Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 1/15 kur. 7-9
  • Mashahidi wa Yehova Katika Umisionari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Katika Umisionari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utofautiano Katika Maoni
  • Kujaza Mahitaji ya Kiroho ya Watu
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kufanya Wanafunzi wa Kweli Leo
    Amkeni!—1994
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 1/15 kur. 7-9

Mashahidi wa Yehova Katika Umisionari

WAMISIONARI wa Mashahidi wa Yehova katika Esia na kwingineko wanaulizwa mara nyingi hivi: “Mbona ninyi hamuwi na madarasa ya kufunza watu Kiingereza kama wamisionari wengine?” “Je! ninyi mna shule ambako mimi ninaweza kupeleka watoto wangu au hospitali za wagonjwa?” Bila shaka, jibu ni la. Lakini ni kwa sababu gani? Kwa kweli, lengo la Mashahidi ni nini hasa? Nao wamefanya nini kwa ajili ya watu kwa nchi hizo?

Utofautiano Katika Maoni

Haiwezi kukanwa kwamba wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo wamefanya waongofu wengi kwa kutumia huduma za kusaidia watu. Lakini kwa sababu kazi hizo zinaelekezwa hasa ili kutosheleza mahitaji ya kimwili ya watu badala ya mahitaji yao ya kiroho, wamisionari hao hawakupata mafanikio katika kufanya wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo. (Mathayo 7:22, 23; 28:19, 20) Lililo la maana zaidi ni kwamba, wao hawakuweza kueleza watu suluhisho lo lote la kudumu kwa matatizo yao makubwa ya kijamii ambayo wanajaribu kushinda.

Mashahidi wa Yehova, kwa upande ule mwingine, wanashughulikia tume iliyo ya maana zaidi ya kuzihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Hiyo si kwa sababu wao hawana habari au hawajali taabu za kibinadamu na matendo ya udhalimu wanayoyaona. Bali, ni kwa sababu wao wanatambua kwamba dawa moja tu kwa matatizo hayo mazito inategemea, si mikono ya kibinadamu, bali Ufalme wa Mungu.—Zaburi 146:3-10.

Hilo ndilo jambo ambalo Yesu na wafuasi wake walihubiri katika karne ya kwanza. “Ni lazima mimi nizitangaze habari njema za ufalme wa Mungu,” Yesu akasema, “kwa sababu kwa ajili ya hilo mimi nilitumwa niende.” (Luka 4:43, NW) Yesu alielekeza kwenye Ufalme wa Mungu na akahubiri juu yao kuwa ndiyo tu dawa kamili, kwa sababu alijua kwamba matatizo ya ulimwengu ni makubwa mno mwanadamu kuyatatua akiwa peke yake. Ingawa Yesu alifanya maponyo mengi ya kimuujiza, yeye alihimiza wafuasi wake ‘waendelee, basi, kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wa Mungu, na hivi vitu vingine vyote vitaongezwa kwenu ninyi.’—Mathayo 6:33, NW.

Baadaye, wakati Yesu alipotuma wafuasi wake kwenda nje, kwanza aliwaambia hivi: “Katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.” Halafu akaongeza hivi: “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo.” (Mathayo 10:7, 8) Jambo hilo linawawekea wafuasi wa kisasa wa Yesu Kristo mfano wa jambo linalopasa kutangulizwa kwanza. Wao, pia, ni lazima wawe wakizihubiri habari njema za Ufalme zikiwa ndilo lengo lao la kwanza, linalopita na kuzidi kufanya kazi za kuwafadhili wanadamu tu. Hivyo ndivyo wamisionari wa Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kufanya.

Kujaza Mahitaji ya Kiroho ya Watu

Wakiwa kama kikundi cha Wakristo, Mashahidi wa Yehova wanajitia katika programu kubwa sana ya kujitolea ya kuandalia watu elimu ya Biblia. Kwa kuwa wao ni wahubiri wa habari njema, wanapendezwa na kusaidia wengine wanufaike kutokana na hekima na mashauri ya Biblia, sasa na hata katika wakati ujao. (Zaburi 68:11) Kwa sababu gani wanafanya hivyo?

Mashahidi wanatambua kwamba wakati watu wanaposaidiwa kufahamu na kufuata mashauri ya Biblia, wanakuwa katika hali bora ya kuweza kushughulika na matatizo na mikazo ya maisha. Kwa upande mmoja, watu hao wanapata imara ya kiadili inayohitajiwa ili washinde tabia zenye kuwatumikisha na kuwadhuru kimwili kama vile kuvuta sigareti kunywa kupindukia, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, hali mbaya ya kutotunza usafi wa kiafya, kucheza kamari, na kufanya ngono za ovyo-ovyo. Kwa upande ule mwingine, ukweli wa Biblia unawasaidia wabadili akili zao, kufanya hivyo kukiwaletea kusudi katika maisha na tumaini la kikweli kwa ajili ya wakati ujao.

Hivyo, kwa kuandalia watu elimu ya namna iliyo ya juu zaidi—ile inayotokana na Neno la Mungu, Biblia—Mashahidi wa Yehova wanafanya mchango wa moja kwa moja kuelekea kuinua afya ya kiadili na kimwili ya jamii wanamoishi na kuhubiri. Mara nyingi jambo hilo linaonwa na wengine ambao wanawatazama wakiwa na kusudi zuri. Kwa mfano, Dakt. Bryan Wilson wa Chuo Kikuu cha Oxford, aliyechunguza utendaji wa Mashahidi wa Yehova katika Afrika, alisema hivi katika barua moja aliyoandikia gazeti The Times la London:

“Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi kwa bidii na mara nyingi ni wenye kudhamiria mambo na kuthubutu kutenda yaliyo magumu zaidi kuliko mtu wa wastani miongoni mwa raia wenzao. Wanahimizwa na viongozi wao walipe kodi zao kwa wakati unaofaa, wajiepushe na jeuri, na kuepuka kuudhi watu. Wao ni wenye utaratibu, wanyofu na wenye akili timamu. Sifa hizo bora zilikuwa zenye umaana mkubwa katika usitawi wa kiuchumi na kijamii wa watu wa nchi za Magharibi, na hakungekuwa ni kutia chumvi kusema kwamba Mashahidi wa Yehova wamo miongoni mwa watu walio wanyofu zaidi na wenye bidii kati ya raia wa nchi za Kiafrika.”

Kwa maneno yanayofanana na hayo, mtazamaji mwingine katika Amerika ya Kusini alisema hivi katika makala ya mhariri wa gazeti moja:

“Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi kwa bidii, ni wanyofu, ni watu wenye kumwogopa Mungu. Wao ni wenye kuhifadhi mambo ya kale na wanapenda mapokeo na dini yao inategemea mafundisho ya Biblia.”

Kwa hiyo, ingawa Mashahidi wa Yehova hawatii mkazo wao juu ya ile ambayo kwa kawaida inaitwa injili ya kusaidia watu kimwili, wao wanachangia kwa bidii masilahi ya jamii kwa kuwasaidia wapatanishe maisha zao na viwango vya juu vya Biblia. (Warumi 12:1, 2) Na jambo lililo la maana zaidi ni kwamba, wao wanasaidia pia watu kila mahali watazame kwenye mfumo mpya wenye kufanywa na Mungu, unaokuja karibuni, ng’ambo ya udhalimu na ukosefu mwingi wa usawa wa huu mfumo wa mambo unaozorota haraka.—Ufunuo 21:5.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

Masuluhisho kwa Matatizo Makubwa ya Kijamii Yataletwa na Ufalme wa Mungu

Soma katika Biblia yako mwenyewe maandiko yanayofuata ufarijiwe kuona jinsi Mungu anavyoahidi kuondolea mbali magumu ya leo na matatizo makubwa ya kijamii katika pande zinazofuata:

Afya Isaya 33:24; 35:5, 6 Ufunuo 21:4

Elimu Isaya 11:9; Habakuki 2:14

Kazi ya Kuajiriwa Isaya 65:21-23

Chakula Zaburi 67:6; 72:16; Isaya 25:6

Haki Isaya 11:3-5; 32:1, 2

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki