Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 2/15 uku. 30
  • Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Njooni Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Wewe Waalikwa Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 2/15 uku. 30

Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya

SIKU ya kwanza kabisa ya siku za kuumba iliona uumbaji wa nuru kuhusiana na dunia. Twasoma kwamba Yehova Mungu alisema hivi: “Iwe nuru.” Na “ikawa nuru.” (Mwanzo 1:3) Hilo lapatana na lile ambalo mtume Yohana aliandika: “Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.”—1 Yohana 1:5.

Kwa kuwa Mwana wa Mungu yu katika mwungano pamoja na Baba yake, haishangazi kwamba Yesu alisema hivi wakati mmoja: “Mimi ni nuru ya ulimwengu.” (Yohana 9:5) Twaweza kutoka katika giza na kuingia katika nuru kuweka imani katika Yehova Mungu na Mwana wake. Yesu alishuhudia hivi pia: “Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.” (Yohana 12:46) Kwa hiyo, kwa kufaa, Yesu Kristo alisema hivi kuhusu wafuasi wake wa kweli: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. . . . Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu mbinguni.”—Mathayo 5:14, 16.

Ni baraka kama nini kuwa na kweli, uelewevu wa Neno la Mungu kama unavyoeleweshwa wazi na “mtumwa mwaminifu mwenye akili”! (Mathayo 24:45-47) Hatutataniki tena na imani katika Utatu; hatufadhaishwi tena kuhusu ni kwa nini Mungu mweza yote na mwenye upendo aruhusu uovu na jeuri; hatuna shaka tena kuhusu hali ya wafu. Nuru imetupa sisi tumaini, tumaini la Ufalme. Imetufunulia jinsi Muumba alivyo Mungu wa ajabu. Nuru ya kweli imetupa sisi kusudi maishani, kutumikia kusudi ambalo ni kwa ajili yalo tumeumbwa hasa, kumtukuza Mfanyi wetu, Yehova Mungu. Hilo twafanya kwa kuwa wachukuaji wa ile nuru. Kuwa wachukuaji nuru ni heshima na pendeleo kubwa sana, lakini ni daraka lenye uzito pia. Ili kutimiza wajibu huo, tunahitaji kutumia msaada wote ambao Yehova huandaa. Kwa hiyo inafaa kama nini kwamba mikusanyiko yetu ya wilaya ya 1992 yawe na kichwa “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya!

Kufanyia maendeleo stadi zetu na pia uthamini wetu wa daraka letu tukiwa wachukuaji nuru, tutataka kuhudhuria angalau mmojawapo mikusanyiko hiyo, kuwapo kwa wimbo wa kufungulia na kubaki hadi sala ya kumalizia. Na tutataka kusikiliza kwa makini yote yanayosemwa jukwaani, yawe ni hotuba mbalimbali, mahoji, maono, au drama. Kuandika habari hakutupi tu kitu cha kurejezea baadaye ili kujikumbusha bali kunatusaidia sana kukaza fikira kwenye yale yanayotolewa. Naam, katika programu yote ya mkusanyiko, tutataka ‘kujiangalia jinsi tusikiavyo.’—Luka 8:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki