Makusanyiko ya Wilaya ya 1985
MWAKA baada ya mwaka Mashahidi wa Yehova wamekuwa na vichwa vya kusanyiko la wilaya lao la kila mwaka vikitegemea sehemu za msingi za imani na utendaji wao mbalimbali. Kati ya vichwa hivyo kulikuwako “Imani Ishindayo,” “Wafanya Kazi Wenye Furaha,” “Upendo wa Kimungu,” “Ushikamanifu kwa Ufalme,” na “Umoja wa Ufalme.” Kichwa kilichochaguliwa kwa ajili ya kusanyiko la wilaya la 1985 nacho pia kinategemea utendaji wao wa msingi, yaani, “Washika Ukamilifu” Kusanyiko.
Kushika ukamilifu ni jambo la maana sana! Ni jambo la maana sana hata kwamba Yehova alikubali mwito wa ushindani kuhusu suala hilo, Yehova akiwa na uhakika kabisa kwamba kati ya viumbe vyenye akili vya dunia, kungekuwako wale ambao wangeshika ukamilifu, wamthibitishe Yehova Mungu kuwa wa kweli na Ibilisi kuwa mwongo mkubwa, mbaya sana.
Kushika ukamilifu si jambo rahisi, lililo mboga. Kushika ukamilifu si kufuata mambo yasiyoleta upinzani au yanayokuja kwa asili. Akiwa anajua yanayohusika Shetani Ibilisi anafanya yote awezayo yaliyo kwenye uwezo wake awafanye watumishi wa Yehova wavunje ukamilifu wao. Na si kwamba tunapingwa na Shetani na mashetani wake katika jitihada zetu za kushika ukamilifu bali pia tuna lazima ya kushindana na ulimwengu wake mbovu unaoleta vishawishi na mikazo ya kila namna juu yetu. Zaidi ya hayo, tuna maelekeo yetu mabaya ,tuliyorithi ya kushindana nayo.
Ili tushike ukamilifu kwa kupinga maadui hao watatu kwa kufanikiwa, tunahitaji msaada wote tunaoweza kupata. “Washika Ukamilifu” Kusanyiko limekusudiwa litoe msaada mkubwa zaidi uwezekanao kwa wote wanaohangaikia kushika ukamilifu wao kwa Yehova Mungu na kuthibitisha Ibilisi kuwa mwongo. Kama ambavyo imekuwa katika miaka mingine kusanyiko litaanza, katika nchi nyingi, Alhamisi alasiri na litaendelea kwa siku nne. Fanya mipango sasa uhudhurie siku zote nne, na uje umejitayarisha kufaidika kikamili kutokana na programu na pia ushiriki katika utendaji mwingine mbalimbali wa kusanyiko.