Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 10/15 kur. 3-4
  • Je! Dini Ni Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Dini Ni Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ule Upande Usiofaa
  • Mipaka ya Kiadili Iliyovunjwa
  • Je! Dini za Ulimwengu Zinatoa Uongozi Unaofaa?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Dini Yajiunga
    Amkeni!—1994
  • Dini Ina Faida Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 10/15 kur. 3-4

Je! Dini Ni Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili?

KATIKA kujibu swali hilo, mamilioni wangekubaliana na George Bernard Shaw, aliyeandika: “Dini ni kani kuu—kani ile moja tu ya kweli inayoendesha matendo katika ulimwengu.” Tofauti na hivyo, John Ruskin mtungaji Mwingereza wa karne ya 19, akiandika juu ya msingi wa kuwa na unyofu, alidhihaki kwamba “Dini ya mdanganyifu sikuzote ndiyo inayomfanya awe mwovu zaidi.” Ni maoni yapi ambayo wewe unafikiri yanaukaribia zaidi ukweli?

Kama ushuhuda wa kwamba dini ni kani ya kutokeza maadili, huenda mtu fulani akaelekeza kidole kwa mtu mmoja ambaye alikuja kuwa “mwanamume aliyebadilika” wakati yeye ‘alipoweka maisha yake wakfu kwa Yesu Kristo.’ Hivyo ndivyo gazeti moja la kimataifa lilivyosimulia “wongofu” wa Charles Colson, ambaye alikuwa amehusika katika ile kashifa ya Watergate. Huenda mtu fulani mwingine akaelekeza kidole kwa wale ambao wanadai kwamba dini yao iliwaokoa kutoka maisha ya umalaya au uzoelevu wa pombe. Katika nchi zisizo za Kikristo, mamilioni ya Biblia yamegawanywa, na bila shaka hilo limesaidia watu wengi wafanye maendeleo ya kiadili katika maisha zao. Kwa wazi, dini imetokeza mavutano mema ya kiadili juu ya watu hao.

Ule Upande Usiofaa

Kwa upande ule mwingine, dini ya Hitler haikuwa kizuizi kikubwa kwake. Jambo hilo liliongoza watu wenye moyo mweupe kujiuliza ni kwa sababu gani ombi lililofanywa kwa Papa Pius wa 12 ili Hitler aondolewe katika ushirika halikujibiwa kamwe. Catholic Telegraph-Register la Cincinnati, Ohio, chini ya kichwa “Alilelewa Akiwa Mkatoliki Lakini Ahalifu Imani Yasema Barua ya Simu kwa Papa,” iliripoti kwamba, “Ombi limefanywa kwa Pius wa 12 kwamba Mtawala wa Milki Adolph Hitler aondoshwe katika ushirika.” Kama kitendo hicho kingalichukuliwa, je! ingeweza kuwa kingaligeuza matokeo ya vita na kusaidia kuepusha wanadamu na kutaabika kwingi sana? Linalosikitisha ni kwamba, papa huyo hakujibu kamwe.

Kuwa na masuria wa kuishi nao ni jambo la kawaida sana katika nchi fulani za Kikatoliki katika Amerika ya Kusini. Na katika Amerika ya Kaskazini monsinya mmoja aliandikia afisi ya mhariri hivi: “Andikisheni Kisheria Umalaya—Hilo Ndilo Suluhisho la Utakatifu.” (Philadelphia Daily News) Tazama pia hali zilizo katika nchi fulani za Kiprotestanti ambako tendo la kubadilishana wake, ngono kabla ya ndoa, na ngono bila ndoa ni mambo ya kawaida sana. Tunaona sababu kwa jambo hilo ikiwa imedokezwa katika kichwa hiki cha karatasi yenye habari: “Mapasta Wanyamazia Ngono Kabla ya Ndoa.” Makala hiyo ilisema: “Mapasta wa Amerika wamekuwa na dhambi kwa kunyamaza wasihubiri juu ya ngono kabla ya ndoa . . . Wao wanaogopa watapoteza watu fulani kati ya washiriki wa makanisa ya mitaa yao.” (Telegraph, North Platte, Nebraska) Kwa hiyo je! dini yote ni kani ya kuleta mema ya kiadili?

Katika Jumuiya ya Wakristo, kutokuwa kwa dini na kani ya kiadili kunaonekana sana wakati wa vita. Ebu ona unafikiri nini juu ya madai haya yanayosikika kuwa na ahadi nzuri. Katika 1934 Walter W. Van Kirk, aliyekuwa wakati huo mwandishi wa idara ya Baraza Kuu la Makanisa ya Kristo ya Amerika, aliandika: “Wahubiri na watu wa kawaida wamechukua msimamo wa uthabiti dhidi ya vita . . . Jitihada kali hiyo ya makanisa kutafuta amani inatokana na usadikisho wa kwamba vita ni kinyume kabisa cha mahubiri na mazoea ya Yesu.” (Religion Renounces War) Baada ya kutaja makanisa kadha na viongozi wa kidini, kitabu hicho kilimalizia hivi: “Makanisa, kwa ujumla, yamesema kwa wazi kwamba wao hawapasi tena kuchukuliwa kama washiriki katika ile shughuli ya kuua na kulemaza wanadamu. Wahubiri.. . [wanaosha] mikono yao damu ya watu wenzao, wao wanaacha ushirika pamoja na Kaisari.”

Hata hivyo, matabiri hayo ya kutazamia mazuri kwa kusikitisha hayakutimia. Wakati vita ya ulimwengu ya pili ilipotokea, hakuna hata moja ya dini zile kubwa-kubwa za Jumuiya ya Wakristo iliyochukua msimamo imara ‘kukana vita.’ Je! kanisa lililo katika eneo lako wewe lilifanya hivyo?

Mipaka ya Kiadili Iliyovunjwa

Baada ya kufikiria ushuhuda fulani katika pande zote mbili, je! wewe hungekubali kwamba katika visa vyote ambavyo ni vingi mno, dini za ulimwengu zinazofuatwa na watu wengi hazijakuwa kani yenye nguvu ya kuleta mema ya kiadili? Gazeti Look lilitangaza hivi: “Makanisa . . . yameshindwa kutoa uongozi wa kiadili, na kwa sababu hayo ndiyo yenye daraka lililo kubwa zaidi ya yote, kushindwa kwayo ndiko kubaya zaidi.” The Courier-Mail la Brisbane, Australia, lilieleza juu ya kushindwa kwa dini ya Jumuiya ya Wakristo kuandaa kizuizi juu ya ukosefu wa adili ya ngono: “Kwa habari ya Maaskofu na Makanoni . . . kuandika kwamba ngono nje ya ndoa huenda ikawa ni kitendo cha fadhili ambacho “kinatangaza Utukufu wa Mungu,’.. . kwamba jambo lililo baya si uasherati wenyewe wala uzinzi si kosa kwa lazima; hapo ndipo mwanamume na mwanamke wa kawaida, na hasa mvulana na msichana wanaoendelea kubalehe, wanapovurugika kupambanua kati ya yanayofaa na yasiyofaa. Tokeo la kufanya maamuzi yote hayo kwa ajili ya ile Adili Mpya limekuwa kuvunja mipaka ya kiadili.”

Hapana, kwa ujumla, dini za ulimwengu si kani ya kweli ya kuleta mema ya kiadili. Tofauti na hilo, ni lazima hizo zichukue daraka fulani la kulaumiwa kwa hali ya kusikitisha ya maadili leo. Hata hivyo, kwa kuwa dini inasemwa kuwa inamaanisha “utumishi na ibada kwa Mungu au nguvu zinazozidi zile za asilia,” je! hiyo haipasi kuwa kani ya kuleta mema katika nchi zote ambako imeenea sana? Ni jambo gani linalokosekana? Ni jinsi gani dini yako wewe inavyoweza kutokeza kani hiyo leo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki