa Yehova Mungu na wa Mwana-Kondoo wake, Yesu Kristo, wanaotumikia Mungu kwenye hekalu lake la usemi wa mfano, umetokea tangu mwaka wa 1935. Wale 840 waliobatizwa baada ya hapo huko Washington siku ya Jumamosi, Juni 1, wameongezewa wengine mpaka sasa. Leo katika sehemu zote za dunia kuna hesabu ya zaidi ya milioni mbili na nusu ya hawa “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, ambao wanashirikiana kwa ukawaida na washiriki waliozaliwa kwa roho wa agano jipya na ambao wanashiriki katika kazi ya kutolea Ufalme ushuhuda kama ilivyotabiriwa kwenye Mathayo 24:14. (Yohana 10:16) Kama mtunga zaburi, wanatoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba wanapenda “sheria” anayotoa Yehova kwa ajili ya huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” na kwamba wanatafakari “sheria” yake katika akili zao na kuihangaikia mioyoni mwao.

Wokovu Kupitia Kuamini na Kuungama

7, 8.  (a) Je! wokovu unategemea maarifa ya kichwani tu? (b) Andiko Warumi 10:​5-10 linasema nini juu ya uhusiano wa utendaji kati ya moyo wa usemi wa mfano na akili?

7 Kupata wokovu, uwe ni wa kuwa kwenye Ufalme wa Yehova katika mbingu au kwenye dunia ya Paradiso chini ya utawala wa mileani wa Yesu Kristo, si shauri la kuwa na maarifa ya kichwani tu, kuweka mambo akilini tu. Mtume Paulo anaonyesha wazi jambo hilo kwenye Warumi 10:​5-10. Humo anazungumza habari ya Wakristo waliokuwa na mioyo ya asili, iliyo halisi, si moyo uliopandikizwa wala hata moyo wa aina ya mashine. Anaendelea kutoa sababu ya wazo lake kwa njia hii:

8 “Kwa maana Musa aliandika juu ya haki itokayo kwa sheria, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa hiyo. Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (yaani, ni kumleta Kristo chini), au, Ni nani atakayeshuka kwenda [kaburini?] (yaani, ni kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.) Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo. Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.”

9. (a) Ni nini linalohusika katika kuokolewa, na kwa sababu gani unajibu hivyo? (b) Lazima Mkristo aamini nini kweli kweli katika moyo wake? (c) Ni nia gani ambayo Waathene walifuata, na kwa sababu gani?

9 Hiyo inaonyesha kwamba jambo hilo linahusu sehemu ya ndani zaidi ya mtu, si akili tu. Si shauri la kukusanya habari tu, kuziwaza-waza akilini kisha kuweza kuzikumbuka kwa kichwa bila kuzitazama. Jambo la maana zaidi si akili pamoja na maarifa yaliyomo; lile linalosukuma mtu kutenda ndilo linalohusika hapa mbele za Mungu. Lazima imani ya Mkristo isukumwe na moyo wa usemi wa mfano. Lazima aamini ufufuo wa Kristo kwa moyo wake wote, kwa sababu ya kuthamini moyoni muujiza huo ambao Mungu Mwenye Nguvu Zote amefanya. Hilo ni jambo ambalo Kristo asingaliweza kujifanyia, wala lisingaliweza kufanywa na mwanadamu mwingine, yaani, lile la Mungu kufufua Mwanaye mfu afikie cheo cha kimbingu cha uzima. (2 Wakorintho 4: 13) Tunakumbuka kwamba Waathene wenye akili nyingi wa siku za mtume Paulo walikuwa na maelekeo ya ‘kufanya dhihaka’ waliposikia juu ya “ufufuo wa wafu,” hali wengine hawakufanya uamuzi wa papo hapo, bali walisema: “Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.” Akili zao zilizojawa na maarifa ziliwazuia kukubali habari hiyo, ingawa ilitegemea mambo ya hakika. Ni wengine wao tu waliokuwa waamini wakajishirikisha na Paulo.​—Matendo 17:​21, 32-34.

10. (a) Lazima moyo utoe msukumo gani? (b) Basi, ni mambo gani mawili yanayotakwa na Yehova?

10 Kwa hiyo lazima moyo wa mtu umsukume kuamini. Lazima azoee imani kwa moyo wake. Akifanya hivyo, hapo moyo​—ule utu wa ndani kabisa​—wa mwenye kuamini utamsukuma afanye ungamo la waziwazi kwa kinywa chake. Lazima azoee imani kwa moyo wake wote. Halafu atafanya tangazo la wazi-wazi kwa kinywa chake, kwa kusukumwa na moyo wenye kuamini. Wakati mwamini anapozamishwa katika maji kuonyesha amejiweka wakf kwa Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo, anafanya tangazo la waziwazi linaloongoza kwenye wokovu. Zaidi ya Yehova Mungu kuchunguza moyo wa usemi wa mfano aone kama humo ndani mna imani inayomtia mtu nguvu za kutenda, anasikiliza pia aone kama tangazo la waziwazi linafanywa.

Kuendelea Kuwa Mshikamanifu kwa Sababu ya Moyo “Mkamilifu”

11. (a) Daudi angewezaje kubaki mshikamanifu kwa Yehova? (b) Ijapokuwa alifanya dhambi, kwa sababu gani Daudi angeweza kusali kama alivyofanya kwenye Zaburi 86:11? (c) Ni nani wamefuata mfano mwema wa Daudi?

11 Daudi wa nyakati za kale alikuwa kama sisi sote wanadamu tuliozaliwa katika makosa na tukachukuliwa mimba katika dhambi, lakini aliendelea kuwa mshikamanifu kwa Mungu wake, Yehova, kwa sababu ya kuwa na moyo wa usemi wa mfano uliokuwa “kamili” kuelekea Mungu wa taifa la Israeli. (Zaburi 51:5) Ushuhuda wa jambo hilo umetolewa katika 1 Wafalme 15:3: “Moyo [wa Abijamu] haukuthibitika kuwa kamili kwa Yehova Mungu wake, kama moyo wa Daudi babu yake.” (NW ) Ni kweli kwamba Daudi alitenda dhambi mbaya sana pamoja na mke wa Uria yule Mhiti, lakini alitubu kwa moyo mweupe na moyo wake ukathibitika kuwa usiogawanyika na usioyumbayumba katika hali ya kujitolea Yehova Mungu wake. (1 Wafalme 15:​4, 5) Basi Daudi alikuwa na sababu nzuri ya kuweza kusali hivi: “Unganisha vizuri moyo wangu uogope jina lako.” (Zaburi 86:​11, NW ) Aliwawekea mfano mwema warithi wake katika uufalme juu ya Israeli, na Mfalme Asa alikuwa mwigaji wa Daudi katika jambo hilo, kwa maana kwenye 1 Wafalme 15:14 tunasoma hivi: “Moyo wake Asa ulikuwa mkamilifu kwa [Yehova] siku zake zote.”

12. Ni nini kinachotaka ushujaa na unyofu, na Hezekia alionyeshaje hivyo?

12 Kwa uhakika ushujaa na unyofu mwingi sana unahitajiwa katika mtu binafsi ili aweze kumsihi sana Mungu Aliye Mtakatifu Zaidi, Mchunguzi wa mioyo ya kibinadamu, kumlalamia ampe rehema zake na fikira za upendo. Lakini hivyo ndivyo Mfalme Hezekia wa Israeli alivyofanya. Alipoambukiwa na ugonjwa ambao kwa uhakika ungemuua usipokatizwa na Mungu wake, Hezekia alisali hivi: “Mimi nakuomba sana, Ee Yehova, ukumbuke, tafadhali, namna nimetembea mbele zako katika ukweli na kwa moyo mkamilifu, na lililokuwa jema machoni pako nimefanya.​—Isaya 38:​3, NW.

13. Inawapasa Wakristo waliopakwa mafuta wakumbuke nini sikuzote, kwa kufuata mfano wa Yesu?

13 Kwa kuwa na mfano wa namna hiyo, Wakristo wapakwa mafuta wa leo ambao wameingizwa katika ‘agano kwa ajili ya ufalme’ pamoja na Yesu Kristo katika mbingu wanapaswa kukumbuka sikuzote wajibu wa kutembea mbele za Yehova “kwa moyo kamili.” Kama Daudi babu yake wa kifalme, Yesu Kristo alipokuwa duniani akiwa mwanadamu mkamilifu alitembea “kwa moyo kamili” mbele za Yehova, Baba yake wa kimbingu. Basi, Yehova Mungu, Mwekaji wa wafalme, alipendezwa sana kumpa utawala katika Ufalme wa kimbingu, akiwa huko atawale kama ‘Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana,’ wanafunzi wake wanaoshika ukamilifu wakiwa wafalme na mabwana wadogo.​—Luka 22:29; Ufunuo 19:16.

14. Ni kwa sababu ya nini “kondoo wengine” wameingizwa katika lile “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja”?

14 “Mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo wanatazamia kuwa ndio wa kwanza kuingia wakiwa hai katika utawala wa mileani wa Yesu Kristo pamoja na watawala wenzake 144,000. (Ufunuo 7:​9, 10; Yohana 10:16; Ufunuo 14:1; 20:​4-6) Tangu mwaka ule wenye matukio makubwa wa 1935 washiriki wa “mkutano mkubwa” huo wamekuwa wakishirikiana na mabaki ya hao warithi wa Ufalme, wanaotembea mbele za Yehova Mungu kwa moyo kamili. Kwa sababu “kondoo wengine” hao wa Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, wanatafuta kutembea mbele za Yehova Mungu “kwa moyo kamili,” sasa wanakuwa “kundi moja” pamoja na mabaki ya warithi wa Ufalme chini ya yule “mchungaji mmoja,” Yesu Kristo. Kwa sababu ya kushika ukamilifu wakiwa na mioyo hiyo iliyounganishwa, iliyo kamili, watakuwa na sehemu yenye pendeleo katika kuiondolea lawama enzi kuu ya ulimwengu mzima ya Mungu ambaye wao ni mashahidi wake, yaani, Yehova.​—Isaya 43:​10, 12.

15. Sisi sote tunaweza kushukuru sasa kwa jambo gani?

15 Kwa njia hiyo sisi sote, tukiwa wanafunzi wa Mwana wa Mungu, Mchungaji Mwema wetu, tunajipatanisha na “akili” ya Yehova kama inavyofunuliwa sasa kwa waabudu wake waliojiweka wakf na kubatizwa. Tunaweza na tunapaswa kushukuru sana kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi katika mbingu ametufunulia lililokuja kwanza kwenye “akili” yake, lisilotokana na mwanadamu ye yote mwenye mwili wa nyama na mifupa! Kwa sababu hiyo tunaongozwa kufikiri kama Yehova kwa habari ya kusudi lake tukufu.

16, 17. (a) Kwenye 1 Wakorintho 2:16 (NW ) ni nini linaloonyeshwa juu ya “akili ya Yehova” na “akili ya Kristo”? (b) Wafilipi 2:​5-8 inafunua nini juu ya “akili” ya Kristo?

16 Tunathamini tuliyoandikiwa kwenye 1 Wakorintho 2:16 (NW ), yaani: “Kwa maana ‘ni nani amepata kuijua akili ya Yehova, hata amfundishe? ’ Lakini sisi tuna akili ya Kristo.” Hapo neno la Kigiriki kwa “akili” ni nous mara zote mbili.

17 Kwa njia isiyoweza kupingwa, “akili” ya Kristo ilipatana na “akili ya Yehova.” Maneno yaliyoongozwa na Mungu kwenye Wafilipi 2:​5-8 yanatusaidia kuchungua “akili” ya hata Mwana wa Mungu kabla hajawa mwanadamu, kwa maana hapo tunasoma hivi: “Iweni na nia [ “akili,” AV; AS; RS] iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya [mti wa mateso].”

18. Ni nini Mwana alilotakwa kufanya ili ajipatanishe na “akili” ya Baba?

18 Yehova Mungu anafikiria akilini mwake kukomboa wanadamu kutoka kifo cha milele, na Mwana wa Mungu aliye mzaliwa pekee alikuwa na nia ya kujipatanisha na akili ya Baba yake wa kimbingu katika jambo hilo, ingawa hilo lingemaanisha kuteswa vikali alipokuwa duniani.

19. (a) Tunaweza kutumiaje mioyo yetu ya usemi wa mfano kuhusiana na “akili” ya Yehova? (b) Ni lazima sasa tutimize nini kuhusiana na “akili ya Kristo”?

19 Vivyo hivyo, ikiwa sisi leo tunataka kujipatanisha na “akili ya Yehova,” lazima tujinyenyekeze kwa njia kama ya Kristo na kujitiisha kwa mapenzi ya Yehova bila kuweka masharti. Hilo linatulazimisha kuwa mashahidi wa Yehova. Halafu, kwa kuchochewa na moyo [kar·diʹa] wenye upendo na ulio mshikamanifu, lazima tutimize lile ambalo Yesu Kristo alifikiria katika akili yake yenye kuona mbali, aliposema: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote,” moja kwa moja mpaka kwenye ule mwisho.​—Mathayo 24:​14, NW; Marko 13:​10, UV.

20. (a) Ni nini sasa kinacholeta umoja wa matendo ulimwenguni pote? (b) Ni mafanikio gani ambayo kundi lililoungana la watu wa Mungu linafurahia sasa?

20 Sisi sote tulio mashahidi waliojiweka wakf na kubatizwa wa Mungu Aliye Juu Zaidi leo tunataka kuwa wa “akili ile ile moja” juu ya pendeleo hilo la utumishi. (Wafilipi 4:​2, NW ) Jambo hilo linaleta umoja wa matendo ulimwenguni pote. Kwa sababu ya sisi kufanya hivyo, Yehova Mungu amebariki “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo na hata mabaki wapakwa mafuta wa warithi wa Ufalme wa Kristo kwa kuwapa mafanikio ya kupendeza sana wanayopata ulimwenguni pote leo katika kukusanya “kondoo wengine” wote na kutolea wanadamu wote onyo la mwisho kabla hajapata ushindi mtukufu na kuiondolea lawama enzi kuu yake ya ulimwengu mzima kwenye ­Har–​Magedoni,​—Ufunuo 16:16.​—Kutoka w9/1/84.

Maulizo fulani ya kurudia:

◻ “Moyo” na “akili” zimehusikaje katika kuandika kwa Yehova “sheria” ya agano jipya?

◻ Ni mambo gani mawili yanayohusika katika kupata wokovu?

◻ Moyo “kamili” unatusaidiaje kuendelea kuwa washikamanifu?

◻ Tunaweza kuonyeshaje kwamba tuna “akili ya Yehova” na “akili ya Kristo” pia?

[Picture on page 17]

Yehova ameandika “sheria” ya agano jipya lake juu ya mioyo na akili za wapakwa mafuta. Kwa furaha, sasa “kondoo wengine” wanajiunga nao katika utumishi mtakatifu

[Picture on page 19]

Hezekia alionyesha moyo “kamili” alipokuwa akipatwa na shida. Sisi pia tunaweza kufanya hivyo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki