Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 12/1 uku. 21
  • Baraka ya Mungu Yaonekana Wazi Katika Venezuela

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraka ya Mungu Yaonekana Wazi Katika Venezuela
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Shangwe ya Yubile Kati ya Watu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Katika Maamuzi Yangu Yote, Nilimtanguliza Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 12/1 uku. 21

Ripoti ya Watangazaji Ufalme

Baraka ya Mungu Yaonekana Wazi Katika Venezuela

UTENDAJI wa Mashahidi wa Yehova katika Venezuela umebarikiwa kweli kweli. (Zaburi 3:8) Wakati wa 1985 hesabu ya wahubiri iliongezeka kwa asilimia 16 juu ya mwaka uliotangulia na katika Febuari 1986 ikafikia kilele cha wakati wote cha watangazaji wa habari njema 31,247. Hesabu ya mapainia wa kawaida iliruka ikawa 2,291 katika Febuari, hicho kikiwa ndicho kilele cha mfululizo wa 38! Jumla ya mafunzo ya Biblia 50,659 yanaongozwa kwa watu wanaopendezwa. Wengine wa watu hao mmoja mmoja wameukuta ukweli chini ya hali zisizo za kawaida.

◻ Kijana mwanamume aliyeoa alikuwa na sifa mbaya sana ya kuwa mtu wa kufuata-fuata wanawake. Mambo hayakuwa yakimwendea vizuri. Yeye alihisi akiwa na uhakika wa kwamba mke wake alikuwa ameenda kwa mchawi na kuagiza laana iwekwe juu yake kwa sababu ya kufanya ngono nje ya ndoa. Kwa hiyo mwanamume huyo akatafuta mchawi apinge laana ile naye akaelekezwa kwa mwanamke fulani. Ingawa hivyo mwanamke huyo alikuwa amejifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova na akawa ameacha zoea lake la uchawi. Mwanamke huyo alimwambia kwamba yeye hangeweza kumsaidia, lakini angempa anwani ya ambako angeweza kwenda akapate msaada. Ilikuwa anwani ya Jumba la Ufalme. Mwanamume huyo alifika kule​—akiwa na nywele ndefu, bila kunyoa ndevu, akiwa amevalia vibaya. Yeye alifurahia sana mkutano hata akarudi mwisho-juma huo, pamoja na watoto wake watatu wadogo. Safari hii nywele zake zilikuwa zimekatwa, na alikuwa amevalia vizuri na akiwa amenyoa ndevu zake. Leo, yeye ni mhubiri wa habari njema. Je! mke alifurahi kwamba yeye alikuwa ameacha kufuata-fuata wanawake wengine? Hapana, badala ya hivyo yeye akawa mwenye kupinga sana! Lakini mabadiliko ambayo mwanamume huyo alifanya katika maisha yake yamewashangaza sana watu wengine wengi ambao aliwajua, yakawafungulia wao pia njia ya kuusikia ujumbe wa ukweli.

◻ Katika mji mmoja karibu na mpaka wa Kolombia, padri wa mahali hapo alianzisha kampeni ya kupinga Mashahidi. Aliliweka jina “Mashahidi wa Yehova” katika herufi kubwa nyekundu juu ya ubao wa habari wa kanisa lake na chini yalo akaweka porojo fulani mbaya dhidi yao. Mshiriki mmoja wa kanisa aliliona jina hilo likiwa limeonyeshwa wazi-wazi na, bila kusoma habari zilizofuata, akakata shauri kwamba kanisa liliwakubali Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo mwanamke huyo alienda kwenye mkutano mmoja wa Mashahidi na akapenda mambo aliyoona na kusikia. “Kwa kweli,” inasema ripoti ile, “kampeni ile ya padri imeamsha kupendezwa kwingi badala ya kufanya kinyume.” Sasa wengi wana nia ya kujifunza na hata wanawafikia Mashahidi barabarani na kuwauliza ni wakati gani watakapotembelea tena.

◻ Hotuba fupi ya maziko karibu na kaburi la dada mpya-mpya aliyebatizwa ndiyo iliyowezesha jamaa nyingine katika Venezuela ione Meja wa jeshi na jamaa yake, watu wa ukoo wa mfu, walisikiliza kwa makini yale mahubiri ya Kimaandiko na baada ya hapo wakamwalika msemaji nyumbani kwao ili wakayachunguze kwa urefu zaidi maandiko yale ya Biblia yaliyotajwa. Matokeo yakawa nini? Acheni meja yule ajibu:

“Sisi sote wawili, mke wangu na mimi tukawa wadadisi na kutaka kuichunguza Biblia. Kwanza nililotaka mimi ni kuonyesha kwamba nilikuwa sawa kwa kudai naifuata dini ya Katoliki. Ijapokuwa hivyo, kila wakati nilipokanusha jambo fulani, yule ndugu mwenye kuongoza funzo alikuwa akirudi akiwa na maoni ya kiakili ya Biblia. Kwa unyenyekevu, nilikuja kutambua kwamba ukweli una Mashahidi wa Yehova. Leo, mke wangu na mimi ni Mashahidi wa Yehova, na watoto wangu wanajifunza Biblia. Mimi namshukuru Mungu wa kweli mmoja tu, Yehova, ambaye nafurahia kumtumikia nikiwa askari, si kwa silaha za kimwili za vita bali kwa zile ambazo roho ya Mungu inatoa, kulingana na 2 Wakorintho 10:4, 5.”

Ndiyo, Yehova amewabariki sana watumishi wake katika Venezuela. Hudhurio kubwa ajabu la Ukumbusho likiwa ni mara nne za hesabu ya wahubiri, kuna uwezekano mkubwa wa maongezeko zaidi katika miaka itakayokuja.

[Chati katika ukurasa wa 21]

Vilele fulani kwa Venuzuela vikitegemea ripoti za Febuari 1986:

Wahubiri 31,247

Mapainia 2,291

Mafunzo ya Biblia 50,659

“Baraka yako iko juu ya watu wako.”​—Zaburi 3:8, NW

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki