Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/15 kur. 13-18
  • “Israeli Wote” Wanaokolewa Wabariki Wanadamu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Israeli Wote” Wanaokolewa Wabariki Wanadamu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova​—Watu wa Namna Gani?
  • Ni wa Kubariki, Si wa Kulaani
  • “Israeli Wote Wataokolewa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • ‘Watu wa Mataifa Wataiendea Makundi Makundi’ Ibada Yenye Kutoa Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • “Roho ya Uhai Itokayo kwa Mungu Ikawaingia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Ambayo Kuzaliwa kwa Taifa hilo Kumemaanisha kwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/15 kur. 13-18

“Israeli Wote” Wanaokolewa Wabariki Wanadamu Wote

1. Kwa sababu gani Jamhuri ya Israeli isitazamie kwamba kwa kuwa hiyo imo katika Umoja wa Mataifa ndiyo itakayotumiwa na Mungu kubariki wanadamu wote?

YEHOVA alimwahidi Abrahamu kwamba jamaa na mataifa yote ya dunia yangepata baraka kupitia uzao wa huyo mzee wa ukoo aliyekuwa mwaminifu. (Mwanzo 12:3; 22:17, 18) Lakini ahadi hizo zilizofanywa katika karne ya 20 kabla ya Wakati wa Kawaida wetu hazimaanishi kwamba Mungu atabariki Umoja wa Mataifa, ulioufuata Ushirika wa Mataifa ambao umekufa. Basi, kwa sababu Jamhuri ya Israeli ya kisasa ni mshiriki wa Umoja wa Mataifa isitazamie kutumiwa na Mungu wa Israeli ya kale katika kubariki wanadamu wote. Kwa kweli Umoja wa Mataifa umejiweka mahali ambapo ni Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa “uzao” wa Abrahamu unapasa kuwa. Kwa hiyo, umoja huo ndio “chukizo la uharibifu” la kisasa. (Mathayo 24:15) Umoja wa Mataifa si baraka, hata kama viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo na walimu wa dini ya Kiyahudi wanaomba mbingu zilibariki tengenezo hilo. Kwa kweli huo ni “sanamu ya mnyama,” tengenezo la kisiasa na kibiashara linaloonekana la “mungu wa huu mfumo wa mambo,” Shetani Ibilisi. Kwa hiyo karibuni Umoja wa Mataifa utaharibiwa pamoja na tengenezo hilo lililo kama mnyama.​—Ufunuo 13:1-18, UV; 2 Wakorintho 4:4, NW.

2. Katika mwendo wao, mabaki ya “Israeli wote” wanatofautianaje na Jamhuri ya Israeli?

2 Kwa sasa, Jamhuri ya Israeli inajipigania isije ikamalizwa na washiriki wengine wa Umoja wa Mataifa. Lakini mabaki ya “Israeli wote” hayaigi Jamhuri ya Israeli. (Warumi 11:26) Mabaki hayo hayaabudu “sanamu ya mnyama.” Bali, Waisraeli wa kiroho hao wanafunua wazi namna Umoja wa Mataifa ulivyo kulingana na maoni ya Mungu​—kitu cha bandia kinachoongoza watu wakitegemee badala ya Ufalme wa Yehova ulio mikononi mwa Yesu Kristo. Kwa sababu hiyo mabaki ya “Israeli wote” yanabaki yakiwa sehemu ya tengenezo la ulimwengu mzima la Yehova. Tayari mabaki ya ‘uzao wa kiroho wa Abrahamu’ yanathibitika kuwa baraka kwa mataifa na jamaa zote za wanadamu. Kwa hiyo ahadi za kiunabii za Yehova zimekuwa za kweli.

3, 4. Miaka kama 2,700 kabla ya 1914, Yehova alimwongoza Isaya kwa roho yake aandike nini juu ya “mataifa yote”?

3 Miaka zaidi ya 2,700 iliyopita, Yehova Mungu alielekeza mbele kwenye kipindi ambacho vifaru vya vita na ndege zingetumiwa mara ya kwanza katika pigano, na wakati ambao ujuzi wa kupigana katika mahandaki ungeongezeka, askari walazimike kujifunika usoni ili kujikinga na hewa yenye sumu, kisha mizinga mikubwa yenye kutupa risasi mbali itumiwe katika pigano la ujumla, kama ule uliotumiwa na Wajeremani katika Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Ndiyo, karne karibu 27 kabla ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, Yehova Mungu alimwongoza nabii Isaya kwa roho yake aeleze jambo jingine ambalo lingekuwa likitukia wakati huo, akisema:

4 “Hili ni neno aliloliona Isaya mwana wa Amozi katika habari za Yuda na Yerusalemu. Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya [Yehova] utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa [Yehova], nyumbani kwa Mungu wa Yakobo [Israeli], naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la [Yehova] katika Yerusalemu. Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe. Enyi wa nyumba ya Israeli, njoni, twende katika nuru ya [Yehova].”​—Isaya 2:1-5.

5. Kwa sababu ya mwendo ambao Jamhuri ya Israeli imefuata, ni lazima unabii wa Isaya unaohusu ‘nyumba ya Yehova’ uonwe kwa njia gani?

5 Leo hatuuoni unabii huo mzuri ajabu ukitimizwa katika Yerusalemu wa Mashariki ya Kati, ule mji mkuu wa Jamhuri ya Israeli. Juu ya ule uliokuwa ukiitwa Mlima Sayuni, hatuoni hekalu lo lote la Yehova, bali Kuba la Mwamba la Kiislamu na musikiti uliowekwa wakfu kwa Allah. Watalii kutoka mataifa mengi wanatembelea mahali hapo pa kidini, si kwa kusudi la ibada, bali kukagua tu jengo hilo la Kiislamu lililo la kupendeza macho. Basi, ni jambo lisiloweza kukanwa kwamba sasa katika “siku za mwisho” za mfumo huu wa mambo wenye ugonjwa wa kifo, unabii wa Isaya hautimizwi hata kidogo katika nchi ya kisasa ya Israeli. Siyo inayokusudiwa kuwa “Israeli wote” watakaookolewa ili kubariki wanadamu wote, kwa utimizo wa ahadi ambayo Yehova alitolea Abrahamu. Kwa hiyo, maneno ya kiunabii yanayosema ‘mlima wa nyumba ya Yehova’ yanapasa kuonwa kulingana na maoni ya kiroho kwa habari ya “Israeli wa Mungu.”​—Wagalatia 6:16.

6. (a) Petro alionyeshaje namna taifa la “Israeli wa Mungu” lilivyo? (b) Ni wakati wa tukio gani la ulimwengu “mataifa yote” yalianza kumiminika yakipanda kwenye ‘nyumba ya Yehova’?

6 Huyo “Israeli wa Mungu” ni taifa la kiroho, kama mtume Petro alivyoonyesha kwa kuandika hivi: “Ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.” (1 Petro 2:9) Mabaki ya kisasa ya “taifa takatifu” hilo ni ishara ya kuonyesha ‘nyumba ya Yehova’ na ndiyo kiini cha Mashahidi wa Yehova leo. Yalikuwa yameingia miaka 21 katika “siku za mwisho”​—wakati utawala wa kifashisti wa Katoliki ya Roma na ule wa Nazi ya Hitler ulipokuwa ukivuma sana katika Ulaya​—wakati “mataifa yote” yalipoanza kumiminika kuielekea ‘nyumba ya Yehova’ ya kiroho ambayo kwa njia ya mfano ilikuwa imeinuliwa na Mashahidi wa Yehova juu ya milima.

7. Kwa sababu gani halikuwa jambo dogo tu wakati mataifa yalipoanza kumiminika yakipanda kwenye ‘nyumba ya Yehova’?

7 Mwanzo huo wa maana ulikuwa na mkusanyiko mkuu mwishoni mwa masika ya mwaka wa 1935 huko Washington, D.C., ule mji mkuu wa United States ya Amerika. Wakati wa hotuba mashuhuri sana kwenye mkusanyiko huo, mshiriki wa “Israeli wote”​—J. F. Rutherford, aliyekuwa msimamizi wa Sosaiti wakati huo​—alisahihisha ufahamu wenye makosa uliokuwa umekaa kati ya Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote. Alionyesha kwamba “umati mkubwa,” au “mkutano mkubwa,” ambao ungekusanywa kutoka sehemu zote za jamii ya mwanadamu na ambao ungeabudu Mungu kwenye hekalu la kiroho Lake (kwa kuwa hekalu halisi katika Yerusalemu lilikuwa limeharibiwa na Warumi mwaka wa 70 W.K.) Ungekuwa jamii ya kidunia. (Ufunuo 7:9-17, Authorized Version) Jamii hiyo ilikuwa na taraja la kuokoka Har–​Magedoni na kuingia mfumo mpya wa mambo wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo unaokaribia, naye amekuwa akitawala katika mbingu tangu mwaka wa 1914.

8. (a) Ni tukio gani lenye kuanza kipindi kipya lililofanyika kwenye mkusanyiko wa Washington, D.C., mwaka wa 1935? (b) Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba “mataifa yote” yanamiminika yakipanda kwenye ‘nyumba ya Yehova’?

8 Itikio la nuru hiyo iliyofunuliwa lilianza kipindi kipya. Kwenye kusanyiko hilo la kutazamisha, wakusanyikaji 840 walibatizwa kuonyesha wamejiweka wakfu kwa Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo. Haikuhakikishwa ni mataifa mangapi yaliyowakilishwa katika kikundi hicho, lakini wao walifikiria tumaini la kuishi katika paradiso ya kidunia. Leo, miaka zaidi ya 49 baadaye, hesabu ya Mashahidi wa Yehova ni kubwa sana kuliko “Israeli wote.” Wao ni watendaji katika nchi 205 katika sehemu zote za dunia. Basi, ni hesabu kubwa ya “mataifa yote” inayomiminika kuelekea nyumba ya ibada ya Yehova iliyoinuliwa juu.

Mashahidi wa Yehova​—Watu wa Namna Gani?

9. Tofauti na Jamhuri ya Israeli, ni mwendo gani ambao Mashahidi wa Yehova wamefuata kwa utimizo wa Isaya 2:4?

9 Kwa kulinganishwa na hali ambayo imekuwa katika Jamhuri ya Israeli, tunakuta Mashahidi wa Yehova wakiwa watu wa namna gani leo? Je! wana silaha kama jamhuri hiyo ili wafanye vita ya kimwili juu ya wale wanaotisha kuwamaliza? Hapana! Bali, wao wako kabisa kama namna ya watu waliotabiriwa kwenye Isaya 2:4. Kwa sababu wanainua ibada ya Yehova kwenye nyumba ya kiroho ya Mungu, kwa usemi wa mfano wamefua panga zao zikawa majembe na mikuki yao ikawa miundu. Wanamtumaini Yehova Mungu kuwa Mlindaji wao wanapoiga Kiongozi wao, Yesu Kristo. Ingawa wametoka katika karibu mataifa yote ya dunia, ‘hawaachi chuki za kitaifa ziwaongoze; wala hawajitii katika siasa za kilimwengu. Kwa kweli, wameacha kutumia silaha za kimwili za kujikinga na za kushambulia. Wanaamini aliyosema Yesu Kristo​—kwamba Ufalme wake si “sehemu ya ulimwengu huu.” Ama sivyo, wanafunzi wake wangeupigania kwa silaha za kimwili zilizofanyiwa maendeleo kuliko zote za kijeshi.​—Yohana 18:36, NW.

10. (a) Ni katika vita gani peke yake wanamohusika Mashahidi wa Yehova? (b) Ni “amri mpya” gani ambayo Mashahidi wanatii, na wanafanyaje hivyo?

10 Bali, Mashahidi wa Yehova wanahusika katika vita ya kiroho tu. Pigano lao ni juu ya roho waovu katika mahali pa kimbingu. Kwa hiyo silaha zao si za kimwili, za kumwaga damu. (Waefeso 6:10-18) Vita yao si juu ya wanadamu, na kwa uhakika wao hawapigani na ndugu zao za kiroho ndani ya tengenezo la Yehova. Wanatii amri ya Yesu Kristo ya kupenda ndugu zao za kiroho, sawa na vile yeye alivyotupenda, hata kufikia hatua ya kutolea wanafunzi wake uhai wake wa kibinadamu. Kufanya hivyo kunapatana na “amri mpya” ambayo Yesu aliwapa wafuasi wake, kwamba wapendane kama alivyowapenda.​—Yohana 13:34.

11. Upendo ulioonyeshwa na Mashahidi wa Yehova unatimiza sheria gani?

11 Mashahidi wa Yehova wanasukumwa na namna ya upendo unaotimiza Sheria iliyotolewa kupitia nabii Musa. Upendo huo hauumizi mtu ye yote nao unazidi kutendea watu “fadhili,” kulingana na maana ya karne ya 20 ya neno hilo. Katika Biblia, maneno ya Kiebrania na Kigiriki ya kusema “upendo” yanamaanisha mengi kuliko “fadhili” za kawaida tu.​—Ona 1 Wakorintho, sura ya 13, King James Version; Douay Version ya Kikatoliki.

Ni wa Kubariki, Si wa Kulaani

12. Je! hesabu kamili ya washiriki wa “Israeli wote” ilihitajiwa kabisa iwe mbinguni kabla kubarikiwa kwa “mataifa yote” hakujaweza kuanza?

12 Kutokana na yaliyotangulia tunaweza kuona kwamba kumekuwa hakuna uhitaji mabaki ya “Israeli wote” waingie mbinguni wawe pamoja na aliye Mkuu wa “uzao” huo, Yesu Kristo, ndipo jamaa na mataifa yote waanze kubarikiwa kupitia “uzao” wa Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu. Kwa karibu nusu-karne sasa, washiriki wa jamaa na mataifa ya dunia wamekuwa wakipokea baraka kutoka ule “uzao” ulioahidiwa wa Abrahamu. Tayari “kondoo wengine” zaidi ya milioni mbili na nusu wamekusanywa pamoja kuwa “kundi moja” pamoja na mabaki ya wafuasi wa Mchungaji Mwema waliozaliwa kwa roho ambao wana tumaini la kuishi mbinguni.​—Yohana 10:16.

13. Yesu alikuja hekaluni akiwa na kusudi gani kwa “kondoo wengine,” na karibuni nia yake kuwaelekea itafikishwaje kwenye upeo?

13 “Kondoo wengine” walio wabarikiwa wamependelewa kwa kupewa tumaini la kuirithi Paradiso itakayorudishwa duniani wakati wa Utawala wa Mileani wa Kristo Mfalme, tangu mwanzo wake. Kwa hiyo wakati Yesu Kristo, akiwa ndiye “mjumbe wa agano” wa Yehova, alipokuja kwenye hekalu la kiroho ili kuanza hatua za hukumu, alikuja kwa kusudi la kubariki “kondoo wengine,” si kuwalaani. (Malaki 3:1-3) Baraka hiyo itafikishwa kwenye upeo watakapohifadhiwa waipite “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” inayokaribia kupata adui zake za kidunia watakaokuwa wamekusanyika “Har–​Magedoni.” (Ufunuo 16:14, 16) Nyakati za kale mji wa Megido ndio uliokuwa mahali ambapo Yehova Mungu alijipatia ushindi mara nyingi. (Yoshua 17:11; Zekaria 12:11) Katika mahali pa mfano pa Har–​Magedoni, Mungu atajipatia ushindi ulio mkubwa zaidi ya wote, ajiletee utukufu wa milele. Jemadari wake atakuwa ni Mwanaye aliyepandishwa cheo, Yesu Kristo.​—Ufunuo 19:11-21.

14. (a) “Kondoo wengine” wana sababu ya kufurahia wokovu wa nani? (b) Tayari “kondoo wengine” ni wangapi?

14 “Kondoo wengine” watalindwa waupite wonyesho huo ulio wa kustaajabisha zaidi wa uwezo na fahari ya kimungu. Watazamaji wote watakaoliokoka pigano hilo la kukata maneno watafurahi kama nini kwamba mabaki ya “Israeli wote” ‘waliokolewa’ wakati wa kipindi cha amani kati ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza na Vita ya Ulimwengu ya Pili! Tangu masika ya mwaka wa 1935 na kuendelea Israeli hao waliookolewa wameongezewa “umati mkubwa” usio na hesabu iliyotajwa wazi. Hao wakiwa ni “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, hesabu yao sasa inaelekea kuwa milioni tatu. Wamekuwa wakitoka katika “kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha” za wanadamu, kwa utimizo wa ahadi ambayo Yehova Mungu alimtolea yule aliyetangulia kuwa mfananishi wake, yaani, Abrahamu “rafiki” yake. (Ufunuo 7:9-17; Yakobo 2:23) Na mkusanyo wa hao “kondoo wengine” haujamalizika bado. Hatujui mwishowe watakuwa wangapi wakati Mchungaji Mwema atakapokuwa amekwisha kuwakusanya kabla ya uharibifu wa Babuloni Mkuu na vita ya Mungu juu ya hawara za kisiasa za mwanamke huyo.​—Ufunuo 17:1–18:24.

15. Ushirika wa “kondoo wengine” pamoja na mabaki ya “Israeli wote” ni mwanzo wa ubarikiwa gani?

15 Ushirika wa “kondoo wengine” pamoja na mabaki ya “Israeli wote” katika “kundi moja” chini ya Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, yule aliye Mkuu katika “uzao” wa Abrahamu, umekuwa mwanzo wa jambo fulani. Jambo gani? Umekuwa mwanzo wa baraka kamili ambayo “Israeli wote” wangali wataleta juu ya “kondoo wengine” hao wakati wa Utawala wa Mileani wa Yesu Kristo, ambamo wataingia kwa kuokoka wakiwa chini ya ulinzi wa kimungu.

16. Kwa sababu gani “kondoo wengine” wamepiga moyo konde waendelee kumtumikia Yehova wakiwa kando ya mabaki ya “Israeli wote”?

16 Kwa kutimiza Ufunuo 7:14-17, “kondoo wengine” wamekwisha ‘kufua mavazi yao na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.’ Hiyo ndiyo sababu wanaruhusiwa kumwabudu Mungu “mchana na usiku katika hekalu lake,” kwa njia ya kiroho. Ndiyo, tayari “Mwana-kondoo wa Mungu,” Yesu Kristo, anawalisha chakula cha kiroho hivi kwamba ‘hawaoni njaa tena.’ (Yohana 1:29) Tena, Mchungaji wao mwaminifu anawaongoza kwenye “chemchemi za maji yenye uhai,” yaani, uzima katika dunia ya Paradiso. Wakiwa na shukrani kwa ajili ya baraka zote wanazopokea tayari kupitia mabaki ya “Israeli wote,” “mkutano mkubwa” wataendelea kumtumikia Yehova wakiwa kando ya mabaki hayo yenye uaminifu. “Kondoo wengine” hao watafanya hivyo katika lile “kundi moja” lililo chini ya “mchungaji mmoja” kwa faida ya Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Yesu Kristo. Wao wamepiga moyo konde wafanye hivyo mpaka adui zote za Ufalme wawe wameangamizwa watoke usoni pa dunia, ambapo ni “mahali pa kuweka miguu” ya Mungu.​—Isaya 66:1; Mathayo 5:34, 35; Matendo 7:49.

Wewe Ungejibuje?

◻ Kwa sababu gani Jamhuri ya Israeli siyo njia ya Yehova ya kubarikia wanadamu wote?

◻ Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba sasa “mataifa yote” yanamiminika yakipanda kwenye ‘nyumba ya Yehova’?

◻ Mashahidi wa Yehova wamekuwaje wakitimiza Isaya 2:4?

◻ Ni nia gani Yesu Kristo aliyo nayo kuelekea “kondoo wengine,” na karibuni itafikishwaje kwenye upeo?

◻ Ni ubarikiwa gani umeanza katika ushirika wa “kondoo wengine” pamoja na mabaki ya “Israeli wote”?

[Picha katika ukurasa wa 14, 15]

“Katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.”​—MWANZO 22:18.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Mashahidi wa Yehova wana upendo kati yao wenyewe na ‘wamefua panga zao zikawa majembe’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki