Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 6/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maongezi Kati ya Kakatoliki na Wafuasi wa Marx
  • Je! Ni Ukombozi wa Kweli?’
  • Ubatizo wa Watoto Wakataliwa
  • ‘Viumbe Vyote Vinaugua’—Kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ubatizo wa Vitoto Vichanganga—Sababu Inayofanya Mapadri Wengine Wakatae!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ukombozi—Unatamanika Kama Nini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ubatizo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 6/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Maongezi Kati ya Kakatoliki na Wafuasi wa Marx

Katika Budapest, Hungari, katika Oktoba 1986, wanachuo wa kidini Wakatoliki na wanafalsafa 15 walikutana pamoja na wafuasi 15 wa Marx wenye akili sana. Mkutano huo ulitayarishwa na Afisi ya Wendeshaji kwa Wasioamini ya Vatikani na Chuo cha Sayansi cha Hungari ili kuzungumzia mabadiliko ya ubora wa maadili.

Miongoni mwa Wakatoliki waliokuwapo ni Poupard Kardinali Mfaransa, aliye mwenyekiti wa Afisi ya Wendeshaji kwa Wasioamini, na Koenig Kardinali Mwaustria, aliye mstadi anayeshughulikia mahusiano ya Kanisa Katoliki na mataifa ya kikomunisti. Wafuasi wa Marx walikuwa ni pamoja na wakuu wa Taasisi ya Falsafa ya Hungari na wa Taasisi ya Sayansi ya Kutokuamini Kuwako kwa Mungu ya Urusi.

Gazeti la kila siku la Kifaransa linaloitwa Le Monde liliripoti hivi: “Wafuasi wenye akili sana wa Marx wanatambua kwamba wanaelekewa na tatizo kubwa la ubora wa maadili, ambalo wanapima uzito walo kwa hesabu ya visa vya watu kujiua wenyewe, matumizi ya dawa za kulevya, na unywaji wa vileo. Kulingana na ujumbe wa Kikatoliki, katika kutafuta kwao utatuzi fulani wao [wafuasi wa Marx] wanategemea ushirikiano wa makanisa ya Kikristo. Upande wa [Katoliki ya] Roma, kusudi lenye malengo mawili lilikuwa kukadiria vizuri zaidi ni mahali gani panapofaa wanadamu na maadili katika jamii ya wafuasi wa Marx na ‘kuuchunguza msingi wa kiadili wa kukaa kwa mapatano mazuri kati ya Wakristo katika nchi za Mashariki [za ukomunisti] na wafuasi wa Marx.’”

Utatuzi wa kweli kwa matatizo ya kiadili ya siku hizi hautapatikana kwa kufanya mashauriano kati ya vikundi vyenye mawazo yanayohitilafiana. Bali, utapatikana wakati Ufalme wa Yehova mikononi mwa Mwanaye, Yesu, utakapopindua mfumo wa sasa wa mambo, na mahali pao ujenge ulimwengu mpya chini ya Ufalme huo wa kimbingu.​—Danieli 2:44; Ufunuo 21:4, 5.

Je! Ni Ukombozi wa Kweli?’

Theolojia ya ukombozi​—harakati inayokubali jeuri iwe kama njia ya ‘kukomboa walio maskini na wenye kuonewa,’ hasa katika nchi zinazositawi, inazidi kupendwa na watu wengi. Hicho kilikuwa ndicho kichwa cha mazungumzo kwenye Kusanyiko la Pili la Kimataifa la Shirika la Kiekumeni la Wanatheolojia wa Nchi Zinazositawi lililofanywa katika Oaxtepec, Meksiko, Desemba 8-13, 1986. Ni kwa sababu gani wanachuo hao wa kidini wamepiga moyo konde zaidi kutimiza miradi yao ya kuleta badiliko la kijamii zaidi ya wakati mwinginewo wote uliopita?

Ingawa katika 1985 Vatikani ilitoa agizo lenye kulaumu theolojia ya kutafuta ukombozi, agizo hilo lenye kuitwa Instruction on Christian Freedom and Liberation lililopelekwa nje katika 1986 lilisema kwamba ni “halali kabisa kwamba wale wanaoonewa na matajiri au wanasiasa wenye mamlaka wachukue hatua.” Sasa inakubaliwa kutumia “pambano lenye silaha” kama “hatua ya mwisho” ikiwa hakuna njia nyingine.

Hata hivyo, wakati Yesu Kristo alipokuwa hapa duniani, je! yeye alijihusisha katika harakati za kijamii za ulimwengu? Hapana, bali, wakati mtume Petro alipogeukia utumizi wa “upanga” ili amlinde Mwana wa Mungu, Yesu alimkemea kwa kusema: “Rudisha upanga wako; maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.” (Mathayo 26:52) Biblia inaahidi kwamba ukombozi wa kweli utakuja kupitia hatua ya kimungu ya kutatua mambo wakati Mungu atakapoondolea ulimwengu si umaskini, ugomvi wa kimataifa, ubaguzi wa rangi, na uonevu tu bali pia machozi, maumivu, huzuni, na kifo. (Ufunuo 21:4) Kwa uhakika, huo utakuwa ukombozi wa kweli!

Ubatizo wa Watoto Wakataliwa

Mhudumu mmoja Mprotestanti wa Ujeremani kutoka Frankfurt alijulisha wakuu wa kanisa hivi majuzi kwamba tangu hapo yeye angekataa “kubatiza watoto wasio na ufahamu wa parokia yake.” Akieleza kwa nini ubatizo wake mwenyewe alipokuwa kitoto kichanga haukustahili kuitwa jina ubatizo, Klaus Hoffmann mwenye umri wa miaka 58 alisema: “Ubatizo huo haukutimiza takwa lile linalopasa kutimizwa kabla ya ubatizo wa Kibiblia, yaani imani, wala haukuwa na ishara inayofaa, yaani, uzamisho.” Kuunga mkono maoni yake, yeye alichagua kubatizwa tena na hivyo “akapata ubatizo wa Kibiblia wa uzamisho,” linaripoti gazeti la Kijeremani Frankfurter Allgemeine Zeitung.

Kwanza, maafisa wa kanisa walimwachisha Hoffmann kazi zake zote kwa muda, lakini hukumu hiyo ikabadilishwa kuwa “likizo la miezi mitatu kwa makusudi ya uchunguzi.” Matokeo yalikuwa nini? Gazeti hilo linaripoti kwamba uchunguzi ambao yeye alizidi kufanya juu ya jambo hilo ulithibitisha tu “kwamba ndani ya Biblia hakuna jambo linalounga mkono ubatizo wa vitoto vichanga. Pia, maandishi ya Wakristo wa kwanza hayasemi lo lote juu ya kuanzishwa kwa tendo hilo mpaka karne ya tatu.”

Haishangazi kwamba wenye mamlaka ya kidini wanataja kwamba msingi wa tendo hilo ni mapokeo. Hata hivyo, kujapokuwa na mambo hayo ya hakika, ubatizo wa vitoto vichanga unaendelea kuzoewa katika sehemu zilizo nyingi za Jumuiya ya Wakristo. Je! ubatizo huo unakuwa sawa kwa sababu unaungwa mkono na viongozi wa kidini? Yesu aliagiza wafuasi wake wabatize, si watoto wachanga, bali waamini waliofunzwa kushika amri zake zote. Yeye mwenyewe hakuwa mtoto mchanga bali “alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini” alipozamishwa katika maji ya Mto Yordani.​—Luka 3:21-23; Mathayo 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki