Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 10/15 kur. 10-15
  • “Taifa” Linaloujaza Matunda Uso wa Dunia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Taifa” Linaloujaza Matunda Uso wa Dunia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kitu Tofauti—‘Mzabibu wa Dunia’
  • Kukombolewa Uhamishoni
  • Kuzaa Matunda Kunakomtukuza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Mzabibu Unaotoa Divai Inayofurahisha Mungu na Mwanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Mkono wa Yehova Wainuliwa
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 10/15 kur. 10-15

“Taifa” Linaloujaza Matunda Uso wa Dunia

‘Katika siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi, Israeli atachanua maua na kwa kweli achipuke; nao watajaza mazao kweli kweli katika uso wa ile nchi yenye kuzaa.”​—ISAYA 27:6, Biblia ya New World Translation.

1. Mtume Petro alilitajaje taifa la Israeli wa kiroho?

KUHUSU kuzaliwa kwa kundi la wanafunzi wa Kristo wakiwa “taifa” mwaka 33 W.K., mtume Petro aliandika maneno haya muda mfupi kabla ya uharibifu wa Yerusalemu mwaka 70 W.K.: “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili [sifa bora, NW] zake yeye aliyewaita gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.” (1 Petro 2:9, 10) Hilo lilikuwa jambo la neema kama nini upande wa Mungu!

2, 3. Wakiwa ndio milki ya pekee ya Yehova Mungu, ni wajibu gani unaowashukia Israeli wa kiroho, na Yesu Kristo anawafananisha na nani katika Yohana sura ya 15?

2 Leo, karne 19 baada ya Petro kuandika maneno hayo, kungali hapa duniani mabaki ya “taifa” hilo lililozaliwa kwa roho. Sasa hesabu yao imepungua wakawa chini ya elfu kumi kulingana na ripoti za mwadhimisho wa kila mwaka wa Chakula cha Jioni cha Bwana. Wao ni ‘watu wa milki ya pekee ya Yehova,’ nao wakiwa hivyo ni lazima watangaze kote kote sifa bora za Yehova Mungu, ambaye aliwaita watoke kwenye ‘giza la kilimwengu waingie katika nuru yake ya ajabu.’ “Nuru” hiyo imekuwa iking’aa hasa tangu mwisho wa “majira ya Mataifa,” au “nyakati zilizowekwa za mataifa,” mwaka 1914.a (Luka 21:24, UV; NW) Wakiwa ndio “milki” ya pekee ya Mpaji wa Kimungu wa nuru hiyo ya ajabu, wao wanathaminiwa sana naye. Kwake wao ni kama shamba la mizabibu la kiroho.

3 Hapa tunakumbuka yale ambayo Yesu Kristo aliwaambia mitume wake, waliowakilisha wote ambao wangekuwa wafuasi wake waliozaliwa kwa roho: “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa. Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. Kaeni ndani yangu [katika muungano pamoja na mimi, NW], nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.”​—Yohana 15:1-5.

4. (a) Mfano wa Yesu unatukumbusha juu ya simulizi gani katika Isaya sura ya 27? (b) Ni wakati gani unabii huo unapopata utimizo wa kisasa, na juu ya nani? (c) Ni mwelekeo gani ambao Mungu hawaonyeshi tena watu wake?

4 Ulinganisho, au mfano huo, uliotolewa na Yesu Kristo unatukumbusha juu ya maneno ya Yehova katika Isaya 27:2-4 (NW), ambapo tunasoma hivi:

“Katika siku hiyo liimbieni, enyi watu: ‘Shamba la mizabibu lenye divai inayotoa mapovu! Mimi, Yehova, ninalilinda. Kila dakika mimi nitalitia maji. Ili kwamba mtu ye yote asipate kuelekeza fikira zake alipinge, mimi nitalilinda hata usiku na mchana. Hakuna hasira kali niliyo nayo mimi.’”

“Shamba la mizabibu lenye divai inayotoa mapovu” leo duniani laweza kulinganishwa na mabaki ya matawi yaliyo katika “mzabibu” ule wa mfano ambamo Wakristo waliozaliwa kwa roho wa lile “taifa takatifu” ni washiriki wenye mazao. Kwa hiyo, wanakaliwa na wajibu wa kuzaa matunda mengi. (Yohana 15:5) Kulingana na unabii wa Isaya, ule wimbo juu ya “shamba la mizabibu lenye divai inayotoa mapovu” ungeimbwa wakati wa kurudishwa kwa watu wa Yehova kwenye upendeleo wake. (Linganisha Isaya 27:13) Hiyo ingeonyesha kuwa utimizo wa kisasa wa unabii huo wenye uchangamshi ulitokea katika mwaka ulioifuata vita wa 1919, nayo mambo hakika ya historia yanahakikisha kwamba umeendelea kutimia mpaka sasa. Leo Yehova hana “hasira kali” juu ya watu wake, wala juu ya mabaki ya “taifa takatifu” lake, “watu wa milki” yake ya pekee, wala juu ya Wakristo washikamanifu wanaotazamia kupata uzima wa milele duniani. Kwa rehema yeye amewageuzia upendeleo wake, na huo ndio umefanya wawe na ufanisi wa kiroho na kuzaa matunda.

5. Watu wamefurahishwa na nini kutokana na hilo shamba la mfano la mizabibu, nao wanaweza kusimulia nini kulihusu?

5 “Taifa” hilo la kiroho, pamoja na washirika walo wenye bidii, limekuwa kama shamba la mizabibu lenye mazao ambalo limetokeza ‘divai nyingi inayotoa mapovu.’ Ni divai ya kiroho ambayo imefurahisha moyo wa Yehova na wa mwanadamu. (Waamuzi 9:13) Kwa sababu hiyo inayofaa, watu ambao wamefurahishwa kwa kunywa kinywaji hicho cha kiroho wanaweza kuimba kwa furaha na wanaweza kusimulia mambo yote ambayo Mkulima wa Kimungu wa hilo “shamba la mizabibu” amelifanyia “shamba” hilo la mfano. Kwa usemi wa mfano, yeye ‘amelitia maji’ kweli kweli hilo “shamba la mizabibu” ili liwe bichi daima, hivi kwamba matunda yenye utomvu-utomvu yaliyo matamu sana yamezaliwa, matokeo yakawa ni kufurahisha.

Kitu Tofauti—‘Mzabibu wa Dunia’

6. Hata hivyo, ni jambo gani litakaloupata ‘mzabibu wa dunia,’ kulingana na Ufunuo sura ya 14?

6 Hivyo sivyo imekuwa kwa ule ambao kitabu cha mwisho cha Biblia kinauita ‘mzabibu wa dunia.’ Karibuni, vikosi vya kimbingu vyenye kuua vitapewa amri hii ya kimungu: “Tia upanga wako mukali, ukachume vichala vya muzabibu wa dunia, maana zabibu zake zimeiva.” Ndipo, kama vile Ufunuo wa kiunabii unavyoendelea kuonyesha, “malaika yule akatupa upanga wake hata dunia, akachuma muzabibu wa dunia, akatupa zabibu katika kikanyagiyo kikubwa cha matunda cha gazabu ya Mungu. Kikanyagiyo cha matunda kikakanyagwa inje ya muji, damu ikatoka katika kikanyagiyo cha matunda hata mupaka wa kamba ya kuongoza farasi, kama mwendo wa kilometres mia tatu makumi mbili.” (Ufunuo 14:18-20, ZSB) Ndivyo itakavyokuwa kwa sehemu ya kiserikali ya tengenezo la Ibilisi linaloonekana duniani; yeye ndiye mkulima walo, nalo linaupinga ule “mzabibu wa kweli” ambao Yehova Mungu ndiye Mkulima wao. Ule ‘mzabibu wa dunia’ hautarudishwa kamwe!

7-9. Isaya 27:7-13 ina utimizo gani maradufu, na katika nyakati gani?

7 Hata hivyo, kwa kweli unabii huu wa Isaya sura ya 27 ni unabii wa kurudishwa, kwanza kwa taifa la Israeli wa asili kisha kwa Israeli wa kiroho katika karne yetu wenyewe ya 20. Jambo hilo linaonekana kutokana na yanayosemwa na unabii katika mstari 7 mpaka mstari 13, unaomalizia sura hiyo. Mistari hiyo inasomwa hivi (NW):

8 “Kama kwa dharuba ya mmoja anayempiga dharuba, je! ni lazima mmoja ampige dharuba hivyo? Au kwa machinjo ya wenye kuuawa naye, je! ni lazima auawe hivyo? Kwa mlio wa kutia woga utapambana naye unapompeleka aende zake. Yeye lazima amfukuze kwa kishindo cha upulizaji wake, mmoja ulio wenye nguvu katika siku ya upepo wa mashariki. Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafanyiwa upatanisho, na hayo ndiyo matunda yote wakati yeye achukuapo dhambi yake kuiondoa, wakati afanyapo mawe yote ya madhabahu yawe kama mawe ya chokaa ambayo yamepondwa yakawa unga, hivi kwamba zile nguzo takatifu na vinara vya uvumba hazitainuka. Kwa maana ule mji wenye ngome utakuwa peke yao, nayo nchi ya malisho itahamwa na kuachwa kama jangwa. Hapo ndama atakula majani, na hapo atalala chini; na kwa kweli yeye atakula ayamalize matanzu yake. Wakati vichipukizi vyake vimekwisha kukauka, wanawake wanaoingia watavivunja, waviwashe moto. Kwa maana hiyo si jamia ya watu wenye ufahamu ulio na makini. Hiyo ndiyo sababu Mfanyiza wayo hataionyesha rehema, na Muumbaji wayo yenyewe hataionyesha kibali cho chote.”

9 Na lazima itukie siku hiyo kwamba Yehova atayapukutisha matunda, kutoka kile kijito kinachotiririka cha ule Mto mpaka kwenye bonde lenye bubujiko la maji la Misri, na kwa hiyo ninyi wenyewe mtasombwa mmoja baada ya mwingine, Enyi wana wa Israeli. Na lazima itukie siku hiyo kwamba kutakuwa na mpulizo kwenye mbiu kubwa, na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru na hakika wale ambao wametawanywa katika nchi ya Misri watakuja na kuinamia Yehova katika ule mlima mtakatifu katika Yerusalemu.”

10. Ni serikali gani kubwa ya ulimwengu iliyokuwa mashuhuri wakati wa kutolewa kwa unabii wa Isaya, na je, ilifaulu katika shambulio ililokusudia kufanya juu ya mji mkuu wa ufalme wa Yuda?

10 Katika siku za unabii huu wa Isaya, Ashuru ilikuwa imekuwa ndiyo serikali kuu ya ulimwengu katika dunia, ikachukua mahali pa ile ya kwanza ya mfululizo wa serikali saba kubwa za ulimwengu, ingawa Misri bado ilikuwa ikiendesha shughuli zayo ikiwa serikali ndogo kwa hiyo. Ufalme wa Israeli wenye makabila kumi ulikuwa umejiondoa katika utawala wa nyumba ya kifalme ya Mfalme Daudi wa kabila la Yuda. Kwa hiyo mji wa Yerusalemu ndio mfalme wa Ashuru aliujia kudai usalimu kabisa amri yake kama haukutaka kuharibiwa. Lakini, Yehova aliupigania ufalme wa Yuda na kumrudisha nyumbani kwake Mfalme Senakeribu mwenye kiburi hali akipepesuka kwa ushinde wenye aibu.​—Isaya, sura 36 na 37.

11. Ni mfalme wa serikali gani kubwa ya ulimwengu aliyetumiwa kupindua ufalme wa Yuda, na Isaya 27 inatajaje tukio hilo?

11 Kwa sababu hiyo, mfalme wa serikali kuu ya ulimwengu iliyoifuata hiyo nyingine, yaani, Serikali ya Ulimwengu ya Kibabuloni, alipewa mamlaka ya kuuharibu mji mtakatifu wa Yerusalemu na hekalu lake. Kulingana na vionyesho vya Kibiblia, jambo hilo lilitukia mwaka 607 K.W.K., mikononi mwa Mfalme Nebukadreza. Yeye ndiye aliyepeleka mateka ndani ya nchi ya Babulonia, wakakae miaka 70 ya uhamisho wakiwa humo. Ni kwa sababu ya uharibifu uliokuwa ukikaribia kupata Yerusalemu na kupeleka wahamishwa ndani ya utumwa wa Kibabuloni kwa muda wa miaka 70 kwamba maulizo yalitokezwa kwa njia inayofaa:

“Kama kwa dharuba ya mmoja anayempiga [taifa la Israeli] dharuba, je! ni lazima mmoja ampige dharuba hivyo?” (Isaya 27:7, NW)

Kama isivyopata kuwa katika historia ya kitaifa tangu mwaka 1513 K.W.K., taifa la Mungu lilipigwa dharuba yenye msiba mwaka 607 K.W.K., dharuba ambayo karibu iliharibu kabisa. Watu wengi walikufa katika mji wa Yerusalemu uliofanyiwa mazingiwa. Ndiyo, Yehova aliona uhitaji mkubwa kwamba hatua hiyo kubwa sana ichukuliwe, na ilikuwa lazima iwe hivyo. Yeye aliuona uhitaji mwingi sana wa kupambana na wale ambao wangalipaswa kubaki wakiwa rafiki zake, masahibu wake mwenyewe, ambao alikuwa ameingia pamoja nao ndani ya agano la Torati kupitia mpatanishi Musa.

12. Yehova angeweza kumwongoza nabii Isaya kwa roho yake aulize ulizo gani kuhusu yaliyowapata Israeli, na hivyo matokeo yalikuwa nini juu ya uhusiano wa Israeli na Yehova?

12 Hivyo Yehova angeweza kuendelea kuuliza:

“Au kwa machinjo ya wenye kuuawa naye, je! ni lazima [taifa la Israeli, au Yakobo] auawe hivyo?” (Isaya 27:7, NW)

Ah, ndiyo, kwa maana sasa ilikuwa imehitajika kabisa Yehova apambane na watu waliokuwa na kibali chake hapo kwanza, apaaze mlio wenye kuogopesha, “mlio wenye kutia woga,” utoke kwenye majeshi ya Serikali ya Ulimwengu ya Kibabuloni, hiyo ikiwa ndiyo ya tatu katika historia ya Biblia. Ndiyo sababu maneno ya kimungu yalisema:

“Kwa mlio wa kutia woga utapambana naye unapompeleka aende zake. Yeye lazima amfukuze kwa kishindo cha upulizaji wake, mmoja ulio wenye nguvu katika siku ya upepo wa mashariki [kuonyesha upande ambako ule mlio wa kivita wenye kutia woga ungetokea].” (Isaya 27:8, NW)

Kwa kuanza mambo hivyo angelipeleka liende zake lile taifa lisiloaminika ambalo wakati mmoja lilikuwa limekuwa mke wake wa mfano likiwa tengenezo lake lenye kuonekana duniani. Sasa alikuwa akilifukuza liiache nchi lililopewa na Mungu lichukuliwe na watekaji Wababuloni kupelekwa kwenye nchi ya mbali, kama kwamba limepewa talaka kwa muda.​—Linganisha Isaya 50:1.

13. Kulingana na unabii wa Isaya, taifa la Israeli lingefanyaje upatanisho kwa sababu lilivunja agano la Mungu?

13 Sasa wakati ulikuwa umefika ili hilo taifa la Israeli, au Yakobo, litumie kitu cha bei kubwa kuliko dhabihu za wanyama zilizotolewa juu ya madhabahu ya hekalu katika Yerusalemu ili lifanye upatanisho kwa ajili ya “kosa” lililotenda. Hii ndiyo dawa ambayo Yehova aliandikia tengenezo lake lililo mfano wa mke, akisema:

“Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafanyiwa upatanisho, na hayo ndiyo matunda yote wakati yeye achukuapo dhambi yake kuiondoa, wakati afanyapo mawe yote ya madhabahu yawe kama mawe ya chokaa ambayo yamepondwa yakawa unga, hivi kwamba zile nguzo takatifu na vinara vya uvumba hazitainuka.” (Isaya 27:9, NW)

Kweli utimizo wa unabii huo ungekuwa wonyesho wa hasira kali ya kimungu, na ilikuwa haki uwe hivyo! Zile nguzo takatifu zenye kuabudiwa kama sanamu na vile vinara vya uvumba havingeinuka tena ndani ya taifa lake lililotakaswa kwa kuadhibiwa.

14. Nchi ya Israeli ingefanywa iwe ukiwa wa namna gani, na ukuzi wayo ikiwa kama mti wa mfano ungeshughulikiwaje?

14 Kuonyesha ukiwa ambao ungeletwa juu ya taifa hilo la Israeli wa kale lililo mfano wa mke, Yehova anaongeza hivi:

“Kwa maana ule mji wenye ngome utakuwa peke yao, nayo ardhi ya malisho itahamwa na kuachwa kama nyika.”

Nchi ile ambayo wakati mmoja ilikuwa na halaiki ya watu ingehamwa, kwa muda huo iwe mahali pa kulisha mifugo.

“Hapo ndama atakula majani, na hapo atalala chini; na kwa kweli yeye [Yehova, kwa kutumia mtekelezaji wake] atakula ayamalize matanzu yake. Wakati vichipukizi vyake vimekwisha kukauka, wanawake wanaoingia watavivunja, waviwashe moto [viteketee].” (Isaya 27:10, 11, NW)

Hivyo taifa la Yehova lililo mfano wa mke lingefanywa liwe kama kuni tu za kuwashia moto, kwa maana ile jinsia ya kike ingekuwa na nguvu za kujipatia kwa urahisi visehemu vilivyobaki vya taifa hilo. Ingekuwa hali ya kusikitisha kama nini tengenezo la Israeli lililo mfano wa mke kubaki likiwa hivyo! Lakini ni kwa sababu gani Mungu, Yehova, aliye mfano wa mume, achukue hatua hizo zenye kuvunja moyo? Sikiliza:

15. Kwa sababu ya kutendewa na Yehova mambo ya pekee, taifa la Israeli lingalipaswa kuwa watu wa namna gani, lakini kwa sababu gani wakaja kuwa kama mataifa yenye kuabudu sanamu?

15 “Kwa maana hiyo si jamia ya watu wenye ufahamu ulio na makini. Hiyo ndiyo sababu Mfanyiza wayo hataionyesha rehema, na Muumbaji wayo yenyewe hataionyesha kibali cho chote.” (Isaya 27:11, NW)

Kwa sababu ya uandalizi wote ambao Yehova alikuwa amefanya ili kuelimisha na kuliangazia ufahamu tengenezo lake lililoumbwa vizuri ajabu, Waisraeli wangalipaswa kuwa jamia ya wafu wenye akili nyingi. Wangalipaswa kuwa wepesi na wenye kutambua mambo vya kutosha hata waone kwamba ibada ya sanamu ilikuwa kazi-bure, ndiyo, watambue mambo vya kutosha hata waweze kuona upumbavu wa kuabudu sanamu, iliyozoewa na mataifa yenye ujinga yaliyokuwa nje ya uhusiano wa agano pamoja na Mungu yule mmoja tu aliye hai na wa kweli, Yehova. Lakini kwa sababu Mfanyiza na Muumbaji wao wa kimbingu hakuwa akionekana kwa macho, wao walipoteza imani kisha wakachagua kugeukia miungu yenye kuonekana iliyofanywa na wanadamu, wakajiletea uangamivu. Ndiyo sababu kibali na rehema ya kimungu ilizidi kuondolewa kwa watu hao wenye kujitakia yao wenyewe.

Kukombolewa Uhamishoni

16. Ili kurudisha watu wake, ingekuwa lazima Yehova aelekeze fikira zake kwenye nini?

16 Basi sasa, ili kuwarudisha kwenye ibada yake katika nchi ya kwao, ingehitajika Yehova arudishe fikira zake kwenye nchi ya Babulonia ambako ule “Mto” mkuu, ule Eufrate, ulitiririkia. Angeelekeza fikira upande wa chini kuelekea kusini kwenye nchi ya Misri, kwa maana ni katika sehemu hizo watu wake walikuwa wamehamishiwa, wakatolewa kwake wapate nidhamu. Kwa ajili ya jambo hilo Yehova akalazimika kutimiza taarifa ya alivyokusudia kufanya baada ya hapo:

“Na lazima itukie siku hiyo kwamba Yehova atayapukutisha matunda, kutoka kile kijito kinachotiririka cha ule Mto [Eufrate] mpaka kwenye bonde lenye bubujiko la maji la Misri [lile bonde lenye mto kwenye mpaka wa magharibi-kusini ya Nchi ya Ahadi], na kwa hiyo ninyi wenyewe mtasombwa mmoja baada ya mwingine, Enyi wana wa Israeli.”​—Isaya 27:12; linganisha Hesabu 34:2, 5.

17. Yehova aliwakoboaje watu wake kutoka hali ya uhamisho, na kwa kutumia njia gani?

17 Ili Yehova arudishe watu wake kwenye nchi yao ya Yuda, angepaswa kuwakoboa wahamishwa hao kama matunda, hivyo awafungue wawe huru. Alifanya hivyo kwa kuipindua serikali kubwa ya ulimwengu ya Babulonia na kuanzisha upesi Milki ya Muungano wa Wamedi na Waajemi, ile serikali kubwa ya ulimwengu iliyo ya nne katika historia ya Biblia. Agizo lililotolewa na mfalme Mwajemi Koreshi Mkuu mwanzoni mwa utawala wake lilikuwa la kuwafungua wahamishwa wa Yehova warudie mahali ulipokuwa Yerusalemu wa kale ili wajenge upya hekalu la Yehova. Marudi hayo yalitukia katika mwaka 537 K.W.K., mwishoni mwa ile miaka 70 ya Wayahudi kukaa uhamishoni.​—Isaya 45:1-7.

18. Lazima iwe wahamishwa walitendaje lilipotolewa agizo waachiliwe huru?

18 Waisraeli watiwa nidhamu wakiwa katika Babulonia, na pia katika Ashuru na Misri, walikuwa mali ya Yehova, naye alikuwa na haki ya kuwakoboa kama matunda ya mfano watoke katika uhamisho na utawanyiko wasiokuwa wamejitakia wenyewe, na hivyo awaonyeshe rehema, fadhili zisizostahilika. Lazima iwe Waisraeli hao wa kale walilifurahia kweli kweli agizo hilo la Koreshi, na lazima iwe walionyesha ni wenye bidii kweli kweli kwa kuitumia kikamili hiyo nafasi nzuri sana waliyopewa! Basi ingesemwa nini juu ya “siku” hiyo yenye upendeleo?

19. (a) Waisraeli waliotawanywa katika Ashuru na katika Misri walitabiriwa kuwa wangeinamia nani? (b) Hiyo ingemaanisha nini kuhusu ibada ya Yehova mahali ambapo hekalu lilikuwa hapo mwanzoni, na hiyo ikifananisha taifa gani la kiroho la kisasa?

19 “Na lazima itukie siku hiyo kwamba kutakuwa na mpulizo kwenye mbiu kubwa, na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru na hakika wale ambao wametawanywa katika nchi ya Misri watakuja na kuinamia Yehova katika ule mlima mtakatifu katika Yerusalemu.” (Isaya 27:13, NW)

Hiyo ilimaanisha kwamba Nchi ya Ahadi ingekuwa tena na watu na hekalu katika Yerusalemu lingejengwa upya, lirudishwe kwa ajili ya ibada ya Muumbaji na Mfanyiza wa taifa la Israeli lililohuishwa? Ilikuwa lazima iwe hivyo kulingana na maneno ya nabii Isaya yaliyotangulia kuonyeshwa katika mstari wa 6. Ilikuwa lazima nchi ya watu wake waliorudishwa iwe nchi yenye kusongamana na wakaaji, wenye kufuata kwa umoja ibada yake kwenye hekalu lake, ingawa mahali hapo pa ibada paliporudishwa hapakuwa na fahari kama ile ya hekalu tukufu lililojengwa na Mfalme Sulemani. Kwa njia hiyo jambo hilo lingetangulia kuwa kivuli cha utimizo wa kiroho katika siku hizi, unaohusu “Israeli wa Mungu” kwa kujaza matunda yenye kupa watu uhai, au “mazao,” katika sehemu zote za ile “nchi yenye kuzaa.”​—Wagalatia 6:16; Isaya 27:6, NW.

[Maelezo ya Chini]

a Jambo la kupendeza ni kwamba, kichapo Oxford NIV Scofield Study Bible (1984) kinatoa maelezo haya juu ya Luka 21:24: “‘Majira ya Mataifa’ yalianza Nebukadreza alipoteka Yuda (2 Nya. 36:1-21). Tangu wakati huo Yerusalemu ‘umekanyagwa na Mataifa’ kama vile Kristo alivyosema.

Wewe Unajibuje?

◻ Ni wakati gani na jinsi gani Waisraeli wa asili walipopigwa “dharuba,” kama ilivyotabiriwa katika Isaya 27:7?

◻ Waisraeli ‘walitiaje mizizi’? (Isaya 27:2,6, NW)

◻ Ni akina nani nyakati za kisasa wanaohusika katika utimizo wa unabii ulio katika Isaya sura ya 27?

◻ Wao wamekuwaje kama shamba la mizabibu lenye mazao, linalotokeza “divai inayotoa mapovu”?

[Picha katika ukurasa wa 13]

Kupitia Wababuloni, Yehova alipiga pigo kali mwaka 607K.W.K.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki