Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 10/15 kur. 21-24
  • Kumsifu Yehova kwa Muziki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumsifu Yehova kwa Muziki
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Matokeo ya Muziki
  • Matumizi Yaliyo Bora Zaidi
  • Sehemu za Utungaji-Sauti-Tamu
  • Maendeleo Katika Mawazo Yaliyomo
  • Hazina za Kiroho
  • Ninaweza Kuwekaje Muziki Mahali Pao Panapofaa?
    Amkeni!—1993
  • Muziki Unaomfurahisha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Jihadhari na Muziki Unaovunja Heshima!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kupata Shangwe Yamuziki—Ni Nini Ufunguo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 10/15 kur. 21-24

Kumsifu Yehova kwa Muziki

KUNA njia nyingi ambazo watumishi wa Yehova wanaweza kutumia wamletee yeye sifa. Bila shaka, kati ya njia zinazopendeza zaidi na kati ya zile zinazoletea moyo wake furaha kubwa ni ile ya ‘kuimba kumfanyia muziki mtamu.’ (Zaburi 105:2, NW) Imeonekana sana kwamba muziki ni moja ya “chapa zinazotambulisha utu wa wanadamu.”

Muziki umeitwa pia “ile zawadi ya kibinadamu isiyo na kifani, ya kugundua ustadi wa kufanya mambo mapya na kuendelea kugundua mwingine.” Wanyama, wawe ni wa mwitu au wa kufugwa, hawana uwezo wa kufanya muziki. Ni kweli kwamba ndege wengine wanaimba nyimbo za kupendeza, lakini wanafanya yote hayo kwa silika tu. Wao hawana ufahamu wa muziki kama vile kasuku wasivyo na ufahamu wa maneno yo yote ambayo huenda wakazoezwa kusema. Lakini sisi tukiwa na muziki wa kupendeza, tunaweza kufikia mioyo ya wengine, kama vile tunavyoweza kupashana habari na akili za wengine kwa kutumia usemi.

Ndiyo, muziki ni zawadi ambayo Muumba amewapa wanadamu, na lo, hiyo ni zawadi kama nini! Uchunguzi uliofanywa hivi majuzi unaonyesha kwamba watoto wachanga wanaonyesha hata kabla hawajazaliwa ni muziki gani wanaopenda​—mtamu na wenye kufurahisha​—na ni muziki gani wasiopenda​—wenye mdundo wa nguvu nyingi na wenye makelele, kama vile muziki wa roki. Tunaambiwa pia kwamba mtoto asiyezaliwa anaweza kusitawisha uhodari wa mambo ya muziki anaposikia muziki wa kupendeza. Kwa hiyo muziki unaletea wanadamu furaha kubwa, si tangu utotoni mpaka kufa tu, bali pia tangu tumboni mpaka kufa! Kwa kuwa kwa kawaida muziki hauonwi kuwa unahitajiwa kabisa ili binadamu aweko, jambo la kwamba Muumba aliwezesha wanadamu kutunga muziki na kufurahia ni mfano mwingine wa hekima na upendo wake. “Waebrania walikuwa taifa mashuhuri katika muziki,” tunaambiwa. Na ni jambo linalostahili sifa kweli kweli kwamba muziki ulikaziwa mapema sana katika historia ya kibinadamu, pamoja na ukulima na utengenezaji wa vitu, hiyo ikiwa ni moja ya shughuli za wanadamu.​—Mwanzo 4:20-22

Matokeo ya Muziki

Lakini, tusikose kamwe kuangalia uhakika wa kwamba muziki unaweza ama kuwa wenye kujenga ama wenye kushusha heshima. Muziki mzuri unaunganisha milio ya kupendeza yenye midundo mitamu, upatani, na mfuatano wa sauti za namna mbalimbali; huo unavutia mambo yaliyo ya tabia bora katika wanadamu. Lakini muziki mbaya unavutia maelekeo yenye dhambi ya wanadamu. Muziki huo umeitwa “Ule utatu usio mtakatifu wa . . . jeuri, ngono na kelele.

Jambo la kusikitisha ni kwamba, wanamuziki fulani wanaodai kuwa wanatumikia Yehova Mungu wamepungukiwa katika jambo hilo. Watu kadha kati ya hao wamejikodisha wenyewe ili wapige muziki kwenye arusi kisha wakaonyesha ukosefu wa kuthamini kanuni za Biblia kwa aina ya muziki waliopiga. Muziki wao ulikuwa na kelele nyingi sana hata ikawa haiwezekani kuwa na maongezi ya kikawaida. Inaelekea walisahau kabisa kwamba sababu hasa iliyowafanya wale wageni wa arusi waje haikuwa kusikia wanamuziki wenye kujionyesha uhodari wao wa kupiga muziki.

Muziki mzuri unatimiza makusudi mengi yenye mafaa. Muziki wenye sauti pole ya chini unaweza kutuliza mawazo na kustarehesha mtu. Kiasi kikubwa cha ule unaoweza kuitwa “muziki mzuri ajabu,” kama vile muziki wenye mchanganyiko ya sauti nyingi tamu-tamu unaopigwa na kikundi cha watu wengi na ule unaosikiwa katika jumba la mawonyesho ya muziki, huenda ukavutia uwezo wa kufikiri, au huenda ukaamsha nguvu za kuweza kuwazia mambo na maoni mbalimbali ya moyoni. Isiyopaswa kusahauliwa kati ya muziki huo ni ule ambao kwa kawaida unategemea vichwa vya Kimaandiko, ambao unaopigwa na okestra na korasi zenye waimbaji wengi. Mmoja wa muziki wa namna hiyo ulio mashuhuri ni ule wa Handel unaoitwa “Masihi.”

Muziki unaweza kuwa baraka kwa watu wazee-wazee, wasioweza kuondoka nyumbani kwa sababu ya matatizo fulani, na wale walio wagonjwa. Muziki umetumiwa ili kusaidia watoto wenye matatizo ya akili wakati jitihada nyingine zote ziliposhindwa. Inadaiwa kwamba muziki fulani huenda ukatimiza kusudi lenye mafaa la kutuliza watu katika afisi za madaktari na wataalamu wa meno. Muziki wa aina inayofaa unasemwa kuwa umesaidia wafanya kazi wa viwandani wafanye maendeleo na kufanya kazi nyingi zaidi. Jambo la kupendeza ni kwamba thamani yenye maponyo ya muziki ilithaminiwa zaidi ya miaka 3,000 iliyopita na Mfalme Sauli wa Israeli.​—1 Samweli 16:14-23.

Matumizi Yaliyo Bora Zaidi

Bila shaka, njia bora zaidi ambayo muziki unaweza kutumiwa ni kumsifu Yehova Mungu. Kuimba sifa kwa njia hiyo kunarudi nyumba kama miaka 3,500 kwenye wakati ambao Israeli waliimba sifa ya Yehova baada ya kukombolewa kwenye ile Bahari Nyekundu. (Kutoka 15:1-21) Kumsifu Yehova kwa wimbo na vyombo vya kimuziki kulifanywa kuwa jambo kubwa sana katika ibada kwenye hekalu la Mungu. Muziki wa hekaluni ulihusisha zaidi ya sehemu moja kwa kumi ya hesabu yote ya Walawi. (1 Mambo ya Nyakati 23:3, 5) Okestra na korasi kubwa sana ya waimbaji walikuwapo kwenye kuwekwa wakfu kwa hekalu la Sulemani. (2 Mambo ya Nyakati 5:12, 13) Kwa kufaa kabisa, Maandiko ya Kiebrania (hasa katika kitabu cha Zaburi) yanatuhimiza tena na tena tuimbe na kumfanyia Yehova Mungu muziki mtamu-mtamu.

Tukija kwenye Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, tunasoma kwamba Yesu na mitume wake waliimba wakati wa Chakula cha Jioni cha Bwana. Mtume Paulo na Sila waliimba walipokuwa gerezani katika Filipi. (Mathayo 26:30; Matendo 16:25) Andiko la Wakorintho wa Kwanza 14:15 linadokeza kwamba kuimba kulikuwa sehemu ya ukawaida ya ibada ya makundi katika nyakati za mitume. Kwa kufaa kabisa, Paulo alishauri kama vife tunavyosoma kwenye Wakolosai 3:16, NW: “Endeleeni kufundishana na kuonyana kwa upole kwa zaburi, sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho pamoja na upendezi mkiimba katika mioyo yenu kwa Yehova.” Utapata maagizo yanayofanana na hayo kwenye Waefeso 5:18-20.

Kwa kupatana na amri hizo, tangu nyakati za zamani sana Mashahidi Wakristo wa Yehova wametumia vizuri ile zawadi ya muziki katika ibada yao rasmi. Mwaka ule ule uliokuwa ndio wa kwanza wa kuchapisha Mnara wa Mlinzi wa Sayuni (1879) ndipo kilipochapishwa pia kitabu cha nyimbo, kilichoitwa Songs of the Bride (Nyimbo za Bibi-Arusi). Mwaka 1896 Sosaiti ilichapisha toleo la Mnara wa Mlinzi wa Sayuni ambalo lote kabisa lilikuwa na nyimbo zilizotungwa na Wanafunzi wa Biblia. Toleo lililofuata la gazeti hilo lilisema: “Kuuimba ukweli ni njia nzuri ya kuingiza ukweli huo katika vichwa na mioyo ya watu wa Mungu. . . . Sisi tunamshukuru Mungu kwa ustadi wa kimuziki na wa kishairi waliopewa wengine wa watakatifu wake.” Baada ya miaka mia moja ya kuchapisha vitabu vya nyimbo, kile chenye kuonyesha wazi ustadi ulio mkubwa zaidi wa kimuziki na kishairi kilichapishwa katika Kiingereza mwaka 1984. Kinaitwa Mwimbieni Yehova Sifa.

Sehemu za Utungaji-Sauti-Tamu

Kile kitabu cha nyimbo kilicho cha karibuni zaidi kina kurasa ambazo ni mara mbili za kitabu cha nyimbo kilichotangulia. Kinatokea kikiwa na ukubwa wa kuweza kuwekwa mfukoni na pia cha kadiri kubwa zaidi, kikiwa na maneno na muziki ulio rahisi sana kusomwa. Mashairi na sauti tamu ni mtungo uliochangwa na Mashahidi kutoka pembe zile nne za dunia, kutia ndani Australia, Brazili, Kanada, Udeni, Uingereza, Jamhuri ya Muungano wa Ujeremani, Ufini, Ufaransa, Italia, Japani, na United States.

Tofauti na vitabu vya nyimbo vyote vilivyotangulia kuchapishwa na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, ile sehemu ya upatano wa sauti ya kikawaida imeachwa. Badala ya hiyo, mipigo yenye midundo mitamu zaidi na yenye kueleweka kwa urahisi zaidi ilitayarishwa. Alama za upigaji gitaa ziliongezwa pia.

Maneno yanayopendwa sana yalitungiwa sauti tamu mbili mpya kwa sababu ilikuja kujulikana kwamba zile sauti tamu zilizotumiwa hapo kwanza hazikuwa zimetungwa na Mashahidi. Jambo hilo lingaliweza kuwa lilitukiaje? Huenda mtungaji akaingiwa masikioni na sauti fulani ya wimbo usiojulikana sana. Anapoikumbuka baadaye, anaweza kuwazia kwamba yeye ndiye aliyeitunga.

Maendeleo Katika Mawazo Yaliyomo

Wakati ile nuru yenye kuangaza juu ya ukweli wa Mungu ilipozidi kung’aa kupatana na Mithali 4:18, ilionekana ilihitajiwa kubadili nyimbo zilizokuwa zimekuwa katika vitabu vya nyimbo vilivyotangulia. Ndivyo ilivyokuwa kuhusiana na ule wa sasa ambao ni Wimbo Nambari 215. Mwaka 1974 tulipata kufahamu kwamba safina ya Noa ilifananisha paradiso ya kiroho yetu, wala si Ufalme. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Kiingereza, mwaka 1974 ukurasa 634.) Kwa hiyo ule mstari uliokuwa katika kitabu cha nyimbo cha zamani, wenye kusema “Safina mutaikimbilia, Muje kwenye Ufalme hapa!” ulibadilishwa ukawa “Tenda sasa Jiweke wakifu; Uutumikie Ufalme,”

Kati ya marekebisho mengine ya kuchuja ambayo yamefanywa ili kuleta usahihi ni haya yanayofuata: Katika mfumo mpya wa mambo, hakutakuwa tena na “maovu” ya kuogopwa, badala ya hakuna kuogopa tena “mashetani,” kwa maana watu wa Mungu hawaogopi mashetani. (Wimbo 129) Kupatana na maneno ya Yesu kwenye Mathayo 6:22, Wimbo 26 unatuonya kwa upole kwamba ‘jicho letu liwe rahisi’ badala ya kusema ‘shabaha yetu iwe moja tu.’

Katika visa kadha sauti tamu fulani zilipewa fungu jipya la maneno yaliyoonekana kuwa ni yenye matokeo na mafaa zaidi. Wimbo 60, “Ufalme wa Mungu wa Miaka Elfu Moja,” unatumia sauti tamu ile ile ya Wimbo 86 katika kile kitabu cha nyimbo kilichotangulia. Maneno ya Wimbo 2, “Kumtii Mungu Kuliko Wanadamu,” ni mpanuko wa yale ya ule uliokuwa Wimbo 79. Ilionekana kwamba kichwa hicho kilistahili kupewa ukurasa kamili wala si nusu-ukurasa.

Hazina za Kiroho

Hicho kitabu cha nyimbo kilicho cha karibuni zaidi kimeitwa kwa kufaa Mwimbieni Yehova Sifa, kwa kutegemea Zaburi 96:1, 4. Nyimbo nyingi zimeelekezwa kwa Yehova na zinasifu sana sifa zake. Angalia chache tu zinazofanya hivyo: “Mungu Mkuu, Yehova!” (Huo ukiwa ni wimbo unaoorodhesha sifa au majina ya vyeo vya Yehova karibu 20); “Yehova, Rafiki Yetu Bora Zaidi”; “Yehova Anajali Kweli Kweli”; “Baraka ya Yehova Hutajirisha”; “Yehova, Mwandalizi wa Wokovu”; “Uumbaji Unafunua Utukufu wa Yehova”; na “Yehova, ‘Mungu wa Faraja Yote.’ “

Tunaambiwa ‘tufundishane na tuonyane kwa zaburi, sifa kwa Mungu na nyimbo za kiroho,’ na hakika kitabu cha nyimbo hicho kinafanya hivyo. (Wakolosai 3:16, NW) Unaweza kuona jambo hilo kutokana na vichwa kama hivi: “Iweni Imara, Bila Kuondoleka!”; “Endeleeni Kama Wanaume”; “Fanya Zaidi​—Kama Walivyofanya Wanadhiri”; “Haya Mbele, Enyi Wahudumu wa Ufalme!”; “Kutii Kishikamanifu Utaratibu wa Kitheokrasi”; “Kaeni Macho, Simameni Imara, Mwe Hodari.”

Ili kutusaidia tutii agizo hili la mtume Paulo, “Furahini Katika Bwana Sikuzote” (Wafilipi 4:4), tuna: “Wimbo wa Kushangilia”; “Furahia Tumaini la Ufalme!”; “Wenye Furaha Mchana Kutwa”; “Imba Wimbo wa Uchangamshi wa Ufalme”; “Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha”; na “Zile Furaha na Matunda ya Utumishi wa Ufalme.”

Baraka za Ufalme pia zimepewa nafasi katika kitabu cha nyimbo hicho kilicho cha karibuni zaidi: “Ufalme wa Mungu wa Miaka Elfu Moja”; “Ahadi ya Mungu ya Paradiso”; “Hatimaye​—Uzima Bila Mwisho!”; “Pamoja na Kristo Katika Paradiso.”

Vijana wetu hasa wamefurahia nyimbo mpya kama vile: “Vijana! Fuateni Mfano wa Imani Yao”; “Mahali pa Vijana Katika Mpango wa Mungu”; “Watoto​—Zawadi Bora za Kutoka kwa Mungu.” Wimbo unaoonyesha uthamini kwa kazi nzuri sana ya dada zetu ni ule unaosema “Wanawake Ni Jeshi Kubwa.”

Tunaweza kuonyeshaje uthamini kwa nyimbo hizo zilizo nzuri sana? Kwa sehemu, ni kwa kuchukua kwa uzito pendeleo na wajibu wetu wa kuziimba zikiwa sehemu ya ibada yetu rasmi kwenye Majumba ya Ufalme yetu. Inatupasa tujaribu kufika mikutanoni kabla ya wakati, kisha tubaki mpaka mwisho, ili tushiriki kuziimba nyimbo hizo. Acheni tuimbe kwa moyo wetu wote, mdomo ukiwa umefunguka wazi kabisa, na tukiwa na uchangamfu na shauku. Tunaweza pia kuonyesha uthamini kwa nyimbo hizo kwa kuzitumia wakati tunapokuwa na vikusanyiko vya starehe. Tunaweza kujipatia kanda za muziki uliotolewa katika hicho kitabu cha nyimbo ili tuzifungulie wakati tunapotaka kufurahia muziki uliorekodiwa. Hivyo tunaweza kujengwa kiroho kila wakati tunapofurahia muziki huo wa kupendeza.

Jambo lililo la maana zaidi ya yote ni kwamba tuonyeshe uthamini kwa nyimbo hizo zilizo za kupendeza kwa kuishi kila siku kulingana na mawazo mazuri sana yaliyomo, kwa habari ya mwenendo wetu wa kila siku pia wajibu wetu mbalimbali wa kihuduma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki