Wewe Waalikwa Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya
TANGU Novemba 1989, habari ya uhuru imefanywa mashuhuri kuliko wakati mwingine wowote. Vikundi vya watu wa nchi za Ulaya ya Mashariki hasa vimekuwa vikiona shangwe ya uhuru mwingi zaidi wa kisiasa kuliko ule wamekuwa wakiwa nao kwa miaka 40 na zaidi.
Lakini kuna uhuru mmoja wenye umaana mkubwa kuliko uhuru wowote wa kisiasa. Twaweza kusoma juu yao katika Neno la Mungu, Biblia. Yesu Kristo alisema hivi wakati mmoja: “Mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32) Ndiyo, Wakristo waliojiweka wakfu wamewekwa huru kutokuwa na hofu ya binadamu na katika utumwa wa dhambi na kifo, kama tusomavyo kwenye Warumi 6:18, 22. Pia twasoma kwamba ‘ilipo roho ya Bwana, hapo ndipo penye uhuru.’ (2 Wakorintho 3:17) Kwa uhakika, Neno la Mungu latoa lile tazamio jangavu kwamba “viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.”—Warumi 8:21.
Ikiwa mtu yeyote ataka kupata uhuru wa Kikristo wakati wa sasa, ni lazima atie jitihada halisi. Hilo si jambo la kuchagua hata kidogo kuepa kukabiliana na magumu kwa kufuatia mwendo usio na matatizo mengi sana. Na kuendelea kuona shangwe ya uhuru huu hutaka jitihada ya ziada, kwa sababu ya nguvu zielekeazo kutunyang’anya uhuru wetu: Shetani Ibilisi, ulimwengu wake mwovu, na maelekeo yetu wenyewe yenye dhambi tuliyoyarithi. Yehova Mungu ametoa msaada kwa njia ya Neno lake lililotiwa roho yake, kwa njia ya roho takatifu yake, na kwa njia ya tengenezo lake lionekanalo.—Luka 11:13.
Ili kusaidia wote wapendao uhuru kuimarisha mshiko wao juu ya uhuru, mikusanyiko ya wilaya ya mwaka huu ya Mashahidi wa Yehova itatekeleza vizuri kile kichwa “Wapendao Uhuru.” Mikusanyiko hii itakuwa na urefu wa siku tatu, kuanzia asubuhi ya Ijumaa saa 3:30 na kuendelea mpaka saa 10:00 ya jioni Jumapili. Wote watakaokuja kwenye mikusanyiko hii wataburudishwa kiroho na kujengwa na hotuba zenye kuchochea, mahoji yenye kupendeza, maonyesho yenye matokeo mazuri, na mchezo wa kuigiza wa ki-siku-hizi ulio na uvutio thabiti; wala tusikose kuzifikiria shangwe za ushirika wenye kuchangamsha moyo pamoja na marafiki wa zamani na wapya, furaha ya kujiunga na maelfu ya wengine katika kuimba nyimbo zetu za Ufalme, na kushiriki katika sala za peupe zenye kuhisiwa moyoni.
Watumishi wote wa Yehova wasiache jambo lolote kamwe livuruge kuwako kwao asubuhi ya Ijumaa wakati mikusanyiko hii ianzapo. Nanyi hakikisheni kuja mkiwa si na Biblia tu na kitabu cha nyimbo bali pia na penseli (kalamu) na kitabu cha kuandikia habari. Njoni, pia, mkiwa mnauona uhitaji wenu wa kiroho mkiwa sehemu ya watu huru.—Mathayo 5:3.