Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 2/15 uku. 30
  • Njooni Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njooni Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Njooni Kwenye “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Mkusanyiko wa “Wasifaji Wenye Shangwe”
    Amkeni!—1995
  • Karibuni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Wewe Waalikwa Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 2/15 uku. 30

Njooni Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu”

WATUMISHI wa Yehova katika nyakati za kale walitakwa chini ya Sheria ya Kimusa kukusanyika pamoja mara tatu kila mwaka kwa ajili ya sikukuu fulani. Hizo zilikuwa pindi zenye furaha na za kujenga kiroho.—Kumbukumbu la Torati 16:16.

Vilevile katika nyakati za ki-siku-hizi watumishi wa Yehova hukusanyika mara tatu kila mwaka: kwa ajili ya siku ya kusanyiko la pekee, kwa ajili ya kusanyiko la mzunguko la siku mbili, na kwa ajili ya mkusanyiko wa wilaya wa siku tatu au nne. Katika mwaka wa utumishi wa 1994, Mashahidi wa Yehova watakusanyika kwa ajili ya Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu.”

Neno la Mungu haliachi shaka lolote juu ya umaana wa hofu ya kimungu. Hofu ya aina hiyo inatajwa humo mara 200 hivi. Hofu ya kimungu ni ulinzi, kama vile iwezavyo kuonwa kutoka Mithali 16:6: “Kwa kumcha BWANA [katika hofu ya Yehova, NW] watu hujiepusha na maovu.” Kwani, twaambiwa kwenye Zaburi 111:10 kwamba hofu ya kimungu ndio mwanzo wa hekima!

Yaweza kusemwa kwamba kuna sehemu mbili za hofu ya kimungu. Kwanza, hofu hiyo inaendelezwa na upendo. Twahofu kutompendeza Mungu kwa sababu ya kumpenda sana. (Mithali 27:11) Kisha, hekima kwa upande wetu itasaidia kukaza hofu ya kimungu kikiki ndani yetu, kwa kuwa twajua kwamba Mungu ni “moto ulao” kwa wote watendao mabaya.—Waebrania 12:29.

Kwenye Mkusanyiko wetu wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu,” tutapokea maagizo na kitia-moyo kingi ili kukua katika hofu ya kimungu. Mafundisho hayo yatatolewa kupitia hotuba, maonyesho, na drama, pamoja na kusimuliwa kwa maono.

Sawa na vile Waisraeli wa kale walivyoamriwa wasije kwenye makusanyiko yao wakiwa mikono mitupu, ndivyo sisi twapaswa kuchanga sehemu yetu kwenye mafanikio ya mikusanyiko yetu. (Kumbukumbu la Torati 16:17) Twaweza kufanya hivyo kwa kudhihirisha staha kwa ajili ya meza ya Yehova. Jinsi gani? Kwa kufika mapema, kwa kukaza fikira zote kwenye yale yanayosemwa kutoka jukwaani, kwa kujiunga kwa moyo wote katika kuimba nyimbo. Tusingekuwa tukishiriki katika mazungumzo au kutembea-tembea wakati wa programu. Tutataka pia kuchanga kadiri tuwezavyo kwa kujitolea kwa utumishi wetu mbalimbali. Mipango ya kitengenezo ya mkusanyiko yatia ndani idara nyingi, zote ambazo huhitaji wafanyakazi. Tutataka pia kutoa michango ya kifedha kwa kadiri ambavyo Yehova ametubariki.

Acheni kila mtumishi wa Yehova afanye mipango sasa ya kuwapo kwa siku zote tatu za Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu,” kuanzia wimbo wa kufungua Ijumaa asubuhi hadi sala ya kufunga Jumapili alasiri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki