Je! Unakumbuka?
Je! umeyafurahia matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kukumbuka mambo yanayofuata:
◻ Ni nini kinachoweza kusaidia Wakristo washinde makosa ya siri?
Wakristo wanaotaka kumpendeza Yehova wanapaswa kuishi kwa kutambua kwamba hawawezi kumficha Mungu makosa yao. Pia, inawapasa kuukubali msaada wa Yehova washinde udhaifu huo. (Mhubiri 12:14; Wafilipi 4:13)—10/15/85, ukurasa 30.
◻ Ni mwito gani wa ushindani unaohusu ukomavu wa Kikristo ambao kila mtumishi wa Yehova anapaswa kuufikiria kwa uzito?
Je! mtumishi wa Yehova ana nia na hamu nyingi ya kulikubali daraka linaloambatana na kuwa mtu mzima aliyekomaa kiroho? Au yeye anatosheka tu kuambaa-ambaa, kuwaacha wengine ndio wamchukulie daraka hilo? (Wagalatia 6:4,5)—11/1/85, kurasa 24, 25.
◻ Ni baadhi ya mambo gani ya hakika yanayokanusha kwamba Yesu hakuzaliwa Desemba 25?
Desemba ni wakati wa majira yenye mvua na baridi katika Bethlehemu, kwa hiyo wachungaji hawangekuwa nje usiku pamoja na mifugo yao. Haielekei kuwa Kaisari Mroma angewaamuru watu wasafiri katika majira ya baridi wakajiandikishe kwa sababu tayari Wayahudi walikuwa wakikaribia kufanya maasi juu ya Waroma.—9/15/85, ukurasa 24.
◻ kwa sababu gani ubatizo unapasa kuwa wakati wa wataka kubatizwa kutafakari na kufikiria mambo kwa uzito mwingi?
Ubatizo ni wakati ambao mtu peke yake anaonyesha kwamba amefanya uamuzi wa maana sana—kujitiisha mbele za Mungu akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu na Shahidi wa Yehova, asiwe sehemu ya ulimwengu. (Luka 3:21; Mathayo 4:10; 1 Yohana 5:19)—8/1/85, ukurasa 31.
◻ Watu wa Yehova leo wanajilishaje “kila neno litokalo katika kinywa cha [Yehova]” (Mathayo 4:4)?
Kujilisha huko hakufanywi kwa kusoma na kujifunza kibinafsi tu Neno la Mungu Biblia, bali kunafanyika wakati watu wa Yehova, kwa ujumla na kama mtu mmoja mmoja, wanapojionea njia nzuri ajabu anayoitumia Yehova ili kutimiza maneno yake kuelekea watu wake, akichukua hatua kuwasaidia.—2/1/86, makala ya pili ya funzo, mafungu 14-17.
◻ Wakristo katika karne ya kwanza walitendaje kuelekea mtu ambaye hakuwa mtenda kosa aliyefukuzwa, lakini mwenye kuikana njia ya Kikristo kwa makusudi?
Mtume Yohana alitoa shauri juu ya watu waliokuwa ‘wametoka kwetu’ na juu ya wale walioleta fundisho la uwongo. (1 Yohana 2:19) Kwenye 2 Yohana 10 alishauri kwamba Wakristo hawakupaswa ‘kukaribisha nyumbani mwao’ wala kuwasalimu watu wa namna hiyo. Neno “uasi-imani” limetokana na neno la Kigiriki lililo na maana ya ‘kuondoka, kuacha, au uasi,’ na mtu aliyekuwa amejitenga rasmi na kundi la Kikristo kwa kupenda kwake mwenyewe angepatana na maelezo hayo. Wakristo washikamanifu wasingepaswa kutaka kushirikiana na mwasi-imani huyo.—1/15/86, “Maswali. Kutoka kwa Wasomaji.”