Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 8/15 kur. 3-4
  • Matumizi Mabaya ya Uwezo Je! Kweli Yataisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matumizi Mabaya ya Uwezo Je! Kweli Yataisha?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yalianza Wakati Gani?
  • Sababu Gani Yatamalizika Pasipo Shaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Wenye Furaha ni Wale Wanaotumia Uwezo kwa Njia Inayofaa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kuzuia Nyumbani
    Amkeni!—1993
  • Jilinde Usitumie Vibaya Uwezo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 8/15 kur. 3-4

Matumizi Mabaya ya Uwezo Je! Kweli Yataisha?

KATI ya njia ambazo watu wasio wakamilifu wanaonyesha jinsi walivyo wachoyo ni kutamani sana kuwa na uwezo. Mwandikaji Mwingereza anayejulikana sana, Malcolm Muggeridge, alionyesha kwamba watu wanaopenda uwezo “kwa sababu [wao] hawajatambua kwamba msingi wa maisha ya kibinadamu ni upendo . . . Lakini kwa msingi tamaa nyingi ya kutaka uwezo ni hatari sana. Hiyo ndiyo Yesu Kristo alikataa kuwa nayo.”

Kwa sababu ya kuenea kwa tamaa hiyo nyingi ya kutaka uwezo, pamoja na madhara makubwa inayoweza kuleta, Mababa Waanzilishi wa United States walitunga katiba iliyogawanya mamlaka za kiserikali katika sehemu tatu: ya utekelezaji, ya kutunga sheria, na ya kuhukumu. Sehemu hizo zingechunguza ili kusiwe na matumizi mabaya ya uwezo.

Ijapokuwa Waanzilishi hao walikuwa na makusudi mazuri sana, matumizi mabaya ya uwezo yameenea sana katika nchi hiyo. Lakini huenda wewe ukawa unajua kutokana na mambo unayojionea mwenyewe kwamba kumekuwa na matumizi mabaya ya uwezo katika sehemu zote za ulimwengu. Historia imejawa na kumbukumbu za wanadamu waliotumia uwezo vibaya wakajitukuza sana wao wenyewe na kudhuru wanadamu wenzao. Kwa mfano, fikiria Alekizanda Mkuu, Charlemagne, Napolina, na Hitler.

Yalianza Wakati Gani?

Ingawa hivyo, wewe una sababu nzuri ya kuuliza ni wakati gani matumizi hayo mabaya ya uwezo yalianza? Jibu la kutegemeka linapatikana katika kitabu cha historia ya zamani zaidi ya mwanadamu, ambacho ndicho Biblia. Humo unaweza kusoma juu ya matukio yaliyotendeka katika bustani ya Edeni. Shetani Ibilisi, ambaye Biblia inaonyesha ni kiumbe halisi, aliona njaa ya kutaka uwezo. Alishawishi jamii ya kibinadamu ianze kufuata barabara ya kuelekea kwenye dhambi. Udhihirisho mmoja wa dhambi ni tamaa mbaya ya mwanadamu iliyoenea sana ya kutaka uwezo na kuutumia vibaya. (Mwanzo 3:1-19; Warumi 5:12) Zamani za kale Shetani aliyafanya mataifa yaje chini ya uongozi wake, hata yeye akaweza kumtolea Yesu Kristo utawala juu yayo. (Mathayo 4:8-10) Ibilisi amedanganya karibu wanadamu wote, hivi kwamba inaweza kusemwa “ulimwengu mzima umo katika uwezo wa yule muovu.”​—1 Yohana 5:19; Ufunuo 12:9, NW.

Hapa pana wazo linaloweza kukugutusha: Kati ya wale ambao wametumikia zaidi kusudi la Ibilisi wamekuwa ni viongozi wengi wa kidini. Jinsi gani hivyo? Wao wametumia uwezo vibaya kwa kufundisha watu mafundisho ya uwongo, hivyo wakawafanya kuwa watumwa. Viongozi wa dini wa uwongo wametumia uwezo wao vibaya kwa kuwatesa pia watumishi wa kweli wa Mungu. Stefano, Mkristo mfia-imani wa kwanza, alionyesha kumbukumbu ya kusitikisha ya viongozi wa kidini wa Israeli: “Enyi wenye shingo [n]gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio . . . Ni yupi katika nabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? nao waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake, mkamwua.”​—Matendo 7:51, 52.

Stefano alikuwa mmoja wa wale wa kwanza-kwanza wa mstari mrefu wa Wakristo waaminifu ambao wameteswa. Maneno ya mtume Paulo yamethibitika kuwa ya kweli: “Wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa [watateswa, NW].” (2 Timotheo 3:12) Kumbukumbu ya mambo ambayo yamepata Mashahidi wa Yehova nyakati za kisasa inashuhudia hivyo. Hata sasa, katika nchi zipatazo 40 Wakristo hao wanaona matumizi mabaya ya uwezo kwa sababu huduma yao inazuiwa na wenye mamlaka.

Na kuna namna nyingine nyingi kama nini za kutumia uwezo vibaya! Po pote tunapotazama, tunaona watu wakiungua moyoni kwa sababu ya jambo hilo. Matumizi mabaya ya uwezo kwa upande wa waajiri-kazi ndiyo yaliyotokeza chama cha kutetea haki za kufanya kazi. Lakini leo ni wazi kwamba viongozi fulani katika matengenezo ya kikazi wana hatia pia ya kutumia uwezo vibaya. Makabila yenye watu wachache yanaumizwa na matumizi mabaya ya uwezo wa walio wengi. Namna nyingine ya matumizi mabaya ya uwezo ni ile inayofanywa na wanaume wenye vyeo vya usimamizi wanaochezea vibaya wanawake walioajiriwa kazi, na wanawake hao huenda wakahisi kulazimishwa kutii matakwa ya wanaume hao kwa kuogopa wasipoteze kazi zao. Kwa mfano, mwanamke mmoja mwenye hamu nyingi ya kuwa mcheza-dansi katika sherehe za pekee alipewa toleo la kuwa na sehemu kubwa katika dansi fulani kama angekubali akalale na mwenye kuitayarisha.

Ndiyo, ulimwengu umejawa na watu wanaotumia uwezo wao vibaya. Wote hao wanaofanya hivyo kwa uchoyo wanatoa ushuhuda wa kwamba hawamwogopi Mungu. Kwa sababu hiyo ni kweli? Kwa sababu, kama linavyosema Neno la Mungu “[kumwogopa Yehova] ni kuchukia uovu.” (Mithali 8:13; Zaburi 97:10) Kutumia uwezo isivyofaa ni jambo baya kweli kweli, lakini hilo halitaendelea kuwapo sikuzote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki