Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 9/15 kur. 26-30
  • Je! Historia ya Kidini Ina Manufaa Yo Yote Kwako Wewe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Historia ya Kidini Ina Manufaa Yo Yote Kwako Wewe?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yaliyofunuliwa na Mauzo ya Rehema za Dhambi
  • Yaliyofunuliwa na Hoja 95 za Lutheri
  • Jinsi Kuacha Imani ya Kweli Kulivyoanza
  • Yale Mageuzo ya Kanisa—Hakuna Mrudisho wa Hali ya Kwanza
  • Somo Kutokana na Historia ya Kidini ya Kisasa
  • Je! Historia ya Kidini Ina Manufaa Yo Yote?
  • Martin Luther na Mageuzi Aliyoleta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Yale Mapinduzi Makubwa ya Kidini
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Sehemu 16: Karne ya 9-16 W.K—Dini Iliyohitaji Sana Marekebisho
    Amkeni!—1990
  • Wessel Gansfort—“Mrekebishaji Aliyetangulia Marekebisho”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 9/15 kur. 26-30

Je! Historia ya Kidini Ina Manufaa Yo Yote Kwako Wewe?

“SHULENI, mimi sikupenda historia hata kidogo,” Barbara anakiri waziwazi. Lakini sasa mwanamke huyo anathamini maarifa juu ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, kwa mfano. Pamoja na Biblia yake, habari hiyo inamsaidia kueleza kwa matokeo mazuri zaidi ni kwa sababu gani ulimwengu tangu 1914 umekuwa bila amani. (Ufunuo 6:4) Vivyo hivyo, historia ya kidini inaweza kutusaidia tufahamu ulimwengu tunamoishi.

Kwa sababu gani mataifa, jumuiya za watu, na hata jamaa zimegawanywa-gawanywa kati ya imani za Kikatoliki na Kiprotestanti tangu karne ya 16? “Katika mpambano wa kutetea fundisho safi la Injili, ambao ulianzishwa wakati huo sana-sana na walimu na kanisa Wajeremani, Wasuisi na Wafaransa, Roma haikuwa na nia ya kukubali kushindwa,” anaeleza mwanahistoria Friedrich Oehninger. Jambo hilo liliongoza kwenye kuundwa kwa makanisa ya kimadhehebu.

Lakini je! “fundisho safi la Injili” lilithibitishwa tena kweli kweli? Mtazamo wa historia ya kidini utatusaidia tugundue lililotukia hasa.

Yaliyofunuliwa na Mauzo ya Rehema za Dhambi

“Yale Mageuzo ya Kanisa yalianza na pambano la Lutheri dhidi ya matumizi mabaya katika kuuza rehema za dhambi, jambo ambalo lilionekana kana kwamba lilikuwa na mafaa kwa kanisa tu,” anaeleza mwanahistoria Gottfried Fitzer. “Lakini kwa kweli lilifunua kwamba mambo ya kikanisa yalikuwa yamefungamana kwa ukaribu pamoja na pesa, uchumi na siasa.” Acheni tutazame kwa ukaribu zaidi.

Mwana-Mfalme Albert wa Brandenburg alijipatia vyeo kadhaa vya umashuhuri katika kanisa. Alipaswa kuilipa Vatikani kiasi kinacholingana na dola robo moja ya milioni zikilipiwa kwa mkopo wa benki. Papa alimweka rasmi Askofu Mkuu Albert awe mwanatume wake wa kuuzia rehema za dhambi kwa ajili ya Ujeremani ya kati na akamruhusu atumie nusu ya faida zilizopatikana kulipia madeni yake.

Wahubiri wa Albert wa rehema za dhambi walifanya shughuli yao kati ya watu kwa matokeo mazuri, wakiwahakikishia “ondoleo kamili la dhambi zote” na ufungulio wa mara hiyo kutoka purgatori. Ikisemwa kama mambo yalivyo hasa, kanisa lilitolea watu ondoleo la adhabu za kanisa tu, lakini watu waliamini kwamba barua zile za rehema za dhambi zingewaweka huru na dhambi yote. Martin Lutheri alichukizwa sana na, katika 1517, akachapisha hoja zake 95 zinazojulikana sana, “kwa sababu ya kupenda ukweli,” kama yeye alivyoandika katika utangulizi.a

Hoja hizo ziliandikwa katika Kilatini kwa sababu alilokuwa akitafuta Lutheri ni mazungumzo miongoni mwa wanachuo, naye alikuwa na haki hiyo maana alikuwa profesa. Lakini wao walitokeza “msisimuko wa kugutusha,” kulingana na Friedrich Oehninger. “Katika muda wa siku 14 hizo [tafsiri za Kijeremani zilizopigwa chapa] zilijulikana katika sehemu zote za Ujeremani, na katika muda wa majuma 4 zikajulikana katika Jumuiya ya Wakristo yote. Watu fulani walifurahi sana kwamba hatimaye mwanamume mmoja alikuwa amechukua msimamo dhidi ya uonevu wa Kiroma; kwa wengine, Lutheri akawa kitu cha kuchukiwa.” Tokeo la hoja zake zilimshangaza Lutheri mwenyewe. Zilifunua nini?

Yaliyofunuliwa na Hoja 95 za Lutheri

Kulingana na hoja yake ya kwanza, “maisha yote ya waamini yanapasa kuwa tubio.” Mtenda dhambi angeweza kupata amani pamoja na Mungu si kupitia barua za kuomba rehema ya dhambi bali kupitia toba ya kweli na mwenendo wa Kikristo. Moja ya hoja hizo za mwisho ilisema hivi: “Basi, waondoleeni mbali manabii hawa wote wanaohubiria Wakristo hivi: ‘Amani, amani,’ na bado hakuna amani.” —Hoja ya 92.

Lazima injili iwe ndiyo “hazina ya kweli kweli” iliyo “ya juu zaidi,” si mapokeo, akaandika Lutheri. (Hoja za 55, 62, 65) Ni kweli. Yesu alikiweka kigezo kwa kufunza akitumia Maandiko yaliyoongozwa na Mungu akisema hivi juu ya Neno la Mungu: “Neno lako ndiyo kweli.” (Yohana 17:17; Luka 24:44) Kwa kukengeuka kutoka kigezo hicho, viongozi wa kidini walikataa Biblia isiwe mamlaka iliyo juu zaidi na wakanaswa katika mtego wa mafundisho ya kibinadamu. Lutheri aliwasuta, akisema: “Mafundisho ya wanadamu yanahubiriwa na wale wanaosema kwamba nafsi inaruka hewani (kutoka purgatori) mara tu pesa zikiisha kutumbukizwa sandukuni.”—Hoja ya 27.

Lutheri alionya kwamba “faida na pupa vinaongezeka” kupitia kuhubiri kwa jinsi hiyo. (Hoja ya 28) Historia ya kidini inathibitisha kwamba viongozi wa kidini walipuuza maonyo ya Kimaandiko na wakawa wafungwa wa kupenda pesa. (Waebrania 13:5) Kitabu kimoja cha historia ya Kikatoliki kinakiri hivi: “Sababu ya msingi ya mchakao wa kipindi hicho katika kanisa ilikuwa mwongozo wa mapato wa baraza la wakuu wa kanisa, lililokuwa linaingiwa kweli kweli na mawaa ya usimoni.”

Wakati Lutheri alipoinua sauti yake dhidi ya “yale yaliyoitwa ati mapokeo ya kanisa ‘yaliyotakaswa’ ““akalaumu vikali mzoroto wa kanisa wa kuingia katika mambo ya pesa na kutafuta mamlaka,” kama vile mwanahistoria mmoja Mprotestanti alivyoeleza jambo lile, yeye alikigusa kiini cha tatizo lenyewe; kuacha kwa ujumla mafundisho ya Kikristo ya kwanza-kwanza.

Jinsi Kuacha Imani ya Kweli Kulivyoanza

Hoja ya 11 ilieleza fundisho moja lisilo la Kimaandiko kuwa ni “gugu ambalo kwa wazi lilipandwa wakati maaskofu walipokuwa wamelala.” Jambo hilo linatukumbusha juu ya mfano wa Yesu wa ngano na magugu, ambamo yeye alitoa unabii wa kupandwa kwa Wakristo wa mwigizo tu. (Mathayo 13:36-43) Baada ya kifo cha mitume, Wakristo hao wasio wa kweli, pamoja na walimu waasi-imani, walichanganya mafundisho safi ya Biblia pamoja na falsafa ya Kigiriki na wakaanzisha mafundisho yasiyo ya Kimaandiko kama vile kutokufa kwa nafsi, moto wa mateso na Utatu.b—Matendo 20:29, 30.

Kwa mfano, Wakristo wa kwanza-kwanza hawakuwa na sanaa za picha, na walioitwa Mababa wa Kanisa waliuona kuwa “ukengeufu na kosa” kuheshimu sana mfano. Hata hivyo, kufikia mwisho wa karne ya nne makanisa yalikuwa tayari yamejawa na mifano ya maumbo ya Yesu, Mariamu, mitume, malaika, na manabii. Kulingana na Epifanio wa Salamis, walioonyeshwa na mifano walipokea heshima nyingi isiyowapasa wakati watu walipoinama mbele yao. Pole kwa pole, lile onyo “jilindeni nafsi zenu na sanamu” likaanza kupuuzwa.​—1 Yohana 5:21; linganisha Matendo 10:25, 26.

Wakristo wa kujidai walikataa amri ya Yesu walipoanza ‘kupiga ubwana’ juu ya ndugu zao kwa kupanga kitengenezo madaraja ya viongozi wa kidini. (Mathayo 20:25-27; 23:8-11) Baadaye, maaskofu wa Roma walidai wapewe cheo kikubwa kuliko wengine. Ingawa “mchakao wa maisha ya kikanisa chini ya utawala wa upapa uliofuatisha maongozi ya kilimwengu uliendelea bila kuzuiwa,” kanisa lilifanya majaribio ya “kujifanyia mageuzo lakini lisiweze kufanya hivyo,” anaeleza mwanahistoria Oehninger.

Karne ya 16 iliona mabadiliko zaidi. “Hali ya wakati huo ilimpendelea yeye [Lutheri],” anasema Oehninger, akiongeza kwamba “wapinzani walimshambulia, wakitisha kumwua kama mzushi wa kidini, lakini kwa kufanya hivyo walimsukuma tu afanye uchunguzi mwingi zaidi na mpya zaidi juu ya msingi wa Maandiko Matakatifu, mpaka mfumo mzima wa Kiroma, ukiwa ni mfanyizo wa kibinadamu tu, ukaanza kubomoka-bomoka mbele ya macho yake.” Lakini je! makanisa yale yaliyokuwa yametokea karibuni yalikuwa huru kikweli na “desturi mbaya sana na mafundisho yasiyo ya kweli,” kama yalivyodai?

Yale Mageuzo ya Kanisa—Hakuna Mrudisho wa Hali ya Kwanza

Ule mwito wa kufanya mageuzo ya kanisa katika karne ya 16 haukuongoza kwenye kurudishwa kwa kanisa “la ulimwengu mzima” wala mafundisho ya kwanza-kwanza ya Kikristo bali uligawanya-gawanya Jumuiya ya Wakristo yenye uasi-imani katika sehemu-sehemu za uasi-imani zilizo tengana tena. Maaskofu wa leo, kutia na warithi wa Lutheri, wangali wanaonekana ni kama “wamelala” kama vile hoja ya 11 ilivyotaja.

Waprotestanti walilikataa fundisho la rehema za dhambi lakini wakachagua kufuata mafundisho mengine mengi yasiyo ya kweli. “Kutokana na falsafa ya Kigiriki, theologia ya Kikristo ilikubali pia fundisho la kutokufa kwa nafsi,” kinasema kichapo Evangelischer Erwachsenenkatechismus (Katekisimu ya Kiprotestanti kwa watu wazima). ‘Iliunganishwa na ushuhuda wa kibiblia juu ya ufufuo wa mwili.’

Kwa kutumia mafundisho ya wanadamu na kuchanganya huduma yao na mambo ya kilimwengu, kutia na siasa, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo wanadhoofisha mamlaka ya Biblia kama katika siku za Lutheri. Basi, “namna ya bidii ya kujitolea Mungu” waliyo nayo kwa juu juu tu inathibitika kuwa bila nguvu na haiwezi kubadili mpunguo wa hudhurio kwenye ibada za kanisa, ubaridi wa washiriki wa kanisa, kuingizwa kwa siasa katika mazungumzo ya kanisa, na ongezeko la wenye kuacha ushiriki.—2 Timotheo 3:5, NW.

Kama vile habari zinazohusu wakati uliopita wa mgonjwa inavyoweza kusaidia daktari achunguze ugonjwa wa mtu, ndivyo historia ya kidini inavyoweza kutusaidia sisi tufahamu sababu inayofanya Jumuiya ya Wakristo ibaki na ugonjwa wa kufisha katika siku zetu. Basi, je! hakuna tumaini la kupata Ukristo safi? Kunalo! Mfano wa Yesu ulionyesha kwamba wafuasi wake wenye mfano wa ngano, wale “wana wa ufalme” walio wa kweli, wangetambuliwa kwenye mavuno katika “wakati wa mwisho.” (Mathayo 13:38, 39; Danieli 12:4) Jambo hilo lingetukiaje?

Somo Kutokana na Historia ya Kidini ya Kisasa

Katika 1891 kikundi cha Wanafunzi wa Biblia kilitembelea yaliyokuwa makao ya Lutheri katika Wittenberg. “Jambo hilo lilikumbusha waziwazi sana nyakati zile za kivumbi,” msafiri mmoja akaripoti. Miongoni mwa wale walioingia katika “chumba cha uchunguzi na kuketi katika kiti cha zamani chake” Lutheri alikuwa Charles Taze Russell. Ripoti hiyo inaendelea kusema: “[Sisi] tuna sababu kubwa ya kufurahi sana leo kwamba, ingawa waanzishi wa yale mageuzo makubwa ya kanisa hawakuimaliza kazi na walisonga mbele wakipanga kitengenezo mifumo mingine ya makosa, hata hivyo, chini ya uongozi wa kimungu, kusafishwa kwa patakatifu kulisonga hatua kwa hatua mpaka ukamilisho, na vile vyombo vya kidhahabu vya ukweli wa kimungu vinaendelea sasa kurudishwa katika utaratibu.” Jambo ambalo Lutheri alishindwa kufikia, mgeni huyu alisaidia kulitimiza.

Lilikuwa tukio kubwa kihistoria wakati Russell—akiwa pamoja na wanaume na wanawake wengine wenye kupenda ukweli—alipoanza funzo la Biblia la kujitegemea katika miaka ya 1870. Hata hivyo, kati ya 1870 na 1875 wao walikuwa “wakipata sehemu za nje-nje tu za Mpango wa Ramani ya Mungu na kuondoa mambo mengi yenye makosa waliyoyapenda sana, ukiwa haujafika kwa ukamili wakati wa utambuzi wa wazi wa ufahamu mzima,” kama Russell alivyoandika baadaye. Lakini miaka iliyofuata ikawa hatua-hatua za mrudisho wa viwango vya mwanzoni vya Kikristo.

Kupitia gazeti Zion’s Watch Tower, Wanafunzi wa Biblia walitangaza kwamba jina la Aliye Juu Zaidi ni Yehova, kwamba nafsi inakufa (1881), kwamba Utatu si wa Kimaandiko (1882), na kwamba hell ya Biblia ndilo kaburi (1883). Sawa na vile mafundisho yasiyo ya kweli yalivyoingia pole kwa pole, ndivyo sasa nuru ya ukweli ilivyozidi kunurika na kunurika pole kwa pole. (Mithali 4:18, 19) Kutoka mwanzo, Wakristo hao waliufahamu ukweli wa msingi kuhusu Yesu, aliyetoa uhai wake uwe ukombozi, nao walifanya kiini cha utendaji wao kikawa juu ya kurudi kwake kusikoonekana na juu ya Ufalme wa Mungu.—1 Timotheo 2:6.

Ili kuwe na “utoaji wa kweli za Biblia katika lugha mbalimbali” kwa njia iliyopangwa vizuri zaidi kitengenezo ya kutumia vichapo, Wanafunzi wa Biblia katika 1884 waliandikisha kisheria Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi wa Sayuni iliyokuwa tayari imeanzishwa. Tayari mwaka uliotangulia vichapo vilikuwa vimetokea katika Kisweden, halafu katika 1885 vikatokea vitabu vya kwanza vya Kijeremani. Katika 1892 kazi ya umisionari katika nchi cha kigeni ilifikiriwa. Leo, Wanafunzi wa Biblia​—wanaojulikana sana kuwa Mashahidi wa Yehova—​wanahubiri “habari njema hizi za Ufalme” katika nchi na maeneo 208 na katika lugha karibu 200.—Mathayo 24:14, NW.

Walio wengi wa Mashahidi walikuwa washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo au wa dini nyinginezo na waliamini mafundisho yenye kuvunjia Mungu heshima. Baada ya wao kutwaa maarifa sahihi juu ya Mungu na kujizoeza imani, walitubia mwendo wao wa makosa, wakageuka, wakawa watumishi wa Yehova waliojitoa wakfu na kubatizwa. ‘Kutenda matendo yanayopatana na kutubu kwao’ kuliwapa dhamiri safi na amani pamoja na Mungu.—Matendo 26:20; Yohana 17:3.

Je! Historia ya Kidini Ina Manufaa Yo Yote?

Ndivyo, inayo. Sehemu kubwa za Biblia zina historia ya kidini yenye manufaa. (Warumi 15:4) Vile vitabu vya Injili vinaonyesha jinsi Yesu alivyofunza ukweli juu ya Mungu na kusudi Lake kwa dunia. Wafuasi wa Yesu walipaswa kungojea Ufalme wa kimbingu ambao ungetatua matatizo ya kidunia. “Endeleeni kulinda, basi, kwa sababu hamjui wala siku hiyo wala saa hiyo,” Yesu akasema.—Mathayo 6:9, 10; 25:1-13, NW.

Historia ya kidini inathibitisha kwamba Wakristo wa mwigizo tu waliotabiriwa walikuja, nao wakaanzisha utawala wao wenyewe wa kidunia. Yale Mageuzo ya Kanisa yalibadili sura ya ulimwengu lakini hayakurudisha mafundisho safi ya Biblia. Historia inaonyesha pia kuwako kwa Wakristo wa kisasa ‘wanaoendelea kulinda’ ambao “si sehemu ya ulimwengu” na wanaweka Ufalme wa Mungu kwanza. (Yohana 17:16, NW) Habari hizi zinasaidia watu wengi watambue wafuasi wa kweli wa Yesu leo.

Barbara aliyetajwa mwanzoni mwa makala hii, ni mmoja wa Mashahidi watendaji zaidi ya 3,000,000 ulimwenguni pote wanaojaribu kufikia watu wanyofu wakiwa na lile “fundisho safi la Injili.” Kadiri fulani ya maarifa juu ya historia ya kidini inakuwa yenye manufaa pia kwa hao watangazaji wa Ufalme.

[Maelezo ya Chini]

a Katika nyakati za kisasa, wanahistoria wa Kanisa Katoliki la Kiroma wameshikilia kwamba kugongomewa kwa hoja hizo na Lutheri kwenya mlango wa kanisa lenya ngome katika Wittenberg katika Oktoba 31, 1517 ni “hadithi ya kimapokeo ya makanisa ya Kiprotestanti.” Hata hivyo, uhakika usiofanyiwa ushindani ni kwamba yeye alimwandikia Askofu Mkuu barua ya heshima siku hiyo na akaingiza ndani nakala ya hoja hizo. Lutheri alimwomba awakaripie wahubiri wake wenye kuuzia watu rehema za dhambi na ayafute maagizo ya kufanya hivyo. Barua ile asilia ingali katika Jumba la Hifadhi za Kiserikali Sweden katika Stockholm.

b Ona “Shamba Lenye Kuzaa Ngano na Magugu” katika gazeti Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1982, kurasa 9-13, na “‘Kuingiza Kisiri-siri Madhahebu Zenye Kuharibu’,” la gazeti Mnara wa Mlinzi katika Februari 15, 1984, kurasa. 8-14.

[Sanduku katika ukurasa wa 28]

Rehema ya dhambi ni ile ondoleo la adhabu (ya kidunia) kwa dhambi. . . Ondoleo linakuwa na matokeo hapa au katika purgatori.​—Catholic Scholar Joseph Lortz.

Hata leo, wanachuo hawakubaliani juu ya maana ya rehema ya dhambi na mambo inayomaanisha kwa maisha ya Mkatoliki.​—Protestant Historian Heinrich Bornkamm.

Rehema ya Dhambi—Fundisho Maalum la Kikatoliki

Padri muungamiwa aliweka juu ya Mkatoliki mwenye kutubu wajibu wa kufanya kitubio (kama vile sala, kufunga, upaji kwa maskini, au kufunga safari ya kuabudu). Papa anaweza kuondoa adhabu hizo kwa sababu, kulingana na nadharia ya Kanisa Katoliki, yeye ni bwana wa kusimamia adhabu zote za kidunia (kutia na purgatori) naye anatoa rehema ya dhambi kutokana na ile inayoitwa hazina ya mastahili ya Kristo na watakatifu. Katikati ya karne ya 11 na 15 pendeleo hilo liliingia katika hali ya matumizi mabaya sana na likaelezwa kuwa “shughuli ya kibiashara iliyopanuka sana, yenye kufanywa kwa kuachilia mbali viwango vya kiadili na katika kupingana na mafundisho ya Maandiko Matakatifu.”

Kanisa halikioni kitubio kuwa sawa na kusamehe dhambi. Lakini, hata katikati ya karne ya 11 na 15, watu walibaki na “ile imani nyepesi ya kwamba kwa kutoa malipo lile deni [la dhambi] lilifutwa,” na wahubiri wa kuuza rehema za dhambi wakaunga mkono wazo hilo. Hoja za Lutheri zilielekezwa dhidi ya “hekaya” hizo zikasema hivi kwa muhtasari: “Rehema za dhambi ni kazi za wanadamu na hazina uhusiano pamoja na ile injili safi.”

Papa Clement wa Sita alianzisha fundisho hilo katika 1343 lakini hakulifasili wazi-wazi. Hivyo Lutheri angeweza kutetea msimamo wake kwa kutumia hali hiyo ya mambo kutosemwa wazi katika fundisho hilo. Kanisa liliziba tendo hilo kwa haraka kwa kutoa ufafanuzi rasmi juu ya rehema ya dhambi katika 1518. Lakini tangazo rasmi la Papa Leo wa Kumi halikutoa “uthibitisho wa kibiblia kwa sababu ya kufanya ustahili wa Kristo na watakatifu ulingane na hazina ya rehema za dhambi.” Jambo hilo lilichokora Lutheri Mkatoliki afanye uamuzi mkubwa sana. Katao lake juu ya mfumo wa rehema za dhambi zisizo za Kimaandiko lilifungulia njia yale Mageuzo ya Kanisa, na kutupiliwa mbali kwa maandishi yake yenye kuchambua kukaongoza kwenye ule mgawanyiko mkubwa wa kanisa.

Katika nyakati za kisasa, uchambuzi mkali wenye kufanywa na walio ndani ya Kanisa Katoliki la Kiroma “haukuongoza kwenye badiliko la mfumo huo bali uliongoza tu kwenye mageuzo ya zoea hilo.” Katika 1967 Papa Paulo wa Sita aliamua kwa kupendelea ile nadharia ya zamani ya rehema za dhambi. Kwa Wakatoliki, swali la kukata maneno lingali ni hili: Je! mimi nafuata Neno la Mungu, au naamini mafundisho ya wanadamu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki