Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 5/1 uku. 21
  • ‘Yeye Aonaye Hekima Aona Uzima’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Yeye Aonaye Hekima Aona Uzima’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Aliazimia Aishi Kulingana na Viwango vya Adili za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Watu wa Namna Zote Wataokolewa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 5/1 uku. 21

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

‘Yeye Aonaye Hekima Aona Uzima’

“UKWELI unavutia ‘watu wa aina zote,’ kutoka mitaa mbali-mbali inayojumlika kuwa Taifa la Israeli,” inaandika afisi ya tawi ya Sosaiti yetu katika nchi hiyo. watu hawa wanaotafuta ukweli kwa moyo mnyofu wanahakikishiwa hivi: “Yeye anionaye mimi [hekima] aona uzima, naye atapata kibali kwa [Yehova].” (1 Timotheo 2:4; Mithali 8:35) Jambo lililoonwa kuhusu mwanamke mmoja katika Israeli linaonyesha hivyo.

◻ Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alifikia mwandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na kupanga kuongoza pamoja naye funzo la Biblia. Mama huyo alifurahi kuwa na funzo. Jirani yake akapata habari juu ya jambo hilo na alihudhuria funzo. Jirani huyo “alitambua bila kukawia kwamba hiki ndicho kitu alichokuwa akikitafuta kwa muda wa miaka kadha iliyopita,” inasema ripoti hiyo. Naye alifanya upesi upesi mabadiliko makubwa kama nini katika maisha yake! Yeye na mume wake walikuwa wamebakiza siku chache tu kabla ya kupata amri ya kisheria watalikane lakini wakaifuta amri hiyo na kufanya amani. Mwanamke huyo alikuwa akifuata sana unajimu na dini fulani ya kifumbo lakini alitupa vitabu vya gharama kubwa na kila kitu kinginecho kilichohusiana na mambo ya mashetani. Akaanza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na kueleza watu wa ukoo na marafiki juu ya imani mpya aliyokuwa ameipata. Kwa habari ya marafiki aliowapoteza kwa sababu hiyo, mwanamke huyo anasema: “Inaonekana hawakuwa marafiki wa kweli.”

Sasa mwanamke huyo anawatolea ushahidi kwa shauku wanunuzi katika duka la jamaa yao na kushiriki kwa ukawaida kuzihubiri habari njema nyumba kwa nyumba. Yeye anafurahi kama nini kwamba amepata hekima na kujifunza juu ya maandalizi ya ajabu ya Yehova kwa ajili ya uzima wa milele katika mfumo mpya wake! Jirani yake ambaye hapo kwanza aliandika barua awe akipata uandikisho ameendelea pia kujifunza na anafanya maendeleo.

◻ Lloyd anaishi katika Guyana. Safari yake ya kuelekea kwenye uhuru wa kidini ilikuwa ndefu. Kuhama kwake kulianza akiwa Mpresbiteri. Yeye alioa Mhindu na mwanamke huyo akawa Mpresbiteri pia. “Mimi nilihuzunishwa sana na unafiki uliopatikana kwa wingi” katika kanisa hilo, akakiri mwanamume huyo baadaye. Kwa hiyo akaugeukia Uislamu, lakini haukuridhisha utafutaji wake wa uhuru. Ndipo akajaribu dini ya Hindu. Baada ya kujifunza mengi juu ya imani ya kufa na kwenda kuzaliwa mahali pengine na sheria za Karma alianza kutia mashaka juu ya mafundisho haya. Akabadili dini na kufuata imani ya mafumbo, akajenga madhabahu na kuikazia jamaa yake mafundisho ya imani hiyo. “Lakini mambo ya kuogopesha na kufadhaisha ambayo mimi na jamaa yangu tulipatwa nayo yalitufanya tukaiacha dini hiyo,” akasema. Alichagua njia ya maisha ya kufuatia vitu vya kimwili, lakini jamaa yake ikawa ikibomoka-bomoka. Kwa hiyo akasema: “Nilimpelekea sala Mungu, Baba, Allah, Ram nikamwambia kwamba ninasema na Muumba wa vitu vyote. Nilimjulisha kwamba nilitaka kumpendeza yeye wala si mwanadamu.”

Hapo Shahidi wa Yehova “aliyevaa vizuri, mwenye kusema kwa upole, mtu mwanana” alifika mlangoni pa Lloyd na kumjibu maulizo yake kwa njia yenye kuridhisha. Shahidi huyo alimwachia kitabu, Kweli longozayo Kwenye Uzima wa Milele na Biblia. Baada ya muda mfupi funzo la Biblia likaanzwa pamoja na Lloyd na mkeye, wakafanya maendeleo katika kupata maarifa, wakajitenga na Babuloni Mkuu—ule mfumo wa ulimwenguni pote wa dini ya uwongo. Baada ya muda wakajiweka wakfu na kubatizwa. Lloyd alisema: “Upendo, upendo wa kweli ulikuja mahali pa chuki na hasira; na jambo la maana zaidi ya yote ni kwamba maana na kusudi vimeongezwa kwenye maisha yetu.”

Sasa wao wanaufurahia ‘ukweli uliowaweka huru.’—Yohana 8:32.

◻ Mwanamke kijana katika Ushelisheli alijifunza pia juu ya Yehova, naye Yehova akambariki. Alikuwa akiishi pamoja na mwanamume fulani wa kupanga tu, naye alikuwa amepata watoto kadha kutokana na mwanamumu huyo. Mwanamke huyo aliuthamini ukweli aliokuwa akijifunza kutoka katika Biblia lakini akaona ni vigumu kuchukua msimamo ili astahili kufanya utumishi wa Yehova. Alikuwa akiishi katika nyumba nzuri yenye starehe nyingi zisizofurahiwa na watu wengi. Baada ya kusali na kutiwa moyo na mwangalizi wa mzunguko, alimpa mwanamume yule aliyekuwa akiishi pamoja naye chaguo la kufanya—ama walazimike kuoana kisheria ama watengane. Mwanamume yule hakutaka kuchukua hatua mojapo, kwa hiyo mwanamke yule akamwacha. Alifurahi kama nini kwamba sasa alistahili kuzihubiri habari njema na kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova na kubatizwa! Alifanya hivyo. Jambo la kupendeza ni kwamba, mwanamume aliyekuwa akiishi naye alivutwa sana na msimamo wake wa ujasiri wa kutetea kanuni za Biblia mpaka yeye akaanza kufanya mipango ya kuunganisha jamaa kupitia ndoa ya kisheria.

Mtunga zaburi aliungama hivi: “Maana kwako Wewe [Yehova] iko chemchemi ya uzima.” (Zaburi 36:9) Watu hao walikubali hivyo, pia, na wakatafuta hekima ili wamjue Yehova na matakwa yake kuhusu uzima. Wao wanathamini sana uhakika wa kwamba “yeye [aonaye hekima] aona uzima”!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki