Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 2/15 uku. 31
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Wewe Waalikwa Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • “Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Hudhuria “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1987
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 2/15 uku. 31

Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya

TOFAUTI za lugha zimekuwa kani yenye kugawanya tangu Babeli. Huko Yehova alivuruga lugha ya ainabinadamu na akazuia kusudi la watu ‘kujenga mnara na kujifanyia wenyewe jina lenye sherehe.’ (Mwanzo 11:4, NW) Jinsi tofauti katika lugha yaweza kugawanya yaonwa katika jambo lililotukia katika Ubelgiji. Miaka kadhaa iliyopita, Chuo Kikuu cha Kikatoliki kwenye Louvain kiligawanyika kilugha kikawa nusu.

Lugha ni moja tu ya sababu za migawanyiko miongoni mwa wanadamu. Sababu nyingine ni utaifa, rangi ya ngozi, elimu, na kiwango cha uchumi. Lakini Mashahidi wa Yehova wamejitahidi ili washinde visababishi vyote hivi vya mgawanyiko nao wameungamana kikweli.

Kiangazi kilichopita kiliona wonyesho wa kutazamisha sana wa muungamano huu katika majiji ya Chorzów (karibu na Katowice), Poznan, na Warsaw katika Polandi. Mashahidi, wakinena angalau lugha 20 tofauti, walikuwapo kutoka mabara 37 hivi. Hata hivyo, umoja wa kutazamisha ulidhihirishwa na wote. Sababu ya hili ilikuwa nini? Wote walinena “lugha iliyo safi” ya ukweli wa Kimaandiko. Hiyo ilitabiriwa kiunabii kwenye Sefania 3:9: “Hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Bwana [Yehova, NW], wamtumikie kwa nia moja [bega kwa bega, NW].”

Kwa hiyo, kuna sababu nzuri ya kwamba mikusanyiko ya wilaya ya 1990 itakuwa na kichwa “Lugha Iliyo Safi.” Kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu, mavutano yenye kutoka katika ulimwengu mwovu wa Shetani, na vitendo vya kiufundi vya Ibilisi na roho waovu wake, kunena ile “lugha iliyo safi” hakuji kwa urahisi sikuzote. Ni lazima tulinde sikuzote dhidi ya mielekeo ya ubinafsi ambayo ingeweza kutugawanya.

Kwa nini Mungu ametupa sisi hii lugha iliyo safi? Ni ili kwamba sisi tuweze kutumikia Yehova “bega kwa bega.” Tafsiri nyinginezo huonyesha kwamba hii yamaanisha kutumikia Mungu “chini ya nira ile ile” (The Jerusalem Bible); “kwa kibali moja” (Moffatt); na “kwa kauli moja” (An American Translation) na “kushirikiana katika utumishi wake.”—Byington.

Kwa njia ya hotuba, maonyesho, mambo yaliyoonwa, hotuba mfululizo, na drama za Biblia kwenye mikusanyiko hii, tutatiwa moyo na kusisimuliwa tunene lugha iliyo safi kwa ufasaha zaidi. Pia zitatusukuma tutumikie pamoja na ndugu zetu kwa matokeo makubwa zaidi na upatano zaidi.

Mikusanyiko hii itaanza Alhamisi mara tu baada ya saa 7:00 alasiri na itamalizika karibu saa 10:00 alasiri Jumapili. Fanya mipango sasa ili uwepo kwa ajili ya wimbo wa kufungua na uhudhurie vipindi vyote mpaka sala ya kumalizia Jumapili alasiri.

Njoni mkiwa na Biblia zenu na vitabu vya nyimbo, na mwe tayari kuandika mambo. Njoni pia mkiwa na hamu nzuri ya chakula cha kiroho, nanyi mtaondoka mkiwa mmetayarishwa kwa vifaa vya kunena lugha iliyo safi na kutumikia Yehova bega kwa bega.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki