Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 5/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wakati Ambapo Ukubwa Haufai
    Amkeni!—1997
  • Naweza Kupunguzaje Uzito?
    Amkeni!—1994
  • Je, Kunenepa Kupita Kiasi ni Tatizo?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 5/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! Mashahidi wa Yehova wako imara juu ya ulafi kati ya washiriki wao kama walivyo juu ya zoea lenye madhara la kutumia tumbaku?

Mashahidi wa Yehova wanachukua msimamo wenye msingi wa Biblia dhidi ya tumbaku, na wanalikubali kwa kadiri iyo hiyo katazo la Kimaandiko juu ya ulafi.

Wanaamini kwamba kuvuta tumbaku kunavunja kanuni za Biblia. Kuvuta tumbaku kunahusu kuzoelea sumu iliyo ndani ya tumbaku. Tena, si jambo la asili kuvuta moshi. Kuvuta tumbaku kunauchafua mwili, kunaleta matatizo ya kiafya, na kumefupisha maisha ambazo zingalipasa kutumiwa kumsifu Mungu. Kuvuta tumbaku pia kunachafua kwa njia hatari hewa inayovutwa na wengine; hakika huo si upendo kwa jirani.—2 Wakorintho 7:1; Warumi 12:1; Marko 12:33.

Ingawa hivyo, namna gani kula mno kwa njia ya ulafi? Kwa kutoboa wazi, Biblia inakataza ulafi, ambayo ni pupa ya kula, au kula mno kwa uroho. Mwana Mwisraeli aliyekuwa “mlafi na mlevi” asiyetubu alipaswa kuuawa. (Kumbukumbu la Torati 21:18-21, NW ) Mithali inaonya dhidi ya kuwa “rafiki wa walafi” (Mithali 28:7; 23:20, 21) Ulafi ni mbaya pia kwa kuwa tunaambiwa kwamba “watu wenye pupa” hawataurithi Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 6:9 10, NW; linganisha 1 Petro 4:3; Wafilipi 3: 18, 19) Waangalizi Wakristo wanapaswa kuwa ‘wenye kiasi,’ wala si ‘walafi, wavivu.’ (Tito 1:8, 12) Hili ni jambo zito sana hivi kwamba waangalizi wengine wameondolewa kwa sababu ya kula bila kujizuia.

Lakini, ni lazima itambuliwe kwamba si jambo rahisi kuamua kwamba mtu amekuwa mlafi. Kula (tofauti na kuvuta moshi wa tumbaku) ni jambo la asili na lenye kufaa. Wala mtu akiwa na mwili wenye mafuta-mafuta, hiyo pekee yake siyo inayoonyesha yeye ni mlafi; mtu mwembamba sana anaweza kuwa mlafi. Uzito wa kupita kiasi silo jambo linalolaumiwa vikali na Biblia, bali ni kula mno kupindukia, jambo ambalo huenda likafanya au lisifanye mtu awe bwana au mama tumbo (mnene mno).

Watu wengine wana uzito wa kupita kiasi kwa sababu ya ugonjwa au viungo vyao vya mwili havifanyi kazi vizuri, ingawa Profesa Judith Rodin anashikilia kwamba “asilimia 5 ya visa vyote vya unene wa kupita kiasi vinasababishwa hasa na matatizo ya kitiba.” Au hali ya kurithi huenda ikafanya mtu aelekee kuwa mnene-mnene. Dakt. William Bennett anaeleza: “Wengi wa watu waliona miili yenye mafuta-mafuta wanadumisha uzito wao kwa kula karibu kiasi kile kinacholiwa na mtu mwenye uzito wa kawaida, . . . Mapokezi ya chakula ndani ya miili yao ni tofauti.” Wanasayansi fulani hata wanaona kwamba mtu aliye na mwili wa mafuta-mafuta akipunguza ulaji wake, mwili wake ‘unapunguza mwendo wa kukipokea chakula hivi kwamba kalori zake zinayeyushwa polepole zaidi.’ Lakini hata ikiwa mtu aliye na mwili mwenye mafuta-mafuta si mlafi katika maana ya kuwa mlaji mwenye uroho, yeye (awe mwanamume au mwanamke) huenda akahitaji kutumia kwa uzito zaidi mashauri ya Mungu.

Kwa mfano, Wakristo wanapasa wasitawishe kujiweza, na hiyo inahusu kula pia. (Wagalatia 5:22, 23 NW; 2 Petro 1: 5-8) Mtume Paulo aliwahimiza Wakristo wawe kama mwanariadha ambaye “anajizoeza kujiweza katika mambo yote.” Paulo ‘aliupiga-piga ngumi mwili wake na kuufanya kama mtumwa asije akakatiliwa.’ (1 Wakorintho 9:24-27, NW ) Mtu mnene anaweza kuwa na sababu ya kumpasa ‘aupige-pige ngumi mwili wake’ juu ya ni kiasi gani, ni chakula gani, ni wakati na jinsi gani atakula.a

Kuwa na mwili mwenye mafuta-mafuta kunaweza kuwa na hatari. Ripoti zinaonyesha kwamba unene wa kupita kiasi, unaweza kufanya mkazo wa damu uongezeke na kuzidisha kolesteroli, ugonjwa wa sukari unaoingia baada ya kuwa mtu mzima, namna kadha za kansa, ugonjwa wa moyo na wa nyongo, yabisi kavu, na matatizo ya kupumua. “Mtu aliye na uzito wa kupita kiasi kwa asilimia 20 anaelekeana na kiwango cha kufa kilicho mara tatu kuliko kile cha wastani; kwa wale walio na uzito wa kupita kiasi wa asilimia 30 na 50, kiwango cha kufa ni asilimia 50 na 100 juu ya kile cha wastani, kulingana na uzito wa mtu.” (The New York Times, Februari 27, 1985) Ripoti zinazofanana na hizo za matatizo ya kiafya zinakuja kutoka Uingereza, Ujeremani na Italia.

Mkristo anataka kweli kweli ‘kumpenda Yehova kwa moyo wake wote, nafsi [au, uhai], akili na nguvu zote.’ (Marko 12:30, NW )Watu wengi, wakiisha kujifunza Ukristo, wanaacha kuvuta tumbaku ili wahifadhi afya na uhai wao. Je, haiwapasi Wakristo wahangaike jinsi iyo hiyo kwamba kuwa na uzito wa kupita kiasi kwa sababu ya kula na kunywa kupita kiasi kunaweza kuharibu afya na uhai wao uliowekwa wakfu kwa Yehova?

Watu wengine wanakula chakula kingi zaidi wanapokuwa wamehuzunika, wamevurugika mawazo, wakiwa wapweke au wakikasirika. Ingawa kuwa Mkristo hakuzuii hisia hizo, badala ya Mkristo kujituliza kwa kula ovyo-ovyo, yeye anaweza kutaka msaada wa Mungu na ndugu zake. Katika habari hiyo soma Wafilipi 4:6, 7,11-13. Hata wanasayansi wanaoshikilia ya kwamba mtu ana maelekeo ya asili ya kupata uzito fulani wa mwili wanakiri kwamba jambo hilo linaweza kubadilishwa. Wanakazia kupunguza chakula chenye mafuta mengi na kuongeza mazoezi ya kimwili. Jambo la kupendeza ni kwamba, katika maeneo mengi Mkristo anayeishiriki kwa ukawaida huduma ya nyumba kwa nyumba anatembea-tembea na kupanda-panda sehemu zenye miinuko kwa njia yenye kumpa afya. Paulo, pia, ‘alifanya kazi ngumu na kutoa jasho’ katika huduma.—2 Wakorintho 11:26,27, NW.

Hivyo, Mashahidi wa Yehova hawakubalii ulafi kwa sababu ya inayosema Biblia. Hata wawe wana uzito gani wa mwili, wao wanajitahidi ‘kujizoeza kujiweza katika mambo yote,’ kutia na ulaji. Hiyo siyo kwa sababu hasa ya uamuzi uliofanywa kulingana na utamaduni wa mahali fulani, bali ni kwa sababu wao wanataka kuishi kulingana na kanuni za Biblia na kuwa Wakristo watendaji wenye kibali ya Mungu.

[Maelezo ya Chini]

a Ni kiasi gani: kula kiasi kidogo bila ugeu-geu wakati wa kila chakula. Kula nini: kupunguza vyakula visivyojenga mwili na vyenye wanga mwingi na soda, tamutamu na shahamu, kama siagi na mafuta, na badala yake kuwa na ulaji wenye afya, uliosawazika. Ni wakati gani: kutotafuna-tafuna vyakula vidogo vidogo kati ya milo mikubwa wala kula kwa siri. Ni jinsi gani: kula pole-pole zaidi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki