Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 2/15 uku. 31
  • “Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Wewe Waalikwa Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Hudhuria “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1987
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 2/15 uku. 31

“Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya

MTUME Paulo aliandika hivi: “Katika siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa. Kwa maana watu watakuwa . . . wapenda raha kuliko kuwa wapenda Mungu, wenye umbile la kujitoa kimungu lakini wakithibitika kuwa bandia kwa nguvu zayo.”​—2 Timotheo 3:1-5, NW.

Maneno hayo yanaeleza kwa usahihi sana jinsi walivyo wengi sana kati ya wale wanaodai kuwa ni Wakristo! Kulingana na kasisi mmoja, “leo makanisa mengi mno yamekuwa . . . vitovu vya vitumbuizo.” Kwa utofauti mkubwa, wafuasi wa kweli wa Kristo ni watu “walio na bidii katika matendo mema.” (Tito 2:14) Wafuasi wa Yesu ndio “chumvi ya dunia” na “nuru ya ulimwengu.”​—Mathayo 5:13, 14.

Mikusanyiko yetu ya kila mwaka, ya wilaya, ya kitaifa, na ya kimataifa, ni pande fulani za ibada yetu zinazotufanya kuwa watu wasio na kifani. Kichwa chenyewe cha mikusanyiko yetu ya wilaya ya 1989, “Kujitoa Kimungu,” kinaelekeza kwenye sifa moja ya ibada yetu inayotufanya tutokeze wazi kuwa tofauti.

Maandiko yanakazia umaana wa kujitoa kimungu. Mkusanyiko huu utakuwa fursa zaidi ya ‘kuwa ukijizoeza mwenyewe kujitoa kimungu kuwa shabaha yako. Kwa maana mazoezi ya kimwili yana manufaa kidogo; lakini kujitoa kimungu kuna manufaa kwa mambo yote, kwa kuwa kuna ahadi ya uhai wa sasa na ule ambao utakuja.’ (1 Timotheo 4:7, 8, NW) Na 1 Timotheo 6:6 inataarifu zaidi hivi: “Kwa hakika, humaanisha pato kubwa, huku kujitoa kimungu pamoja na ujitoshelevu.” Yesu Kristo ndiye kielelezo bora kabisa cha kujitoa kimungu.​—1 Timotheo 3:16, NW.

Neno la Kigiriki lililofasiriwa “kujitoa kimungu” ni eu·seʹbei·a. Kwa Wakristo huko ndiko “kujitoa kimungu ambako ni kwa aina bora zaidi.” Kujitoa kimungu ni “kuwa na moyo wote na bidii katika kufanya wajibu wa kidini.” Kujitoa kimungu ni itikio la moyo ambalo litachochea mtu aishi kwa njia inayofurahisha Mungu. Humaanisha kujielekeza kwa Mungu. Ni lazima tuwe waangalifu kama nini kwamba ingawa sisi tumo katika ulimwengu, tusiwe sehemu yao! Kuhofu Mungu kutatuzuia tusitende ubaya, lakini kujitoa kimungu hutusukuma tutende linalofurahisha Mungu. Jambo la kutia moyo ni kwamba, kwenye 2 Petro 2:9 tunahakikishiwa kwamba “Bwana [Yehova, NW] ajua kuwaokoa watauwa [watu wenye kujitoa kimungu NW] na majaribu.”

Ili mtu awe na kujitoa kimungu anatakwa achukue Mungu na Neno lake kwa uzito. Ili ajizoeze kujitoa kimungu, mmoja anahitaji kumjua Mungu kwa usahihi kisha atende kwa upatano na maarifa ya kujua hivyo. Anahitajiwa auone uhitaji wake wa kiroho. Kwa sababu ya umaana wa sisi kujizoeza kikweli kujitoa kimungu, tunahitaji msaada wote tunaoweza kupata. Mikusanyiko yetu ya wilaya itafanya mengi kutuandalia msaada huo. Kupitia hotuba, maonyesho, na mahoji, tutafundishwa jinsi ya kujitoa kimungu katika njia zote za maisha zetu.

Sisi tunataka kuwa Wakristo wa kweli na kwa njia hiyo tutokeze wazi kuwa tofauti na ulimwengu. Kwa hiyo njoo kwenye mikusanyiko hii ukiwa na hamu njema ya kiroho. Hakikisha utakuwako kwa ajili ya wimbo wa kufungua asubuhi ya Ijumaa, na ubaki muda wote wa wimbo na sala ya kufunga alasiri ya Jumapili. Kaza uangalifu wako kwenye jukwaa programu inapoendelea. Kinza kishawishi au mbetuko wa kutembelea wengine wakati wa vipindi. Njoo ukiwa tayari kuandika habari. Kwa kutoa uangalifu wa karibu sana kwenye programu, zaidi ya wakati mwingine wowote utakuwa umejipatia vifaa ili ujizoeze kujitoa kimungu katika njia zote za maisha: katika jamaa, katika kundi, na kuelekea watu wa nje.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki