Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/15 uku. 29
  • “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • “Kujitoa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Hudhuria “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1987
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • “Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1986
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/15 uku. 29

“Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya

NI MTESEKO mkubwa kama nini ulio katika ulimwengu kwa sababu ya ukosefu wa haki! Utumizi mbaya wa nguvu ambao umeenea sana kwa upande wa watawala fulani wa kisiasa umetokeza mteseko mwingi usio wa haki. Mapendezi ya biashara yenye pupa yanaleta uonevu juu ya watu, hiyo ikitokeza magumu mengi. Halafu kuna ule uonevu wenye kufanywa na viongozi wa kidini leo ambao ni kama walinganifu wao katika siku ya Yesu, na ambao juu yao yeye alisema: “Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.” (Mathayo 23:4) Ndani ya jamaa pia mna utumizi mbaya mwingi wa nguvu na ukosefu wa haki unaotokana na jambo hilo.

Historia inaonyesha kwamba ungekuwa ubatili kutegemea wanadamu wasiokamilika walete dawa ya mambo hayo, hata kama wao wana makusudi mazuri kama nini. Lakini katika mbingu yumo Aliyeko Mkuu Zaidi na Mwamuzi, Yehova. Yeye ndiye Mungu wa haki. Kwa kufaa, Musa aliimba hivi: “Yule Mwamba, mkamilifu ni utendaji wake, kwa maana njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye pamoja naye hapana ukosefu wa haki; mwenye uadilifu na unyofu ni yeye.”​—Kumbukumbu 32:4, NW.

Yehova amechukuliana kwa muda mrefu na matendo yote ya ukosefu wa haki ya ulimwengu huu, lakini yeye hatafanya hivyo kwa wakati wote. Kuna wakati uliowekwa rasmi wa yeye kutenda na ndipo ule unabii unaopatikana kwenye Isaya 14:4-7, NW utakapotimizwa, ambao unaahidi kwamba namna yote ya udhalimu itakoma na ‘dunia nzima itakuja kwenye pumziko.’

Kwa sababu ya imani yao yenye uthabiti katika ahadi hizo za kiunabii, Mashahidi wa Yehova wanakuwa na upendezo wa kutangaza kote kote kwamba karibuni Yehova ataleta mwisho wa uonevu wote, ukosefu wa uadilifu, na ukosefu wa haki kwa kuharakisha utawala kamili wa Ufalme. Wakati huo hakuna mmoja atasababisha dhara lo lote wala uharibifu, kwa maana ‘dunia itajawa na kumjua Yehova, kama vile maji yanavyoifunika bahari.’​—Isaya 11:9.

Ili kuimarisha imani yetu katika hukumu za Yehova zenye uadilifu, ile mikusanyiko ya wilaya ya 1988 itakuwa na kichwa “Haki ya Kimungu.” Kukazia kichwa hicho hakutatuchochea sisi tuongeze mwendo tu katika kujulisha tumaini letu kwa haki ya kimungu bali kutatutia moyo pia tutende kupatana na haki ya kimungu katika shughuli zetu zote.

Sote tulio watumishi wa Yehova tunajua kwamba kwa sababu ya kukiuka sheria kwa wazazi wa kwanza wetu, mwinamio wetu ni kuelekea ubinafsi, kuelekea ukosefu wa haki. Kwa hiyo sisi tutathamini habari nzuri ambazo tutapokea kwa njia ya hotuba za Biblia, mawonyesho, mahoji, na drama ambazo zitakazia ule uhitaji wa kutegemeza haki ya kimungu. Hilo linapatana na ile amri kwenye Mika 6:8, NW, ‘kujizoeza haki, kupenda fadhili, na kuwa mwenye kiasi katika kutembea pamoja na Mungu wetu.’ Hilo linafanyiza upatani, uradhi, na furaha; linasaidia pia kuendeleza zaidi kuhubiriwa kwa habari njema katika dunia yote.

Upande wa kutokeza wa mikusanyiko hii utakuwa kwamba hesabu fulani ya miji itaunganishwa kusikia hotuba za pekee zenye kutolewa na washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Pia, kwa ajili ya mikusanyiko hii wamisionari katika sehemu zote za ulimwengu wataandaliwa usafirishaji; jambo hili pia litawasaidia kutembelea jamaa zao tena.

Yehova akipenda, ile “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya itaanza Alhamisi yapata saa 7:30 na itamalizika saa 10:00 Jumapili. Acheni sisi tupange mambo yetu tuwepo wakati programu inapoanza na tupange kukaa mpaka wimbo na sala ya kumalizia kila siku. Uje ukiwa na hamu nyingi ya kiroho na ukiwa na vifaa vya kuandikia mambo. Uwe na uhakikisho wa kwamba Yehova ameweka akibani kwa ajili yetu “karamu nono” ya vitu vizuri ambavyo vitatuimarisha na kutusisimua kwa ajili ya kazi iliyoko mbele.​—Isaya 25:6; Wimbo Ulio Bora 2:4.

Ndiyo, acheni kila mmoja aje akiwa amepiga moyo konde kupata baraka ya kiroho kwa kadiri kubwa iwezekanavyo kutokana na ile “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki