Hudhuria “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1987
NI KICHWA kizuri kama nini tulicho nacho kwa mikusanyiko ya wilaya yetu ya 1987: “Tumaini Katika Yehova”! Kwa uhakika kuwa kwetu na tumaini katika Yehova kunatutenganisha na sehemu ile nyingine yote ya ulimwengu. Wengine wote wanaweka tumaini lao katika vitu kama vile mali, hekima yao, uwezo mwingi walio nao au watawala na viongozi wao wa kisiasa na kidini. Karibuni vitu vyote hivyo vitawakatisha tamaa kwa njia yenye uchungu mwingi.—Zaburi 146:3, 4.
Inamaanisha nini kuweka tumaini letu katika mtu au kitu fulani? Kulingana na wanakamusi, “Tumaini linatoa wazo la egemeo la kabisa kabisa na lenye uhakikisho juu ya kitu fulani au mtu fulani.”a Ndiyo, na hivyo ndivyo sisi tunavyohisi juu ya jambo hilo. Sisi tunaegemeza kabisa kabisa na kwa uhakikisho utumainifu wetu hakika juu ya Yehova.
Umaana wa kuweka tumaini katika Yehova unavutwa kwenye fikira zetu mara nyingi sana katika Neno la Mungu. Watunga zaburi wanaeleza kwa kurudia-rudia juu ya walivyoweka tumaini lao katika Yehova: “Lakini kwa habari yangu mimi, katika Yehova mimi ninatumaini.” “Katika wewe mimi nimeweka tumaini langu, O Yehova.” Maneno yao yanakumbusha yale maneno ya mmoja wa nyimbo zetu za Ufalme: “Yehova kimbilio, Tumaini letu . . . Yehova ndiye ngome, Kimbilio kwa wa haki.”—Zaburi 31:6, 14, NW.
Maandiko yanatuamuru sisi tena na tena tuweke tumaini letu katika Mungu, kama vile: “Weka tumaini katika Yehova na utende mema.” “Weka tumaini katika Yehova kwa moyo wako wote na usiegemee ufahamu wako mwenyewe.” (Zaburi 37:3; Mithali 3:5, NW) Neno la Mungu pia linatuambia kwamba watumishi waaminifu wa Yehova walithawabishwa kwa sababu ya kuweka tumaini lao katika yeye nyakati za hatari kubwa. Miongoni mwa hao walikuwa Mfalme Hezekia, Ebed-Meleki, wale Waebrania watatu, na Danieli.—2 Wafalme 18:5; Yeremia 39:18; Danieli 3:28; 6:23, NW.
Tunaonyeshaje kwamba sisi tuna tumaini katika Yehova? Njia moja ni kwa kupata kumjua Yehova na kuamini kabisa yanayosemwa katika Neno lake. Yesu Kristo alitupa sisi ufunguo rahisi sana wa kufanyia hivyo: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, na mambo yote hayo mengine mtaongezewa.” Ndiyo, tukiweka tumaini letu katika Yehova kwa moyo wetu wote, tutatanguliza faida za Ufalme wake kwanza katika maisha zetu na kufuata mwenendo ulio wima.—Mathayo 6:33, NW.
Kwa sababu gani tumaini letu katika Yehova linahitaji kuwa na nguvu? Ni kwa sababu ya mikazo inayoletwa dhidi yetu kila upande. Kwa wengine ni mateso ya kabisa kabisa, kwa wengine ni vishawishi vya kutenda makosa. Bado kwa wengine ni kwamba tumaini lao linajaribiwa na kutakwa wawe na uvumilivu. Mkusanyiko wa wilaya wetu unaokuja ni miongoni mwa misaada mingi ambayo Yehova ameandaa katika siku za mwisho hizi.
Mwaka huu mkusanyiko utakuwa kwa muda wa siku tatu kamili-kamili, Ijumaa, Jumamosi, na Jumapili. Kwa sababu ya marekebisho kufanywa katika urefu wa vipindi, programu itakuwa na kiasi karibu kile kile tu cha habari chenye kulingana na kile cha mwaka uliopita. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba kusudi la mambo yote ya programu litakuwa kutia nguvu tumaini letu katika Yehova na pia katika tengenezo linaloonekana ambalo yeye anatumia katika wakati uliopo.
Kwa hiyo acheni kila shahidi Mkristo wa Yehova aazimie kuhudhuria angalau mmoja wa mikusanyiko hiyo. Leta watoto wako. Uwepo kwa ajili ya wimbo wa kufungua na sala asubuhi ya Ijumaa na ubaki mpaka wimbo na sala ya kufunga alasiri ya Jumapili. Uje ukiwa umejitayarisha kwa Biblia, kitabu cha nyimbo, kitabu cha maandishi, na kalamu. Jiingize kwa ukamili ndani ya roho ya mambo yanayotokezwa, kutia ndani nyimbo na sala. Kaza fikira za ukaribu kwenye mambo yatakayokuwa yakitolewa. Kisha acheni sisi tuhakikishe kwamba nyakati zote tutakuwa tumejipamba na kujiendesha kwa njia ambayo haitaweza kuleta suto.
Kanuni ya Kimaandiko, ‘panda kwa ukarimu, vuna kwa ukarimu,’ inatumika kuhusu kuhudhuria kwetu “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya. Kadiri tutakavyozidi kujikaza katika kuitwaa programu nzima, ndivyo zitakavyozidi kuwa nyingi baraka tutakazochukua kutoka mkusanyikoni na ndivyo tutakavyozidi kuwa baraka kwa wengine.—2 Wakorintho 9:6.
Zifuatazo ni tarehe na mahali pa mikusanyiko
Mombasa: Desemba 18-20,1987 Kisumu na Jinja: Januari 1-3,1988
Nairobi: Desemba 25-27,1987
a [Maelezo ya Chini]
Kamusi Webster’s New Dictionary of Synonyms.