Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 8/1 uku. 3
  • Je! Wafu Wako Hai? Yanayosemwa na Wanadamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wafu Wako Hai? Yanayosemwa na Wanadamu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wafu Wako Hai? Yanayosemwa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Je! Ibada ya Mababu Waliokufa Yawapasa Wakristo?
    Amkeni!—1990
  • Wazazi Wetu wa Kale Wako Wapi?
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Ukweli Kuhusu Helo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 8/1 uku. 3

Je! Wafu Wako Hai? Yanayosemwa na Wanadamu

MWANAMKE mzee huyo mweusi alionekana mgonjwa-mgonjwa sana. Miguu yake ilimwuma sana ikawa ni shida kutembea. Kuonekana kwake kulikuwa kwa kiajabu-ajabu—nywele zake zilikuwa zimepakwa-pakwa udongo mwekundu, alikuwa amevaa vitambaa vingi vya shingoni, na mikono na miguu yake ilikuwa imepambwa kwa hirizi nyingi. Kwa sababu gani? Kwa sababu kwa muda wa miaka zaidi ya 50 yeye aliamini kwamba alipagawa na roho za wazazi wake wa kale waliokufa. Wachawi ndio walikuwa wamemwagiza ajipake udongo, avae vile vitambaa vya shingoni, na hirizi ili ‘kumponya.’

Je! hiyo ni imani ya watu wachache tu? Sivyo. Katika Afrika tu maisha za watu wasio na hesabu zinategemea imani ya kwamba wazazi wa kale waliokufa wana uwezo wa “kulinda wazao wao au kuwaadhibu kwa magonjwa madogo-madogo au mkosi,” kama vile kinavyoeleza kitabu African Heritage. Ibada ya wazazi wa kale waliokufa inayofanana na hiyo inazoewa katika sehemu nyingine nyingi za ulimwengu. Ingawa huenda likaonekana kama kwamba ni jambo la kushangaza, ibada ya namna hiyo inaelekea kuwa ina uhusiano fulani na imani za kidini za mahali unapoishi. Jinsi gani?

Wahindu na wengine wanaamini juu ya kuzaliwa kwa nafsi katika umbo jipya. Wenye kuwasiliana na ulimwengu wa roho wanaamini kwamba mtu anaweza kuwasiliana na wafu kwa kutumia vyombo vya kuwasiliana na ulimwengu wa roho. Wakatoliki wanafundishwa kwamba watu walio wengi wakifa inakuwa lazima dhambi zao zikasafishwe katika purgatori (tohara) kabla ya kufika mbinguni hatimaye, lakini kwamba walio waovu wa kupindukia wanaenda kwenye moto wa mateso. Waprotestanti walio wengi wanaamini kwamba watu wema wanaenda mbinguni na wabaya wanateswa-teswa katika moto wa mateso, na wengi wanasadiki kwamba hivyo ndivyo Biblia inavyofundisha. Watu fulani ambao wamepatwa na vituko vya kukaribia kufa wanasadiki kwamba kitu fulani kinauacha mwili na kuendelea kuishi wakati mtu anapokufa.

Ingawa dini zina maoni mbalimbali juu ya mawazo yao hasa juu ya maisha baada ya kufa, zilizo nyingi kati yazo zina jambo hili moja kwa ujumla—imani ya kwamba wafu wako hai.

Hakika kifo ni adui mbaya sana, mwenye kuua watu wa rangi zote, matajiri na maskini, vijana na wazee. Ni kama vile Biblia inavyosema: “Ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka.” (Yakobo 4:14) Kila siku hesabu kubwa za watu wanapoteza wapendwa katika kifo.

Kwa hiyo watu wengi wanataka kujua wakijiuliza hivi: ‘Wameenda wapi? Je! kweli wamekufa au bado wako hai mahali fulani? Je! tutapata kuwaona tena? Tunaweza kupata wapi majibu ya ukweli? ’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki